KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,139
Nova Kambota
Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang'ang'ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.
Nkwazi Mhango
Kambota nakushukuru, kwani umevua gamba,
Kumbuka umekufuru, matapishi utaramba,
Siku kweli ikizuru, utajiona mshamba,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.
Kwa wachumiao tumbo, Lowassa mtu shujaa,
Wafikirio kwa matumbo, Lowassa tiba ya njaa,
Watapigana vikumbo, kwenda kwake ganga njaa,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.
Hebu rudi darasani, jifunze misamiati,
Udhaifu tabaini, uijue tofauti,
Kamanda na marhuni, vina kubwa tofauti,
Shairi lako la hovyo, wamsifia fisadi.
Kama Lowassa Kamanda, basi ni wa mafisadi,
Kwa hili sitamponda, kulhali ni fisadi,
Kwake nilichokipenda, kukubali yu fisadi,
Kamueleza Kikwete, kuwa sote mafisadi.
Kambota nakushangaa, sijaona kicho chako,
Tafuta dawa ya njaa, si kuvua nguo zako,
Kesho kaka ni balaa, mafisadi si wenzako,
watakutumia sana, utatupwa ja nepi.
Kambota umenikuna, kufichua sura yako,
Ila la maana huna, kwa huo mradi wako,
Wamtumikia ngwena, kitoweo mwisho wako,
Uliza waliowini, kihalali si jinai.
Uchangu kimaadili, umegeuka mradi,
Wachovu waona dili, kutumiwa na fisadi,
Watupia senti mbili, kusafisha mafisadi,
Mwisho wa siku walia, warambapo matapishi.
Kaditamati kituo, mbele sitaendelea,
Onyo wapiga chapuo, fisadi kunyenyekea,
Ipo siku mlo huo, puani utatokea,
Kambota u mmojawapo,wapi utaficha sura?
Nova Kambota
Lowassa Ni Msafi, Hahitaji Kusafishwa ( Jibu)
Mjengwa naomba tena, jukwaani nirejee
Niliyoandika jana, napenda niyatetee
Mkuranga kimanzichana, Lowassa aendelee
Nkwazi hujaelewa, umefakamia mada
Mhango kajichanganya, kujibu asichojua
Kauropoka unyanya, pasipo kulitambua
Si hasi wala si chanya, Nkwazi kasimamia
Mhango wajipotosha, kujibu usichojua
Lowassa ni mtu safi, tegua kitendawili
Angelikuwa ni ni fisi, mahakama mhimili
Hojazo ni mufilisi, wewe ndumilakuwili
Nkwazi rudi shuleni, kaisome CCM
Mhango wanishangaza, ukweli kutofahamu
Waonekana kilaza, rejea Dar es salaamu
Kwa hoja ntakuchakaza, wewe mwana wa Adamu
CCM huijui, fitina wamezoea
Lowassa ni kiongozi, hili unalitambua
Achana na upuuzi, ule walomzushia
Usijifanye dandizi, kudandia usojua
Nkwazi mwana Mhango, uliza nakusikia
Beti sita natuama, nimefikia tamati
Lowassa mtu wa maana, hodari wa mikakati
Nkwazi soma kwa sana, tambua hizi nyakati
Lowassa ni mtu safi, hahitaji kusafishwa.
Nkwazi Mhango
Kambota achaujuha, CCM siyo fani,
Kijana acha mzaha,kunambia sina fani,
Sema yenyemkutadha, siyo kuleta uhuni,
Kama kakaumehongwa, tulia kula kizani
Najua uko kazini,wataka akusikie
Lowassa ni yakodini, lazima umsifie,
Ila jua u kizani,ni heri ujililie,
Kambotaunachekesha, noisome CCM!
Sikujua tokamwanzo, ninakinzana na zoba,
Mwenye mgandomawazo, aso kifani mjuba,
Sikujua hamnazo,nilomvisha kikuba
Kambota achaujuha, soma maoni ya watu.
Wasema nirudi Dar,nipambane na mgao!
