Maji yameingiliwa na Mdudu!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
[h=3]Zingatia Haya![/h]

Kumpata mwenza au mke au mume ambaye utaishi naye maisha yako yaliyobaki hapa duniani ni jambo la msingi sana katika maisha ya binadamu.

Na kwa kupenda wenyewe hupelekana hadi kwa viongozi wa dini na kutangaza hadharani kwamba mimi na mwenzangu tunataka kuwa mke na mume na ulimwengu ujue.
Huwa tunakuwa tumejawa na mioyo yenye furaha na kutaka siku ifike upesi ili nianza kuishi na mwenzangu haraka iwezekanavyo.

Mungu bariki mioyo ya maharusi wapya maana hawajui kazi halisi wwanayoenda kuianza kazi halisi (real life) na kuachana na maisha ya uchumba ambayo mengi ni tambarare kama nyikani.
Baada ya honeymoon tu wengine siku ya pili tu, wengine mwezi wa kwanza tu na wengine mwaka wa kwanza tu wa ndoa huanza kujiuliza hili swali;
Lakini hakuna aliyeniambia itakuwa kama hivi?

Alikuwa anaacha mialiko ya watu kwa ajili yako lakini baada ya kukuoa si hivyo tena, unadhani kwa kuwa alikuwa ana cancel mialiko ya kwenda kufanya mambo yake kwa ajili yako kabla hamjaona na mkioana itakuwa the same?
You are wrong!

Ili usipoteze matarajio ya mahusiano yako ya ndoa jaribu kuzingatia mambo yafuatayo (kama unategemea kuoa au kuolewa please print na kafiche haya unaenda kuyasoma na baada ya kuanza ndoa soma tena na pia ukiyaweka moyoni na ukizingatia utakuwa candidate mzuri sana)

Hakuna binadamu anaweza kutimiza mahitaji yako yote:
Mtu ambaye anaweza kutimiza mahitaji yako yote ni BWANA, na ilimpasa kufa ili aweze kukutimizia yote.
Usitegemee ndoa au uliyeoana naye atakutimizia mahitaji yako yote au ahadi zake zote alizoahidi kabla hamjaoana.

Kiwango cha mapenzi hakiwezi kuwa juu kama ilivyo mwanzo wa ndoa.
Jinsi anavyokwambia ‘I love you” huweza kupungua hadi ukashangaa kadri ziku zinaenda ingawa neno “I love u” huleta raha sana kwa mwanamke akisikia kutoka kwa mumewe hata hivyo siku zinavyoenda mwanaume hujisahau na kuanza kula jiwe kusema " I love u"
je, utadai?
Pia wanawake nao (wachache sana) akishazaa huanza kujisahau na kujiona mama na si mrembo bado. Huku ni kukosa ustaarabu na kinyume cha maadali.
shame on you!

Mwanaume anaweza kuwa anakupenda mno lakini bado hatajua unahitaji kitu gani.
Wanawake wengi huja na sentensi ‘ Kama ananipenda angefanya kile napenda afanye” kumbuka usiposema na kumwambia ujue hawezi kujua unataka kitu gani au nini kinakusumbua.
If you don’t ask the answer is NO.
Men read newspapers not minds!

Si mara zote uliyeoana naye atapenda kuimarisha mahusiano.
Katika mazingira ya kawaida wanawake hupenda hata kuimarisha kitu kizuri (mfano ndoa ambayo hata haina mgogoro) hata hivyo wanaume wana msemo wao
“If it is not broken, don’t fix it”
Hivyo tumia hekima na kuomba Mungu ili Mungu awape moyo wa umoja na juhudi ya kuishi kwa amani.

Ndoa haiwezi kukufanya uwe umekamilika.
Si mara zote ukiongeza nusu na nusu unapata kitu kizima.
Wengi ambao ni ‘Single’ hudhani wakioa au kuolewa watakamilika na kujiona complete na kuwa na furaha ya kweli.
Na wengine hufika mbali zaidi kwa kujinyima vacation, kununua vitu vizuri wakisubiri kufanya hivyo wakioa au kuolewa.
Unapoteza muda wako anza kukamilika kwanza kabla ya kuolewa au kuoa na ingia ukiwa si tegemezi kwamba mwenzako atakukamilisha hadi kukupa furaha.
Ndoa ni kuunganisha strength na ku-balance weakness siyo kukaa tu kutegemea mwenzako akukamilishie furaha yako.

