Yussuf Makamba amwinda Reginald Mengi, yeye awataja mafisadi Papa rasmi!

Mwanakijiji kwa nini uchore mipaka kati ya JK na kundi linalomwingiza?

Mimi tena? angalia mada yangu ya "Kikwete si safi; yes I said it!" yawezekana ilikuwa ya kwanza kumhusisha Kikwete na ufisadi miaka karibu miwili iliyopita. Mpaka ninauchora ni strategic in nature.

Au ndiyo strategy ya Mengi ili mwishowe yeye ndiyo aanze kucall the shots. Kama unakubali kwamba kundi lililomwingiza ni chafu kwa nini yeye awe msafi?

angalia jibu langu la awali..

Leo hii mwanakijiji unakuja na kusema kwamba JK atofautishwe na kundi lake kwi kwi kwi kwi.

Ndiyo na hili siliombei radhi; kosa walilolifanya Marekani kule Iraq ilikuwa ni kuihusisha Baath yote na ufisadi na kuwatimua watu wote waliokuwa kwenye baath (hasa viongozi wa juu) kutoka kwenye utumishi jeshini; matokeo yake waliyaona. Ni lazima katika mapambano ujue mipaka yako na upange vizuri.

Nimesema, siku JK atakaposimama kuwatetea mafisadi au kuwatafutia kinga na hapo yeye naye nitamuita fisadi. Na hilo mimi sina haya nalo na hata Mengi akigeuka na kuwatetea wezi wa nchi yetu na yeye ataitwa fisadi na atakuwa amechagua upande wa dhulma.

Au kwa sababu bosi wako Mengi kamsifia na wewe unaanza kuimba sifa za JK.

Sasa na wewe bosi wako Rostam kuguswa ndiyo imekuwa vurugu sasa?

Mwanakijiji sikuchagulii nani umpigie kampeni, lakini tambua kuwa ukimpigia kampeni fisadi ukija kuniambia unapambana na ufisadi nitakuuliza hata wewe?? Au unafanya usanii

Usanii wa kwangu au wa kwako; huwezi kunichagulia kitu chochote ambacho mwenyewe sijakichagua. Huna nguvu hiyo wala nafasi hiyo. Na mimi sina kwa upande wako. Chukua msimamo unaouona unafaa na uusimamie; si lazima wote tuone jambo moja sawasawa kama maroboti.

In this case, nakubaliana na Mengi kuhusu mafisadi nchini na juu ya nafasi ya JK katika mapambano haya. Kwa hili hakuna utata.
 
Hivi huyu Mengi na mshikaji wake Idd Simba hawakuwemo kwenye ule uuzaji wa hisa za NICO wakati kampuni ilikuwa haijaanza rasmi uzalishaji?? Huo pia ni ufisadi kwenda kuwauzia hisa walimu wa shule za msingi kwa kuwadanganya kuwa watapata gawiowakati kampuni haioperate. Mengi kama unataka ufisadi utokomee kuweni na nyie ni wasafi na pia acheni tabia ya kujikombakomba kwa JK. JK ni fisadi na hata wewe Mengi ukijifanya kumpamba haitasaidia. JK ametumia magazeti kwa muda wa miaka 10 kuwachafua wenzie ili aingie ikulu na hiyo dhambi mpaka leo inawaandama akina Jenerali Ulimwengu na Salva Rweyemamu. Wewe leo unakuja unasema JK shujaa!!! Kama huna jipya kaa kimya, ukikaa kimya hawatakuchinja kama kondoo kama ulivyosema mwenyewe. Maana utakuwa huwatishi, ila kwa kitabia chako cha kupambana na ufisadi selectively unabore stiff

inaonekana hujui nico ni nini?????

nico sio kiwanda wala kampuni ya usalishaji bali ni fund ambayo ilianzishwa ili kuwawezesha wazawa kununua makampuni ya ki TZ yaliyokua yanabinafishwa.
na ukiangalia sehemu walizo invest na hela ni kama shares za NMB

pili ukimwita manji rostam na kikwete inamaanisha unawapa nguvu wakina manji......
watZ bado hawajaamka kwa hiyo mengi akimwita kikwete fisadi watu watamuambia unagombana na kila mtu, kwa ajili wananchi wa tz(dar) wamelala kupita kiasi basi hamna mtu ataye msupport mengi sanasa watamuambia anagombana na kila mtu
mengi huyo huyo ndio awataje mafisadi hivi hawa vyama vya upinzani vinafanya nini ukiondoa dr slaa...
 
inaonekana hujui nico ni nini?????

nico sio kiwanda wala kampuni ya usalishaji bali ni fund ambayo ilianzishwa ili kuwawezesha wazawa kununua makampuni ya ki TZ yaliyokua yanabinafishwa.
na ukiangalia sehemu walizo invest na hela ni kama shares za NMB

Wewe ndiyo unaonekana hujui unachoongea nenda kasome sheria za masoko ya mitaji au hisa uone kama hicho unachosema kinaruhusiwa. Kama siyo usanii ambao unaendelea kuwaibia watanzia.

