Mapendekezo na ushauri wangu kwa Bodi ya Mikopo

jonas amos

JF-Expert Member
Jul 4, 2016
3,621
4,400
Habari Tanzania
Habari African

Leo napenda nitoe wazo la juu ya mikipo inayotolewa na bodi ya mikopo chuo kikuu
Binafsi nimeona ni wazo jema mpaka nalileta hapa mkekani japo wapo watakao ungana na mimi ila sitoshangazwa na watakao kuwa tofauti na mimi hii si tatizo hata na huo ndo uhuru wa mawazo kikatiba.

Kwa muda mrefu selikal imekuwa ikiwapa wanafunzi wake mkopo mara baada ya kumaliza masomo ya form six kwenda chuo ikiwa ni fedha kwa ajili ya ada na matumizi mengine ya kibinaadamu kama malazi na chakula.

Na kwakuwa bodi hii husika ya mikopo imefika mahali ni kama inazidiwa kutokana na wanafunzi wengi kuwa na sifa stahiki ili kupata mkopo na wanakosa na kwakuwa wengi wao wanategemea kuajiliwa na ndipo waanze kulipa mkopp huo na wengine kuukwepa kabisa kuulipa mpaka selikal kufikia kuanza kudai kinguvu kwa wadaiwa wote sugu wa mkopo baada ya kuongeza asilimia saba hivi za makato na kufikia 15 jambo ambalo linapigiwa kelele na wengi sana na ahii ni kutokana na wakati ambapo fedha imekuwa adimu kidogo na mishahara kutopanda hali inayoelekea kuwaumiza zaid watumishi
Ushaur wangh ni kama ifuatavyo:-


SELIKALI INGEANZA KUWAKOPESHA WANAFUNZI HAO WA FORM 6 FEDHA HIZO KWA AJILI YA KUANZISHA BIASHARA AMBAPO. BAADA YA MUDA WATAKUWA NA UWEZO WA KUREJESHA MKOPO KWA WAKATI NA PIA SELIKAL ITAKUWA NA NAFASI NZURI YA KUONGEZA WIGO WA UKUSANYAJI WA MAPATO YA HALMASHAUR NA TRA KWA UJUMLA.
NA hii
Ingewekwa flat rate kwa ujumla wake kama m. 5 basi watoe hizo watu wapige maisha kusoma sana ni uoga wa maisha na pia tunachelewashana maisha
Hapo sasa selikal ingeunda bodi maalumu ya kupitia business plan mbali mbali ili vijana wapewe wakiwa tayar wanamalengo sio kwenda kulewea
Hiyo ni kama changamoto tu mana hata mkopo huu wa sasa baadhi wanatumia kwa matumiz yao binafs tofaut na mkataba wao na bodi, wapo walioanzisha biashara kwa mikopo hiyo na wametusua sasa kimaisha

Nawasilisha kwenu mim jonas amos mjasilia mali wa kawaida jaman matusi tu naogopa sina moyo wa daud
 
Inaitwa bodi ya mikopo kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya juu.
Siyo bodi ya mkopo kwa ajili ya wanafunzi waliomaliza kidato cha sita.
Labda itengenezwe bodi nyingine kwa ajili ya kazi hiyo..
 
Inaitwa bodi ya mikopo kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya juu.
Siyo bodi ya mkopo kwa ajili ya wanafunzi waliomaliza kidato cha sita.
Labda itengenezwe bodi nyingine kwa ajili ya kazi hiyo..
Nimesema hapo iundwe bodi maalum kwa ajili ya hilo
 
Nimesema hapo iundwe bodi maalum kwa ajili ya hilo
Hiyo iliyopo tu inawapwelepweta itakua hiyo unayotaka iundwe? Kiufupi ushauri wako hauna Tija kwa Taifa, nadhani muda umefika sasa serikali kuwekeza katika vyuo vya kati zaidi kuliko vyuo vya elimu ya juu,vyuo vya kati hutoa watu wasio subiri ajira mfano VETA hutoa ujuzi ambao mlengwa akiwezeshwa huweza kujiajiri bila ya kumsubiri Raisi afungue ajira, nadhani ni wakati muafaka sasa hata ma bank kuwekeza katika vijana wanaomaliza vyuo vya kati kwa kuwapa mikopo iliyo na riba nafuu zaidi na hii yote itawezekana ikiwa serikali itaweka msisitizo kwenye hilo la ku expand wigo wa vyuo vya kati hasa vya ufundi pamoja na kutengeneza mazingira rafiki kwa ma benk kuwakopesha vijana wanaohitimu
 
Hiyo iliyopo tu inawapwelepweta itakua hiyo unayotaka iundwe? Kiufupi ushauri wako hauna Tija kwa Taifa, nadhani muda umefika sasa serikali kuwekeza katika vyuo vya kati zaidi kuliko vyuo vya elimu ya juu,vyuo vya kati hutoa watu wasio subiri ajira mfano VETA hutoa ujuzi ambao mlengwa akiwezeshwa huweza kujiajiri bila ya kumsubiri Raisi afungue ajira, nadhani ni wakati muafaka sasa hata ma bank kuwekeza katika vijana wanaomaliza vyuo vya kati kwa kuwapa mikopo iliyo na riba nafuu zaidi na hii yote itawezekana ikiwa serikali itaweka msisitizo kwenye hilo la ku expand wigo wa vyuo vya kati hasa vya ufundi pamoja na kutengeneza mazingira rafiki kwa ma benk kuwakopesha vijana wanaohitimu
LadyAj hilo nalo neno kweli umefumbua zaid sista
Nadhan ni wakati wa selikal ibadilike kweli katika utekelezaji wake
 
Back
Top Bottom