Usitegemee kufanya kila kitu pamoja
Kufanya kazi pamoja, kupanga mipango pamoja, kuweka malengo pamoja ni suala zuri sana hata hivyo kila mmoja huhitaji breathing room.
Usitegemee kila kile unapenda basi na mwenzio atakuwa excited nacho si kweli hivyo kuna wakati utahitaji kuwa mwenye na yeye kuwa mwenyewe.
Nakwambia mapema ili siku ikifika usiseme hakuna aliyeniambia, mimi nimekwambia!

Mtu ambaye anaweza kumbadilisha ni yeye mwenyewe si wewe.
Kama unategemea ukioa au kuolewa utambadilisha (change) mpenzi wako basi utakuwa very much disappointed.
Kama kuna vitu vinasumbua kwa mpenzi wako kabla humjaona viangalia vizuri, kutegemea kwamba utamsaidia kubadilika baada ya honeymoon ni kujidanganya kulikokithiri.
Ndoa si mahali pa kulaumiana, kukefyakefya (nagging), hasira na kukosoana.
Kama mpenzi wako hajui UCHAFU ni kitu gani hakikisha anafahamu kabla hamjaoana, na kama unategemea utambadilisha aache ulevi, kuvuta sigara, kuwa mwongo nk shauri yako!

Maswali ya kujadili
Wewe ambaye upo kwenye ndoa sasa je, unaona maratajio yako yote ya ndoa yalitimia?
Je, una matarajio yoyote ambayo unahisi yalikusumbua zaidi?
Je, una ushauri gani kwa wanandoa wapya?
 
[h=3]Coolidge Effect[/h]

Panya dume huwa tayari kwa sex muda wowote kama binadamu mwanaume na panya jike huhitaji mood kuwa sawa ili kujihusisha na sex kama binadamu mwanamke.
Panya jike akiwa akiwa anajisikia vizuri huwa hana shida wakati panya dume akimsogelea kwa ajili ya sex huupeleka mkia wake pembeni kumrahisishia panya dume kumuingilia bila wasiwasi, hata hivyo baada ya dakika chache tu (maskini panya dume) huishiwa nguvu kabisa kwa kuchoka na tendo hilo (mating).
Huku panya jike akiwa bado hajachoka na anahitaji panya dume huwa amelala kama vile amepooza na hutoa mlio kama wa filimbi (mluzi) ambao huashiria kwamba ondoka nimechoka, basi panya jike huridhika, hujivuta na kuondoka kukaa mbali na panya dume ambalo linaugulia uchovu wa sex.

Kitu cha kushangaza ni kwamba akija panya jike mwingine na awe tayari kwa sex, panya dume yuleyule aliyekuwa choka mbaya haijalishi alikuwa amechoka namna gani ataanza sex upya na panya jike mpya na baada ya in and out mara tatu tu anakuwa hoi bin taabani kwamba hawezi tena kuendelea, hata hivyo ukimleta kike mwingine ataendelea na kitendo chake cha kuchangamkia hadi unaweza kumpoteza kwa kufia mwilini mwa panya jike wapya!
Hii huitwa Coolidge Effect, jina ambalo linatokana na rais wa Marekani ambaye wakati wake aliwahi kutembelea shamba la Kuku, na mke wa rais alipata muda kuongea na mtunza shamba ambaye alimwambia tuna huyu jogoo ambaye huwapanda tetea hata elfumoja kwa siku.

Na mke wa rais alimuomba mtunza shamba kumwambia rais (mumewe) hicho kisa hata hivyo huyu rais aliuliza
"je, jogoo huyo humpanda tetea mmoja?"
Na mtunza shamba akasema "hapana," huwapanda tetea tofauti.

Tabia kama hii imeonekana kwa wanyama (males) na kwamba wakati mwingine imeleta shida kidogo.

