Mambo ambayo tukiyafanya njaa itakuwa historia

Njaa ni swala la kujitakia! Kama serikali inavyoshindwa kutekeleza mipango ya maendeleo na leo hii bado tupo ktk umaskini ndivyo wananchi wanavyoshindwa kutekeleza vipaji vyao na njaa imekuwa matokeo ya mfumo huu wa maisha ya kuiga..Umaskini na njaa ni vitu vya kujitakia!

Tanzania hatukuwahi kufa njaa ktk Ujamaa wa Nyerere pamoja na adha zote za ukosefu wa mali za viwandani kama sukari, sabuni na kadhalika ambavyo takwimu zinaonyesha wazi kuwa viwanda vyetu havikuzalisha kulingana na kiwango chake na hata ile mali chache ilopatikana iliporwa na kuuzwa na walanguzi nchi za jirani. Hata kilimo cha cash crops kilishuka baada ya mashamba kushindwa kusimamiwa vizuri na wataalam wetu. Ujamaa wa Nyerere ulishindwa kwa mchango mkubwa wa UVIVU wa watanzania wenyewe (viongozi na wananchi).

Kwa hiyo, baada ya kuingia Ubepari Watanzania kwa uvivu wetu tumekimbia kabisa kilimo na kusema kweli Kilimo Kwanza kimechukua mkondo wa kilimo cha kukodisha, ardhi ikiuzwa kwa wageni wakati wananchi wakikimbia vijijini kwenda mijini kujishughulisha na biashara za Umachinga (uchuuzi wa finished product). Kifupi watanzania tumeshindwa kujituma wenyewe ktk uzalishaji na leo hii tunazungumzia KILIMO KWANZA kwa uchungu ni kwa sababu tu tunaona ardhi yetu ikipewa wageni lakini sisi wenyewe hatuwezi kurudi ktk kilimo.

Kama navyosema siku zote kabla hujafikiria mkakati wowote ni muhimu sana kutazama WATU na MAZINGIRA. Watanzania ktk mazingira haya ya utandawazi wametupa zana zao, wametupa vipaji vyao na kwa asili ni wavivu wa uzalishaji tumejikita zaidi ktk biashara rahisi za umachinga. NI vigumu sana kuondoa njaa nchini ikiwa sisi wenyewe tunataka tukabidhiwe ardhi ambayo hatuna mawazo ya kulima bali kuihodhi kibiashara na pengine sisi wenyewe ndio tutaiuza kwa wageni badala ya kulima.

Mwisho nasema kwamba viongozi wetu ni reflection yetu, wao hawana akili na wavivu kama sisi kiasi kwamba ktk uvivu wao swala la Uzalishaji ni la wageni na wananchi watajikita ktk biashara rahisi za umachinga. Kwa mtaji huu hatutaweza kuondoka ktk umaskini wala kuondokana na njaa! Isipokuwa siku wananchi wenyewe wakiweza kusoma alama za wakati wakaondoa uvivu wa akili na kimwili warudi vijijini na kuanza KULIMA mashamba kwani hiki ndicho kipaji kikubwa cha Mbatu Mtanzania na pekee ndicho kitamwondoa ktk umaskini..
 
