Malecela aionya CCM; asema kama inataka kuendelea kushika dola iwafukuze watuhumiwa wa ufisadi

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Monday, 22 August 2011 09:06
07cela.jpg
Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela​
ASEMA KAMA INATAKA KUENDELEA KUSHIKA DOLA IWAFUKUZE ATUMUMIWA WA UFISADI
Boniface Meena
WAZIRI Mkuu mstaafu, John Malecela amekitaka Chama chake cha Mapinduzi (CCM) kuwachukulia hatua za haraka wala rushwa walioko ndani yake kuanzia ngazi ya juu hadi chini kama kinataka kuendelea kushika dola.Kauli ya Malecela ambaye ni Mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu (CC) ya CCM, inakuja kipindi ambacho mpango mkakati wa chama hicho wa kujivua gamba unaonekana kupigwa kalenda.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi nyumbani kwake Sea View, Upanga Dar es Salaam jana, Malecela alisema ni muhimu wala rushwa wakaondolewa haraka bila kucheleweshwa ili chama kiendelee kuwapo.

Malecela alinukuu maandiko ya Mungu katika Ukristo akisema: "Mimi ni Mkristo, maneno ya Mungu yanasema ukiwa na jicho bovu na ukiona linakuzuia kuingia mbinguni litoe ili uweze kuingia."

"Kama kuna corrupt people in the party (wala rushwa ndani ya chama), ni kuwaondoa ili CCM iendelee kuwapo."

Hata hivyo, alisema suala la kujivua gamba haliwezi kuwa kwa watu wanne au watano, bali chama kisafishe wala rushwa wote waliopo ndani yake kuanzia ngazi ya juu hadi chini.

Kujivua gamba
Mpango wa kujivua gamba kwa CCM ulianza kutangazwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete wakati wa maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni akisema yalikuwa na lengo la kukihuisha.

Rais Kikwete alisema chama hicho kiliwahi kufanya mabadiliko mbalimbali kuanzia TANU kwa lengo la kujisafisha na kujipanga upya, baada ya kujifanyia tathmini kuhusu mwelekeo wake kwa wakati husika.

Mpango huo baadaye ulijadiliwa katika CC iliyokutana Mjini Dodoma mnamo Aprili ambayo pamoja na mambo mengine utekelezaji huo ulianza kwa Kamati hiyo Kuu kujiuzulu yote na kusukwa upya huku baadhi ya watuhumiwa akiwamo Andrew Chenge kutupwa nje.

Katika kikao hicho, ilitangazwa watuhumiwa wa ufisadi ukiwamo wa Richmond, Rada na Kagoda iliyochota Sh40 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wangepaswa kujipima na kuachia nafasi zao ndani ya siku 90 lakini hadi kikao cha CC cha mwezi uliopita, watuhumiwa hao walikuwa hawajajiuzulu.

Badala yake, CC ilitoa muda zaidi kusubiri uamuzi wa kikao cha Halmashauri Kuu (Nec) ya chama hicho inayotarajiwa kukutana mwezi ujao.Hata hivyo, hakuna dalili zozote za watuhumiwa wakubwa wanaotajwa katika kashfa hizo za rada na Richmond kujiuzulu huku chama kikionekana kuwa katika wakati mgumu kuwafukuza, huku hatua ya kutowafukuza ikitajwa kama kitanzi kinachoweza kukimaliza kisiasa.

Tuhuma za kumiliki shamba hekta 100
Akizungumzia madai yaliyotolewa Bungeni hivi karibuni na Waziri Kivuli wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halima Mdee kwamba anamiliki hekta 100 za shamba huko Mvomero, Morogoro, Malecela alisema hana habari juu ya umiliki huo akisema: "Sina hati yake na wala sijawahi kufika kuliona, hata sijui liko sehemu gani ya Mvomero."