Pia imejulikana kwamba baadhi ya wanaume huwa jogoo hawiki wakiwa na wake zao ila akifanya cheating jogoo wake huwika kama si yeye.
Wapo mabinti ambao bada ya kupata wachumba wakaamua kufanya nao mapenzi hata kabla ya ndoa na baada ya moja, mbili, tatu na nne siku ameachwa kwenye mataa maana mchumba kapata binti mwingine.
Hata hivyo Binadamu ni tofauti na wanyama wengine, yeye anaongozwa kwa ufahamu, malezi, taratibu za maisha, dini nk,

Pia jambo la msingi kufahamu ni kwamba Mungu ndiye aliyefanya ubunifu wa binadamu kuwa na sex, si binadamu ambao wameumba sex; hivyo Mungu ndiye mwenye uwezo wa maamuzi yoyote tunayojisikia kuhusu miili yetu kuhusu sex na yeye ndiye mwenye blue print halisi ya sex iweje na si hilo tu bali ukipata matatizo yanayohusiana na mahusiano, ndoa, mapenzi nk yeye ndiye anaweza kutupa majibu ya kudumu.

 
[h=3]Maji yameingiliwa na Mdudu![/h]
CHIMBA KISIMA CHAKO MWENYEWE
By Faustin Munishi:

Uchimbe kisima wewe mwenyewe unywe maji yako peke yako na usiyashiriki nao wengine ni hatari kubwa eeh!
Maji ya kisima cha watu wengi yameingiliwa na mdudu ukiwa na kiu usiyaonje utaambukizwa eeh.
Na kiu ya maji imeongezeka watu wanayanywa kila wakati na yanauzwa kote barabarani nani atapona eeh?
Kwa sababu maji yana mdudu yanapatikana kirahisi ukipita kote utayaona wacha kuyachota eeh.​






Ukiwa na njaa ni ya chakula huwa ni vigumu upatiwe lakini sigara na hata pombe watakupatia eeh.
Unajua kwa nini?
kwa sababu pombe na sigara zinaua wanataka na wewe ufe na wao wanakupatia eeh.
Tena na siku hizi na hayo maji yaliyo yaliyoingiwa na mdudu utapewa bure bila kuomba ili mfe wote eeh.​
Yapo kwenye chupa kubwa na ndogo watu wanazipenda zile ndogo wanafikiliria zipo salama wamedanganyika eeh.
Wanazifunika nusunusu wamefanya hivyo makusudu ili waamushe kiu ya maji usidanganyjike eeh!

Ndugu jihadhari na maji ya rahisi kachimbe kisima wewe mwenyewe ukiwa na kiu uyanywe maji uliypoyachimba heri.
Dawa ya mdudu hawajaipata wanaitafuta kotekote umwamini Yesu akuokoea amalize kiu

Unaweza kusikiliza wimbo hapa chini
 
[h=3]Epuka Makosa Haya![/h]

Hutaki kuanza.
Tatizo kubwa na sugu la wanawake wengi ni kitendo cha kutoanzisha kwamba anataka sex na mume wake (initiating) na kumwachia mwanaume kama wajibu wake katika ndoa.
Je ina maana hakuna siku unakuwa umemtamani mume wako na ukaamua wewe kuanza?

Kushindwa kuanzisha kwamba unahitaji sex ni biggest mistake wanawake wengi wanfanya kwani wanaume wengi hujiona kama si sahihi (disequillibrium) katika kuimarisha mahusiano kama kila siku ni mwanaume tu ndo anachokoza.
Kimsingi hata mwanaume anajisikia vizuri pale mke wake anapolianzisha kwamba na yeye anataka.

Je, ni kueleza kwamba wanaume tunakuwa na interest kubwa wa sex na wanawake hawana au huwa hawapendi siku zote.
Naamini kuna wanawake ambao nao wanapenda sex kama wanaume.
Ni vizuri mwanamke kuonesha interest kwa kuchukua hatua kusema kila unapenda kwa mumeo na kwamba leo unamtamani na kumuhitaji siyo kila siku yeye tu miezi 12 na siku 365 na robo naamini mumeo akiona juhudi yako ya kulianzisha atafurahi na kukupa appreciation kubwa na unaweza kupata level upya ya satisfaction.
Hivyo kama wewe ni mwanamke anza leo.

Wasiwasi kwamba mwili wako upoje:
Kufikiria jinsi mwili unavyoonekana kwa mume wako na kuwa na wasiwasi kwamba anaweza kukuona labda mnene sana (fat zimejaa vipande vipande), au matiti makubwa sana au madogo sana au makeup ulizoweka usoni na mtindo wako wa nywele kichwani au sijui sehemu zingine zina rangi ipoje husababisha ushindwe ku-enjoy tendo la ndoa na mara nyingi unaweza kuharibu kila kitu hadi ushindwe kufika kileleni.

