Maoni yangu: Tume na bunge la katiba ni kitanzi cha Muungano

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
302
Nimeisoma mara mbilimbili sheria ya mabadiliko ya katiba iliyosainiwa juzi na rais na kugundua kuwa composition ya wajumbe ilivyo itapelekea kuvunjika kwa Muungano. Nitafafanua.

Kwa mujibu wa sheria hiyo wajumbe wa tume wanatakiwa kuwa sawa 50-50 kutoka pande zote hivyo kuwapa wajumbe kutoka Zanzibar nafasi nzuri ya ushawishi wakati wa kutoa maoni kudai nchi yao ipewe madaraka kamili kama nchi. Hali hii itaendelea kuwepo hadi kwenye bunge la katiba.

Kwa mujibu wa sheria hii bunge maalum la katiba litakuwa na jumla ya wajumbe 595, na kati yao angalau 219 watatoka Zanzibar ambao ni sawa na 37% ya wajumbe wote hivyo kuwafanya wawe na uwezo wa kupata walichokuwa wanakitafuta kwa muda mrefu, na safari hii wakifanya makosa tena hawatakipata kwa muda mrefu ujao.

Kwa mtazamo huu wa sheria hii ni dhahiri kuwa wazanzibari wataondoka na Nchi yao na hivyo kupelekea Muungano uliodumu kwa takriban miaka 50 kuvunjika rasmi.
 
Tatizo kubwa ni kuwa hii katiba mpya ya Tanzania inajadiliwa kwa njia za kisiasa zaidi kuliko kujadiliwa katika ujumla wake.

Ndiyo maana serikali ya Kikwete aliweka vigezo vya kujadilia katiba hiyo na Kikwete mwenyewe akatumia lugha ya vitisho kuwa atasaini muswada huo uliotayarishwa na serikali yake hata kama waasisi wa madai ya katiba mpya (yaani CHADEMA) watasemaje.

Baada ya CHADEMA kuamua kukutana naye ili kumwonyesha mapungufu ya njia anayofuata, CCM wakaja na lugha nyingine, kuwa ni lazima mkutano huo ukutanishe vyama vingine hata vile ambavyo vilipiga kura kukubaliana na muswada huo.

Tangu mkutano wa Chadema na Kikwete kuhusu katiba ufanyike, mambo yameendelea kama mchezo wa kuigiza tu- ni kama tunaangalia sinema za Kanumba na Ray vile.

Kikwete asaini muswada baada ya mkutano wake na CHADEMA ambao walikuwa wakipinga muswada huo, CHADEMA waamua kuandamana nchi nzima kupingwa muswada huo, CUF wakutana na Kikwete kuzungumzia muswada huo ambao tayari ulishasainiwa na kuwa sheria, na sijui NCCR, UDP, UODP, CHAUSTA, na utitili mwingie wa vyama vya upinzani nao watakwenda Ikulu kuzungumzia muswada huo ambao tayari ni sheria.

Nchi zote zilizoandika Katiba zake mpya miaka ya karibuni zilitumia zaidi wataalamu wa mambo ya katiba ambao hawafungamani na upande wowote wa kisiasa ndani ya nchi hiyo; wengine wakitoka nje ya nchi husika.

Hebu angalia muundo wa tume iliyotayarisha katiba mpya ya Kenya ili ujue nina maana gani. kwa leo hapa Tanzania, nchi ambayo imekuwa inajiendesha bila dira yoyote, tunataka katiba mpya kwa maana ya kupaka rangi mpya katiba iliyopo bila kubadili msingi wake badala ya kubomoa katiba hiyo na kujenga mpya na msingi mpya.

Tutaendelea kucheza kwenye matope hadi ambapo raslimali za zote ndani ya nchi zitakapokuwa zimeshatoweka ndipo tutagundua kuwa Katiba mpya ingesaidia kutuachia raslimali hizo. madini yetu yanahamia nje ya nchi kwa kasi ya haraka sana bila kuwasidia watu wetu huku serikali iliyopo haiangaliaa na hilo na katiba ya nchi inaifanya serikali hiyo iwe na uhakika wa kuendelea kuwapo miaka yoye ya maisha yetu.

