Kama wewe ni mfuatiliaji wa siasa za Tanzania nafikiri utakubaliana nami nitakachokisema. Kitendo cha hivi karibuni cha Makamba kukimbilia upesi upesi kwenye tukio la mauaji ya Maswa na kusema anauhakika Shibuda amehusika ni cha kusikitisha sana. Vilevile kitendo chake cha kufika Maswa na kumtembelea mgombea CCM na kumwacha wa Chadema Shibuda aliyekuwa anashikiliwa pia na polisi akiwa mahabusu zinadhihilisha kuwa Makamba ana siasa za fitina ugomvi na kisasi na bado ana fikra za kuona upinzani ni uadui. Inawezekana kabisa maneno yanayosikika mitaani kuwa matukio mbalimbali ya vurugu za kisiasa yanayotokea sehemu mbalimbali (Arusha, Moshi, Tarime, Musoma, Mwanza, Busanda nk) huwa yamepangwa au kupewa baraka na Makamba, na inawezekana kabisa hata tukio la Maswa lilipangwa na Makamba ili kumchafua Shibuda mpango ambao umeshindwa kufanikiwa. Niko tayari kusahihishwa.
Hayo kwenye bold ndiyo ninayoyasema yeye ni mwepesi sana kusema wenzake wanatumia udini wakati mwenyewe ni mdini nambari wani, siku za mwanzo tu wa kampeni akarukia siasa za maji taka ambazo zilimtia aibu mbele ya jamii hakutegemea vinginevyo leo angekuwa anayaendeleza hayo kama mtaji wa siasa. Naomba Makamba siku tanzania itakapopata uhuru wa kweli awe bado hai.Makamba ni mdini, mchochezi na adui wa mstakabali wa amani ya taifa hili. Kati yake na polisi ni wapi wanajua zaidi ni yupi amehusika katika tukio fulani? Makamba alisema mbele ya vyombo vya habari kuwa wanaushahidi wa kimazingira kuwa Shubuda alihusika, siku chache baadaye polisi wamesema hahusiki katika vurugu zilizosababisha kifo.
Makamba utajuta siku uhuru wa kweli utakapopatikana Tanzania, utashitakiwa kwa uchochezi
Hayo kwenye bold ndiyo ninayoyasema yeye ni mwepesi sana kusema wenzake wanatumia udini wakati mwenyewe ni mdini nambari wani, siku za mwanzo tu wa kampeni akarukia siasa za maji taka ambazo zilimtia aibu mbele ya jamii hakutegemea vinginevyo leo angekuwa anayaendeleza hayo kama mtaji wa siasa. Naomba Makamba siku tanzania itakapopata uhuru wa kweli awe bado hai.