Malenga wetu na sakata la Richmond

KIM KARDASH

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
5,139
1,139
Nova Kambota

Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia

Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang'ang'ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.

Nkwazi Mhango

Kambota nakushukuru, kwani umevua gamba,
Kumbuka umekufuru, matapishi utaramba,
Siku kweli ikizuru, utajiona mshamba,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.

Kwa wachumiao tumbo, Lowassa mtu shujaa,
Wafikirio kwa matumbo, Lowassa tiba ya njaa,
Watapigana vikumbo, kwenda kwake ganga njaa,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.

Hebu rudi darasani, jifunze misamiati,
Udhaifu tabaini, uijue tofauti,
Kamanda na marhuni, vina kubwa tofauti,
Shairi lako la hovyo, wamsifia fisadi.

Kama Lowassa Kamanda, basi ni wa mafisadi,
Kwa hili sitamponda, kulhali ni fisadi,
Kwake nilichokipenda, kukubali yu fisadi,
Kamueleza Kikwete, kuwa sote mafisadi.

Kambota nakushangaa, sijaona kicho chako,
Tafuta dawa ya njaa, si kuvua nguo zako,
Kesho kaka ni balaa, mafisadi si wenzako,
watakutumia sana, utatupwa ja nepi.

Kambota umenikuna, kufichua sura yako,
Ila la maana huna, kwa huo mradi wako,
Wamtumikia ngwena, kitoweo mwisho wako,
Uliza waliowini, kihalali si jinai.

Uchangu kimaadili, umegeuka mradi,
Wachovu waona dili, kutumiwa na fisadi,
Watupia senti mbili, kusafisha mafisadi,
Mwisho wa siku walia, warambapo matapishi.

Kaditamati kituo, mbele sitaendelea,
Onyo wapiga chapuo, fisadi kunyenyekea,
Ipo siku mlo huo, puani utatokea,
Kambota u mmojawapo,wapi utaficha sura?


Nova Kambota

Lowassa Ni Msafi, Hahitaji Kusafishwa ( Jibu)
Mjengwa naomba tena, jukwaani nirejee
Niliyoandika jana, napenda niyatetee
Mkuranga kimanzichana, Lowassa aendelee
Nkwazi hujaelewa, umefakamia mada

Mhango kajichanganya, kujibu asichojua
Kauropoka unyanya, pasipo kulitambua
Si hasi wala si chanya, Nkwazi kasimamia
Mhango wajipotosha, kujibu usichojua

Lowassa ni mtu safi, tegua kitendawili
Angelikuwa ni ni fisi, mahakama mhimili
Hojazo ni mufilisi, wewe ndumilakuwili
Nkwazi rudi shuleni, kaisome CCM

Mhango wanishangaza, ukweli kutofahamu
Waonekana kilaza, rejea Dar es salaamu
Kwa hoja ntakuchakaza, wewe mwana wa Adamu
CCM huijui, fitina wamezoea

Lowassa ni kiongozi, hili unalitambua
Achana na upuuzi, ule walomzushia
Usijifanye dandizi, kudandia usojua
Nkwazi mwana Mhango, uliza nakusikia

Beti sita natuama, nimefikia tamati
Lowassa mtu wa maana, hodari wa mikakati
Nkwazi soma kwa sana, tambua hizi nyakati
Lowassa ni mtu safi, hahitaji kusafishwa.


Nkwazi Mhango

Kambota achaujuha, CCM siyo fani,
Kijana acha mzaha,kunambia sina fani,
Sema yenyemkutadha, siyo kuleta uhuni,
Kama kakaumehongwa, tulia kula kizani

Najua uko kazini,wataka akusikie
Lowassa ni yakodini, lazima umsifie,
Ila jua u kizani,ni heri ujililie,
Kambotaunachekesha, noisome CCM!

Sikujua tokamwanzo, ninakinzana na zoba,
Mwenye mgandomawazo, aso kifani mjuba,
Sikujua hamnazo,nilomvisha kikuba
Kambota achaujuha, soma maoni ya watu.

Wasema nirudi Dar,nipambane na mgao!
Nani amekuhadaa,huyo kakupiga bao
Lowassa kaka balaa,ndiye chanzo cha mgao,
Kambota hebukomaa, mambo ya kitoto acha.

Mie kwako nimwalimu, hilo kaka walijua,
Kaiulize kaumu,najua wanitambua,
Nii mwalimu wawalimu, Bongo nzima watambua,
Kambota shikaadabu, kiatu changu huvai.

Hata utetee vipi,Lowassa bado fisadi,
Wenye mawazomafupi, humuona maridadi,
Awatumia ja chupi,waona wanafaidi,
Kambota achautani, haramu haishibishi.

Wino umeniishia,mbele sitaendelea,
Karima akijalia,hoja itaendelea,
Muhimu toto sikia,adabu upate tia,
Lowassa atakuponza,ukweli ukidhihiri.



