Vito Ferari
JF-Expert Member
- Mar 31, 2022
- 290
- 412
Sehemu ya 1:
Nyasule Suleiman, mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya wasichana ya Jangwani, alimuaga mama yake aliekuwa kwenye genge lake la kuuza nyanya asubuhi hii ya jumatatu,kuwa anaelekea shule. " Mama, mimi naenda shule, tutaonana baadae", Nyasule alimuambia mama yake ,"Sawa mwanangu, nakutakia masomo mema".
Mama Nyasule alimjibu.
Mama Nyasule akamuangalia biniti yake akielekea shule, kisha kumbkumbu ya miaka kumi na sita iliyopita ikamjia kwenye akili yake.
Mama Nyasule jina lake kamili ni Zainabu Suleiman ,mzaliwa wa Ujiji , Kigoma, kwenye kijiji cha Usawile,baba yake mzazi alikuwa mvuvi, mama yake mkulima, Zainabu alikuwa anaishi na wazazi wake hapo kijijini, baba yake mara nyingi anasafiri kwenda ziwani kuvua samaki, anaweza kukaa huko ziwani zaidi ya wiki moja , Zainabu anabaki nyumbani na mama yake.
Zainabu alipofika darasa la saba, akiwa na umri wa miaka kumi na sita akaanza kujihusisha na wanaume, alipata kijana jirani yake , aliekuwa mvuvi akamrubuni, na hatimae kuanzisha uhusiano wa kimapenzi, waliendelea na yule kijana kwa muda wa miezi sita, siku moja,wiki kadhaa kabla ya kufanya mtihani wa darasa la saba, walikuja madaktari shuleni kwao, walipima wanafunzi wa kike ujauzito, Zainabu alipopimwa akakutwa na mimba.
Kesho yake asubuhi, akiwa darasani, aliitwa na mwalimu mkuu." Zainabu, mwalimu mkuu anakuita ofisini kwake", rafiki yake Anna wanaesoma wote darasa moja alimuambia. Zainabu akafunga kitabu chake alichokuwa anasoma, na kuelekea kwenye ofisi ya mwalimu mkuu. "Ingia ukae", mwalimu mkuu akamuambia. Mwalimu Mkuu akamuangalia Zainabu kisha akamuuliza, 'Una miaka mingapi"?.
" Kumi na sita", Zainabu akajibu. ""umeanza kujihusisha na mapenzi",? Mwalim mkuu akamuuliza , " Hapana", Zainabu akajibu, akamkumbuka mpenzi wake mvuvi John.
"Hapana?, sasa hiyo mimba umeipata wapi"? Zainabu aliposikia alipata mshtuko, kidogo azimie. "Sina mimba mwalimu". "Huna mimba, wakati jana umepimwa umekutwa na mimba"?. Zainabu akaanza kulia"Mimi sina mimba mwalimu". "Kwa hiyo nakusingizia sio, unadhani mimi ni mtoto mwenzio "? Mwalimu mkuu alimuambia, "Ondoka,rudi nyumbani,nenda kalete wazazi wako hapa sasa hivi, haya, tokaa, malaya we"!
Zainabu akaondoka ofisini huku analia, akarudi darasani, na kubeba begi lake,akaondoka, wanafunzi wenzake wakamuangalia kwa mshangao,huo ndio ukawa mwisho wa Zainabu kusoma.
Zainabu hakurudi nyumbani, akaenda moja kwa moja kwenye chumba cha John, mpenzi wake alikuwa nje ya chumba chake anaandaa samaki wake aliowavua kwa ajili ya kwenda kuwauza sokoni Ujiji.Akamuona Zainabu, yuko na nguo za shule anakuja .
John akashangaa, sio kawaida ya Zainabu kuja kwake na nguo za shule, " Vipi Zainabu kulikoni asubuhi hii na nguo za shule?, umetoroka shule"?, Zainabu hakujibu, moja kwa moja akapitiliza chumbani kwa John huku akilia, John akamfuata ndani, " Zainabu una nini, umefiwa"?. Zainabu hakujibu ,akaendelea kulia."
Kuna nini'? , John akamuuliza.