Ni lazima tuwe makini sana na swala la Katiba, kwani ndilo linalotofautisha nchi na nchi.
 
Asante Kichuguu, ni kweli katiba inajadiliwa kwa misingi ya kiitikadi kitu ambacho ni hatari sana kwa mstakabali wa taifa, tumejionea wabunge hasa wa bara walivyogawanyika badala ya kutetea maslahi ya taifa wao wanatetea maslahi ya vyama vyao.

Nimemsikia jana Seif akiwataka Wazanzibari wawe na msimamo mmoja juu ya mambo wanayotaka katika katiba mpya na waweke kando itikadi zao za kisiasa katika jambo hilo.

Wakati wao wakiwekana sawa sisi huku ndio bado kabisa tunavutana tunaoneshana nani zaidi tutakapozinduka tayari katiba itakuwa imeshaandikwa inasikitisha sana.
 
Nimeisoma mara mbilimbili sheria ya mabadiliko ya katiba iliyosainiwa juzi na rais na kugundua kuwa composition ya wajumbe ilivyo itapelekea kuvunjika kwa Muungano. Nitafafanua.

Kwa mujibu wa sheria hiyo wajumbe wa tume wanatakiwa kuwa sawa 50-50 kutoka pande zote hivyo kuwapa wajumbe kutoka Zanzibar nafasi nzuri ya ushawishi wakati wa kutoa maoni kudai nchi yao ipewe madaraka kamili kama nchi. Hali hii itaendelea kuwepo hadi kwenye bunge la katiba. Kwa mujibu wa sheria hii bunge maalum la katiba litakuwa na jumla ya wajumbe 595, na kati yao angalau 219 watatoka Zanzibar ambao ni sawa na 37% ya wajumbe wote hivyo kuwafanya wawe na uwezo wa kupata walichokuwa wanakitafuta kwa muda mrefu, na safari hii wakifanya makosa tena hawatakipata kwa muda mrefu ujao. Kwa mtazamo huu wa sheria hii ni dhahiri kuwa wazanzibari wataondoka na Nchi yao na hivyo kupelekea Muungano uliodumu kwa takriban miaka 50 kuvunjika rasmi.
Mbona unahamisha yale unayoyawaza kwenda katika vichwa vya Wazanzibari? Wazanzibar wanatambua umuhimu wa Muungano na wanachotaka ni marekebisho ya kasoro ndogondogo na ambazo ni wazi zipo si kwamba zinawaathiri upande mmoja tu wa muungano bali ni pande zote.
 
Mbona unahamisha yale unayoyawaza kwenda katika vichwa vya Wazanzibari? Wazanzibar wanatambua umuhimu wa Muungano na wanachotaka ni marekebisho ya kasoro ndogondogo na ambazo ni wazi zipo si kwamba zinawaathiri upande mmoja tu wa muungano bali ni pande zote.
Najua Zanzibar imesema Mafuta hayamo kwenye muungano kama tukiendelea kufumbia mambo makubwa kama haya kwa kuyaita kasoro ndogondogo muungano utaendelea kutuumiza milele.
 