Nova Kambota



MHANGO ACHA UJUHA

Mhango acha ujuha, heshima wajishushia
Wasababisha karaha,kuimba kuitikia
Wajiletea jeraha,moyoni hutalilia?
Kwa hili umechemsha, zumbukuku nakuita.

Lowassa wamtamka, uzushi wamtungia
Hoja zako za kubaka, maneno unadandia
Hakika u kibaraka, leo nakupasulia
Ikulu ya kutumia, Kikwete swahiba wako.

Huijui Richmond, kwanini unaropoka
Tena wajifanya fundi, huku unaweweseka
Punguza wako upimbi, punguza kubwekabweka
Nkwazi acha ujinga, heshima wajishushia.

Kanada umetopea, hupakumbuki nyumbani?
Halafu wajitetea, uhesabiwe kundini
Tatizo lako sikia, upeo wa kiganjani
Miaka umenizidi, Kwa hoja usithubutu.

Wamtukana Lowassa, nini amekukosea?
Umegeuzwa galasa, uzushi kufakamia
Kwani kamanda Lowassa, nani alimteua?
Nkwazi wewe mjinga, fumbo hutaling'amua.

Hapa mwisho nagotea, tamati nimefikia
Nkwazi nakushangaa, nini unajivunia?
Siri zako nafichua, Ikulu yakutumia
Nkwazi nipe jawabu, unalipwa bei gani?


Nkwazi Mhango

Kabota nitakubota, hata kama kiroboto,
Yote unayolumbata, si chochote ni kokoto,
Huna mpata na kata, nijuacho u limpyoto,
Kabota acha unywanywa, naona unatumiwa.

Lowassa bado fisadi, hata mmpambe vipi,
Kambota wewe hasidi, watumika kama nepi,
wajiona wafaidi, kumbe kesho ni makapi,
Kabota acha unywanywa, Lowassa akutumia.

Wauliza nalipwaje, Nani huyo anilipe?
Sijalipwa hata punje, mie mwezio si kupe,
Shurti nijikunje, niishi si kwa mahepe,
Kabota acha ushamba, Lowassa atakuponza.

Naijua Richmond, Richmond ni Lowassa,
Kikwete ni Richmond, Richmond ni mkasa,
Kambota nawe ni bundi, Richmond takutesa,
Japo wachumia tumbo, Kambota acha ujuha.

Utajaliwa ja ng'oda, Siku yako ikifika
Ja ng'oda utakonda, Lowassa akikutoka
Ukuuishie ukuda, ubaki kulalamika
Fisadi hana rafiki, Jifunze kwake Lowassa

Mambo yalipombana, Kikwete kaumuumbua,
Hawa marafiki sana, Itakuwa wewe bua,
Leo sana wajiona, ujinga wakusumbua,
Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.

Huna mpaka na nune, Kambota wala jaani,
Leo wewe ujivune, kumbe wenda majilini,
Sema sana utukane, itafika arobaini,
Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.

Kaditamati natua, mbele sitaendelea,
Kwa hapa naomba dua, wadudi anisikia,
Ninamuomba mulua, Kambota aone jua,
Kambota chumia tumbo, hebu tumia ubongo.


ROYALS
Ninakuunga mkono, wewe mr kambota
Tena kwa maandamano, ya Dar hadi Msata
Ulosema ni manono, kama ya nyama ya bata
Laigwenan msafi, wao walimchafua.



Nova Kambota

MHANGO WAJUA NINI?

Nkwazi nakuuliza, nini kimekuingia?
Mwenyewe wajishangaza, kubisha usiyojua
Kwa hoja nakuchakaza, hili unalitambua?
Mhango wajua nini? Zaidi ya kutumiwa?

Nakuuliza hasidi, nijibu nikulipue
Nitoe na ushahidi, watu wote wakujue
Watumiwa kama pedi, kanusha nikuumbue
Nyumba unayoringia, mimi ni mjenzi wake.

Lowassa mchapakazi, Leigwani maridadi
Tena yu baba mlezi, wa viwango na spidi
Muda wake hapotezi, Kulumbana nawe kidi
Nkwazi unachekesha kumtuhumu Lowassa.

Unalipwa bei gani, kwanini jibu hunipi?
Nimekutoa manani, wamung'unywa kama pipi
Unazungumza nini?, msimamo wako upi?
Nkwazi wanichekesha, kupungukiwa na hoja

Richmond mali ya mtu, Kikwete namtangaza
Punguza roho ya kutu, uongo kuutandaza
Wewe ni kidudu mtu, kwa hoja nakuchakaza
Mimi naitwa Kambota, "Kabota" waweweseka

Kwa hoja nakuadhibu, tamati nimefikia
Nakufundisha adabu, Zinduka umesinzia
Kwa hoja wewe ni bubu, leo nakupasulia
Nkwazi wajua nini? zaidi ya kutumiwa?