" Nina mimba mpenzi, nina mimba yako".
" Unasemaje"?, John akamuuliza huku akionekana amechanganyikiwa . "Nimesema nina mimba yako". Zainabu akamuambia kwa msisitizo.. " Hapana Zainabu, utakuwa umekosea,hiyo mimba sio yangu, tena unikome sikujui", unajua adhabu ya kumpa mimba mwanafunzi"? unataka nifungwe kifungo cha maisha jela"?, we mtoto tokaa,sikujui mimi na usinijue"!. Zainabu akaduwaa,ingawa alitegemea hili, " Leo unanikana mpenzi"? Zainabu akamuuliza.
"Nimesema tokaa,sikujui tokaa,unikome,"! John akaongea kwa ukali,huku hasira zikimpanda. Zainabu akamuangalia John usoni, akajua John anamaanisha anachokisema. " Niende wapi sasa"?,
"Unaniuliza mimi kweni huna kwenu"? nenda popote mimi hainihusu". Zainabu kwa hasira akasimama na kuondoka.
Baada ya Zainabu kuondoka, John akajitupa juu ya kitanda akifikiria kitu cha kufanya, alikuwa anasikia tu habari za jela, lakini sasa jela inamuita, Akamfikiria baba yake Zainabu alivyo mkorofi, na ni balozi wa nyumba kumi, "Baba Zainabu hawezi kuniacha, atahakikisha nafungwa,tena kifungo cha maisha", John akafikiria. Nifanye nini sasa? Akajiuliza.
Akamkumbuka rafiki yake Mrundi, aitwae Hizzmana, ambae kila siku anamsihi aende Burundi kumtembelea, " Labda huu ndio wakati muafaka wa kumtembelea, na sio kumtembelea kwa muda,ni kumtembelea moja kwa moja, Akaweka nguo zake zote kwenye begi, akampigia simu rafiki yake wanaevua wote samaki. " Hallo, Kabwe, naomba uje uchukue vitu vyangu hapa kwangu ukae navyo, nimepata safari ya ghafla ,sitakuwepo kwa miezi mingi, narudisha chumba" funguo utaikuta kwa mwenye nyumba", John akasema, alivyokubaliana na rafiki yake akakata simu, Akaelekea kwa mwenye nyumba na kumuambia anachia chumba, amepata kazi Mwanza, kodi iliyobaki haiitaji, atafute mpangaji mwingine, kodi ilibaki miezi minne, mwenye nyumba akafurahi,akajua atapata kodi nyingine kabla ya muda kuisha, wakaagana, John akabeba begi lake na kuelekea Burundi kwa rafiki yake, hana haja ya pasipoti, maana njia zote za panya anazijua. Na huo ndio ukawa mwisho wake kuonekana Kigoma.
Zainabu alivyotoka kwa John akatembea kwa nusu saa hajui aende wapi. Akafikiria, niende nyumbani? Hapana, baba ataniua, niende wapi sasa? Akamkumbuka shangazi yake alieko Kigoma Mjini, shangazi yake anampenda sana Zainabu,ingawa haelewani na mama yake. Nitapata wapi nauli? . Zainabu akajiuliza.
Akakumbuka mama yake anafichaga pesa zake za akiba kwenye chaga za kitanda, na akajua muda huo mama yake atakuwa shambani, baba hayuko yuko ziwani anavua samaki. Zainabu haraka akaelekea nyumbani, akakuta mlango umefungwa. Anajua funguo mama yake anaweka juu kwenye upenyo wa mlango wa jikoni.
Zainabu akaelekea jikoni, akapanda juu ya mlango,akaingiza mkono kwenye upenyo na kutoa ufunguo, Akafungua mlango na kuingia ndani. Alivyofika ndani akavua nguo za shule na kuvaa nguo za nyumbani. Akachukua begi lake akaweka nguo zake zote pamoja na viatu,na kila kitu alichokuwa nacho ,akaweka kwenye begi akaridhika hamna kitu alichosahau, akaelekea chumbani kwa mama yake, akasogeza godoro na kuangalia kwenye chaga, akaona pesa za mama yake, zilikuwa zimejaa vumbi, Zainabu akazihesabu, kulikuwa ana elfu hamsini na tano.