Lazima tukubali wakati kuna watu wanajitangaza kuwa ni majemadari wa kupambana na ufisadi ni lazima tuwamulike vizuri nao
 


Rostam mwaka jana kasimama na kuwasema akina Mengi pamoja na Mtikila je hiyo nayo inahitaji moral authority? Mengi naye leo kaongea kamsema Rostam je hiyo nayo inahitaji moral authority gani? Mwakyembe naye si alikuja kwa waandishi na yeye akamsema Rostam wakati yeye mwenyewe anahisa kwenye kampuni ya umeme je alikuwa na moyo authority, Je Mtikila alivyokuja kumsema Rostam wakati amevuta milioni tatu toka kwake je alikuwa na moral authority gani? Ndiyo maana nakwambia issue ni nini kimeongelewa na mtu siyo nani kaongea. Sasa Mengi anamsifia JK ambaye mimi binafsi namwona ni zao la ufisadi sasa kwa nini nisimtilie shaka?

Usitoke nje ya mada mweshimiwa..naona hata mimi unanisogeza kumjadili mengi badala ya aliyosema mengi leo...unakubaliana nae au la?
 
Wewe ndiyo unaonekana hujui unachoongea nenda kasome sheria za masoko ya mitaji au hisa uone kama hicho unachosema kinaruhusiwa. Kama siyo usanii ambao unaendelea kuwaibia watanzia.

Lazima tukubali wakati kuna watu wanajitangaza kuwa ni majemadari wa kupambana na ufisadi ni lazima tuwamulike vizuri nao

kwanini hutaki kuwamulika mafisadi wenyewe ambao hawawezi kujitangaza hata viranja wa kupambana na ufisadi?
 
Lazima tukubali wakati kuna watu wanajitangaza kuwa ni majemadari wa kupambana na ufisadi ni lazima tuwamulike vizuri nao

- Sawa sawa, ila tuwamulike na ushahidi wa ukweli, na tuuweke wazi badala ya blah! blah! blah!

- Kama Makamba na wanaomtuma wanaamini kwamba Mengi ana kesi ya kujibu kisheria kwa kuwaanika ufisadi wao mara kwa mara, kwa nini wasiende kwenye sheria, ambako wana nguvu nyingi sana, kuliko kwenye CC?

FMEs
 
Mimi tena? angalia mada yangu ya "Kikwete si safi; yes I said it!" yawezekana ilikuwa ya kwanza kumhusisha Kikwete na ufisadi miaka karibu miwili iliyopita. Mpaka ninauchora ni strategic in nature.

Kwangu naiona kama ni wrong strategy kwa sababu naona kama JK akiendelea hakutakuwa na jipya. Na kwa kweli umeniwahi maana nilitaka nikukumbushe hiyo mada yako.


angalia jibu langu la awali..

Nimeshaangalia

Ndiyo na hili siliombei radhi; kosa walilolifanya Marekani kule Iraq ilikuwa ni kuihusisha Baath yote na ufisadi na kuwatimua watu wote waliokuwa kwenye baath (hasa viongozi wa juu) kutoka kwenye utumishi jeshini; matokeo yake waliyaona. Ni lazima katika mapambano ujue mipaka yako na upange vizuri.

Nakubaliana na wewe kabisa hapa, lakini cha msingi ujue kwamba upande wa pili na wenyewe haujalala. Kwa hiyo wanaweza kuitumia strategy uliyoitumia kukuangamiza

Nimesema, siku JK atakaposimama kuwatetea mafisadi au kuwatafutia kinga na hapo yeye naye nitamuita fisadi. Na hilo mimi sina haya nalo na hata Mengi akigeuka na kuwatetea wezi wa nchi yetu na yeye ataitwa fisadi na atakuwa amechagua upande wa dhulma.

