Makongoro Nyerere ana mtizamo potofu kuhusu watanzania na Afrika Mashariki!

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,012
Posted by JokaKuu | May 15, 2012

..kwa jinsi nilivyomuelewa Makongoro Nyerere kutokana na maelezo yake anakwenda ktk bunge la EAC kuhakikisha kwamba Tanzania inaondoa pingamizi lake ktk masuala ya ARDHI, na kupigania kuanzishwa kwa SHIRIKISHO LA KISIASA la Afrika Mashariki.

..Makongoro Nyerere anafikiri kinachohitajika ni wa-Tanzania "kuelimishwa" ili kuondoa "hofu" waliyonayo kuhusu masuala ya ardhi. anadai kwamba wa-Tanzania hatuna "elimu" juu ya "matumizi endelevu" ya ardhi na ndiyo maana tuna "hofu" kuhusu raia wa EAC kuwa na haki ya kumiliki ardhi ya Tanzania.

..Kuhusu kuanzishwa kwa Shirikisho, Makongoro Nyerere anadai tunapaswa kuanzisha shirikisho la kisiasa ili nchi za Afrika Mashariki ziwe na "sauti moja."

..mimi nadhani wabunge walikosea ktk kumchagua Makongoro Nyerere kuwa mwakilishi wetu kwenye bunge la EAC. nasema hivyo kwasababu msimamo alio nao na mambo aliyoazimia kuyatetea ktk bunge la EAC ni kinyume na matakwa ya wa-Tanzania kama walivyoelezea ktk Tume ya kukusanya maoni ya Prof.Samwel Mwita Wangwe.

..inatia wasiwasi sana lakini sidhani kama wenzetu[makongoro, etc] wanajifunza kutokana na matatizo waliyonayo majirani zetu kuhusu suala hili la ardhi. Kenya wamekuwa na migogoro isiyokwisha kutokana na sera zao mbaya za umiliki wa ardhi. Pia mauaji ya halaiki yaliyotokea Rwanda chanzo chake ni ukabila na matatizo ya ardhi. Sijui kwanini wanasiasa kama Makongoro Nyerere wanakosa umakini na kauli zao kuhusu suala la ardhi hapa Tanzania, wakati there r lessons to learn all around us.

..kuhusu Shirikisho malengo ya Kenya na Uganda ilikuwa 2013 tuwe na shirikisho la kisiasa. Mimi nadhani mawazo hayo ni ya hatari kabisa ukizingatia what it takes kuunda shirikisho hilo. Sijaona duniani shirikisho la kisiasa linalotumia sarafu tofauti za fedha, but that was what was about to happen in East Africa.

..kwa mitizamo yake nadhani Makongoro Nyerere amepotoka kimtizamo na atakuwa mbunge wa Kenya na siyo wetu wa-Tanzania.


mnaweza kusoma zaidi kupitia linki hii hapa : Makongoro: Tusihofie Shirikisho | Gazeti la MwanaHalisi (Makongoro: Tusihofie Shirikisho | Gazeti la MwanaHalisi)


NB:

..Alhaji Adam Kimbisa amesikika akisema kwamba atatetea msimamo wa wa-Tanzania kuhusu ardhi kwa nguvu zake zote.
 
Last edited by a moderator:
Ndio watu watakao tetea maslahi yetu kweli hawa, by the way duuh i was thinking we were in crisis maana imechukua muda sana kazi ya safari hii poleni wahusika na asanteni kwa JF.
 
..Kuhusu kuanzishwa kwa Shirikisho, Makongoro Nyerere anadai tunapaswa kuanzisha shirikisho la kisiasa ili nchi za Afrika Mashariki ziwe na "sauti moja."
...Sauti moja juu ya nini? Sidhani kama anafahamu maana ya Shirikisho.

...inatia wasiwasi sana lakini sidhani kama wenzetu [makongoro, etc] wanajifunza kutokana na matatizo waliyonayo majirani zetu kuhusu suala hili la ardhi. Kenya wamekuwa na migogoro isiyokwisha kutokana na sera zao mbaya za umiliki wa ardhi. Pia mauaji ya halaiki yaliyotokea Rwanda chanzo chake ni ukabila na matatizo ya ardhi.
...Atajifunza kitu gani, wakati kaenda kula maisha.

..kuhusu Shirikisho malengo ya Kenya na Uganda ilikuwa 2013 tuwe na shirikisho la kisiasa. Mimi nadhani mawazo hayo ni ya hatari kabisa ukizingatia what it takes kuunda shirikisho hilo. Sijaona duniani shirikisho la kisiasa linalotumia sarafu tofauti za fedha, but that was what was about to happen in East Africa.
...Tuna kiasi kikubwa cha watu wasiojali wala kupoteza muda kuumiza vichwa, kutafiti na kutafakari mambo yenye maslahi ya kitaifa.
 
Namuunga mkono Makongoro Nyerere,tuache kulialia kama watoto wadogo,tutengeneze sheria na taratibu ambazo zitawezesha wageni kupata ardhi,walime na nchi yetu kunufaika,siyo kumiliki. Hii inawezekana,tatizo hatuna viongozi wenye maono!
 