Tatizo kubwa ni kuwa hii katiba mpya ya Tanzania inajadiliwa kwa njia za kisiasa zaidi kuliko kujadiliwa katika ujumla wake. Ndiyo maana serikali ya Kikwete aliweka vigezo vya kujadilia katiba hiyo na Kikwete mwenyewe akatumia lugha ya vitisho kuwa atasaini muswada huo uliotayarishwa na serikali yake hata kama waasisi wa madai ya katiba mpya (yaani CHADEMA) watasemaje. Baada ya CHADEMA kuamua kukutana naye ili kumwonyesha mapungufu ya njia anayofuata, CCM wakaja na lugha nyingine, kuwa ni lazima mkutano huo ukutanishe vyama vingine hata vile ambavyo vilipiga kura kukubaliana na muswada huo. Tangu mkutano wa Chadema na Kikwete kuhusu katiba ufanyike, mambo yameendelea kama mchezo wa kuigiza tu- ni kama tunaangalia sinema za Kanumba na Ray vile: Kikwete asaini muswada baada ya mkutano wake na CHADEMA ambao walikuwa wakipinga muswada huo, CHADEMA waamua kuandamana nchi nzima kupingwa muswada huo, CUF wakutana na Kikwete kuzungumzia muswada huo ambao tayari ulishasainiwa na kuwa sheria, na sijui NCCR, UDP, UODP, CHAUSTA, na utitili mwingie wa vyama vya upinzani nao watakwenda Ikulu kuzungumzia muswada huo ambao tayari ni sheria.

Nchi zote zilizoandika Katiba zake mpya miaka ya karibuni zilitumia zaidi wataalamu wa mambo ya katiba ambao hawafungamani na upande wowote wa kisiasa ndani ya nchi hiyo; wengine wakitoka nje ya nchi husika. Hebu angalia muundo wa tume iliyotayarisha katiba mpya ya Kenya ili ujue nina maana gani. kwa leo hapa Tanzania, nchi ambayo imekuwa inajiendesha bila dira yoyote, tunataka katiba mpya kwa maana ya kupaka rangi mpya katiba iliyopo bila kubadili msingi wake badala ya kubomoa katiba hiyo na kujenga mpya na msingi mpya. Tutaendelea kucheza kwenye matope hadi ambapo raslimali za zote ndani ya nchi zitakapokuwa zimeshatoweka ndipo tutagundua kuwa Katiba mpya ingesaidia kutuachia raslimali hizo. madini yetu yanahamia nje ya nchi kwa kasi ya haraka sana bila kuwasidia watu wetu huku serikali iliyopo haiangaliaa na hilo na katiba ya nchi inaifanya serikali hiyo iwe na uhakika wa kuendelea kuwapo miaka yoye ya maisha yetu. Ni lazima tuwe makini sana na swala la Katiba, kwani ndilo linalotofautisha nchi na nchi.

Unachekesha sana kusema waasisi wa KATIBA MPYA NI CHADEMA. Inawezekana wewe chama cha kwanza kukifahamu ni CHADEMA. CUF walishapigia kelele KATIBA MPYA miaka mingi sana. CHRISTOPHA MTIKILA suala la Katiba mpya ni wimbo wake wa siku zote. Kuhusu muundo wa Katiba mpya , wewe unaongelea ushabiki tu. Aidha inawezekana hujua wajibu wa SERIKALI yoyote dunia iliyoko madarakani katika uundwaji wa katiba Mpya, Inamaana hata wakati wakenya wanafanya Sherehe za uundwaji wa Katiba Mpya kuhufuatilia kuona ni jinsi gani Mchakato ulianza hadi kufikia uzinduzi ule, hii ya Tanzania kwa vile CDMA wanapinga kwa makusudi tu muundo wake unaona itakuwa haifai. Hebu jaribu kubukua vitabu zaidi uone Serikali zingine zilivyohusika moja kwa moja juu ya Katiba zao Mpya. Au ninyi watu wa CDM mnafikri rais ni SLAA? Rais wa nchi hii ni Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Atakumbukwa kwa kuruhusu vyombo vya habari kusema walipendalo, aliruhusu uundwaji wa Katiba mpya na mengine mazuri.

HONGERA RAIS DR.JAKAYA MRISHO KIKWETE.
 
Najua Zanzibar imesema Mafuta hayamo kwenye muungano kama tukiendelea kufumbia mambo makubwa kama haya kwa kuyaita kasoro ndogondogo muungano utaendelea kutuumiza milele.

wewe ni kama mbayuwayu. Ulisema muungano ni kilio cha Wazanzibari wakichezea nafasi hiyo hawataipata tena, sasa umegeuka unasema muungano utatuumiza sisi. Kumbe fitina tu. Hizo ndizo kasoro zenyewe sasa zitamalizika vipi kama hazitajadiliwa?
 