Kwi kwi kwi kwi Mwanakijiji inawezekana tunatofautiana maana ya neno kutetea au kuwatafutia kinga mafisadi. Kwangu mimi JK kuwa mshirika hawa jamaa na kukaa kimya ni kuwatetea na kuwakingia kifua basi na yeye ameshachagua upande wa dhulma. Na kwa Mengi kumsifia kaenda upande huo huo.


Sasa na wewe bosi wako Rostam kuguswa ndiyo imekuwa vurugu sasa?

Usanii wa kwangu au wa kwako; huwezi kunichagulia kitu chochote ambacho mwenyewe sijakichagua. Huna nguvu hiyo wala nafasi hiyo. Na mimi sina kwa upande wako. Chukua msimamo unaouona unafaa na uusimamie; si lazima wote tuone jambo moja sawasawa kama maroboti.


Sawa hapo umesema, lazima watu tuwa na mawazo tofauti maana sisi siyo maroboti. Kwa hiyo wakati wewe unamwona Mengi kama shujaa wako mimi namwona kama msanii mwingine tu kama walivyo akina Rostam anaowasema. Kwa hiyo let us agree to disagree. I rest my case Mkuu
 
Wewe ndiyo unaonekana hujui unachoongea nenda kasome sheria za masoko ya mitaji au hisa uone kama hicho unachosema kinaruhusiwa. Kama siyo usanii ambao unaendelea kuwaibia watanzia.

Lazima tukubali wakati kuna watu wanajitangaza kuwa ni majemadari wa kupambana na ufisadi ni lazima tuwamulike vizuri nao

huko kunaitwa una invest kwenye start up company
ni sawa sawa na ku invest kwenye research , kama hizo kampuni za exploration huko songo songo hazijaanza kuvuna lakini ziko kwenye stock exchange kubwa tena sio hiyo ya bongo ya kampuni kumi

ni sawa sawa na kununua nyumba kabla haijajengwa
mwizi ni yule aliyechukua mkopo kwa kampuni ya mfukuoni ya kuzalisha umeme na akawa guranteeed na serikali
 
[/COLOR][/COLOR]

Sawa hapo umesema, lazima watu tuwa na mawazo tofauti maana sisi siyo maroboti. Kwa hiyo wakati wewe unamwona Mengi kama shujaa wako mimi namwona kama msanii mwingine tu kama walivyo akina Rostam anaowasema. Kwa hiyo let us agree to disagree. I rest my case Mkuu

bila ya shaka; na wewe unayo haki ya kukwepa kuwagusa kina Rostam na wenzako kwa sababu wanatajwa na Mengi. Sawa tukubaliane kutokubaliana. I rest my case too.
 
Mimi nadhani Mengi ajiandae kujilinda (Self defence)...kwani anapambana na watu ambao wana mtandao mkuubwa kama ni Italia basi ni Mafia... Ni hayo tu...
 
Mengi anaweza kuwa na nia njema ya kupambana UFISADI,lakini mbona MENGI anakuwa mbaguzi kiasi hiki?Ubaguzi nao ni aina ya UFISADI.
Nasema baba yangu MENGI ni mbaguzi kwa sababu kwenye taarifa yake amesema MAFISADI wanaoitafuna nchi hawazidi kumi na kwa msisitizo akawataja walau watano,kati yao hakuna MTANZANIA KWA ASILI.JE KWANINI ASITAJE MASIFISADI WOTE ILI KUJUA KAMA WOTE SI WAZAWA WAFUTWE URAIA ?AU KUNA MASWAHIBA WAKE WAZAWA AMBAO ANASHIRIKIANA NAO KUFISADI NCHI?
Ushauri kwa baba MENGI,JIWEKE UPANDE SALAMA KWA KUWATAJA WOTE UNAOAMINI NI MAFISADI WANAOIFILISI NCHI AMBAO UNASEMA HAWAZIDI KUMI.

Mkuu, mbona unaonekana una jazba wakati hoja unayojenga haina mashiko? ... Unasema Mengi kasema Mafisadi hawazidi kumi na akataja watano, sasa tatizo liko wapi hapo?, Kutozidi kumi maana yake ni mtu mmoja mpaka watu tisa. Tano ipo chini ya kumi, mi nilidhani Mengi kasema Mafisadi wakubwa wanazidi kumi halafu akataja watano, hapo pengine hoja yako ya ubaguzi ingejijengea uhalali.
 
