AUGUSTINO CHIWINGA
JF-Expert Member
- Apr 23, 2017
- 220
- 689
Leo tarehe 1/6/2018 nikiwa katika Jiji la Mbeya nimekutana na kijana aliyenitajia jina moja la David ambaye anafanya biashara ya usafirishaji maarufu kwa jina la Bodaboda.
Alinisafirisha kutoka eneo la Soko Matola mpaka Sangu.
Tukiwa njiani tulifanya mazungumzo mbalimbali,David akataka kusikia maoni yangu kuhusu Rais MAGUFULI,nikamuambia Rais MAGUFULI anafanya kazi ngumu ya kung'oa kupe wanaomnyonya Ng'ombe.
Rais MAGUFULI ana taka Ng'ombe asiwe na kupe ili atoe maziwa yatakayotutesheleza watu wote tunywe mpaka tusaze.
Hata hivyo kazi ya kung'oa kupe hao sio rahisi, tuzidi kumuombea. Ni kiongozi mwenye maono anayetaka wote tunufaike na raslimali zilizopo ataifikisha nchi hii pazuri.
Akakaa kimya akatikisa kichwa, kisha akanitwika swali jingine, "mbona Mbunge wetu walimfunga"
Nikamjibu Mbunge wenu alifungwa kutokana na kutoa matamshi ya matusi, nikazidi kumuambia kwamba Mbunge wenu hatimizi majukumu yake hivyo anafanya vurugu na fujo ili nyinyi mumuone kama anafanya kazi kumbe hafanyi kitu.
Nikamuambia msikae vijiweni mkadanganyana kuwa Mbunge wenu alifungwa kwa kuonewa sio kweli.
Hata hivyo Rais MAGUFULI ni muungwana sana akaamua kumtoa kwa msamaha siku ya Muungano naamini atakuwa ameshajifunza kwamba siasa bila matusi inawezekana.
Nikaendelea kumuambia Rafiki yangu huyu kwamba CCM inawajali na kuwathamini vijana wa Jiji la Mbeya na ndio maana imetoa fursa ya vijana wa Mbeya kusoma mafunzo ya ufundi bure, Katibu wa Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole alipofanya ziara Jijini hapa mnamo mwezi wa February mwaka huu alitoa ahadi hiyo na tayari imeshaanza kutekelezwa, nikamgeukia yeye nikamuuliza je ameshawahi kusikia juu ya fursa hiyo?
Akanijibu ndio lakini hakuwa na taarifa kamili, nikamuambia aache kufuatilia masuala ya CHADEMA kwani hayatamsaidia katika maisha yake bali aanze kutafuta taarifa sahihi za CCM na Serikali ndizo zitakazomsaidia kwani fursa nyingi kama mikopo na mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana.
Nikaendela kumuambia kwamba sasa hivi awamu ya 5 Boda Boda na machinga wa Mbeya mnafanya biashara zenu kwa Uhuru bila bughudha; Rais MAGUFULI anawalinda msiweze kuonewa ili mpate riziki zenu kwa halali na kwa amani kabisa. Kama kina Sugu na wapinzani wenzie wanaona huo ndio udikteta basi ni udikteta mzuri.
Kutahamaki nikawa nimeshafika Sangu na rafiki yangu David akaishia kuniomba namba ya simu na kuniahidi anaenda kuichoma kadi yake ya Chadema kwani sio chama chenye agenda ya kumkomboa kijana bali kumtumia kama karatasi ya plastiki na kisha kumtupa.
Alinisafirisha kutoka eneo la Soko Matola mpaka Sangu.
Tukiwa njiani tulifanya mazungumzo mbalimbali,David akataka kusikia maoni yangu kuhusu Rais MAGUFULI,nikamuambia Rais MAGUFULI anafanya kazi ngumu ya kung'oa kupe wanaomnyonya Ng'ombe.
Rais MAGUFULI ana taka Ng'ombe asiwe na kupe ili atoe maziwa yatakayotutesheleza watu wote tunywe mpaka tusaze.
Hata hivyo kazi ya kung'oa kupe hao sio rahisi, tuzidi kumuombea. Ni kiongozi mwenye maono anayetaka wote tunufaike na raslimali zilizopo ataifikisha nchi hii pazuri.
Akakaa kimya akatikisa kichwa, kisha akanitwika swali jingine, "mbona Mbunge wetu walimfunga"
Nikamjibu Mbunge wenu alifungwa kutokana na kutoa matamshi ya matusi, nikazidi kumuambia kwamba Mbunge wenu hatimizi majukumu yake hivyo anafanya vurugu na fujo ili nyinyi mumuone kama anafanya kazi kumbe hafanyi kitu.
Nikamuambia msikae vijiweni mkadanganyana kuwa Mbunge wenu alifungwa kwa kuonewa sio kweli.
Hata hivyo Rais MAGUFULI ni muungwana sana akaamua kumtoa kwa msamaha siku ya Muungano naamini atakuwa ameshajifunza kwamba siasa bila matusi inawezekana.
Nikaendelea kumuambia Rafiki yangu huyu kwamba CCM inawajali na kuwathamini vijana wa Jiji la Mbeya na ndio maana imetoa fursa ya vijana wa Mbeya kusoma mafunzo ya ufundi bure, Katibu wa Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole alipofanya ziara Jijini hapa mnamo mwezi wa February mwaka huu alitoa ahadi hiyo na tayari imeshaanza kutekelezwa, nikamgeukia yeye nikamuuliza je ameshawahi kusikia juu ya fursa hiyo?
Akanijibu ndio lakini hakuwa na taarifa kamili, nikamuambia aache kufuatilia masuala ya CHADEMA kwani hayatamsaidia katika maisha yake bali aanze kutafuta taarifa sahihi za CCM na Serikali ndizo zitakazomsaidia kwani fursa nyingi kama mikopo na mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana.
Nikaendela kumuambia kwamba sasa hivi awamu ya 5 Boda Boda na machinga wa Mbeya mnafanya biashara zenu kwa Uhuru bila bughudha; Rais MAGUFULI anawalinda msiweze kuonewa ili mpate riziki zenu kwa halali na kwa amani kabisa. Kama kina Sugu na wapinzani wenzie wanaona huo ndio udikteta basi ni udikteta mzuri.
Kutahamaki nikawa nimeshafika Sangu na rafiki yangu David akaishia kuniomba namba ya simu na kuniahidi anaenda kuichoma kadi yake ya Chadema kwani sio chama chenye agenda ya kumkomboa kijana bali kumtumia kama karatasi ya plastiki na kisha kumtupa.