Namuunga mkono Makongoro Nyerere,tuache kulialia kama watoto wadogo,tutengeneze sheria na taratibu ambazo zitawezesha wageni kupata ardhi,walime na nchi yetu kunufaika,siyo kumiliki. Hii inawezekana,tatizo hatuna viongozi wenye maono!
...Nani kakwambia hakuna sheria za ardhi Tanzania, ambazo zinaruhusu wageni kumiliki ardhi? Kule mpanda anapotaka kupewa yule mmarekani, sheria hazitumiki? Mashamba ya maua Arusha na yale ya Jatropha Pwani yanamilikiwa vipi?

...Issue ya ardhi katika majadiliano ya EAC iko tofauti kabisa.

...Tafiti, utajua kinachoendelea.
 
...Nani kakwambia hakuna sheria za ardhi Tanzania, ambazo zinaruhusu wageni kumiliki ardhi? Kule mpanda anapotaka kupewa yule mmarekani, sheria hazitumiki? Mashamba ya maua Arusha na yale ya Jatropha Pwani yanamilikiwa vipi?

...Issue ya ardhi katika majadiliano ya EAC iko tofauti kabisa.

...Tafiti, utajua kinachoendelea.
nimeandika hapo juu kwamba tutengeneze sheria na taratibu ambazo zitawawezesha wageni kutumia ardhi yetu kuzalisha,siyo kumiliki!
 
Namuunga mkono Makongoro Nyerere,tuache kulialia kama watoto wadogo,tutengeneze sheria na taratibu ambazo zitawezesha wageni kupata ardhi,walime na nchi yetu kunufaika,siyo kumiliki. Hii inawezekana,tatizo hatuna viongozi wenye maono!

OMG!!! Hawa ndio watanzanai tulio nao...
 
nimeandika hapo juu kwamba tutengeneze sheria na taratibu ambazo zitawawezesha wageni kutumia ardhi yetu kuzalisha,siyo kumiliki!
...Kabla hujazalisha, iwe juu ya ardhi au ndani ya kiwanda, lazima umiliki au kuikodi raslimali hiyo. Kama hauna umiliki wa ardhi hiyo, utapata wapi mikopo ya kuwekeza kwenye uzalishaji hasa kwa wageni unaowazungumzia?
 
Namuunga mkono Makongoro Nyerere,tuache kulialia kama watoto wadogo,tutengeneze sheria na taratibu ambazo zitawezesha wageni kupata ardhi,walime na nchi yetu kunufaika,siyo kumiliki. Hii inawezekana,tatizo hatuna viongozi wenye maono!

Hojayako ni sahihi kabisa, tuwe na sheria zinazoruhusu watu wote (wageni na wenyeji) kuitumia ardhi hiyo. Ila sheria za kuwamilikisha wageni ardhi ni jambo ambalo nadhani hata wewe hutakubaliana nalo. Tatizo letu Tanzania kama taifa, na hoja zilizoko kwenye EAC ni pale wanapotaka kufungulia ardhi iwe mali ya watu wote ndani ya EAC wakati ambapo nchi zote za Afrika ya Mashariki hazina Ardhi isipokuwa Tanzania tu. Kosa lililofanyika nchini ni kuwa baada ya kuamua kuua siasa za Nyerere hatukufanya juhudi za kuendeleza matumizi ya ardhi miongoni mwa wananchi. Badala yake ardhi ambayo chini ya Nyerere ilikuwa ni mali ya Taifa ikawa inachukuliwa kiholela na akina Sumaye na Mkapa bila kuwatayarisha wananchi katika kutumia ardhi yao. Madai ya kuwa watanazania wanalalama wakati watanzania hao hao hawaelimishwi kujua thmani ya ardhi zaidi ya maisha ya kijijini kwao ni kuwaonea sana watanzania kwa vile wengi wao wamekulia katika mazingira ambayo ardhi ilikuwa siyo tatizo kabisa.
 
Namuunga mkono Makongoro Nyerere,tuache kulialia kama watoto wadogo,tutengeneze sheria na taratibu ambazo zitawezesha wageni kupata ardhi,walime na nchi yetu kunufaika,siyo kumiliki. Hii inawezekana,tatizo hatuna viongozi wenye maono!

Timbilimu,

..suala la ardhi ni zaidi ya hayo unayoyazungumzia.

..sheria yetu ya uwekezaji inaruhusu watu wa nje kuja kufanya shughuli za kilimo nchini.

..sijui kwanini majirani zetu hawaridhiki na utaratibu huo.

..pia ingependeza kama wa-Tz tungeshiriki wenyewe kilimo kikubwa ili kuweza kuuza mazao yetu ndani na nje ya nchi.

..hao wananchi wa mataifa mengine wanaokuja kulima hapa Tanzania kwa minajili ya ku-export wametuzidi nini wa-Tz??
 
Back
Top Bottom