Nani amekuhadaa,huyo kakupiga bao
Lowassa kaka balaa,ndiye chanzo cha mgao,
Kambota hebukomaa, mambo ya kitoto acha.
Mie kwako nimwalimu, hilo kaka walijua,
Kaiulize kaumu,najua wanitambua,
Nii mwalimu wawalimu, Bongo nzima watambua,
Kambota shikaadabu, kiatu changu huvai.
Hata utetee vipi,Lowassa bado fisadi,
Wenye mawazomafupi, humuona maridadi,
Awatumia ja chupi,waona wanafaidi,
Kambota achautani, haramu haishibishi.
Wino umeniishia,mbele sitaendelea,
Karima akijalia,hoja itaendelea,
Muhimu toto sikia,adabu upate tia,
Lowassa atakuponza,ukweli ukidhihiri.
Nova Kambota
MHANGO ACHA UJUHA
Mhango acha ujuha, heshima wajishushia
Wasababisha karaha,kuimba kuitikia
Wajiletea jeraha,moyoni hutalilia?
Kwa hili umechemsha, zumbukuku nakuita.
Lowassa wamtamka, uzushi wamtungia
Hoja zako za kubaka, maneno unadandia
Hakika u kibaraka, leo nakupasulia
Ikulu ya kutumia, Kikwete swahiba wako.
Huijui Richmond, kwanini unaropoka
Tena wajifanya fundi, huku unaweweseka
Punguza wako upimbi, punguza kubwekabweka
Nkwazi acha ujinga, heshima wajishushia.
Kanada umetopea, hupakumbuki nyumbani?
Halafu wajitetea, uhesabiwe kundini
Tatizo lako sikia, upeo wa kiganjani
Miaka umenizidi, Kwa hoja usithubutu.
Wamtukana Lowassa, nini amekukosea?
Umegeuzwa galasa, uzushi kufakamia
Kwani kamanda Lowassa, nani alimteua?
Nkwazi wewe mjinga, fumbo hutaling'amua.
Hapa mwisho nagotea, tamati nimefikia
Nkwazi nakushangaa, nini unajivunia?
Siri zako nafichua, Ikulu yakutumia
Nkwazi nipe jawabu, unalipwa bei gani?
Nkwazi Mhango
Kabota nitakubota, hata kama kiroboto,
Yote unayolumbata, si chochote ni kokoto,
Huna mpata na kata, nijuacho u limpyoto,
Kabota acha unywanywa, naona unatumiwa.
Lowassa bado fisadi, hata mmpambe vipi,
Kambota wewe hasidi, watumika kama nepi,
wajiona wafaidi, kumbe kesho ni makapi,
Kabota acha unywanywa, Lowassa akutumia.
Wauliza nalipwaje, Nani huyo anilipe?
Sijalipwa hata punje, mie mwezio si kupe,
Shurti nijikunje, niishi si kwa mahepe,
Kabota acha ushamba, Lowassa atakuponza.
Naijua Richmond, Richmond ni Lowassa,
Kikwete ni Richmond, Richmond ni mkasa,
Kambota nawe ni bundi, Richmond takutesa,
Japo wachumia tumbo, Kambota acha ujuha.
Utajaliwa ja ng'oda, Siku yako ikifika
Ja ng'oda utakonda, Lowassa akikutoka
Ukuuishie ukuda, ubaki kulalamika
Fisadi hana rafiki, Jifunze kwake Lowassa
Mambo yalipombana, Kikwete kaumuumbua,
Hawa marafiki sana, Itakuwa wewe bua,
Leo sana wajiona, ujinga wakusumbua,
Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.
Huna mpaka na nune, Kambota wala jaani,
Leo wewe ujivune, kumbe wenda majilini,
Sema sana utukane, itafika arobaini,
Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.
Kaditamati natua, mbele sitaendelea,
Kwa hapa naomba dua, wadudi anisikia,
Ninamuomba mulua, Kambota aone jua,
Kambota chumia tumbo, hebu tumia ubongo.
