Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Wana Bodi
Jumanne jioni 19/6/2012 katika mjadala wa bajeti, Mbunge wa Viti Maalum, Chadema aitwaye Conchesta Rwamlaza amenivunja mbavu. Katika hali ya kujiamini sana, alidai kuwa serikali hii kila mwaka inaleta bajeti ya mamilioni ya kununua viti vipya. Akaendelea kusema kuwa, amekuwa bungeni akikalia kiti kile kile na wala hakijaharibika. Ndipo akahoji, "KWANI HAWA WATU WA SERIKALI, MAKALIO YAO YANA MISUMENO?"
Piga picha mwanabodi, ufikirie makalio (masaburi) yenye msumeno, ambayo kila yakikalia kiti kinachanwa na huo msumeno!
Pamoja na kwamba hii ni lugha ya picha, lakini kimsingi, watu wa serikali yetu wana misumeno vinywani mwao na mifukoni mwao kwa sababu kasi ya kutafuna fedha ya serikali sawa na kasi ya msumeno unaokata mbao.
Ahsante sana kamanda Rwamlaza.
Jumanne jioni 19/6/2012 katika mjadala wa bajeti, Mbunge wa Viti Maalum, Chadema aitwaye Conchesta Rwamlaza amenivunja mbavu. Katika hali ya kujiamini sana, alidai kuwa serikali hii kila mwaka inaleta bajeti ya mamilioni ya kununua viti vipya. Akaendelea kusema kuwa, amekuwa bungeni akikalia kiti kile kile na wala hakijaharibika. Ndipo akahoji, "KWANI HAWA WATU WA SERIKALI, MAKALIO YAO YANA MISUMENO?"
Piga picha mwanabodi, ufikirie makalio (masaburi) yenye msumeno, ambayo kila yakikalia kiti kinachanwa na huo msumeno!
Pamoja na kwamba hii ni lugha ya picha, lakini kimsingi, watu wa serikali yetu wana misumeno vinywani mwao na mifukoni mwao kwa sababu kasi ya kutafuna fedha ya serikali sawa na kasi ya msumeno unaokata mbao.
Ahsante sana kamanda Rwamlaza.