Jambo la msingi ukishakuwa na mumeo ni kuwa na total concentration kwa tendo lenyewe kwa raha zako zote.
Wanaume hufurahia mwanamke ambaye anajiamini na mwili wake na jinsi alivyo na anahusika mia kwa mia katika furaha ya tendo la ndoa na si kuwa na hofu na kujipiga kufuli kihisia.​
 
[h=3]Je, ni Skills tu?[/h] Hata kama skills ni jambo la msingi sana katika sex, kuwa na moyo ulio wazi na hamu ya kujikabidhi kwa mume wako au mke wako husaidia kuwa na uzoefu wa sex inayokupa ridhiko zaidi.
Hata hivyo njia bora ya kujifunza au kutojifunza ni actions; kumbuka mwili wako ni uhuru wako na upo responsible ni kitu cha lazima au hiari na unaweza kuupa uhuru mwili wako kwa kufanya Yafuatayo

KWANZA
Husika na mwili wako. Usikilize unakwambia kitu gani hasa jinsi unavyojisikia na nini unataka na unachohitaji ili kufanya kazi katika kiwango chake cha juu. Upe chakula kizuri, muda wa kupumzika, mazoezi kiasi cha kutosha na milango ya fahamu iliyo imara.

PILI
Uwe mwepesi kutambua message negative kuhusu mwili wako hasa zile ambazo wengine wanakwambia na zile wewe unawapa wengine.
Hakikisha unafanya replacement na positive messages kwa mwili wako na wengine.

TATU
Ukiwa na mpenzi wako hakikisha unampa mguso wa mwili (touch) ulio mwororo na caring.

NNE
Badilisha mtazamo wako kuhusu sex kutoka kufanya na kufika kileleni (performance and orgasm) na kuwa kupeana raha na kuunganishwa (pleasure and union)
 
[h=3]
YAANI BE BLESSED

Siri ya Kuvutia.....
[/h]
SIRI YA KUMVUTIA MUME MUDA WOTE:
Ni kweli upo kwenye mahusiano na katika mahusiano yako mwanaume uliyenaye ni wa uhakika, safi kabisa na hongera sana.
hata hivyo linakuja wazo kwamba hivi inawezekana huyu mwanaume akaendelea kunipenda kama hivi?
Je, atakuwa yupo interested na mimi muda wote?


Haijalishi mnapendana kiasi gani ukweli ni kwamba mahusiano huhitaji kazi, huhitaji efforts, inahitaji kuwekeza jitihada kidogo ili kuvuna mambo makubwa.
Kama unapenda mume uliyenaye awe anavutiwa na wewe wakati wote kuna tips na siri nyingi unahitaji kuzifahamu vingenevyo unaweza kujikutana anakukwepa na kukuona huna lolote (huna jipya, unachosha)

Jambo la kwanza ni kweli mahusiano ni kitu cha ajabu sana huweza kupanda na kushuka kwa kiwango cha kutisha hata hivyo siri kubwa ya mahusiano unatakiwa usiwe mtu ambaye mpenzi wako anaweza kujua au kutabiri au kutarajia mara zote utasema nini au utafanya kitu gani, unahitaji kuwa na vitu vizuri ambavyo hawezi kutegemea, waingereza wanaita unakuwa spontaneous and fun na unakuwa na adventure ambazo hategemei.

Hakuna kitu mwanaume hapendi kama mwanamke aliye na usumbufu wa uhitaji (too needy). Kumtaka mume kila kitu hadi anajiona usumbufu huweza kuua mwanamke kumvutia mwanaume, ninachozungumzia hapa si ile hali ya kuonesha unamuhitaji bali ile hali inayoonesha unasumbua kwani hata kile ambacho kipo kwenye uwezo wako bado unataka mume akutimizie.
Kama anataka kutoka na rafike zake wa kiume mruhusu siyo kulalamika tu hadi anajiona mkosaji.
Kwani ukimruhusu naye akaenda kufurahi na rafiki zake na wewe ukatumia muda huo na rafiki zako kuna tatizo gani, wewe unataka kumganda all the time hadi anashindwa kupumua, kwa mwanaume hiyo ni dalili kwamba wewe mwanamke hupo huru bali upo desparate na maisha.

Pia si vizuri kumpigia simu au kumtumia sms kila dakika kutaka kujua yupo wapi anafanya nini na yupo na nani as if wewe ni auditor wa mienendo yake.
Ukiona message au simu haipokelewi ujua unamsumbua badala ya kuonesha upo caring.
Pia angalia usiwe ni mwanamke ambaye anatuma sms kwa mume au kumpigia simu mara moja kwa mwaka, this is too much!

Jambo lingine na la msingi sana mwanamke lazima ukumbuke kwamba wanaume wanasoma magazeti huwa hawasomi mawazo ya kwenye akili yako (mind) hivyo basi ni muhimu sana kumwambia mume wako kila unajisikia pale mkijadili suala lolote na siyo kukubaliana tu na kila kitu ukiamini kwamba unamfurahisha na unataka avutiwe na wewe.
Mwanaume mwenye akili timamu anafahamu fika kwamba mwanamke mwema na mwenye busara kichwani mwake ana ubongo hivyo huwezi kukubaliana na kila kitu na kusema ndiyo, ndiyo ndiyo ….
Mwanaume anahitaji mwanamke ambaye naye anaweza kupendekeza wazo jipya na kwa njia hiyo huonekana ni mwanamke strong na wanaume hupenda strong woman ambaye anaonesha uwezo hivyo kuvutia zaidi.

Hakikisha mume wako anasoma kitu kipya kuhusu wewe baada ya muda fulani na hiyo itasaidia kukuangalia kwa upya zaidi na maana yake unamvutia. Kama ulishaonesha kila kitu basi unahitaji kuwa mbunifu kwani mwanaume huhitaji kitu kipya kutoka kwa mwanamke baada ya muda fulani katika maisha.

Pia ni muhimu sana kuachana na imani potofu kama vile
"The key to a man's heart is through his stomach"
Ni kweli wanaume huwasifia sana wanawake wanaokaangiza vizuri hata hivyo si misosi mizuri tu ndiyo ticket ya mume kuvutiwa na wewe.
Pia wapo wanaoamini kwamba ili mume avutiwe na mke ni pale mke anapotoa sex kwa kwenda mbele, ni kweli mwanaume akipewa hiyo offer hawezi kulazia damu hata hivyo mwanaume anaweza kufanya sex na asiwe amevutiwa na wewe kwani kwa mwanaume sex na love ni vitu viwili tofauti.

Je, kama si chakula kitamu au sex kila siku ni kitu gani muhimu ili kumvutia mwanaume?
Jibu ni rahisi mno mwanaume anahitaji heshima, kumjali, kutukuzwa, kuenziwa, kusifiwa, thaminiwa na kunyenyekewa, kuhusudiwa (respect, admire).
Hakuna hitaji kubwa kwa mwanaume kama lile la kwamba anahitajiwa (needed) na mke wake.

Weekend njema!

God Bless you!
Dieu vous bénisse!


Mungu akubariki!
 
Inawezekana unahusika na matatizo yaliyopo au matatizo yaliyopita katika ndoa yako.
Ni ngumu sana kukubali kwamba unahusika hata hivyo kumbuka kwamba ndoa ni mkusanyika wa watu wawili, mume na mke ambao huja na issues tofauti kwenye mahusiano. Kabla hujaanza kumlalamikia (complain) kwa mke wako au mume wako kwamba hafanyi vile unataka kwanza jicheki mwenyewe kwanza.
Lazima ukubali kwamba hata wewe ni perfect asilimia mia kwa mia, ndiyo maana haiwezekani mke wako au mume wako awe ndiye anayekosea kila siku, mara zote na kila mahali.
Jaribu kujiuliza maswali yafuatayo:

Je, ni majaraha yoyote kutokana na maisha yangu ya huko nyuma iwe kwa wazazi au mahusiano ya kwanza au vyovyote vile?

Je, kila ninalofanya nafanya kwa hofu na mashaka na wasiwasi kutokana na hisia zangu?

Je, ninamlaumu mke wangu au mume wangu kwa vitu vile ambavyo nimefanya mwenyewe?

Je, ninajidanganya mwenyewe kwa kwenda kinyume na ukweli kutoka watu wengine wanavyosema kuhusu wanawake au wanaume walivyo?

Je, ninakubali kwamba naweza kubadilika kwanza mimi mwenyewe?

Je, nina mahusiano mazuri na Mungu au nimerudi nyuma na kumkimbia Mungu? Kumbuka unaweza kumkimbia Mungu ingawa huwezi kujificha!

