Je, Malkia anamiliki eneo ndani ya nchi yetu?

hiyo sehemu iko Njombe tena pembeni ya barabara ya Njombe Songea. Katika ziara ya mwisho rasmi ya Prince Charles Tanzania alilala hiyo sehemu
 
Ndugu wana JF

Kuna taarifa ambazo sijazithibitisha kwamba, Malkia wa Uingereza anamiliki Eneo Kubwa sana Ndani ya Nchi yetu, ambapo Hata Serikali yetu haina Mamlaka ya Kuingia.

Eneo linasemekana liko Mkoa wa Iringa

Naomba mwenye taarifa kamili anijuze
Egongos, japo sijui kuhusu Iringa, ila kwa taarifa too, mali zote za serikali ya Uingereza duniani kote, kisheria zinamilikiwa na Malkia, na zimeorodheshwa kama HM properties, hivyo nyumba zote za wanabalozi wa Uingereza ni mali ya Malkia.

Kwa Tanzania, wanamiliki nyumba nyingi, prime properties maeneo ya O-bay na Sea View ambayo walijimilikisha tangu wakati wa kutupa uhuru. Pia walimiliki baadhi ya majengo ya kihistoria ya Zanzibar likiwemo jumba maarufu la Hammerton House next to nyumba ya Salmin.

Ardhi zote hizi, zina kinga ya kibalozi (diplomatic immunity), hivyo mtu akikimbilia humu na kufanikiwa kuingia ndani ya uzio, polisi wetu hawa ruhusa ya kukukamata, maana hata kutia mguu ni kosa kisheria.

Pia Malkia anamiliki baadhi ya maeneo ya public, yakiwemo makaburi ya vita kuu ya kwanza na ya pili ya dunia ambayo yametapakaa mahali kwingi hapa nchini ikiwemo Iringa. Kwa Dar es Salaam, makaburi ya vita kuu ya kwanza yako pale mjini next to Hellenic club opposite Red Cross. Na ya vita kuu ya pili yako Kijitonyama nyuma ya Millenium Park.

Ni serikali ya Uingereza inagharimia kila kitu mpaka utunzaji wa maeneo hayo, hivyo sio vibaya mkitembelea mkajionea jinsi wenzetu wanavyotunza makaburi ya mashujaa wa vita vyao ambao miongoni mwao wapon Watanzania wengi tuu, halafu na tutembelee kule Mutukula mkaone jinsi serikali yetu inavyotunza makaburi ya mashujaa wa vita vya Kagera.
 
hivi hawa watanzania wenye hela wanazipeleka wapi hadi wageni wanakuja jinyakulia mali kirahisi rahisi? uko mbele uvumilivu utatushinda wakati tuliwapa wenyewe. wajukuu zetu watateseka sana kwa sababu ya wajinga wachache wanaofanyaga maamuzi ya kipuuzi yanayoangamiza hasa kizazi kijacho cha watanzania.
 
Ni mashamba ya miwati na chai huko Lupembe na Njombe kama sikosei inaendeshwa chini ya kampuni iitwayo Crown(sorry nimesahau jina)

Ni kweli ni shamba la hiyo miti na watu wa kule walisema ni tangu kipindi cha ukoloni tulikuwa huko juzi juzi tunafanya baseline survey ya mambo ya kilimo,by the way miti hiyo inatumika kutengeneza kiwi za viatu.na lease waliyopewa ni ya miaka mingi tu.
 
Ndo hapo sasa unaishi nchini kwako kumbe mali zote zinatawaliwa na wengine..
Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote. mtu mwingine wa mbali anasema
mmmhhhh haka ka nchi kangu kakichukuliwa na sunami au earthquake nina sehemu
babu kubwa Africa nchi moja inaitwa Tanzania.. dahhhhh baadaye
 
Nchi siyo yetu,viongozi watajibu kwa kuuza nchi,masikini kilimo kwanza inamaana hizi project zao ni uhuni tu,kama wageni wanamiliki maeneo makubwa na mazuri kwa ajili ya kilimo kwanza inakuwaje?isitoshe kwa mujibu wa sheria mgeni haruhusiwi kumiliki ardhi inakuwaje hawa wanamiliki? hao singasinga lazima wana mdau wa kitanzania kwa mujibu wa sheria yetu ya uwekezaji,tupeni taarifa kamili ni watanzania gani wamo humo ndani?
 
Ndugu wana JF

Kuna taarifa ambazo sijazithibitisha kwamba, Malkia wa Uingereza anamiliki Eneo Kubwa sana Ndani ya Nchi yetu, ambapo Hata Serikali yetu haina Mamlaka ya Kuingia.

