Majambazi Kuua watu 14 Mwanza; Waziri Masha jiuzuru!

Mbiu ya kila siku ya CCM ilikuwa ni kujivunia utulivu na amani miongoni mwa watz,lkn leo hii watz wanauawa kila siku na majambazi bila mikakati yeyote endelevu toka serikalini hasa wizara ya Mambo ya ndani ya nchi kuwalinda watz wasio na hatia!

Tumevumilia sana,tumevumilia toka mauaji ya kutisha ya albino hadi vifo vya watz maelfu vitokanavyo na madereva wazembe lkn kwa hili la majambazi bila uoga kuua watu 14 huko Sengerema-Mwanza tunasema sasa basi!

Tuwe na hulka ya kujizuru kama likitokea kosa kubwa kwenye nafasi zetu za kazi,kumbuka uongozi ni dhamana na kuwajibika ni sehemu ya uongozi uliotukuka!

Masha jiuzuru kwani umeshindwa kazi;serikali isiyoweza kuwalinda watu wake haifai kuwepo madarakani!Kumbuka Rais mstaafu Mwinyi alijizuru nafasi hii kwenye miaka ya 70 kwa sababu tu ya mauaji ya vikongwe huko Shinyanga.
Kaka hapa umelonga. Ila naomba ufanye 'editing', anatakiwa ajiuzulu siyo ajiuzuru. Huyu jamaa ni mwanasheria, unapaswa usikosee herufi kabisa unapotaka kumsulubu kama anavyostahili.

Hafu huyo jamaa si ameingia kiushkaji... kampuni yake inampa mtoto wa JK uzoefu na ubobevu kwenye sheria, na yeye in return kapewa shavu dodo au vipi... HAYA MANYANG'AU HAYANA UCHUNGU NA WANANCHI HATA KIDOGO. ALIWEZA MZEE MWINYI TU.

KAZI YAO KULA TU HALAFU MATUMBO YAO HAYASHIBI. VITAMBI TU... PUFFFF!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom