Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Mbunge wa viti maalum, Halima Mdee, amewatoa 'knock out' Makamba na Londa, ambao walilazimika kuondoa malalamiko yao kwa Spika wa Bunge dhidi yake Mbunge huyo kutokana na kauli yake (Mdee) akiwatuhumu kwa ufisadi katika sakata la ugawaji viwanja huko Kinondoni.
Baada ya Mdee kutoa kauli hiyo Bungeni, Makamba na Londa walipeleka malalamiko kwa spika lakini wakati kamati inayafanyia kazi, Makamaba alimwandikia spika akisema anajitoa kwenye mashitaka kwa sababu machungu aliyokuwa nayo yalishakwisha.
Baadaye, wakati kamati inaendelea, baada ya Londa kuhojiwa, aliposikia kuwa Mdee naye amehojiwa na kutoa vielelezo lukuki, Londa naye alimwandikia Spika akimweleza kujiondioa kwenye shauri hilo.
Katika ‘hukumu' aliyoisoma Bungeni jioni hii, Spika Sitta amesema kutokana na hali hiyo, maneno ya Mdee dhidi ya vigogo hao wawili yanabaki kama yalivyo na hakuna haja ya kuwaomba radhi
Baada ya Mdee kutoa kauli hiyo Bungeni, Makamba na Londa walipeleka malalamiko kwa spika lakini wakati kamati inayafanyia kazi, Makamaba alimwandikia spika akisema anajitoa kwenye mashitaka kwa sababu machungu aliyokuwa nayo yalishakwisha.
Baadaye, wakati kamati inaendelea, baada ya Londa kuhojiwa, aliposikia kuwa Mdee naye amehojiwa na kutoa vielelezo lukuki, Londa naye alimwandikia Spika akimweleza kujiondioa kwenye shauri hilo.
Katika ‘hukumu' aliyoisoma Bungeni jioni hii, Spika Sitta amesema kutokana na hali hiyo, maneno ya Mdee dhidi ya vigogo hao wawili yanabaki kama yalivyo na hakuna haja ya kuwaomba radhi