Njaa ni swala la kujitakia! Kama serikali inavyoshindwa kutekeleza mipango ya maendeleo na leo hii bado tupo ktk umaskini ndivyo wananchi wanavyoshindwa kutekeleza vipaji vyao na njaa imekuwa matokeo ya mfumo huu wa maisha ya kuiga..Umaskini na njaa ni vitu vya kujitakia!Tanzania hatukuwahi kufa njaa ktk Ujamaa wa Nyerere pamoja na adha zote za ukosefu wa mali za viwandani kama sukari, sabuni na kadhalika ambavyo takwimu zinaonyesha wazi kuwa viwanda vyetu havikuzalisha kulingana na kiwango chake na hata ile mali chache ilopatikana iliporwa na kuuzwa na walanguzi nchi za jirani. Hata kilimo cha cash crops kilishuka baada ya mashamba kushindwa kusimamiwa vizuri na wataalam wetu. Ujamaa wa Nyerere ulishindwa kwa mchango mkubwa wa UVIVU wa watanzania wenyewe (viongozi na wananchi). Kwa hiyo, baada ya kuingia Ubepari Watanzania kwa uvivu wetu tumekimbia kabisa kilimo na kusema kweli Kilimo Kwanza kimechukua mkondo wa kilimo cha kukodisha, ardhi ikiuzwa kwa wageni wakati wananchi wakikimbia vijijini kwenda mijini kujishughulisha na biashara za Umachinga (uchuuzi wa finished product). Kifupi watanzania tumeshindwa kujituma wenyewe ktk uzalishaji na leo hii tunazungumzia KILIMO KWANZA kwa uchungu ni kwa sababu tu tunaona ardhi yetu ikipewa wageni lakini sisi wenyewe hatuwezi kurudi ktk kilimo.Kama navyosema siku zote kabla hujafikiria mkakati wowote ni muhimu sana kutazama WATU na MAZINGIRA. Watanzania ktk mazingira haya ya utandawazi wametupa zana zao, wametupa vipaji vyao na kwa asili ni wavivu wa uzalishaji tumejikita zaidi ktk biashara rahisi za umachinga. NI vigumu sana kuondoa njaa nchini ikiwa sisi wenyewe tunataka tukabidhiwe ardhi ambayo hatuna mawazo ya kulima bali kuihodhi kibiashara na pengine sisi wenyewe ndio tutaiuza kwa wageni badala ya kulima.Mwisho nasema kwamba viongozi wetu ni reflection yetu, wao hawana akili na wavivu kama sisi kiasi kwamba ktk uvivu wao swala la Uzalishaji ni la wageni na wananchi watajikita ktk biashara rahisi za umachinga. Kwa mtaji huu hatutaweza kuondoka ktk umaskini wala kuondokana na njaa! Isipokuwa siku wananchi wenyewe wakiweza kusoma alama za wakati wakaondoa uvivu wa akili na kimwili warudi vijijini na kuanza KULIMA mashamba kwani hiki ndicho kipaji kikubwa cha Mbatu Mtanzania na pekee ndicho kitamwondoa ktk umaskini..
mkuu una pointi kubwa sana ni kweli kabisa tanzania ni wavivu
 
munachochangia kinaweza kuwa kweli lakini hebu tujiulize kama kweli tunataka kuendeleza kilimo hapo hapo tunabinafisisha mashamba ambayo tulisha yaendeleza kwa hela nyingi tunawapa wawekezaji natoa mifano michache ndipo utajua kama kweli ni kilimo kwanza au ulaji kwanza
1' mashamba ya kapunga more than 360ha. mbalali more than 5000ha. ukija kilosa kunaeneo linamilikiwa na jitu pateli more than 2000ha hiyo mifano kilombero kunaeneo kubwa ambalo ukifika huwezi kuamini kama kweli leo hii tunalia njaa. kila kitu kipo maji yapo, kama rutuba ipo. kilichobakia nia akili tu. nenda Mpanda utaona mazao yanavyo patika tatizo ni mpango isiyo na maendeleo ndio inayosababisha haya yote hasa pale siasa inapoingilia kilimo.
 
HAPA KWENYE RED MKUU
NI NGUMU SANA KUSEMA TUNAFUTA KODI KWA ASSUMPTION KWAMBA HILO LITACHOCHEA UWEKEZAJI KWENYE SEKTA. NASEMA HIVYO KWA KUWA UZOEFU UMEONESHA HATA KAMA UKIONDOA KODI, FURSA KUBWA NI KWA WAFANYABIASHARA WALA SIO WAKULIMA WENYEWE. MWAKA HUU WA FEDHA ULIOMALIZIKA JUNI 30 ZILIONDOLEWA KODI NYINGI. KI UKWELI HII IMESABABISHA UINGIZAJI WA MATRKTA NA POWERTILLER KIBAO. SWALI LA MSINGI HAPA NI JE KWA KIPINDI CHA MIAKA 5 YA AGRIC SECTORDEVELOPMENT PROGRAMME (ASDP) BEI YA ZANA HIZO IMEPUNGUA?JIBU NI HAPANA? JE WANANCHI WAKAWAIDA WAMEHAMASIKA KUNUNUA? HAKUNA JIBU LA UHAKIKA, LAKINI USHAHIDI NI POWER TILLER NA TRAKTA KIBAO ZILIZOPOMAKAU MAKUU YA WILAYA ZIKISUBIRI WAKULIMA KUJA KULIPIA.
PILI KWA KUHAMASISHA USAFIRISHAJI NJE MAZAO YALIYOSINDIKWA, SERIKALI ILIPUNGUZA EXPORT LEVY KWA PROCESSED AGRIC COMMODITIES NA KUONGEZA KWA UNPROCESSED (RAW) PRODUCE HASA MAZAO KAMA KOROSHO. SWALI HAPA NI JE TANGU WAKATI HUO HADI SASA NI VIWANDA VINGAPI VIMEFUFULIWA KATI YA VILE 11 AMBAVYO VILIKUWA-GROUNDED MIAKA YA 1990?
1. Serikali inatakiwa kufuta kodi zote kwenye bidhaa zinazotumika kwenye kilimo.
2. kisha izuie kabisa wageni kujihusisha na kilimo katika namna yoyote
3. Kisha ama ipunguze au ifute kiwango cha kodi (tax rate) kwenye faida inayopatikana
kutokana na biashara yoyote inajihusisha moja kwa moja na sekta ya kilimo.
4. Katika kila manispaa, serikali itenge maeneo ambayo ni kwa ajili ya kilimo tu
kama hakuna shughuli za kilimo zitakazokuwa zikifanyika katika maeneo hayo yaachwe wazi.
5. Elimu ya kilimo iwe ni lazima kama ambavyo lugha na computer ni lazima
6. Elimu ya kilimo iwe reginalized, kwa maana ya maeneo ambayo kuna wafugaji wafundishwe juu
ya ufugaji, wanakolima pamba wafundishwe kwa undani wa kipekee juu ya kilimo cha pamba,
kadharika na katani, na korosho, karafuu nk.