Alisema wakati Serikali ilipoipa Mvomero hadhi ya wilaya, iliwapa baadhi ya viongozi mashamba ili waendeleze maeneo hayo au wavute wawekezaji katika wilaya hiyo."Mimi niliambiwa nimepewa hekta 100 lakini sijawahi kufika kwenye eneo hilo, hata hati ya shamba hilo sina hivyo ni kusema sina shamba Mvomero."

"Ambaye analitaka shamba hilo akalichukue au kama kuna mtu anayefikiri kuwa ana hati ya shamba hilo aende wizarani athibitishe."

"Ni miaka 10 imepita tangu niambiwe suala hilo, wakati huo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero akiwa ni (Samwel) Kamote, lakini sheria za kutoendeleza mashamba si zinajulikana kama lipo tu kwa nini lisichukuliwe?"

Malecela alisema asingeweza kupeleka trekta kutoka Dodoma kwenda kulima Mvomero hekta 100 kwa kuwa uwekezaji unahitaji zaidi ya hekta 300.

Alichokisema Mdee bungeni
Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe (Chadema), akisoma bajeti mbadala ya upinzani kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka 2011/12 aliwataja baadhi ya viongozi wa CCM wakiwamo Marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa akiwatuhumu kuhodhi maeneo makubwa ya ardhi mkoani Morogoro huku wakishindwa kuyaendeleza. Hata hivyo, Mkapa anaelezwa kuendeleza shamba lake.

Katika orodha hiyo pia ametajwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Philip Mangula, aliyekuwa Naibu wake (Tanzania Bara), Hassan Ngwilizi na Mwenyekiti wa CCM mkoani Mbeya, Nawab Mulla.

Mdee alisema umiliki wa maeneo makubwa ya ardhi unawanyima fursa wananchi wa kawaida kupata maeneo kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kuongeza kwamba, vigogo hao kwa kutumia nafasi zao waliwanyang’anya wananchi ardhi hiyo na kujimilikisha wenyewe lakini kwa sehemu kubwa wameshindwa kuyaendeleza.

“Mheshimiwa Spika, matatizo ya ardhi kwa wakubwa kunyang’anya wanyonge imekumba pia Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ambako mgogoro huu unakumba shamba namba 299 iliyokuwa Narco Ranches lenye ukubwa wa hekta 49,981," alisema na kuongeza:

“Taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha kuwa maeneo yaliyokuwa yamepangwa kugawiwa kwa wanavijiji wa Kijiji cha Wami, yamegawiwa wanavijiji wafuatao,’’ alisema na kuanza kuwataja vigogo hao kwa majina mmoja baada ya mwingine.

Akitoa orodha hiyo, Mdee alisema Mangula anamiliki hekta 2,000, Mwinyi hekta 2,000 na Mkapa hekta 1,000 ambaye hata hivyo, ndiye pekee aliweza kuliendeleza shamba lake.

Katika orodha ya Mdee alimtaja pia Sumaye kwamba anamiliki hekta 500, Malecela hekta 100 na Ngwilizi ambaye anamiliki hekta 100 huku akisisitiza orodha hiyo ni ndefu.Mdee alitaka Serikali itoe maelezo kwamba ni vigezo vipi vilitumika kuwagawia ardhi viongozi hao huku wakiwanyima ardhi wananchi wa maeneo husika.
 
Namshauri mzee Malecela ingekuwa vema waseme mtu anatakiwa ajivue gamba akishakuwa amefikia kiwango gani cha ufisadi maana kila kukicha tunasikia ufisadi mpya ktk chama cha magamba.
 
Mwacheni mzee aseme tu
Inabidi atambue kwamba kuwaondoa mafisadi wote ndani ya CCM ni sawa na kuua chama,kwa maana nyigine ni kuvunja kila kitu waanze kuandikisha wanchama upya.

Wakifanya hivyo hata yeye Malicela anaweza asipate kadi.
 
Mwacheni mzee aseme tu
Inabidi atambue kwamba kuwaondoa mafisadi wote ndani ya CCM ni sawa na kuua chama,kwa maana nyigine ni kuvunja kila kitu waanze kuandikisha wanchama upya.

