KilazaHata Idd Amin hakuangushwa madarakani na wanajeshi wa Tanzania bali aliangushwa na wanajeshi wake ambao walijiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
CHADEMA itaangushwa na wanachama na viongozi wake wanaokihama chama na kujiunga na vyama vingine.
Siasa za chama Kikuu cha Upinzani nchini zina muda wa uhai kama ilivyokuwa kwa NCCR-Mageuzi na CUF.
Hata vyama vya NCCR-Mageuzi na CUF vilipoanza kupukutika, kuna viongozi wao waliojitokeza na kupiga bla bla huku wakiukataa ukweli kama anavyofanya Tundu Lissu.
Maelezo ya Tundu Lissu yanasadifu ukweli unaosemwa kuwa CHADEMA ni chama cha Mbowe. Yaani chama kinamwagiza Mbowe akakope popote kwa mtu yeyote halafu baada ya kukopa hawaambii amekopa wapi na kiasi gani bali anachowaambia ni kiasi anachotaka walipe. Gosh!
Maisha ya CHADEMA kama chama kikuu cha Upinzani yako ukingoni.
Waingereza wana msemo usemao, ''Beware the last kicks of a dying horse''.
Swali la kujiuliza kwa sasa ni hili, Baada ya Uchaguzi Mkuu 2020, Chama gani kitakuwa ni chama kikuu cha upinzani baada ya CHADEMA?