Akachomoa elfu arobaini akaweka mfukoni, akaacha zilizobaki, akarudishia godoro na shuka na kuelekea chumbani kwake, akabeba begi lake na kuanza kuondoka,akasita ,akamkumbuka mama yake. Akajua mama yake atamtafuta sana asipomuona, akachukua kalamu na karatasi, kisha akaandika:
Wazazi wangu wapenzi.
Mimi mtoto wenu wa pekee Zainabu, nimeamua kuondoka nyumbani,pamoja na kuacha shule,huu ni uamuzi wangu binafsi,nimefanya kosa ambalo siwezi kuwaeleza,ni kosa litakalonipa aibu mimi,pamoja na nyie hapa kijijini, siwezi kuivumilia hiyo aibu, naomba msinitafute.
Nawatakia maisha mema.
Mimi mtoto wenu
Zainabu.
Alivyomaliza akaiweka barua juu ya meza, akabeba begi lake na kuondoka, alivyofika sebuleni akaangalia juu ya ukuta, Akaiona picha ya wazazi wake iko kwenye fremu kubwa imetungikwa ukutani, akaiangalia kwa muda. Na hiyo ndio ikawa mara ya mwisho kuwaona wazazi wake.
Zainabu akaelekea stand ya Ujiji, alipofika stand, akapanda basi la kuelekea Kigoma Mjini, alipofika Kigoma Mjini akaelekea nyumbani kwa shangazi yake.Shangazi yake alikuwa ndani anajiandaa kutoka,maana anafanya biashara ya mama ntilie. " Hodi", Karibu. Shangazi yake akajibu, kisha akafungua mlango, " Zainabu? Vipi ingia ndani,karibu sana mwanangu". " Asante," Zaunabu akaingia ndani, Shangazi akampokea begi na kuliweka kwenye kabati, Shangazi yake ameachika anaishi mwenyewe, " Vipi Zainabu,kulikoni, mmefunga shule"? Shangazi akamuuliza.Akamuangalia Zainabu usoni, akagundua alikuwa analia."Hapana shangazi hatujafunga shule,bali nina matatizo". Zainabu akamjibu, kisha akamueleza ukweli.Shangazi yake baada ya kusikia alichoelezwa na Zainabu, akavuta pumzi ndefu, kisha akatafakari kwa muda, kama wazazi wa Zainabu wakigundua mtoto wao anaishi nae,watamletea matatizo, wanaweza kumshtaki kwa kumtorosha mtoto wao. "Sasa wazazi wako wakigundua uko kwangu ,si wataniletea matatizo, si unajua mimi na mama yako hatuelewani"?. Shangazi akamuuliza." Niwewaachia barua", Zainabu akajibu, alikuwa amesahau kumwambia Shangazi yake kuhusu barua."Umewaandikia barua"?. "Ndio shangazi,nimewaeleza mimi naondoka ,na ni uamuzi wangu binafsi". Zainabu akamueleza. Na hivyo ndivyo mambo yalivyokuwa.
•••••••••••••••••••••
Baada ya miaka mitatu, bado Zainabu alikuwa Kigoma Mjini, lakini muda huo shangazi yake alikuwa hakai nae, shangazi yake alipata mchumba, akahama na kwenda kuishi nae, Zainabu akabaki na mtoto wake mwenyewe, lakini alikuwa anafanya kazi kwenye mgahawa wa kuuza chakula wa shangazi yake. Mtoto wa Zainabu, Nyasule alishatimiza umri wa miaka mitatu na alishaanza kuchangamka. Zainabu siku moja usiku, alifikiria sana, aliwaza kuhusu maisha yake na ya binti wake Nyasule ya baadae. Hakuona dalili yoyote ya maisha yake kuwa bora, alitamani siku moja na yeye awe na nyumba yake, nguo nzuri, na kuishi maisha bora kwa ujumla, lakini kwa kazi ya umama ntilie anayofanya ,isingempa kitu anachotaka, alikuwa anasikia habari za Dar es Salaam kuwa ni jiji kubwa, litakaloweza kumpa maisha anayohitaji.
itaendelea.......................................