Kwa nini?
Hatua hizi zitasababisha yafuatayo
1. Kwa kufuta kodi kwenye bidhaa za kilimo, itasaidia bidhaa hizi kupatikana
kwa unafuu zaidi.
2. kuzuia wageni ni kwa sababu ni kwa ajili ya kuwawezesha watanzania kufaudu
punguzo la kodi ndani ya ardhi yao n.k
3. kuondoa au kupunguza corporate tax kutahamasisha watu wenye mitaji
kuielekeza kwenye kilimo
4. Utengaji wa maeneo utawahakikishia watanzania upatikanaji wa ardhi bora
kwa shughuli za kilimo
5. Elimu itawapatia watanzania uelewa wa kilimo
6. Mambo mengine Forces of demand and supply will take care of them.

La Mwisho
Serikali isijishirikishe kwenye kilimo hata kidogo, ikae pembeni yenyewe isimame
na kuhakikisha kwamba playing field iko respected na watu wote. Inawezekana
kWA hiyo, mi nadhani bado hatujajua vipaumbele vyetu ni vipi kwenye sekta ya kilimo? Hatujajua fursa zilizopo kwenye soko la ndani na lille na nje! Hatujajua comparative advantage ya sekta ya kilimo kwa Tanzania ukilinganisha na nchi majirani! Tunaweza kufanya mengi sana! Kuna mtu ameandikwa kuhusu 'Awakening the Sleeping Giant' na focus yake ni kwenye smallholder farmers! Wakulima wadogo wanaweza KUTUTOA Tanzania endapo tukizingatia mnyororo wa thamani - value chain development! Lakini sasa, ngazi za vijijini/wilayani ambapo shughuli za kilimo zinafanyika zaidi wamelala watendaji wa serikali. Biuiness as usual. Imagine miradi inatengewe fedha kidogo sana, na wanakuwa na vimiradi lukuki ambavyo tija na ufanisi wake una walakini! Wameangalia serikali/halmashauri kama mtendaji mkuu, lakini wanashindwa kung'amuafursa zilizopo kutoka kwa sekta binafsi kwa ajili ya kusindika na kuongeza thamani mazao ya kilimo! We have a long way to go! Je wanasikia watendaji wetu tunapoongea nao??????
 
Mimi nashangaa sana takwimu za serikali yetu eti Tanzania 70% ni wakulima halafu tuna njaa, wakati Marekani wakulima awazidi 30% njaa hamna!
 
munachochangia kinaweza kuwa kweli lakini hebu tujiulize kama kweli tunataka kuendeleza kilimo hapo hapo tunabinafisisha mashamba ambayo tulisha yaendeleza kwa hela nyingi tunawapa wawekezaji natoa mifano michache ndipo utajua kama kweli ni kilimo kwanza au ulaji kwanza
1' mashamba ya kapunga more than 360ha. mbalali more than 5000ha. ukija kilosa kunaeneo linamilikiwa na jitu pateli more than 2000ha hiyo mifano kilombero kunaeneo kubwa ambalo ukifika huwezi kuamini kama kweli leo hii tunalia njaa. kila kitu kipo maji yapo, kama rutuba ipo. kilichobakia nia akili tu. nenda Mpanda utaona mazao yanavyo patika tatizo ni mpango isiyo na maendeleo ndio inayosababisha haya yote hasa pale siasa inapoingilia kilimo.
Mkuu mashamba hayo yanabinafsishwa kwa sababu sisi wenyewe hatuwezi kuyalima. Mashamba hayo yamekuwa vichaka kwa zaidi ya miaka 30 hayalimwi tena yalibadilishw akuwa machungo ya mifugo yaani sisi na Wazimbabwe hatuna tofauti kabisa.