Asante Kichuguu, ni kweli katiba inajadiliwa kwa misingi ya kiitikadi kitu ambacho ni hatari sana kwa mstakabali wa taifa, tumejionea wabunge hasa wa bara walivyogawanyika badala ya kutetea maslahi ya taifa wao wanatetea maslahi ya vyama vyao. Nimemsikia jana Seif akiwataka Wazanzibari wawe na msimamo mmoja juu ya mambo wanayotaka katika katiba mpya na waweke kando itikadi zao za kisiasa katika jambo hilo. Wakati wao wakiwekana sawa sisi huku ndio bado kabisa tunavutana tunaoneshana nani zaidi tutakapozinduka tayari katiba itakuwa imeshaandikwa inasikitisha sana.
CHADEMA hao.
 
Unachekesha sana kusema waasisi wa KATIBA MPYA NI CHADEMA. Inawezekana wewe chama cha kwanza kukifahamu ni CHADEMA. CUF walishapigia kelele KATIBA MPYA miaka mingi sana. CHRISTOPHA MTIKILA suala la Katiba mpya ni wimbo wake wa siku zote. Kuhusu muundo wa Katiba mpya , wewe unaongelea ushabiki tu. Aidha inawezekana hujua wajibu wa SERIKALI yoyote dunia iliyoko madarakani katika uundwaji wa katiba Mpya, Inamaana hata wakati wakenya wanafanya Sherehe za uundwaji wa Katiba Mpya kuhufuatilia kuona ni jinsi gani Mchakato ulianza hadi kufikia uzinduzi ule, hii ya Tanzania kwa vile CDMA wanapinga kwa makusudi tu muundo wake unaona itakuwa haifai. Hebu jaribu kubukua vitabu zaidi uone Serikali zingine zilivyohusika moja kwa moja juu ya Katiba zao Mpya. Au ninyi watu wa CDM mnafikri rais ni SLAA? Rais wa nchi hii ni Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Atakumbukwa kwa kuruhusu vyombo vya habari kusema walipendalo, aliruhusu uundwaji wa Katiba mpya na mengine mazuri.

HONGERA RAIS DR.JAKAYA MRISHO KIKWETE.
Nafikiri ungejikita zaidi kwenye hoja kuliko kutuambia rais ni Dr. Kikwete.
 
Unachekesha sana kusema waasisi wa KATIBA MPYA NI CHADEMA. Inawezekana wewe chama cha kwanza kukifahamu ni CHADEMA. CUF walishapigia kelele KATIBA MPYA miaka mingi sana. CHRISTOPHA MTIKILA suala la Katiba mpya ni wimbo wake wa siku zote. Kuhusu muundo wa Katiba mpya , wewe unaongelea ushabiki tu. Aidha inawezekana hujua wajibu wa SERIKALI yoyote dunia iliyoko madarakani katika uundwaji wa katiba Mpya, Inamaana hata wakati wakenya wanafanya Sherehe za uundwaji wa Katiba Mpya kuhufuatilia kuona ni jinsi gani Mchakato ulianza hadi kufikia uzinduzi ule, hii ya Tanzania kwa vile CDMA wanapinga kwa makusudi tu muundo wake unaona itakuwa haifai. Hebu jaribu kubukua vitabu zaidi uone Serikali zingine zilivyohusika moja kwa moja juu ya Katiba zao Mpya. Au ninyi watu wa CDM mnafikri rais ni SLAA? Rais wa nchi hii ni Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Atakumbukwa kwa kuruhusu vyombo vya habari kusema walipendalo, aliruhusu uundwaji wa Katiba mpya na mengine mazuri.

HONGERA RAIS DR.JAKAYA MRISHO KIKWETE.