JE KUNA MTU ANAWEZA KUINGILIA KATI MALUMBANO HAYA KWA STYLE YA MASHAIRI KAMA HAWA,NA JE NANI ANATUMIWA KATI YA HAWA MALENGA WETU??????????????????????

 
lowasa kukwepa hili hawezi

kilola mwana wa pwani, ebu nishike kalamu,
niingie ulingoni, huku nikiwasalimu,
nami nitoe maoni, kwenye huu udhalimu,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Lowasa tatizo lake, nae alijiingiza,
yeye kwa kauli zake, wizara aliagiza,
na vile vimemo vyake, uzito viliongeza,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Alipoona mkulu, ushauri hautaki,
yeye angetunusuru, na kututendea haki,
sheria angenukulu, na kanuni kuhakiki,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Lakini akasahau, manunuzi nchi hii,
hayahitaji nahau, yanahitaji utii,
sheria kaidharau, kaingiza usanii,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Wangefuata sheria, halisi ya manunuzi,
isingeleta udhia, na hivyo vigugumizi,
maana tungetambua, ni taratibu za kazi,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Kufuata mizania, hupunguza matumizi,
na gharama halisia, sisi tungezimaizi,
thamani ya kulipia, ingefanana na kazi,
lowasa hapa hatoki kukwepa hili hawezi.

Sasa huo ushauri, wa makatibu wakuu,
mbona kaufanya siri, hakutaka kunukuu,
angeuweka dhahiri, ingekuwa ni nafuu,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Lowasa mtu mahili, uamuzi atoapo,
lakini kwa jambo hili, amenasa kama popo,
lazima alikubali, asikwepe kwa viapo,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.
 
lowasa kukwepa hili hawezi

kilola mwana wa pwani, ebu nishike kalamu,
niingie ulingoni, huku nikiwasalimu,
nami nitoe maoni, kwenye huu udhalimu,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Lowasa tatizo lake, nae alijiingiza,
yeye kwa kauli zake, wizara aliagiza,
na vile vimemo vyake, uzito viliongeza,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Alipoona mkulu, ushauri hautaki,
yeye angetunusuru, na kututendea haki,
sheria angenukulu, na kanuni kuhakiki,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Lakini akasahau, manunuzi nchi hii,
hayahitaji nahau, yanahitaji utii,
sheria kaidharau, kaingiza usanii,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Wangefuata sheria, halisi ya manunuzi,
isingeleta udhia, na hivyo vigugumizi,
maana tungetambua, ni taratibu za kazi,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Kufuata mizania, hupunguza matumizi,
na gharama halisia, sisi tungezimaizi,
thamani ya kulipia, ingefanana na kazi,
lowasa hapa hatoki kukwepa hili hawezi.

Sasa huo ushauri, wa makatibu wakuu,
mbona kaufanya siri, hakutaka kunukuu,
angeuweka dhahiri, ingekuwa ni nafuu,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Lowasa mtu mahili, uamuzi atoapo,
lakini kwa jambo hili, amenasa kama popo,
lazima alikubali, asikwepe kwa viapo,
lowasa hapa hatoki, kukwepa hili hawezi.

Ahh mie yangu macho mashairi siyawezi,ngoja tusubiri waje wenye fani,wapi nkwazi,wapi kambota??kazi kwenu,natahakikisha hii kitu inaendelea mpaka tunampata rais mpya 2015 na kuendelea.....
 
[h=2]Mbona malenga wetu wako kimya siku hizi mbili au mpaka lowassa avunje ukimya?[/h]
 
Mashairi yametulia haya. Inanikumbusha kipindi cha malenga wetu miaka ile tukiwa na redio ya taifa pekee.

Tangu ziingie hizi FM stations hata sijui RTD niliipotezea wapi!
 
Mashairi yametulia haya. Inanikumbusha kipindi cha malenga wetu miaka ile tukiwa na redio ya taifa pekee.

Tangu ziingie hizi FM stations hata sijui RTD niliipotezea wapi!

Yah!kweli kabisa,enzi za kina sauti ya kiza ambae alikua akiijiita hivyo kutokana na ulemavu wa macho aliokuwa nao!jamaa alikua kiboko ya njia....
 
Ooooh I am rejuvinated again...this was my passion when I was in primary school! Mashairi yana radha yake bwana.
 
hakyanani mmenikumbusha mbali sana . nilikuwa sipendi hiko kipindi kabisa , nilikuwa nikitoka shule mchana huyo jamaaa alikuwa ananipa kichefu chefu. ilikuwa kila nyumba nayopita namskia huyo jamaaa akisoma mashairi pamoja na harufu ya ugali unaopikwa kila nyumba kweli ilikuwa inanikata stimu sana.
 
Sofia Simba amewahi kutamka kuwa hakuna mwanaume kama Lowasa. Atawaoa wengi huyu.
 
Bora wewe wengine unakuta jiko limenuna halafu malenga wetu ndio anaunguruma redioni!
 
Yote kwa yote Lowassa hawezi kusafishwa kwa mashairi bali kwa kusimama hadharani mchana kweupe na kutueleza anachokijua na asichokijua kuhusu richmond,tunateseka sana na gharama za umeme hatutamsamehe alieileta richmond.
 
Back
Top Bottom