Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Hivi watu wa vijijini ambako Ccm ina wanachama wengi wanajua kuwa chama chao kina mipasuko na hakina dira ya kumkomboa Mtanzania? Ni jukumu letu sisi kuwahamasisha watu wa vijijini na kuwaonyesha ni kwa jinsi gani ambavyo Ccm si mkombozi wao wa kweli.
Saa ya ukombozi ni sasa.
unamaanisha jack mwambi? ccm ni zaidi ya uijuavyo kwani makamba alikuwa na sifa gani hadi akawekwa pale? hata wakikmuweka riz1 sitashaNGAAUkweli Makamba ameigharimu sana CCM na Uraisi wa Mh. JK. Mwaka jana alichukua hela za wagombea sana na kubadilisha matokeo na alimtumia mtoto wake mmojawapo pale kwenye makazi yake Morogoro.
Pia amechukua sana hela za watu aliowaahidi kuwa watapatiwa vyeo vya UKUU WA WILAYA na wengi wao ni wale waliogombea Ubunge wakakosa mwaka jana. Ukweli Makamba ni mtu wa vibahasha na Usalama wa Taifa walishapeleka taarifa nyingi naona busara za JK alikuwa anaamini atajirekebisha. Assishie hapo ajitahidi kufanya uteuzi wa watu wanaoeleweka sasa na Usalama umsaidie maana wanaweza mpindua kama Zuma alivyofanya Afrika ya Kusini. Awatumie vijana kama zamani, vijana wenye maono si type ya lumbilumbi kama akina Shigela na Malisa. Shigela alikuwa kijana mzuri sana lkn alipokubali kutumikia kundi la mafisadi amebadilika sana na mi kwa ushauri wangu hata yeye pale ang,olewe. Watu wanawataja lukuvi, Nchimbi na Wasira nakwambieni hawa hawafai bado ni watu wa makundi na Nchimbi ana ndoto pia za uraisi na Lukuvi anajiona nafasi ya Ukatibu Mkuu haimfai atafutwe mtu mwelewa msikivu na ambaye anaweza shuka chini kuona matatizo ya wananchi. Kuna balozi mmoja amepata kuwa mkuu wa mkoa jina limenitoka angefaa huyo nikipata jina nitawapatieni. tuwe na siasa za kiushindani na zenye muelekeo wa kuthamni zaidi maslahi ya taifa.