Una mzio wa kujipendekeza bin kujikomba, kikwete anapoteza heshima ya taasisi ya urais. nadhani tabia za kabila lake zina play big part kwani ameathirika kwazo.
 
:lol: by wizaga mm nafikiri huyu Wang'ayo ufahamu wake ni mdogo, luteni anaongelea njia inayokwenda kutumika kwa kutengeneza katiba inabidi njia ibadilike badala ile waliozoea ama sivyo ni kuihalalisha chama kimoja kiendele kutawala maana yake nini hakimu na mkosaji ni yule yule do you think dissition itakuwa ipi hii ni black justice.katiba isimamiwe na kundi lingine sasa ww Wang'ayo unaongea kama umeshiba makande au unachako kwenye masilahi lakini watanzania tusiangamie kwa umasikini wa akili wakati wenzetu wanatumia mwanya wa ujinga wetu kuiba rasilimali zetu kiraini. wazanzibari ni kweli wanachosubiria ni kujitangazia nchi sasa ww mwenzangu nami tanganyika ipo wapi.jamani tusi mhisishe nyerere yeye ni binadamu na kama alifanya makosa yasahihishwe sio kumuona kama mungu ambaye hawezi kunenwa .ni kosa tutahukumiwa na kazazi kijacho.so revolution is mandatory
 
Unachekesha sana kusema waasisi wa KATIBA MPYA NI CHADEMA. Inawezekana wewe chama cha kwanza kukifahamu ni CHADEMA. CUF walishapigia kelele KATIBA MPYA miaka mingi sana. CHRISTOPHA MTIKILA suala la Katiba mpya ni wimbo wake wa siku zote. Kuhusu muundo wa Katiba mpya , wewe unaongelea ushabiki tu. Aidha inawezekana hujua wajibu wa SERIKALI yoyote dunia iliyoko madarakani katika uundwaji wa katiba Mpya, Inamaana hata wakati wakenya wanafanya Sherehe za uundwaji wa Katiba Mpya kuhufuatilia kuona ni jinsi gani Mchakato ulianza hadi kufikia uzinduzi ule, hii ya Tanzania kwa vile CDMA wanapinga kwa makusudi tu muundo wake unaona itakuwa haifai. Hebu jaribu kubukua vitabu zaidi uone Serikali zingine zilivyohusika moja kwa moja juu ya Katiba zao Mpya. Au ninyi watu wa CDM mnafikri rais ni SLAA? Rais wa nchi hii ni Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Atakumbukwa kwa kuruhusu vyombo vya habari kusema walipendalo, aliruhusu uundwaji wa Katiba mpya na mengine mazuri.

HONGERA RAIS DR.JAKAYA MRISHO KIKWETE.


(1) Ninajua kuwa swala la kudai katiba mpya lilianza siku nyingi sana. Mwaka 1995 kuna vyama vingi havikutaka kufanya uchaguzi ule bila kuwepo kwa Katiba Mpya, ila NCCR-Magezi kupitia umaarufu wa Mrema wakaendelea na kampeini na hivyo kuzima nguvu ile na uchaguzi ukaendelea. Hali imeendelea hivyo hivyo hadi mwaka 2010 ambapo kulionekana dalili kubwa sana kuwa CCM ililindwa iendelee kubaki madarakani kutokana na katiba ya sasa. Pamoja na kususia sherehe za uapishwaji wa rais pamoja na ile maiden speech yake ya bunge, CHADEMA walisema kuwa wanataka katiba mpya itungwe mara moja na wakaahidi kuweka presha kubwa sana ili katiba mpya itungwe kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015 ili CCM isiendelee kulindwa. Kikwete kuridhia swala la katiba ambalo halikuwa kwenye Ilani ya CCM kulitokana na haja yake ya kutaka kuzima presha hiyo kabla haijaanza kwa vile alijua kuwa ikianza, itakuwa ni ngumu sana kwake kudhibiti. Huu ni ukweli ambao ukitka tujadilianie ilikuwaje Kikwete akaja na hija ya katiba mpya mapema sana huku haikuwa kwenye ilani ya CCM, nitakuwa tayari tufanye hivyo.

