eRRy
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 1,125
- 204
[h=1]MAMA SALMA KIKWETE ALAANI MAUAJI YA RAIA WA CHINA[/h]
WEDNESDAY, 01 SEPTEMBER 2010 14:55 ADMINISTRATOR
Mke wa rais mama Salma Kikwete, amelaani vikali mauaji ya mfanyabiashara wa kigeni raia kutoka China bi Hang Bing aliyeuawa hivi karibuni jijini Dar es Salaam baada ya kushambuliwa na watu wanaosadikiwa kuwa wajambazi.
Mfanyabiashara huyo aliuawa kwa kupigwa risasi Oktoba 11 eneo la Kurasini ambapo majambazi hao inasadikiwa walitoweka na kiasi kikubwa cha fedha.
Akizungumza waakti wa kuaga mwili wa marehemu Hang Bing Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe, Mama Salma Kikwete wameelezea kusikitishwa na tukio hilo ambapo wamemtaja mwanamke huyo kuwa alikuwa mwanaharakati wa maendeleo ya wanawake wa Tanzania kutokana na mchango wake wa hali na mali kwa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) pamoja na jeshi la polisi.
Nae balozi wa China nchini Tanzania Liu Xinsheng pamoja na jumuiya ya wachina wanaoishi nchini ,wameomba waliohusika na mauaji hayo wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Wakati huo huo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova,amesema jeshi la polisi litafanya kila liwezezalo kuhakikisha waliofanya mauaji hayo wakamatwa. Aidha ametangaza zawadi ya shilingi milioni 5 kwa yeyote atakeyetoa taarifa za kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa.
-----------------------------------
WEDNESDAY, 01 SEPTEMBER 2010 14:55 ADMINISTRATOR
Mke wa rais mama Salma Kikwete, amelaani vikali mauaji ya mfanyabiashara wa kigeni raia kutoka China bi Hang Bing aliyeuawa hivi karibuni jijini Dar es Salaam baada ya kushambuliwa na watu wanaosadikiwa kuwa wajambazi.
Mfanyabiashara huyo aliuawa kwa kupigwa risasi Oktoba 11 eneo la Kurasini ambapo majambazi hao inasadikiwa walitoweka na kiasi kikubwa cha fedha.
Akizungumza waakti wa kuaga mwili wa marehemu Hang Bing Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe, Mama Salma Kikwete wameelezea kusikitishwa na tukio hilo ambapo wamemtaja mwanamke huyo kuwa alikuwa mwanaharakati wa maendeleo ya wanawake wa Tanzania kutokana na mchango wake wa hali na mali kwa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) pamoja na jeshi la polisi.
Nae balozi wa China nchini Tanzania Liu Xinsheng pamoja na jumuiya ya wachina wanaoishi nchini ,wameomba waliohusika na mauaji hayo wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Wakati huo huo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova,amesema jeshi la polisi litafanya kila liwezezalo kuhakikisha waliofanya mauaji hayo wakamatwa. Aidha ametangaza zawadi ya shilingi milioni 5 kwa yeyote atakeyetoa taarifa za kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa.
-----------------------------------