Mkuu, mbona unaonekana una jazba wakati hoja unayojenga haina mashiko? ... Unasema Mengi kasema Mafisadi hawazidi kumi na akataja watano, sasa tatizo liko wapi hapo?, Kutozidi kumi maana yake ni mtu mmoja mpaka watu tisa. Tano ipo chini ya kumi, mi nilidhani Mengi kasema Mafisadi wakubwa wanazidi kumi halafu akataja watano, hapo pengine hoja yako ya ubaguzi ingejijengea uhalali.


sijui aliyetoa madai ya ufisadi anataka kusema kuwa ili ufisadi uwe kweli ufisadi basi ni lazima utaje na Watanzania weusi wawili watatu! Haya mawazo nadhani yana kila dalili ya kujiona duni
 
sijui aliyetoa madai ya ufisadi anataka kusema kuwa ili ufisadi uwe kweli ufisadi basi ni lazima utaje na Watanzania weusi wawili watatu! Haya mawazo nadhani yana kila dalili ya kujiona duni

Sisi wahehe tunamsemo "navalonge swela" Mradi tu ukweli umeongelewa. Ki ukweli hao ndiyo billionaires of Tanzania happen to be of either Asian and Arab decent and evidently their means of accumulating wealth has come to question lately. Now, if they had other dudes of other decent as their partners in crime then thats another case. I am ready to rally behind all the people who are against corrupt leaders.
 
Enough already !! No more talking, Mafisadi papa mmetajiwa tayari, watu safi wanajulikana, wachafu wanajulikana. Sasa mtafanya nini ?Mnataka nini cha zaidi? If you people are serious, kuna sheria ya kufungua mashitaka binafsi, twendeni tukafungue kesi. Issue ya Manji na yale magodown ni wazi sana......tuanze na hiyo. Kama nyie kweli mnaipenda TZ anzeni kujadili taratibu za kufungua kesi. Otherwise enough already !!
 
Enough already !! No more talking, Mafisadi papa mmetajiwa tayari, watu safi wanajulikana, wachafu wanajulikana. Sasa mtafanya nini ?Mnataka nini cha zaidi? If you people are serious, kuna sheria ya kufungua mashitaka binafsi, twendeni tukafungue kesi. Issue ya Manji na yale magodown ni wazi sana......tuanze na hiyo. Kama nyie kweli mnaipenda TZ anzeni kujadili taratibu za kufungua kesi. Otherwise enough already !!

Tupo pamoja mkuu, if anything kwa issue hii nadhani mengi yupo vitani na mwamko wa mtanzania na sio hawa so called mafisadi....hawa wakina manji, rostam na patels sio mafia kama most of us like to think..mali zao dubai, london, geneva hazijafichika kihivyo..serikali ya tanzania ni uamuzi tuu na msimamo...watanzania tuache uoga na njaa jamani..recession hii nchi nyingi zimekuwa patriotic..mwingereza hadi taxes kwa matajiri kaongeza ili kulinda uchumi..mafisadi wa kirusi wataanza kupungua sasa..sisi tupo busy kusifia watu walioshikilia uchumi wa nchi mkononi mwao...list ya kitine former usalama na aliyosema mengi hamna tofauti..ni watu hao hao.

UCHAGUZI MWAKANI TUFANYE MABADILIKO.
 
Sema Mengi Sema! Wala usiogope na Watanzania wengi tuko bega kwa bega nawe na tunaunga mkono kauli yako yenye ukweli mtupu.

Date::4/23/2009
Mfanyabiashara maarufu Reginald Mengi ajitoa mhanga kwa mafisadi

Boniface Meena na Mkinga Mkinga

Mwananchi

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Reginald Mengi jana aliamua kujitoa muhanga alipotangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia ambao anadai kuwa ni mafisadi papa wanaoiba mabilioni ya fedha za wananchi na kutaka wachukuliwe hatua kwa madai kuwa wataiyumbisha na kuitingisha nchi.

Kati ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi, wawili wamefunguliwa mashtaka ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), wengine wakiwa wameshatajwa kwenye kashfa mbalimbali, zikiwemo za zabuni ya utoaji umeme wa dharura ya Richmond Development na uuzwaji wa jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye anamiliki kampuni ya IPP yenye kampuni mbalimbali zikiwemo za habari na vinywaji, alitaja wafanyabiashara hao watano akisema kuwa ndio papa kwa ufisadi lakini akasema idadi ya mafisadi wanaofilisi nchi hawazidi 10.

"Wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa hapa nchini zikiwepo kashfa za Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, Bahati Nasibu ya Taifa, mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na kadhalika," alidai Mengi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya kwenye ofisi yake jijini Dar es salaam.