Badala ya kulalamika kila wakati kuhusu mke wako au mume wako karibu kuangalia je wewe unachangia kiasi gani kwa tatizo lililopo.
Anza kwa kumuuliza Mungu akuoneshe vitu vile unakosea ambavyo vinahitaji mabadiliko.
 
Usipokuwa makini unaweza kuligongesha siku ya kwanza tu! Sex mara ya kwanza ni uzoefu wa aina yake na hakuna kitu hufurahisha kama mnakutana wote ni bikira.

Hapa nazungumzia wale ambao amefunga ndoa tayari sizungumzii wale wanaoamua kufanya uasherati kwani ndoa ni baraka na kuwa na mume wau mke wa ujana wako ni baraka.

Je, ni mambo gani mwanaume au mwanamke ambaye ameolewa na yupo kwenye siku yake ya kwanza ya kuwa na tendo la ndoa anatakiwa kuzingatia?

MWANAUME

FAHAMU NDOTO ZAKE
Kila mwanamke ana ndoto siku moja kuwa na mume anayempenda na kumfanya kutimiza ndoto zake za kuwa mke na kuhudumiwa kama mke idara zote.
Ni jambo la msingi kwa mwanaume mpya kuwa na ufahamu wa mwanamke aliyemuoa je ni wa kisasa (contemporary) au si wa kisasa (traditional) na kwamba je response yake kwenye suala la mahaba itakuwaje.
Unavyoweza kumtimizia ndoto zake (kimahaba) ndivyo unazidi kuwa karibu na kufungua hisia zake

JE, NI BIKIRA
Suala la kuwa bikira au kutokuwa bikira halina umuhimu wowote na si tatizo lako. Pia haina haja wewe kuwa na msisitizo wa kutaka kujua kwa nini si bikira hapo si mahali pake kujadili sababu hata hivyo kama ni bikira ni vizuri pia kujua kwani kutakuwa na maumivu kidogo na ikiwezekana hata yeye mwanamke kutoa damu kidogo ingawa si kila mwanamke bikira hutoa damu.

MPE UPENDO KABLA YA KUMTAMANI
Mwanaume na mwanamke ni tofauti sana linapokuja suala la tendo la ndoa kwani mwanaume hutoa upendo ili kupewa sex na mwanamke hutoa sex ili kupewa upendo hii ina maana kwamba kwa mwanamke upendo kwanza na kwa mwanaume sex kwanza, bila kuwa makini kufahamu hii siri mnaweza kuchanganya mambo.
Mke atajiweka tayari (open) pale tu wewe mwanaume utakapoonesha upendo, caring, affections nk.
Kama akili yako na mawazo yako yapo kwenye matiti yake tu na pale chini basi hutafika popote kwani unahitaji kumpa upendo kabla ya kumtamani.

USIWE NA HARAKA:
Mwanamke huchukua muda mwingi au mrefu kuwa tayari kwa sex na akishafika anachukua muda mrefu kurudi kwenye hali yake ya kawaida.
Hivyo usiwe na haraka kama afande.
Take it slow
Au hakikisha ameonesha dalili zote kwamba yupo tayari.

MUULIZE NAMNA GANI NA WAPI
Mara nyingi kwenye shughuli za mahaba wanaume wote ni ma-genius, ndio wanaoshika usukani.
Jambo la msingi ni kukumbuka kwamba kila mwanamke ni tofauti na hata mwanamke huyo mmoja anakuwa tofauti kwa siku kadhaa katika mwezi mmoja.
Kuna siku ukishika matiti husisimka na kuna siku ukishika matiti atajisikia kuumia hivyo using’ang’anie au kuanza kubabaika.
Ni vizuri kumuuliza kitu gani anapenda na ufanye namna gani anaweza kukueleza kwa maneno au kwa ishara.

AKISEMA HAPANA HAINA SHIDA
Kwa kuwa ni mara ya kwanza anaweza akasema hapana, hivyo usiumize kichwa, inawezekana anaona aibu au yupo MP, kumbuka yeye kwanza na si wewe.
Ni rahisi sana kumvua nguo mwanaume yeyote kwa ajili ya sex hata kama hamjuani au hata kama anatoka sayari nyingine ila si mwanamke.

USIJIBU JEURI
Unaweza kuulizwa swali ambalo linakufanya ushangae hata hivyo uwe na subiri na usijibu kijeuri kwani unaweza kumpiga password kwenye feelings zake na ikawa shughuli nzito na mwili mzima ukaji lock ushindwe kufanya chochote.