ROYALS
Ninakuunga mkono, wewe mr kambota
Tena kwa maandamano, ya Dar hadi Msata
Ulosema ni manono, kama ya nyama ya bata
Laigwenan msafi, wao walimchafua.
Nova Kambota
MHANGO WAJUA NINI?
Nkwazi nakuuliza, nini kimekuingia?
Mwenyewe wajishangaza, kubisha usiyojua
Kwa hoja nakuchakaza, hili unalitambua?
Mhango wajua nini? Zaidi ya kutumiwa?
Nakuuliza hasidi, nijibu nikulipue
Nitoe na ushahidi, watu wote wakujue
Watumiwa kama pedi, kanusha nikuumbue
Nyumba unayoringia, mimi ni mjenzi wake.
Lowassa mchapakazi, Leigwani maridadi
Tena yu baba mlezi, wa viwango na spidi
Muda wake hapotezi, Kulumbana nawe kidi
Nkwazi unachekesha kumtuhumu Lowassa.
Unalipwa bei gani, kwanini jibu hunipi?
Nimekutoa manani, wamung'unywa kama pipi
Unazungumza nini?, msimamo wako upi?
Nkwazi wanichekesha, kupungukiwa na hoja
Richmond mali ya mtu, Kikwete namtangaza
Punguza roho ya kutu, uongo kuutandaza
Wewe ni kidudu mtu, kwa hoja nakuchakaza
Mimi naitwa Kambota, "Kabota" waweweseka
Kwa hoja nakuadhibu, tamati nimefikia
Nakufundisha adabu, Zinduka umesinzia
Kwa hoja wewe ni bubu, leo nakupasulia
Nkwazi wajua nini? zaidi ya kutumiwa?
JE KUNA MTU ANAWEZA KUINGILIA KATI MALUMBANO HAYA KWA STYLE YA MASHAIRI KAMA HAWA,NA JE NANI ANATUMIWA KATI YA HAWA MALENGA WETU??????????????????????
Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang'ang'ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.
Nkwazi Mhango
Kambota nakushukuru, kwani umevua gamba,
Kumbuka umekufuru, matapishi utaramba,
Siku kweli ikizuru, utajiona mshamba,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.
Kwa wachumiao tumbo, Lowassa mtu shujaa,
Wafikirio kwa matumbo, Lowassa tiba ya njaa,
Watapigana vikumbo, kwenda kwake ganga njaa,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.
Hebu rudi darasani, jifunze misamiati,
Udhaifu tabaini, uijue tofauti,
Kamanda na marhuni, vina kubwa tofauti,
Shairi lako la hovyo, wamsifia fisadi.
Kama Lowassa Kamanda, basi ni wa mafisadi,
Kwa hili sitamponda, kulhali ni fisadi,
Kwake nilichokipenda, kukubali yu fisadi,
Kamueleza Kikwete, kuwa sote mafisadi.
Kambota nakushangaa, sijaona kicho chako,
Tafuta dawa ya njaa, si kuvua nguo zako,
Kesho kaka ni balaa, mafisadi si wenzako,
watakutumia sana, utatupwa ja nepi.
Kambota umenikuna, kufichua sura yako,
Ila la maana huna, kwa huo mradi wako,
Wamtumikia ngwena, kitoweo mwisho wako,
Uliza waliowini, kihalali si jinai.
Uchangu kimaadili, umegeuka mradi,
Wachovu waona dili, kutumiwa na fisadi,
Watupia senti mbili, kusafisha mafisadi,
Mwisho wa siku walia, warambapo matapishi.
Kaditamati kituo, mbele sitaendelea,
Onyo wapiga chapuo, fisadi kunyenyekea,
Ipo siku mlo huo, puani utatokea,
Kambota u mmojawapo,wapi utaficha sura?
