Solomon David
JF-Expert Member
- Mar 1, 2009
- 1,148
- 16
Yes,
yeye Malaria Sugu, na pacha wake Tumaini, na binamu yake Kanda2.
Kwa kadri ambavyo mods wanayakubali yale wanayobandika hapa na kuacha yaendelee kukaa kwa miezi na miaka kadhaa (kitu ambacho ni kizuri ukichukulia uhuru wa maoni unaoruhusiwa na JF), ikubaliwe kuwa hiyo format wanayotumia inakubalika hapa JF na inaruhusiwa kama sehemu ya kampeni za 2010.
Na kwa jinsi hiyo, na ukifuatilia kuwa wanayoandika hapa yanafanana sana na matamshi ya Makamba, Mkuchika, na wanaccm wengi (akiwemo mgombea wao Jakaya Kikwete), ni kwa asilimia 95 ya uhakika (confidence level) kuwa hawa ni wasemaji wa kampeni ya Kikwete na ccm kwa ujumla.
Kama hii itasaidia kwenye maandalizi yako ya namna ya kuwajibu, kumbuka kuwa kila unachoona hapa toka kwa hao watatu, kichukulie kama tamko maalum la kampeni ya Kikwete na wana ccm kwa mwaka huu wa uchaguzi.
Na kwa kadri ambavyo mod wamekubali matamko yao hapa JF, ni matumaini kuwa mods watakubali hiki ninachobandika hapa na kukiacha hapa kwenye jukwaa la siasa. Hata hivyo, kwa kadri ambavyo JF imeonekana ikioperate karibuni, sitashangaa kuona nilichobandika kikihamishiwa mbali na kufichwa ili kisisomwe na wengi (wakati mabandiko ya MS na wenzake yakiendelea kutamba kwenye siasa na jukwaa la uchaguzi).
Asante
yeye Malaria Sugu, na pacha wake Tumaini, na binamu yake Kanda2.
Kwa kadri ambavyo mods wanayakubali yale wanayobandika hapa na kuacha yaendelee kukaa kwa miezi na miaka kadhaa (kitu ambacho ni kizuri ukichukulia uhuru wa maoni unaoruhusiwa na JF), ikubaliwe kuwa hiyo format wanayotumia inakubalika hapa JF na inaruhusiwa kama sehemu ya kampeni za 2010.
Na kwa jinsi hiyo, na ukifuatilia kuwa wanayoandika hapa yanafanana sana na matamshi ya Makamba, Mkuchika, na wanaccm wengi (akiwemo mgombea wao Jakaya Kikwete), ni kwa asilimia 95 ya uhakika (confidence level) kuwa hawa ni wasemaji wa kampeni ya Kikwete na ccm kwa ujumla.
Kama hii itasaidia kwenye maandalizi yako ya namna ya kuwajibu, kumbuka kuwa kila unachoona hapa toka kwa hao watatu, kichukulie kama tamko maalum la kampeni ya Kikwete na wana ccm kwa mwaka huu wa uchaguzi.
Na kwa kadri ambavyo mod wamekubali matamko yao hapa JF, ni matumaini kuwa mods watakubali hiki ninachobandika hapa na kukiacha hapa kwenye jukwaa la siasa. Hata hivyo, kwa kadri ambavyo JF imeonekana ikioperate karibuni, sitashangaa kuona nilichobandika kikihamishiwa mbali na kufichwa ili kisisomwe na wengi (wakati mabandiko ya MS na wenzake yakiendelea kutamba kwenye siasa na jukwaa la uchaguzi).
Asante