Wakifanya hivyo hata yeye Malicela anaweza asipate kadi.

Maana ya mzee Malecela ni kuwa mwisho wa CCM umefika. Rais anatuhumiwa kwa kuwalinda mafisadi, vigogo wengi wa chama, mawaziri waandamizi wote wanatuhumiwa kwa ufisadi, ambao rais hawezi kuwachukulia hatua. Kwa hiyo maana yake ni kuwa huu ndio mwisho wa chama.
 
Big up mzee waambie ukweli hao akina mkwe re. Tunashukuru pia kwa kulitema shambaletu la heka 100 lililowekwa hadharani na Mhe. Waziri kivuli Halima Mdee
 
CCM sasa wametufikisha pazuri kwani kwa kauli ya huyu Mzee Malecela itawafanya aliowataka waondolewe nao wamfungulie dossier yake ikikumbusha kuwa hata yeye sio msafi kwani Sophia Simba alishasema kuwa harusi yake na Anne Killango ilifadhiliwa kwa fedha za EPA!!
 
Anataka kijisafisha huyu, Unakumbuka wakati wa Azimio La Zanzibar, Nyerere alimuuliza Malecela kwanini anakubaliana na hilo Azimio; Malecelela akamwambia Nyerere wakati wake Umekwisha...

Sababu alijua ni kosa lakini alikuwa anataka Urais kwa hali na Mali; Nyerere akasema watu kama hawa wanaotaka Uongozi kupitia Mlango wa nyuma hawafai....

Huyu Mzee Hatufai....
 
He looks like them he speaks like them he behaves like them he is one of them he can as well go to hell with them, same bird same feathers!
 
Big up mzee waambie ukweli hao akina mkwe re. Tunashukuru pia kwa kulitema shambaletu la heka 100 lililowekwa hadharani na Mhe. Waziri kivuli Halima Mdee
<br />
<br />
Huyu jumanne mnafiki sana wakati anagawiwa kwannini hakuwaambia wanaomgawia wamekosea akakataa mpaka asikie kelele ndo aseme hana hati ya shamba. Mwanao akileta mali isiyo na rissiti unatakiwa mumhoji siku ya kwanza siyo mpaka siku polisi wakija kumkamata ndo useme hiyo mali huitambui
 
"Kama kuna corrupt people in the party (wala rushwa ndani ya chama), ni kuwaondoa ili CCM iendelee kuwapo."

Uswahili mtupu anashindwa nini kusema Fisadi papa pale Magogoni aka JK mwizi, RA, Chenge, Mkapa etc. Nidhamu ya woga na huyu ndiye alikuwa waziri mkuu ... ...
 