Eneo linasemekana liko Mkoa wa Iringa

Naomba mwenye taarifa kamili anijuze


Egongos hawa watu wana land katika kila potential inchi duniani na sio juzi, toka forever....
 
jamani watu wa Iringa tusaidieni,eti malikia amepewa shamba la eka 500 ktk mashamba ya chai ambayopo chini kuna madini na serikali yetu sikivu,nisaidieni wandugu kama mwenye nacho anaongezewa na asiye nacho anapokonywa
 
Niliwahi kufanya kazi kwenye hiyo kampuni upande wa mashamba ya chai eneo la kilolelo mwaka 1995. Tanganyika Wattle Company wakati huo ilikuwa ikimiliki hekta 600 za mashamba ya chai na maelfu ya hekta za mashamba ya miwati. Ni kampuni iliyokuwa inamilikiwa na CDC wakati huo, kwa sasa sielewi. Baadaye ilianzishwa kampuni ya chai kushughulika na mashamba ya chai inayoitwa Kibena Tea Company. CDC pia walianzisha Kampuni ya chai ya TATEPA (Chai bora) ambayo baadaye iliuzwa kwa wakenya.

Kwa muhtasari, TANWAT ilianzishwa tangu mwaka 1945. Na imekuwa kwenye uwekezaji wa misitu kipindi kirefu hadi sasa.
 
Ni kweli ni shamba la hiyo miti na watu wa kule walisema ni tangu kipindi cha ukoloni tulikuwa huko juzi juzi tunafanya baseline survey ya mambo ya kilimo,by the way miti hiyo inatumika kutengeneza kiwi za viatu.na lease waliyopewa ni ya miaka mingi tu.
Matumizi makubwa ya product inayotokana na miwati ni kwenye viwanda vya ngozi' kubadili skin(animal) kuwa leather
 
Kwa namna ninavyofahamu, hiyo ardhi unayoizungumzia ni kampuni ya miwati(Tanganyika Wattle Company) iliyopo Kibena Njombe.

Awali inavyosemekana ilikuwa ni mali ya Royal family ya Uingereza na ambapo CDC(Commonwealth Development Co-operation) walikuwa na hisa na TDFL pia nao walikuwa na hisa(sifahamu % ya hisa ilivyokuwa). Baadae(mwishoni mwa miaka ya 80 kama sijakosea), Royal family waliachia hisa zao zote kwa CDC n kufanya CDC kumiliki 85% ya hisa na TDFL Kuwa na 15% ya hisa.

Baada ya hapo sijui kilichotokea, lakini 2005, ikaonekana kama CDC ilikuwa inamiliki 100% ya hisa na hivyo ikauza hisa zake zote kwa Kampuni ya Kenya ijulikanayo kama KALDORA International, inayomilikiwa na masingasinga ambao asili yao ni Iringa na ndiyo wanamiliki Mufindi Paper Mills(zamani SPM Mgololo)

Katika kipindi chote cha mabadiliko TANWAT ilijipanua hadi Kilombero na kujishughulisha na upandaji wa Mi Tiki wakiwa na kampuni ya KVTC, so KVTC ikatenganishwa na TANWAT na ika fall kwa African Forestry ambayo ina misitu Uganda, Gabon na pia South Sudan.

Kwa hiyo nadhani Malkia alishaiacha hiyo ardhi ya Njombe na kama ana ardhi anayomiliki kwa sasa labda itakuwa hiyo ya Kilombero.

Yawezekana udadavuzi wako ukawa na ka ukweli japo si wa 100%, ila ninachjua mimi ni kuwa Malkia bado anamiliki sehemu kubwa sana ya mkoa wa njombe, na moja ya mkataba wao ni yeye kuihudumia barabara ya Makambako - Songea kwa miaka 99. Kuhusu suala la Malkia kufika huko, ni kweli alishafika miaka ya nyuma sana japo sikumbuki vizuri na moja ya kazi aliyoifanya ilikuwa ni ufunguzi wa ujenzi wa barabara hiyo ya Makambako - Songea (Ruvuma) pamoja na stesheni ya treni ya Makambako.
Bila shaka hiyo ndiyo hali halisi! Tena bila kusaha na ukarabati wa barabara unaoendelea kufanyika humo ni funds kutoka huko kupitia EU.
 
hivi na lile la wa saud arabia nilisikia liko kule loliondo bado wanalimiki??
naskia huwa wanatua na nduge zao na kuondoka bila kuulizwa na yeyote-ni kweli?
 
Uingereza ilipotawala East Africa ilikuwa pia inatawala South Africa nchi za Malawi, Zambia, Lesotho, Botswana nk.

Walianzisha Common Trade ili kudumisha himaya yao. Wawekezeji kutoka South Africa waliruhusiwa kupata ardhi Tanganyika.

Lonrho Brothers pia walimiliki ardhi Iringa, Milima ya Usambara walilima chai. Kama mnakumbuka Brookbond Tea.
 
Adjustments.jpg



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom