Makinda: Waandishi wa habari wanapotosha suala la Posho

MachoMakavu

JF-Expert Member
Feb 6, 2008
367
44
Spika wa Bunge Mh.Anna Makinda leo alikutana na waandishi wa habari baada ya kuahirisha Bunge kutolea ufafanuzi suala la posho na tamko la serikali bungeni kuhusu mgomo wa madaktari.

Katika mkutano huo, Spika kadai kwamba watanzania wengi wanadhani wabunge hulipwa posho za kila siku kwa siku zote 365 za mwaka, jambo ambalo si kweli. Posho hizo hutolewa pale tu wanapokua na mikutano ya bungeni Dodoma.

Spika pia kafafanua kwa nini Serikali haijatoa tamko lolote kuhusu mgomo wa Madaktari bungeni. Kwa maelezo yake, Spika anaeleza kwamba tamko hilo ni lazima liandaliwe kwa maandishi, wabunge wote wagawiwe na kulipitia kabla ya kusomwa rasmi. Mchakato wa kuliandaa bado unaendea wizara ya afya na baada ya wabunge kugawiwa tamko hilo litajadiliwa.

Source: Taarifa ya habari TBC saa 2 usiku.

Hivi tuna kiongozi hapo?
 
Mimi hata sijui hii ni laana au nini??

Yani sasahivi kila jambo ambalo serikali italifanya au kuamua linatuacho hoi Wananchi.

Viongozi wanapojifunga vibwebwe na kutolea ufafanuzi katika hizo sintofaham, Wananchi ndio tunazidi kubaki midomo wazi na kuchanganyikiwa zaidi. Wakati mwingine naona bora wakae kimya japo nayo haisaidii....

Nimejitahidi kuelewa hii serikali pamoja na shutuma kibao zinazo ibuliwa, nimekua navuta subra nikiaamini kuna viongozi makini na watakuja na ufafanuzi ulionyooka lakini kila wanapoibuka ndio nazidi kuchoka kabisa. Hapo hajazungumza Raisi wao, yeye ndio huwa anavuruga mambo kabisa. Hebu nyie wazee wenye busara mliotengwa na hii serikali hovyo jitokezeni muiongoze nchi hii inaangamia kwa kweli. Wapi Salim Ahmed Salim? Wapi walioba? Mzee Malicela uko wapi baba? Jamani mambo huku ni vuruvuru JK nchi imemshinda jamani...

Lowasa uko makini lakini ukimya wako unatutia shaka (huenda kweli ni fisadi)
Sita umepoteza muelekeo(hasira zako za kukosa uspika zimekupoteza, ungetulia ungejijengea heshima sana) otherwise ungeweza kusaidia.

Dah...niko Hoiii....!
 
kwa maana nyingine ni kwamba wananchi tunapaswa kuridhika wabunge walipe hz posho kwani ni ndgo tu kutokana na siku wanazokuwa na vikao vya bunge.
 
Hivi hawa viongozi wetu wanajua emergence, au hawajui kama mgomo wa madaktari ni emergence kwa taifa? Wamekaa wanakula kuku wakati watu wanakufa wanasema tamko linaandikwa!! Hahahaha! Perhaps para moja then wanaenda kula mpaka kesho.
 
huyu mama ni cchp kweli kweli..yaani anafikiri watz ni vilaza kiasihuki..hivi ni mbunge wa wapi huyu?
 
Pia nimeikuta hii katika ukurasa wa Rais JK katika mtandao wa Facebook:

Gazeti la Mwananchi la leo, Jumanne, Januari 31, 2012 limeandika habari zenye kichwa cha habari – JK abariki posho mpya za Wabunge: Kila mmoja kulipwa sh 330,000 kwa siku.

Habari hizi siyo za kweli na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais inataka kutoa ufafanuzi ufuatao:

Maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu suala hili yako wazi kabisa na hakun...a mahali ambako Rais Kikwete amebariki posho hizi.

Maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuhusu suala hili ni kama ifuatavyo:

Kwanza, Mheshimiwa Rais Kikwete anakubali haja ya kuangalia upya posho kwa Wabunge lakini amewataka wabunge kutumia hekima na busara katika kulitafakari suala hili.

Pili, Mheshimiwa Rais Kikwete amewataka Wabunge kutumia Kikao cha sasa cha Bunge kulizungumza upya suala hilo.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
31 Januari, 2012
 
Huyu mama anakatisha tamaa kabisa,hata kwa hizo siku chache that is too much ,halafu sababu sio ya msingi sana,kama ni kupanda kwa maisha dodoma ati anavyodai yeye.

Huyu mama ni tatizo la kitaifa,serikali ndo usiseme kushney hakuna kitu.Kitu urgent kama mgomo wa madaktari huezi kusema ati una andaa makaratasi ya kutoa taarifa,kuandaa makaratasi huko kutachukua muda sana.Serikali haijui ku act,haiwezi kuwekewa matumaini na wananchi,Serikali inapishana katika kusema,Raisi hivi,waziri mkuu vile.This is really the hopeless government.Naona Miaka 4 iliyobaki tutateseka sana.
 
Hakuna mtu aliyesema wanakutana siku 365 achekupotosha na kupiga chenga hoja ya msingi. Hoja ya msingi hapa ni malipo ya TZS.330,000(200,000+80,000+50,000) kwa siku Moja kwa mbunge ambaye ameingia Bungeni.Iwe ameongea au amelala.Hii siyo sawa kabisa.Ubunge siyo professional ni WITO unajitoa kuwatumikia wananchi waliokuchagua sasa wao wamegeuza ajira.....
"Shame on you na hili la posho litawatafuna na kuwagawa mpaka mtashangaa"
 
Mimi hata sijui hii ni laana au nini??

Yani sasahivi kila jambo ambalo serikali italifanya au kuamua linatuacho hoi Wananchi.

Viongozi wanapojifunga vibwebwe na kutolea ufafanuzi katika hizo sintofaham, Wananchi ndio tunazidi kubaki midomo wazi na kuchanganyikiwa zaidi. Wakati mwingine naona bora wakae kimya japo nayo haisaidii....

Nimejitahidi kuelewa hii serikali pamoja na shutuma kibao zinazo ibuliwa, nimekua navuta subra nikiaamini kuna viongozi makini na watakuja na ufafanuzi ulionyooka lakini kila wanapoibuka ndio nazidi kuchoka kabisa. Hapo hajazungumza Raisi wao, yeye ndio huwa anavuruga mambo kabisa. Hebu nyie wazee wenye busara mliotengwa na hii serikali hovyo jitokezeni muiongoze nchi hii inaangamia kwa kweli. Wapi Salim Ahmed Salim? Wapi walioba? Mzee Malicela uko wapi baba? Jamani mambo huku ni vuruvuru JK nchi imemshinda jamani...

Lowasa uko makini lakini ukimya wako unatutia shaka (huenda kweli ni fisadi)
Sita umepoteza muelekeo(hasira zako za kukosa uspika zimekupoteza, ungetulia ungejijengea heshima sana) otherwise ungeweza kusaidia
Dah...niko Hoiii....!
mizee ya ccm nadhani pia imelogwa, wanamuogopa kweli jk nadhani sababu ni yakumwakwembeana ndo inawatisha hawa wazee. Ccm woote vilaza isipokuwa kingwangala na makamba tuu.
 
Spika wa Bunge Mh.Anna Makinda leo alikutana na waandishi wa habari baada ya kuahirisha Bunge kutolea ufafanuzi suala la posho na tamko la serikali bungeni kuhusu mgomo wa madaktari.

Katika mkutano huo, Spika kadai kwamba watanzania wengi wanadhani wabunge hulipwa posho za kila siku kwa siku zote 365 za mwaka, jambo ambalo si kweli. Posho hizo hutolewa pale tu wanapokua na mikutano ya bungeni Dodoma.

Spika pia kafafanua kwa nini Serikali haijatoa tamko lolote kuhusu mgomo wa Madaktari bungeni. Kwa maelezo yake, Spika anaeleza kwamba tamko hilo ni lazima liandaliwe kwa maandishi, wabunge wote wagawiwe na kulipitia kabla ya kusomwa rasmi. Mchakato wa kuliandaa bado unaendea wizara ya afya na baada ya wabunge kugawiwa tamko hilo litajadiliwa.

Source: Taarifa ya habari TBC saa 2 usiku.

Hivi tuna kiongozi hapo?

Hata wanapokuwa bungeni wanalipwa posho kwa lipi? Kusinzia? Kuna mbunge anaenda dom hata mdomo hafungui na aanalampa posho lol!
 
Hivi hawa waandishi wa habari kweli wanajua maadili ya kazi yao? Kuandika habari za uongo ni kosa na ni upotoshaji umma
 
Hivi hawa viongozi wetu wanajua emergence, au hawajui kama mgomo wa madaktari ni emergence kwa taifa? Wamekaa wanakula kuku wakati watu wanakufa wanasema tamko linaandikwa!! Hahahaha! Perhaps para moja then wanaenda kula mpaka kesho.
Heeheeeheeee para moja wanalamba POSHO hadi kesho yake kuendelea na para inayofuata!
 
huko Ikulu sielewi wanakanusha nini waka Rais ni kweli ametia saini kubariki posho hizo na wabunge wamekwishawekewa kwenye accounts zao!
 
huko Ikulu sielewi wanakanusha nini wakati Rais ni kweli ametia saini kubariki posho hizo na wabunge wamekwishawekewa kwenye accounts zao!
 
kwa maana nyingine ni kwamba wananchi tunapaswa kuridhika wabunge walipe hz posho kwani ni ndgo tu kutokana na siku wanazokuwa na vikao vya bunge.
Ndiyo maana yake mkuu anamaanisha kabum kenyewe ni kamda mfupi tukachunie tu.
 
Back
Top Bottom