Nyasule Suleiman, mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya wasichana ya Jangwani, alimuaga mama yake aliekuwa kwenye genge lake la kuuza nyanya asubuhi hii ya jumatatu,kuwa anaelekea shule. " Mama, mimi naenda shule, tutaonana baadae", Nyasule alimuambia mama yake ,"Sawa mwanangu, nakutakia masomo mema".
Mama Nyasule alimjibu.
Mama Nyasule akamuangalia biniti yake akielekea shule, kisha kumbkumbu ya miaka kumi na sita iliyopita ikamjia kwenye akili yake.
Mama Nyasule jina lake kamili ni Zainabu Suleiman ,mzaliwa wa Ujiji , Kigoma, kwenye kijiji cha Usawile,baba yake mzazi alikuwa mvuvi, mama yake mkulima, Zainabu alikuwa anaishi na wazazi wake hapo kijijini, baba yake mara nyingi anasafiri kwenda ziwani kuvua samaki, anaweza kukaa huko ziwani zaidi ya wiki moja , Zainabu anabaki nyumbani na mama yake.
Zainabu alipofika darasa la saba, akiwa na umri wa miaka kumi na sita akaanza kujihusisha na wanaume, alipata kijana jirani yake , aliekuwa mvuvi akamrubuni, na hatimae kuanzisha uhusiano wa kimapenzi, waliendelea na yule kijana kwa muda wa miezi sita, siku moja,wiki kadhaa kabla ya kufanya mtihani wa darasa la saba, walikuja madaktari shuleni kwao, walipima wanafunzi wa kike ujauzito, Zainabu alipopimwa akakutwa na mimba.
Kesho yake asubuhi, akiwa darasani, aliitwa na mwalimu mkuu." Zainabu, mwalimu mkuu anakuita ofisini kwake", rafiki yake Anna wanaesoma wote darasa moja alimuambia. Zainabu akafunga kitabu chake alichokuwa anasoma, na kuelekea kwenye ofisi ya mwalimu mkuu. "Ingia ukae", mwalimu mkuu akamuambia. Mwalimu Mkuu akamuangalia Zainabu kisha akamuuliza, 'Una miaka mingapi"?.
" Kumi na sita", Zainabu akajibu. ""umeanza kujihusisha na mapenzi",? Mwalim mkuu akamuuliza , " Hapana", Zainabu akajibu, akamkumbuka mpenzi wake mvuvi John.
"Hapana?, sasa hiyo mimba umeipata wapi"? Zainabu aliposikia alipata mshtuko, kidogo azimie. "Sina mimba mwalimu". "Huna mimba, wakati jana umepimwa umekutwa na mimba"?. Zainabu akaanza kulia"Mimi sina mimba mwalimu". "Kwa hiyo nakusingizia sio, unadhani mimi ni mtoto mwenzio "? Mwalimu mkuu alimuambia, "Ondoka,rudi nyumbani,nenda kalete wazazi wako hapa sasa hivi, haya, tokaa, malaya we"!
Zainabu akaondoka ofisini huku analia, akarudi darasani, na kubeba begi lake,akaondoka, wanafunzi wenzake wakamuangalia kwa mshangao,huo ndio ukawa mwisho wa Zainabu kusoma.
Zainabu hakurudi nyumbani, akaenda moja kwa moja kwenye chumba cha John, mpenzi wake alikuwa nje ya chumba chake anaandaa samaki wake aliowavua kwa ajili ya kwenda kuwauza sokoni Ujiji.Akamuona Zainabu, yuko na nguo za shule anakuja .
John akashangaa, sio kawaida ya Zainabu kuja kwake na nguo za shule, " Vipi Zainabu kulikoni asubuhi hii na nguo za shule?, umetoroka shule"?, Zainabu hakujibu, moja kwa moja akapitiliza chumbani kwa John huku akilia, John akamfuata ndani, " Zainabu una nini, umefiwa"?. Zainabu hakujibu ,akaendelea kulia."
Kuna nini'? , John akamuuliza.
" Nina mimba mpenzi, nina mimba yako".