<table class="wysiwyg_dashes wysiwyg_cms_table_contentpaneopen"><tr valign="top" class="wysiwyg_dashes_tr wysiwyg_cms_table_contentpaneopen_tr"><td class="wysiwyg_cms_table_contentheading wysiwyg_dashes_td wysiwyg_cms_table_contentpaneopen_td"><br _moz_dirty="" type="_moz" /></td><td class="wysiwyg_cms_table_buttonheading wysiwyg_dashes_td wysiwyg_cms_table_contentpaneopen_td" width="100%" align="right"><br _moz_dirty="" type="_moz" /></td></tr></table><br />
<table class="wysiwyg_dashes wysiwyg_cms_table_contentpaneopen"><tr valign="top" class="wysiwyg_dashes_tr wysiwyg_cms_table_contentpaneopen_tr"><td class="wysiwyg_cms_table_createdate wysiwyg_dashes_td wysiwyg_cms_table_contentpaneopen_td">Monday, 22 August 2011 09:06</td></tr><tr valign="top" class="wysiwyg_dashes_tr wysiwyg_cms_table_contentpaneopen_tr"><td class="wysiwyg_dashes_td wysiwyg_cms_table_contentpaneopen_td"><img src="http://www.mwananchi.co.tz/images/stories/07cela.jpg" border="0" alt="" /><p style="text-align: center;">Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela</p><br />
<span style="font-family: courier new"><font size="4"><font color="#0000ff"><b>ASEMA KAMA INATAKA KUENDELEA KUSHIKA DOLA IWAFUKUZE ATUMUMIWA WA UFISADI</b><br />
Boniface Meena<br />
WAZIRI Mkuu mstaafu, John Malecela amekitaka Chama chake cha Mapinduzi (CCM) kuwachukulia hatua za haraka wala rushwa walioko ndani yake kuanzia ngazi ya juu hadi chini kama kinataka kuendelea kushika dola.Kauli ya Malecela ambaye ni Mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu (CC) ya CCM, inakuja kipindi ambacho mpango mkakati wa chama hicho wa kujivua gamba unaonekana kupigwa kalenda.<br />
<br />
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi nyumbani kwake Sea View, Upanga Dar es Salaam jana, Malecela alisema ni muhimu wala rushwa wakaondolewa haraka bila kucheleweshwa ili chama kiendelee kuwapo.<br />
<br />
Malecela alinukuu maandiko ya Mungu katika Ukristo akisema: &quot;Mimi ni Mkristo, maneno ya Mungu yanasema ukiwa na jicho bovu na ukiona linakuzuia kuingia mbinguni litoe ili uweze kuingia.&quot;<br />
<br />
&quot;Kama kuna corrupt people in the party (wala rushwa ndani ya chama), ni kuwaondoa ili CCM iendelee kuwapo.&quot;<br />
<br />
Hata hivyo, alisema suala la kujivua gamba haliwezi kuwa kwa watu wanne au watano, bali chama kisafishe wala rushwa wote waliopo ndani yake kuanzia ngazi ya juu hadi chini.<br />
<br />
Kujivua gamba<br />
Mpango wa kujivua gamba kwa CCM ulianza kutangazwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete wakati wa maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni akisema yalikuwa na lengo la kukihuisha.<br />
<br />
Rais Kikwete alisema chama hicho kiliwahi kufanya mabadiliko mbalimbali kuanzia TANU kwa lengo la kujisafisha na kujipanga upya, baada ya kujifanyia tathmini kuhusu mwelekeo wake kwa wakati husika. <br />
<br />
Mpango huo baadaye ulijadiliwa katika CC iliyokutana Mjini Dodoma mnamo Aprili ambayo pamoja na mambo mengine utekelezaji huo ulianza kwa Kamati hiyo Kuu kujiuzulu yote na kusukwa upya huku baadhi ya watuhumiwa akiwamo Andrew Chenge kutupwa nje.<br />
<br />
Katika kikao hicho, ilitangazwa watuhumiwa wa ufisadi ukiwamo wa Richmond, Rada na Kagoda iliyochota Sh40 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wangepaswa kujipima na kuachia nafasi zao ndani ya siku 90 lakini hadi kikao cha CC cha mwezi uliopita, watuhumiwa hao walikuwa hawajajiuzulu.<br />
<br />
Badala yake, CC ilitoa muda zaidi kusubiri uamuzi wa kikao cha Halmashauri Kuu (Nec) ya chama hicho inayotarajiwa kukutana mwezi ujao.Hata hivyo, hakuna dalili zozote za watuhumiwa wakubwa wanaotajwa katika kashfa hizo za rada na Richmond kujiuzulu huku chama kikionekana kuwa katika wakati mgumu kuwafukuza, huku hatua ya kutowafukuza ikitajwa kama kitanzi kinachoweza kukimaliza kisiasa.<br />