Kati ya wafanyabiashara hao watano ambao Mengi alidai ni mapapa wa ufisadi, wamo Rostam Aziz, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel), ambao Mwananchi ilipata nafasi ya kuzungumza nao kuhusu tuhuma hizo za Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakuwa tayari kutoa vielelezo kuthibitisha madai yake, lakini akasema iwapo watamshtaki mahakamani na wafanye hivyo kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.

Mengi alirusha tuhuma nyingi kwa watu hao ambao alidai kuwa wamecharuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamua kupambana nao na hivyo wameamua kupambana na yeyote anayemsaidia mkuu huyo wa nchi katika vita hiyo.

"Jitihada kubwa za Mhe. Rais za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania zinazoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa. Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umaskini mkubwa; hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi," alidai Mengi ambaye pia alitoa taarifa ya maandishi aliyoisaini.

"Cha kusikitisha ni kuwa pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umasikini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda. Wanapinga kwa kuwa wanataka Watanzania wafe na njaa na matatizo mengine."

Mengi alikwenda mbali zaidi na kudai mafisadi anaowatuhumu wanaweza wakaunga mkono matatizo yanayotokana na Deci, taasisi inayoendesha mchezo wa kuchangisha fedha na kulipa maradufu na Watanzania kubakia "wakifukuzana na wachungaji bila ya kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu".


Wakiongea na Mwananchi, watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi hawakutaka kujibu kwa kirefu na badala yake walimtuhumu mwenyekiti huyo mtendaji wa IPP kuwa ana wivu, fitina chuki na ambaye ameshindwa kuendesha nyumba na biashara zake, huku mwingine akieleza kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia ya kutoa maoni yake.

"Mengi... (si mstaarabu)," alisema Manji ambaye anamiliki kampuni ya Quality Group. " Biashara zake zimemshinda ndio maana anazungumza ovyo."

Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga anayejishughulisha na biashara mbalimbali za miradi mikubwa ya ujenzi, uchimbaji na habari, alimuelezea Mengi kama mtu ambaye analingana kwa umri na baba yake mzazi na hivyo hawezi kubishana naye.

Lakini akasema: "Mengi amejaa chuki, wivu na fitina. Sina cha kumsaidia isipokuwa kumuombea Mungu ili amsaidie kwa kumpuuzia hayo maana ni adhabu kwa nafsi yake mwenyewe. Kwa malezi niliyopata, siwezi kubishana na mzee."

Jeetu Patel naye alisema haoni busara kujibizana na Mengi na kwamba alichofanya mwenyekiti huyo wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda (CTI) ni kutumia haki yake ya kidemokrasia ya uhuru wa kuongea.

"Hayo ni matatizo yake," alisema Patel, ambaye anakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha za EPA. "Amewaita waandishi kuzungumza nao... sikumsikia lakini ninachoweza kusema ni kwamba anatumia uhuru wake wa kujieleza.

"Binafsi sijui chochote kuhusu hizo tuhuma za Mengi dhidi yangu, ila anayo haki ya kusema chochote. Nina mambo mengi ya kufanya hivyo sioni kama itanisaidia kwenye biashara zangu za kila siku kuanza majibizano na Mengi."

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mengi alidai kuwa watu hao aliowataja si tu kwamba wanaiba rasilimali za Tanzania, bali pia wanaiba muda wa Watanzania.

"Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo, tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao na hawatingishiki," alidai Mengi. "Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa.

"Hata sasa hivi, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi yetu kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao.

Alisema ni muhimu wananchi wakajiuliza hawa mafisadi wanapata wapi ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kutukana na kunyanyasa watu.

Alisema mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji wa ufisadi watapata madhara kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, wananchi wa Tanzania watawawajibisha.

"Ni lazima Watanzania wote tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha," alidai Mengi.

 
Mimi nadhani Mengi ajiandae kujilinda (Self defence)...kwani anapambana na watu ambao wana mtandao mkuubwa kama ni Italia basi ni Mafia... Ni hayo tu...

Wakiamua kumdhuru Mengi kwa lolote lile basi na wao hawatakaa kwa salama, kwa sababu anayoyasema Mengi ni kweli tupu na yanaungwa mkono na Watanzania wengi kwamba ufisadi mkubwa unaofanywa na Wahindi wakishirikiana na Viongozi mafisadi ndiyo unaiangamiza nchi yetu na kamwe kutamka hivyo si ubaguzi wa rangi. Watu wamenyamaza kwa muda mrefu sasa wamechoka maana kiongozi wa nchi tuliye naye tumeshaambiwa "hahusiki kabisa"
 
Back
Top Bottom