Nova Kambota
Lowassa Ni Msafi, Hahitaji Kusafishwa ( Jibu)
Mjengwa naomba tena, jukwaani nirejee
Niliyoandika jana, napenda niyatetee
Mkuranga kimanzichana, Lowassa aendelee
Nkwazi hujaelewa, umefakamia mada
Mhango kajichanganya, kujibu asichojua
Kauropoka unyanya, pasipo kulitambua
Si hasi wala si chanya, Nkwazi kasimamia
Mhango wajipotosha, kujibu usichojua
Lowassa ni mtu safi, tegua kitendawili
Angelikuwa ni ni fisi, mahakama mhimili
Hojazo ni mufilisi, wewe ndumilakuwili
Nkwazi rudi shuleni, kaisome CCM
Mhango wanishangaza, ukweli kutofahamu
Waonekana kilaza, rejea Dar es salaamu
Kwa hoja ntakuchakaza, wewe mwana wa Adamu
CCM huijui, fitina wamezoea
Lowassa ni kiongozi, hili unalitambua
Achana na upuuzi, ule walomzushia
Usijifanye dandizi, kudandia usojua
Nkwazi mwana Mhango, uliza nakusikia
Beti sita natuama, nimefikia tamati
Lowassa mtu wa maana, hodari wa mikakati
Nkwazi soma kwa sana, tambua hizi nyakati
Lowassa ni mtu safi, hahitaji kusafishwa.
Nkwazi Mhango
Kambota achaujuha, CCM siyo fani,
Kijana acha mzaha,kunambia sina fani,
Sema yenyemkutadha, siyo kuleta uhuni,
Kama kakaumehongwa, tulia kula kizani
Najua uko kazini,wataka akusikie
Lowassa ni yakodini, lazima umsifie,
Ila jua u kizani,ni heri ujililie,
Kambotaunachekesha, noisome CCM!
Sikujua tokamwanzo, ninakinzana na zoba,
Mwenye mgandomawazo, aso kifani mjuba,
Sikujua hamnazo,nilomvisha kikuba
Kambota achaujuha, soma maoni ya watu.
Wasema nirudi Dar,nipambane na mgao!
Nani amekuhadaa,huyo kakupiga bao
Lowassa kaka balaa,ndiye chanzo cha mgao,
Kambota hebukomaa, mambo ya kitoto acha.
Mie kwako nimwalimu, hilo kaka walijua,
Kaiulize kaumu,najua wanitambua,
Nii mwalimu wawalimu, Bongo nzima watambua,
Kambota shikaadabu, kiatu changu huvai.
Hata utetee vipi,Lowassa bado fisadi,
Wenye mawazomafupi, humuona maridadi,
Awatumia ja chupi,waona wanafaidi,
Kambota achautani, haramu haishibishi.
Wino umeniishia,mbele sitaendelea,
Karima akijalia,hoja itaendelea,
Muhimu toto sikia,adabu upate tia,
Lowassa atakuponza,ukweli ukidhihiri.
Nova Kambota
MHANGO ACHA UJUHA
Mhango acha ujuha, heshima wajishushia
Wasababisha karaha,kuimba kuitikia
Wajiletea jeraha,moyoni hutalilia?
Kwa hili umechemsha, zumbukuku nakuita.
Lowassa wamtamka, uzushi wamtungia
Hoja zako za kubaka, maneno unadandia
Hakika u kibaraka, leo nakupasulia
Ikulu ya kutumia, Kikwete swahiba wako.
Huijui Richmond, kwanini unaropoka
Tena wajifanya fundi, huku unaweweseka
Punguza wako upimbi, punguza kubwekabweka
Nkwazi acha ujinga, heshima wajishushia.
Kanada umetopea, hupakumbuki nyumbani?
Halafu wajitetea, uhesabiwe kundini
Tatizo lako sikia, upeo wa kiganjani
Miaka umenizidi, Kwa hoja usithubutu.
Wamtukana Lowassa, nini amekukosea?
Umegeuzwa galasa, uzushi kufakamia
Kwani kamanda Lowassa, nani alimteua?
Nkwazi wewe mjinga, fumbo hutaling'amua.