" Unasemaje"?, John akamuuliza huku akionekana amechanganyikiwa . "Nimesema nina mimba yako". Zainabu akamuambia kwa msisitizo.. " Hapana Zainabu, utakuwa umekosea,hiyo mimba sio yangu, tena unikome sikujui", unajua adhabu ya kumpa mimba mwanafunzi"? unataka nifungwe kifungo cha maisha jela"?, we mtoto tokaa,sikujui mimi na usinijue"!. Zainabu akaduwaa,ingawa alitegemea hili, " Leo unanikana mpenzi"? Zainabu akamuuliza.
"Nimesema tokaa,sikujui tokaa,unikome,"! John akaongea kwa ukali,huku hasira zikimpanda. Zainabu akamuangalia John usoni, akajua John anamaanisha anachokisema. " Niende wapi sasa"?,
"Unaniuliza mimi kweni huna kwenu"? nenda popote mimi hainihusu". Zainabu kwa hasira akasimama na kuondoka.
Baada ya Zainabu kuondoka, John akajitupa juu ya kitanda akifikiria kitu cha kufanya, alikuwa anasikia tu habari za jela, lakini sasa jela inamuita, Akamfikiria baba yake Zainabu alivyo mkorofi, na ni balozi wa nyumba kumi, "Baba Zainabu hawezi kuniacha, atahakikisha nafungwa,tena kifungo cha maisha", John akafikiria. Nifanye nini sasa? Akajiuliza.
Akamkumbuka rafiki yake Mrundi, aitwae Hizzmana, ambae kila siku anamsihi aende Burundi kumtembelea, " Labda huu ndio wakati muafaka wa kumtembelea, na sio kumtembelea kwa muda,ni kumtembelea moja kwa moja, Akaweka nguo zake zote kwenye begi, akampigia simu rafiki yake wanaevua wote samaki. " Hallo, Kabwe, naomba uje uchukue vitu vyangu hapa kwangu ukae navyo, nimepata safari ya ghafla ,sitakuwepo kwa miezi mingi, narudisha chumba" funguo utaikuta kwa mwenye nyumba", John akasema, alivyokubaliana na rafiki yake akakata simu, Akaelekea kwa mwenye nyumba na kumuambia anachia chumba, amepata kazi Mwanza, kodi iliyobaki haiitaji, atafute mpangaji mwingine, kodi ilibaki miezi minne, mwenye nyumba akafurahi,akajua atapata kodi nyingine kabla ya muda kuisha, wakaagana, John akabeba begi lake na kuelekea Burundi kwa rafiki yake, hana haja ya pasipoti, maana njia zote za panya anazijua. Na huo ndio ukawa mwisho wake kuonekana Kigoma.
Zainabu alivyotoka kwa John akatembea kwa nusu saa hajui aende wapi. Akafikiria, niende nyumbani? Hapana, baba ataniua, niende wapi sasa? Akamkumbuka shangazi yake alieko Kigoma Mjini, shangazi yake anampenda sana Zainabu,ingawa haelewani na mama yake. Nitapata wapi nauli? . Zainabu akajiuliza.
Akakumbuka mama yake anafichaga pesa zake za akiba kwenye chaga za kitanda, na akajua muda huo mama yake atakuwa shambani, baba hayuko yuko ziwani anavua samaki. Zainabu haraka akaelekea nyumbani, akakuta mlango umefungwa. Anajua funguo mama yake anaweka juu kwenye upenyo wa mlango wa jikoni.
Zainabu akaelekea jikoni, akapanda juu ya mlango,akaingiza mkono kwenye upenyo na kutoa ufunguo, Akafungua mlango na kuingia ndani. Alivyofika ndani akavua nguo za shule na kuvaa nguo za nyumbani. Akachukua begi lake akaweka nguo zake zote pamoja na viatu,na kila kitu alichokuwa nacho ,akaweka kwenye begi akaridhika hamna kitu alichosahau, akaelekea chumbani kwa mama yake, akasogeza godoro na kuangalia kwenye chaga, akaona pesa za mama yake, zilikuwa zimejaa vumbi, Zainabu akazihesabu, kulikuwa ana elfu hamsini na tano.