<br />
<b>Tuhuma za kumiliki shamba hekta 100</b><br />
Akizungumzia madai yaliyotolewa Bungeni hivi karibuni na Waziri Kivuli wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halima Mdee kwamba anamiliki hekta 100 za shamba huko Mvomero, Morogoro, Malecela alisema hana habari juu ya umiliki huo akisema: &quot;Sina hati yake na wala sijawahi kufika kuliona, hata sijui liko sehemu gani ya Mvomero.&quot;<br />
<br />
Alisema wakati Serikali ilipoipa Mvomero hadhi ya wilaya, iliwapa baadhi ya viongozi mashamba ili waendeleze maeneo hayo au wavute wawekezaji katika wilaya hiyo.&quot;Mimi niliambiwa nimepewa hekta 100 lakini sijawahi kufika kwenye eneo hilo, hata hati ya shamba hilo sina hivyo ni kusema sina shamba Mvomero.&quot;<br />
<br />
&quot;Ambaye analitaka shamba hilo akalichukue au kama kuna mtu anayefikiri kuwa ana hati ya shamba hilo aende wizarani athibitishe.&quot;<br />
<br />
&quot;Ni miaka 10 imepita tangu niambiwe suala hilo, wakati huo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero akiwa ni (Samwel) Kamote, lakini sheria za kutoendeleza mashamba si zinajulikana kama lipo tu kwa nini lisichukuliwe?&quot;<br />
<br />
Malecela alisema asingeweza kupeleka trekta kutoka Dodoma kwenda kulima Mvomero hekta 100 kwa kuwa uwekezaji unahitaji zaidi ya hekta 300.<br />
<br />
<b>Alichokisema Mdee bungeni</b><br />
Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe (Chadema), akisoma bajeti mbadala ya upinzani kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka 2011/12 aliwataja baadhi ya viongozi wa CCM wakiwamo Marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa akiwatuhumu kuhodhi maeneo makubwa ya ardhi mkoani Morogoro huku wakishindwa kuyaendeleza. Hata hivyo, Mkapa anaelezwa kuendeleza shamba lake.<br />
<br />
Katika orodha hiyo pia ametajwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Philip Mangula, aliyekuwa Naibu wake (Tanzania Bara), Hassan Ngwilizi na Mwenyekiti wa CCM mkoani Mbeya, Nawab Mulla.<br />
<br />
Mdee alisema umiliki wa maeneo makubwa ya ardhi unawanyima fursa wananchi wa kawaida kupata maeneo kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kuongeza kwamba, vigogo hao kwa kutumia nafasi zao waliwanyang’anya wananchi ardhi hiyo na kujimilikisha wenyewe lakini kwa sehemu kubwa wameshindwa kuyaendeleza.<br />
<br />
“Mheshimiwa Spika, matatizo ya ardhi kwa wakubwa kunyang’anya wanyonge imekumba pia Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ambako mgogoro huu unakumba shamba namba 299 iliyokuwa Narco Ranches lenye ukubwa wa hekta 49,981,&quot; alisema na kuongeza:<br />
<br />
“Taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha kuwa maeneo yaliyokuwa yamepangwa kugawiwa kwa wanavijiji wa Kijiji cha Wami, yamegawiwa wanavijiji wafuatao,’’ alisema na kuanza kuwataja vigogo hao kwa majina mmoja baada ya mwingine. <br />
<br />
Akitoa orodha hiyo, Mdee alisema Mangula anamiliki hekta 2,000, Mwinyi hekta 2,000 na Mkapa hekta 1,000 ambaye hata hivyo, ndiye pekee aliweza kuliendeleza shamba lake.<br />
<br />
Katika orodha ya Mdee alimtaja pia Sumaye kwamba anamiliki hekta 500, Malecela hekta 100 na Ngwilizi ambaye anamiliki hekta 100 huku akisisitiza orodha hiyo ni ndefu.Mdee alitaka Serikali itoe maelezo kwamba ni vigezo vipi vilitumika kuwagawia ardhi viongozi hao huku wakiwanyima ardhi wananchi wa maeneo husika.</font></font></span></td></tr></table>
<br />
<br />
Ukimwi ni ugonjwa hatari kama ulivyo ufisadi kwa ccm. Uktaka uuondoa lazima binadamu afe. Ili uuondoe ufisadi lazima uiue ccm. Ccm bye
 
Back
Top Bottom