Hapa mwisho nagotea, tamati nimefikia
Nkwazi nakushangaa, nini unajivunia?
Siri zako nafichua, Ikulu yakutumia
Nkwazi nipe jawabu, unalipwa bei gani?
Nkwazi Mhango
Kabota nitakubota, hata kama kiroboto,
Yote unayolumbata, si chochote ni kokoto,
Huna mpata na kata, nijuacho u limpyoto,
Kabota acha unywanywa, naona unatumiwa.
Lowassa bado fisadi, hata mmpambe vipi,
Kambota wewe hasidi, watumika kama nepi,
wajiona wafaidi, kumbe kesho ni makapi,
Kabota acha unywanywa, Lowassa akutumia.
Wauliza nalipwaje, Nani huyo anilipe?
Sijalipwa hata punje, mie mwezio si kupe,
Shurti nijikunje, niishi si kwa mahepe,
Kabota acha ushamba, Lowassa atakuponza.
Naijua Richmond, Richmond ni Lowassa,
Kikwete ni Richmond, Richmond ni mkasa,
Kambota nawe ni bundi, Richmond takutesa,
Japo wachumia tumbo, Kambota acha ujuha.
Utajaliwa ja ng'oda, Siku yako ikifika
Ja ng'oda utakonda, Lowassa akikutoka
Ukuuishie ukuda, ubaki kulalamika
Fisadi hana rafiki, Jifunze kwake Lowassa
Mambo yalipombana, Kikwete kaumuumbua,
Hawa marafiki sana, Itakuwa wewe bua,
Leo sana wajiona, ujinga wakusumbua,
Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.
Huna mpaka na nune, Kambota wala jaani,
Leo wewe ujivune, kumbe wenda majilini,
Sema sana utukane, itafika arobaini,
Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.
Kaditamati natua, mbele sitaendelea,
Kwa hapa naomba dua, wadudi anisikia,
Ninamuomba mulua, Kambota aone jua,
Kambota chumia tumbo, hebu tumia ubongo.
ROYALS
Ninakuunga mkono, wewe mr kambota
Tena kwa maandamano, ya Dar hadi Msata
Ulosema ni manono, kama ya nyama ya bata
Laigwenan msafi, wao walimchafua.
Nova Kambota
MHANGO WAJUA NINI?
Nkwazi nakuuliza, nini kimekuingia?
Mwenyewe wajishangaza, kubisha usiyojua
Kwa hoja nakuchakaza, hili unalitambua?
Mhango wajua nini? Zaidi ya kutumiwa?
Nakuuliza hasidi, nijibu nikulipue
Nitoe na ushahidi, watu wote wakujue
Watumiwa kama pedi, kanusha nikuumbue
Nyumba unayoringia, mimi ni mjenzi wake.
Lowassa mchapakazi, Leigwani maridadi
Tena yu baba mlezi, wa viwango na spidi
Muda wake hapotezi, Kulumbana nawe kidi
Nkwazi unachekesha kumtuhumu Lowassa.
Unalipwa bei gani, kwanini jibu hunipi?
Nimekutoa manani, wamung'unywa kama pipi
Unazungumza nini?, msimamo wako upi?
Nkwazi wanichekesha, kupungukiwa na hoja
Richmond mali ya mtu, Kikwete namtangaza
Punguza roho ya kutu, uongo kuutandaza
Wewe ni kidudu mtu, kwa hoja nakuchakaza
Mimi naitwa Kambota, "Kabota" waweweseka
Kwa hoja nakuadhibu, tamati nimefikia
Nakufundisha adabu, Zinduka umesinzia
Kwa hoja wewe ni bubu, leo nakupasulia
Nkwazi wajua nini? zaidi ya kutumiwa?
JE KUNA MTU ANAWEZA KUINGILIA KATI MALUMBANO HAYA KWA STYLE YA MASHAIRI KAMA HAWA,NA JE NANI ANATUMIWA KATI YA HAWA MALENGA WETU??????????????????????