Nigrastratatract nerve
JF-Expert Member
- Sep 4, 2019
- 1,399
- 3,916
đź“Śđź“ŚMAKONDA ASISITIZA UWAJIBIKAJI NA KAULI NZURI KWA WATENDAJI WA SERIKALI.
Katibu wa NEC itikadi, uenezi na mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Paul Makonda amewataka watendaji wa serikali ya mkoa wa Shinyanga kufanya kazi kwa bidii ili kuondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa maeneo yao.
Mwenezi Makonda ametoa kauli hiyo leo wakati alipofika kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kahama ili kukagua utekelezaji wa agizo lake alilolitoa jana jumanne la kutaka siku ya leo itengwe kusikiliza kero za wananchi.
Katika maelezo yake Mwenezi Makonda pia amesisitiza watendaji kuwa na kauli na lugha nzuri kwa wananchi ili kuondoa chuki na hasira zisizokuwa na sababu kwa serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Aidha Chama Cha Mapinduzi kimewataka viongozi wa ngazi za mikoa na wilaya kuwa na utamaduni wa kusikiliza wananchi badala ya kusubiri viongozi wa kitaifa kutoka serikali ama kwenye Chama Cha Mapinduzi.
#VitendoVinaSauti
Katibu wa NEC itikadi, uenezi na mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Paul Makonda amewataka watendaji wa serikali ya mkoa wa Shinyanga kufanya kazi kwa bidii ili kuondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa maeneo yao.
Mwenezi Makonda ametoa kauli hiyo leo wakati alipofika kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kahama ili kukagua utekelezaji wa agizo lake alilolitoa jana jumanne la kutaka siku ya leo itengwe kusikiliza kero za wananchi.
Katika maelezo yake Mwenezi Makonda pia amesisitiza watendaji kuwa na kauli na lugha nzuri kwa wananchi ili kuondoa chuki na hasira zisizokuwa na sababu kwa serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Aidha Chama Cha Mapinduzi kimewataka viongozi wa ngazi za mikoa na wilaya kuwa na utamaduni wa kusikiliza wananchi badala ya kusubiri viongozi wa kitaifa kutoka serikali ama kwenye Chama Cha Mapinduzi.
#VitendoVinaSauti