Mapato na Matumizi ya zaka, sadaka, fungu la kumi na michango 'Makanisa ya Walokole'

Mchekechoni

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
279
19
Tatizo la usiri wa mapato na matumizi katika makanisa ya 'walokole' limechukua sura mpya baada ya kujitokeza vilio vya baadhi ya waumini toka makanisa mbalimbali ya madhehebu hayo wakitaka uwazi juu ya matoleo yao. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na viongozi wakuu wa makanisa hayo kutokuweka bayana mahesabu ya mwaka ya Mapato na Matumizi, kama inavyohitajika chini ya sheria ya usajili wa taasisi zisizo za serikali (makanisa yakiwemo). Sasa ni muda mwafaka wa mambo kuwekwa hadharani mbele ya washarika wa makanisa hayo ili kuweka sawa hali na kuondoa migogoro inayopelekea washirika na viongozi wao kufikishana mahakamani. Makanisa ya Katoliki, Lutheran, Anglikana, SDA, n.k yana utaratibu wa kutangaza mapato mara kwa mara na pia huwasilisha mahesabu ya mwaka tofauti na 'makanisa ya walokole', ni muhimu hatua za haraka zichukuliwe ili kuepusha janga la kitaifa hasa ikizingatiwa kwamba 'makanisa ya walokole' yametapakaa nchi nzima!
 
Tatizo la usiri wa mapato na matumizi katika makanisa ya 'walokole' limechukua sura mpya baada ya kujitokeza vilio vya baadhi ya waumini toka makanisa mbalimbali ya madhehebu hayo wakitaka uwazi juu ya matoleo yao. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na viongozi wakuu wa makanisa hayo kutokuweka bayana mahesabu ya mwaka ya Mapato na Matumizi, kama inavyohitajika chini ya sheria ya usajili wa taasisi zisizo za serikali (makanisa yakiwemo). Sasa ni muda mwafaka wa mambo kuwekwa hadharani mbele ya washarika wa makanisa hayo ili kuweka sawa hali na kuondoa migogoro inayopelekea washirika na viongozi wao kufikishana mahakamani. Makanisa ya Katoliki, Lutheran, Anglikana, SDA, n.k yana utaratibu wa kutangaza mapato mara kwa mara na pia huwasilisha mahesabu ya mwaka tofauti na 'makanisa ya walokole', ni muhimu hatua za haraka zichukuliwe ili kuepusha janga la kitaifa hasa ikizingatiwa kwamba 'makanisa ya walokole' yametapakaa nchi nzima!

Niko kwenye makanisa ya kilokole since 1998..yametofautiana sana.

Kuna mengine yanatangaza na yako wazi kwenye matumizi ya sadaka
Kuna mengine ambayo hayatangazi kabisa, it is even illegal to know it

Mengi ambayo hayatangazi yako kwenye mtindo wa ministries na ni makubwa sana navery powerful.

You are right?who should be blamed on this? followers au wachungaji??
 
I wish to hear directly from the congregation members themselves! Ukweli unabaki kuwa ukweli tu, 'Mtumishi atakula madhabahuni'. Wachungaji na waumini kuweni wakweli, je kuna 'auditing' yoyote katika mapato na matumizi kwenye makanisa yenu? Hususan, makanisa ya 'kilokole', je yanaendesha shughuli zake kwa mujibu wa katiba zao?
 
Hesabu zitatoka wapi, kuna tangazo linatoka channel ten '................tafadhali changia kanisa letu, peleka mchango wako katika benki kwa jina la anthony lusekelo....................' je hapa kuna hesabu au tutazidi kuona magari ya kifahari tu hapa bongo.
 
biashara matangazo na watu wanasaka noti mujini humu!!!! in short naona kama haya makanisa ya kiroho mengi yako kibiashara zaid!!!!!! we nenda kaskilize tuuu af uslipe hiyo sadaka! kwani wanawashkiaga viboko ili mtoe hizo zaka?
 
biashara matangazo na watu wanasaka noti mujini humu!!!! in short naona kama haya makanisa ya kiroho mengi yako kibiashara zaid!!!!!! ukitaka kujua ile mida ya sadaka msistizo unakuwa mwiing muziki na wachungaji utawaskia wananena kwa lugha weeee!!! pesa ni sabuni ya roho bwanaaaa. nenda kaskilize tuuu af uslipe hiyo sadaka! kwani wanawashkiaga viboko ili mtoe hizo zaka?
 