Sasa tumebinafsisha kwa wageni ambao wanaweza kulima lakini kwa faida yao, tunalalamika lakini hata tukirudishiwa sisi tutashindwa kulima vile vile kwa sababu kizazi hiki cha Watanzania ni wavivu sana wa kufikiri (ubunifu) na wavivu wa kimwili (hatupendi usumbufu). Kwa hiyo, tukipewa sisi ardhi hizo la kwanza tutakalo lifanya ni kukodisha au kuuza ardhi hizo kwa wageni kama inavyofanya serikali ndio maana nikasema hao viongozi ni reflection yetu. wao pia wanafikiria kama sisi hawana tofauti isipokuwa wamekabidhiwa tu madaraka.

La muhimu tutambue kwamba sisi Watanzania ni wavivu wa ukufikiri (ubunifu) na wavivu wa kimwili hatupendi kazi ngumu kwa kuzalisha kusubiri mavuno ila zile za kuzungusha na mapato ya haraka. Lakini maajabu ni kwamba chini ya bakora na sheria kali tunaweza kufanya kazi vizuri na kwa ufasaha zaidi maanake nawaona huku majuu. Hivyo, what we need is a DICTATOR chini ya utawala wa sheria!
 
Mkuu, wazo lako mimi nimelipenda sana ila nina maswali mawili matatu hivi:
Hizo hekta 50000 zinapatikana wapi kaka?
Kilimo hiki cha umwagiliaji sawa, lakini kama hizo hekta hazipo karibu na hayo mabonde inakuwaje?
Na kama hatutategemea mvua, nini mbadala ikiwa mashamba yatakuwa mbali na mabonde hayo ulotaja?

mkuu ...... tutachimba visima na kujenga mabwawa .... lakini je umeme wa kuvuta maji kwenye visima upo wapi ?

teeh teeh teeeh .... tatizo linarudi pale pale

megawatts....?
 
Ndugu yangu, elewa kwamba hao watu 100 unaopendekeza wapewe hekali 50,000 kila moja wao na mkopo wa Tshs 15Bn watakuwa ni walewale mafisadi wachache na huo mkopo watakaopewa hautakwenda kwenye Kilimo. Tanzania ina wenyewe, na hawazidi 2% na ndiyo wanaokula keki ya Taifa.

wazo lako litawezekana mara tukiwaondoa mafisadi na uchumi wa nchi ushikwe na wananchi kwa faida ya nchi na wananchi.
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Tatizo jingine kubwa ni ugumu wa kupata mikopo. Wanokopeshwa ni matajiri tayari, watu wa chini ni ndoto kupata mkopo, hivyo kilimo kwanza watafaidi matajiri zaidi
 
Ndugu yangu, elewa kwamba hao watu 100 unaopendekeza wapewe hekali 50,000 kila moja wao na mkopo wa Tshs 15Bn watakuwa ni walewale mafisadi wachache na huo mkopo watakaopewa hautakwenda kwenye Kilimo. Tanzania ina wenyewe, na hawazidi 2% na ndiyo wanaokula keki ya Taifa.wazo lako litawezekana mara tukiwaondoa mafisadi na uchumi wa nchi ushikwe na wananchi kwa faida ya nchi na wananchi.
mkuu hiyo nayo pointi
 
Tatizo jingine kubwa ni ugumu wa kupata mikopo. Wanokopeshwa ni matajiri tayari, watu wa chini ni ndoto kupata mkopo, hivyo kilimo kwanza watafaidi matajiri zaidi
yaani hii tz mmh kazi kubwa sana kuikomboa
 
tatizo siyo mipango, hata iliyopo ikitekelezwa kwa ufanisi inaweza kuleta tija, lakini viongozi wanatekeleza mipango kwa lengo hii kwa lengo la kujinufaisha, mwisho wa yote ni kutokuleta mabadiliko kwenye jamii kubwa
 
Wakuu niwakumbushe tu kwamba hapa Tanganyika (Achana na huko visiwani, si kwetu) tunalo eneo zuri liifaalo kwa kilimo lipatalo hekta 44 Milioni (Hekta moja ni sawa na ekari 2.5) hivyo tunalo eneo la kutosha kabisa kufutilia mbalia mbali umaskini kupitia uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. Soko la chakula ni kubwa mno popote duniani, kama tumeshindwa kupeleka nje madini na vitu vingine sasa tunaweza kupeleka mazao ya chakula hata kama ni Marekani na Ulaya, nao wanahitaji kula! Tatizo ni mipango tu, kila kitu kipo. Mashangingi (magari ya kifahari ya serikali) 10 tu yanaweza kununua zana za kilimo za kutosha kabisa.

Mtoa mada ameanzisha, wazo lake ni zuri wana JF endeleeni kuli-polish ili kuboresha wazo lake na kwa upande wa serikali waziri mwenye dhamana ya kilimo si vibaya kudesa wazo hili na kuwasilisha kwenye baraza la mawaziri kwa hatua zaidi.
 
Back
Top Bottom