Akachomoa elfu arobaini akaweka mfukoni, akaacha zilizobaki, akarudishia godoro na shuka na kuelekea chumbani kwake, akabeba begi lake na kuanza kuondoka,akasita ,akamkumbuka mama yake. Akajua mama yake atamtafuta sana asipomuona, akachukua kalamu na karatasi, kisha akaandika:
Wazazi wangu wapenzi.
Mimi mtoto wenu wa pekee Zainabu, nimeamua kuondoka nyumbani,pamoja na kuacha shule,huu ni uamuzi wangu binafsi,nimefanya kosa ambalo siwezi kuwaeleza,ni kosa litakalonipa aibu mimi,pamoja na nyie hapa kijijini, siwezi kuivumilia hiyo aibu, naomba msinitafute.
Nawatakia maisha mema.
Mimi mtoto wenu
Zainabu.
Alivyomaliza akaiweka barua juu ya meza, akabeba begi lake na kuondoka, alivyofika sebuleni akaangalia juu ya ukuta, Akaiona picha ya wazazi wake iko kwenye fremu kubwa imetungikwa ukutani, akaiangalia kwa muda. Na hiyo ndio ikawa mara ya mwisho kuwaona wazazi wake.
Zainabu akaelekea stand ya Ujiji, alipofika stand, akapanda basi la kuelekea Kigoma Mjini, alipofika Kigoma Mjini akaelekea nyumbani kwa shangazi yake.Shangazi yake alikuwa ndani anajiandaa kutoka,maana anafanya biashara ya mama ntilie. " Hodi", Karibu. Shangazi yake akajibu, kisha akafungua mlango, " Zainabu? Vipi ingia ndani,karibu sana mwanangu". " Asante," Zaunabu akaingia ndani, Shangazi akampokea begi na kuliweka kwenye kabati, Shangazi yake ameachika anaishi mwenyewe, " Vipi Zainabu,kulikoni, mmefunga shule"? Shangazi akamuuliza.Akamuangalia Zainabu usoni, akagundua alikuwa analia."Hapana shangazi hatujafunga shule,bali nina matatizo". Zainabu akamjibu, kisha akamueleza ukweli.Shangazi yake baada ya kusikia alichoelezwa na Zainabu, akavuta pumzi ndefu, kisha akatafakari kwa muda, kama wazazi wa Zainabu wakigundua mtoto wao anaishi nae,watamletea matatizo, wanaweza kumshtaki kwa kumtorosha mtoto wao. "Sasa wazazi wako wakigundua uko kwangu ,si wataniletea matatizo, si unajua mimi na mama yako hatuelewani"?. Shangazi akamuuliza." Niwewaachia barua", Zainabu akajibu, alikuwa amesahau kumwambia Shangazi yake kuhusu barua."Umewaandikia barua"?. "Ndio shangazi,nimewaeleza mimi naondoka ,na ni uamuzi wangu binafsi". Zainabu akamueleza. Na hivyo ndivyo mambo yalivyokuwa.
•••••••••••••••••••••
Baada ya miaka mitatu, bado Zainabu alikuwa Kigoma Mjini, lakini muda huo shangazi yake alikuwa hakai nae, shangazi yake alipata mchumba, akahama na kwenda kuishi nae, Zainabu akabaki na mtoto wake mwenyewe, lakini alikuwa anafanya kazi kwenye mgahawa wa kuuza chakula wa shangazi yake. Mtoto wa Zainabu, Nyasule alishatimiza umri wa miaka mitatu na alishaanza kuchangamka. Zainabu siku moja usiku, alifikiria sana, aliwaza kuhusu maisha yake na ya binti wake Nyasule ya baadae. Hakuona dalili yoyote ya maisha yake kuwa bora, alitamani siku moja na yeye awe na nyumba yake, nguo nzuri, na kuishi maisha bora kwa ujumla, lakini kwa kazi ya umama ntilie anayofanya ,isingempa kitu anachotaka, alikuwa anasikia habari za Dar es Salaam kuwa ni jiji kubwa, litakaloweza kumpa maisha anayohitaji.
itaendelea.......................................