Kuna watu wanadhani kuwa makanisa ya 'kilokole' yako juu ya sheria. Napenda kuwakuwakumbusha kuwa makanisa yote ili yaendeshe shughuli zake kihalali hapa nchini, ni lazima yapate usajili kama NGO's, hivyo uwazi wa mapato na matumizi ni jambo la msingi, na kutojua sheria sio kinga ya kuvunja sheria za nchi. Wachungaji wanatarajiwa kuwa msitari wa mbele katika kuonyesha utii kwa mamlaka na sheria zake, ili wawe mfano kwa waumini wao! Hata katika maandiko matakatifu, tunasoma juu ya mitume wa kwanza walivyojitenga mbali na masuala ya fedha kwa kuteua wazee, ili wao wawe na muda wa kutosha wa kudili na utumishi walioitiwa. Suala la uwazi kwenye mapato na matumizi ni muhimu sana sana, ndio maana katika kanisa la kwanza watu wawili mtu na mkewe walikufa kwa kudanganya hesabu ya kuuza shamba na kupeleka madhabahuni kiasi pungufu, 'mshahara wa dhambi ni mauti'. Aliye na masikio na asikie, neno hili Roho Mtakatifu aliambiayo makanisa!
 
Hata kama wakitangaza haitasaidia aisee, Vipi kama sadaka inapatikana 1,000,000 Then wanatangaza 150,000?
 
what do you mean unaposema makanisa ya kilokole??.Maana usikute unachanganya kanisa na dhehebu.maana nijuavyo mimi labda nisahihishwe ni kuwa kanisa ni moja tu ila madhehebu ni mengi,mfano RC,TAG,FPCT,LUTHERAN,ANGLICAN etc.kwa hiyo hili kanisa moja tu ninalokiri kwenye imani ni tofauti na unachowakilisha hapa.Uwe specific na usigeneralize,mfano sema Lutheran hawakutoa mahesabu yao mwaka ........,TAG etc.kuweka wote kwenye kapu moja haileti.ile dhana ya JF inakuwa haipo tena kama ni kugeneralize hivyo.
 
.....sigh...and with this last gasp of breath..... I fulfill my mission here on earth......dying like Apostle Paul.....a very happy soul indeed. In Jesus name, Amen!
 
Inaonekana kana kwamba kwa sasa kuna mkanganyo mkuu katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na imani. Shetani amefanikiwa kwa kiwango kikubwa kulishutumu kanisa, lakini hata hivyo kanisa ndilo limeruhusu udhaifu kuweza kushutumiwa, maana mashutumu linayotupiwa yana ukweli. Inawezekana vipi mtu kuwa na huduma ndani ya mji na amekubali sheria za nchi kwa kujisajili akusanye pesa bila kuweka wazi ni kiasi gani kapata na zimetumika je. Huu ndio uadilifu na utumishi uliotukuka, kwamba huruhusu mazingira hata ya kutuhumiwa. Inawezekana vipi mtu kutaka cha wengi kiwe chake na chake kibaki kuwa chake? Nazungumza na wale walioanzisha miradi kwa pesa za kanisa ama kupitia kivuli cha kanisa na kuifanya hiyo biashara kuwa mali yake na familia yake lakini sii ya kanisa. Sipati picha hapa. Ni makosa makubwa kwa kanisa kuruhusu ubinafsi huu uliopindukia mipaka kwa kisingizio tu chepesi cha utajiri wa miujiza. Wafanya biashara wafanye biashara zao na watabarikiwa kwa hilo. Lakini kuruhusu injili kuwa biashara ni uhaini ambapo kupitia hali hii kanisa sasa limekosa kuaminiwa, na wala halina tena ujasiri wa kukemea ufisadi. Waamini tuna jambo moja tu la kumshukuru Mungu kwamba, katika nano lake ameahidi kuinua kiwango dhidi ya hila za shetani. Alitumia mfano wa beramu. Beramu ni boya linalopima maji, hivyo hata maji yazidi kiwango gani, boya linangangania kuwa kileleni. Maana yake ni kwamba shetani amefikia kiwango cha kukomaa na mtoto wa Mungu/kanisa limefikia kimo cha mtu mkamilifu. Ndio maana nasema pamoja na injili kupotoshwa na wajasiriamali wa injili, bado kuna jeshi Mungu amejisazia ambalo halijapiga goti kwa baal wala halitafanya hivyo. KANISA LISIRUHUSU MAZINGIRA YA SHUKU BALI KILE LINACHOKIHUBIRI, KIWE NI MAISHA YALO YA KILA SIKU.
.
 
Back
Top Bottom