(2) Rais wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba iliyopo ni Mheshimiwa Kikwete; nadhani ndiyo maana Chadema walikwenda kuonana naye.

(3) Siyo kila mtu anyezungumza kukubaliana na hoja ya CHADEMA au kupinga hoja ya CCM ni CHADEMA tu. Ni vizuri ujifunze kuwa unafikiri kwa kutumia ubongo; utaweza kuwa unaona mambo kwa kina na kuyatafakiwa vizuri kabla ya kushambulia watu usiowajua.
 
Unachekesha sana kusema waasisi wa KATIBA MPYA NI CHADEMA. Inawezekana wewe chama cha kwanza kukifahamu ni CHADEMA. CUF walishapigia kelele KATIBA MPYA miaka mingi sana. CHRISTOPHA MTIKILA suala la Katiba mpya ni wimbo wake wa siku zote. Kuhusu muundo wa Katiba mpya , wewe unaongelea ushabiki tu. Aidha inawezekana hujua wajibu wa SERIKALI yoyote dunia iliyoko madarakani katika uundwaji wa katiba Mpya, Inamaana hata wakati wakenya wanafanya Sherehe za uundwaji wa Katiba Mpya kuhufuatilia kuona ni jinsi gani Mchakato ulianza hadi kufikia uzinduzi ule, hii ya Tanzania kwa vile CDMA wanapinga kwa makusudi tu muundo wake unaona itakuwa haifai. Hebu jaribu kubukua vitabu zaidi uone Serikali zingine zilivyohusika moja kwa moja juu ya Katiba zao Mpya. Au ninyi watu wa CDM mnafikri rais ni SLAA? Rais wa nchi hii ni Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Atakumbukwa kwa kuruhusu vyombo vya habari kusema walipendalo, aliruhusu uundwaji wa Katiba mpya na mengine mazuri.

HONGERA RAIS DR.JAKAYA MRISHO KIKWETE.

nani alitoka tanganyika akashiriki uundwaji wa katiba ya zanzibar?halafu usiseme kitu bila data eti mengi mazuri sema amefanya nini ?kuruhusu kusema chochote sio tija,muhimu ni kutenda mfano kujivua gamba toka april mpaka leo hakuna la maana kusema kimetekelezwa.
kama sio shinikizo la cdm katiba mpya isingekuwepo kumbuka waziri wa katiba na ag walikataa kitu hicho lakini walipo sikia nguvu ya umma jk akafyata kama unafuatilia bunge angalia kila mbunge anawashambulia cdm badala ya kuleta hoja za msingi yaani inauma sana kama wewe kwenye familia yenu mtapitisha sheria ya kununua vitu chakavu 50 yrs shame

 
Yamesemwa mengi sana kuhusu mchakato wa muundo wa katiba mpya..elimu inahitajika kwa watanzania wote ili wapate uelewa wa kutosha na kutambua zipi ni pumba na upi ni mchele...naamini kwa ma great thinkers waliopo humu jamvini kila m1 akimuelewesha mwenzake huko mtaani mambo yatakuwa mazuri sana!!!
 
kwani huu muungano si ndo unaowabeba wazenji wasioisha kulalamika kila kukicha , iweje leo wewe unahofia kuvunjika wakati ndio unafuu wako? acha unafiki uo.
 
kwani huu muungano si ndo unaowabeba wazenji wasioisha kulalamika kila kukicha , iweje leo wewe unahofia kuvunjika wakati ndio unafuu wako? acha unafiki uo.
Nafikiri hujanielewa sitetei wala sioni hasara muungano ukivunjika ila natoa maoni yangu mimi kama mimi kuwa kama (serikali) imetayarisha muundo wa tume na bunge la katiba kwa lengo la kuulinda muungano basi imefanya kosa nina wasiwasi itakuwa kinyume chake na nimefafanua kwenye post yangu ya kwanza.
 
Back
Top Bottom