Shinto
JF-Expert Member
- Dec 6, 2010
- 1,781
- 96
Siku za karibuni kumekuwa na sakata linaloendelea juu ya kile kilichokuwa CCJ.
Kuna makundi matatu makubwa yanahusika hapa. Ninachoshindwa ni kufahamu uhusiano wa makundi haya; kwa sababu wana maslahi yanayotofautiana.
Au ndio paradigm shift? Au ndio ule unafiki wa wanasisa? Chukua mfano wa Marando, alikuwa sauti kuu ya mageuzi wakati wa NCCR, akamuondoa Mrema NCCR, akahamia CCM akapewa ubunge wa Afrika Mashariki, sas tena ni sauti ya ukombozi ndani ya Chadema!
Kumbukeni pia kuwa CCM waliwahi kusema kuwa mapcha watatu wangetumia chama fulani cha upinzani ku-react juu ya hatua hii ya kuvuliwa magamba, je CDM ndio inatumika kwa kujua au bila kujijua?
Kuna makundi matatu makubwa yanahusika hapa. Ninachoshindwa ni kufahamu uhusiano wa makundi haya; kwa sababu wana maslahi yanayotofautiana.
- Kuna mapacha watatu (watuhumiwa wa ufisadi). Hawa ni kundi liliolokuwa na nguvu katika serikali ya kikwete lakini likaharibu! Sihitaji kueleza kwa undani kwani kila mtanzania analifahamu. kwa siku za karibuni CCM imekuja na sera ya kujivua magamba, kwa tafsiri ya nje ni kuliondoa kundi hili kwenye political arean!
- Kuna mapacha watatu wengine ambao walikuwa vinara wa kupambana au kupiga makelele ya ufidsadi ndani ya CCM. Hili kundi halikuwa na nguvu sana, na lilichapwa demotion. Lakini wakaendelea kubaki CCM na madaraka fulani. Hili kundi linashutumiwa kuanzisha directly au indirectly CCJ.
- Kuna Chadema, hili lilizoa wale waliokuwa wanachama wa CCJ baada ya CCJ kukosa usajili wa kudumu. Kwa mtizamo walikuwa wanafanya kazi na kundi la pili kupambana na kundi la kwanza. Msisahau NAPE alishawahi kuonekana na pengine kuhutubia kwenye mikutano ya Chadema kwa spirit hiyo ya kupamabana na ufisadi.
Au ndio paradigm shift? Au ndio ule unafiki wa wanasisa? Chukua mfano wa Marando, alikuwa sauti kuu ya mageuzi wakati wa NCCR, akamuondoa Mrema NCCR, akahamia CCM akapewa ubunge wa Afrika Mashariki, sas tena ni sauti ya ukombozi ndani ya Chadema!
Kumbukeni pia kuwa CCM waliwahi kusema kuwa mapcha watatu wangetumia chama fulani cha upinzani ku-react juu ya hatua hii ya kuvuliwa magamba, je CDM ndio inatumika kwa kujua au bila kujijua?