UZAZI WA MPANGO NI JUKUMU LAKO MWANAUME
Kutofahamu njia za kujikinga na mwanamke kupata mimba kama hamuhitaji kuzaa watoto 35 ni kuonesha mwanaume yupo caring na pia upo selfish.
Siamini kama mnaweza kufika hapa kabla ya kujadili masuala ya uzazi, watoto, mimba na lini muwe na watoto.

MKUMBATIE, BUSU NA AWE KARIBU
Kwa mwanamke tendo la ndoa si sex peke yake bali ni pamoja na hugs, kissing, cuddling na kupeana joto kwa foreplay ya kufa mtu.
Onesha jinsi unavyomuhitaji kwani kuna msema kwamba
“The way man make love demonstrates his character”
kama unamjali mke wako mpya basi kitandani ni mahali ambapo unaweza kuonesha mara 1,000 kwamba unamjali na kinyume na hapo wewe ni
Selfish
Pleasure seeking,
Narrow focused,
Hivyo kiss, touch and feel.

MWANAMKE:

MTAZAMO:
Mwonekano wa nje (appearance) mara nyingi huwezesha wanaume kujipiga switch ya sex haraka iwezekanavyo, pia chemistry ya mwili nni jambo la msingi sana ni kama asset kwa ajili nya sex hata hivyo kwa kuwa na tendo la ndoa zuri siku ya kwanza jambo la msingi kwa mwanamke ni mtazamo wako kuhusu sex.
Ni muhimu sana kujiamini kwamba unaweza na pia mume wako atakufurahia na kwamba anakuhitaji na upo tayari kusaidiana kuhakikisha wote mnakuwa na wakati mzuri pamoja na ni jukumu lenu wote na si kulala kama gogo lisilo na feelings ukiamini mambo yataenda sawa.

USAFI
Ni vizuri sana kuzingatia suala la usafi kwani ni jambo linalopendeza kunukia vizuri katika harufu ya asili ya mwili wako.
Kwani ukiwa unavutia na mwenye kunukia vizuri basi mwanaume atakuwa crazy tu na atafanya kila analoweza kuhakikisha anakupa kile unastahili.

MAANDALIZI
Jambo la msingi ni kwa wewe mwanamke kuwa wazi kuonge na kuongea na kuongea na kuongea, yaani jiweke huru kuwa wazi kuongea kila kitu.
Kumbuka kubusiana huja baada ya kuongea kwani maneno matamu huleta hamu ya kuwa karibu zaidi kimwili.

KAMA UPO MP
Wanaume wengi huwa hawajali kama mwanamke yupo MP au la hata hivyo suala hili hufanya mwanamke mwenyewe asijisikie vizuri ( embarrassed).
Ni vizuri sana kuwa na discussion na wote mfanye kile mmekubaliana kama hapana iwe hapana kwa wote na kama ndiyo iwe ndiyo kwa wote na si vinginevyo.

USIMUHUKUMU
Wanawake wengi wanaamini mwanaume lazima awe kiongozi linapokuja suala la sex hata hviyo wapo wanaume ambao huhitaji ujasiri wa mwanamke ili kila kitu kiende sawa.
Hivyo ukiona mume wako haoneshi dalili ya kwamba anaweza kuanzisha chochote ni vizuri ukachukua jukumu na katika kuchukua jukumu isifanye kwa dhihaka hadi kuumiza utu wake.
Anyway huyo ni mume wako, mwili ni mali yako na tendo la ndoa ni haki yako na mali yenu na kila kitu unafanya ni Baraka.

KILELENI
Kufika kileleni au kutokufika yote hutegemea wewe na mwenzi wako.​
Ufike kileleni usifike jambo la msingi ni wewe ku-enjoy siku yako ya kwanza kuwa na mume wako na zaidi bado ni grade one so bado safari ni ndefu hadi kuwa na PhD ya mahaba kama mke na mume na ndipo utafurahia kufika kilele.

KIASI GANI
Ukweli hakuna kanuni ni kiasi gani inatosha kwani hakuna formula ya how much is too much or too little.

MWAMBIA “NAKUPENDA”
Wakati mwingine mzuri wa kumwambie mume wako nakupenda ni wakati wa sex na hapo itasaidia kuweka memories kwenye ubongo wake na hatimaye unaweza kuwa na better sex and fulfilling
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom