Majaji wa Tanzania hawajui kiingereza - Tundu Lissu

Siyo kweli! Katika Baraza la kwanza la Mawaziri ambao walikuwa kumi kulikuwa Waislamu kama kina:

1. Tewa Saidi Tewa
2. Chief Abdallah Fundikiria
3. Rashidi Mfaume Kawawa
5. Amiri Habib Jamal

Sasa ubaguzi unaosemea uko alioufanya Nyerere (Mwenyezi Mungu amweke pema) uko wapi hapo?

Hawa uliowataja si ndo wale waislamu wa mwanzo waliomsaidia kumsomea dua Nyerere ili waingereza wasimfunge kwa kosa la uhani. Hata yeye alikiri kuwa waislamu walimsaidia sana na ndo chanzo cha Nyerere kuvaa balaghashia mpaka alipokuja kuwasaliti waislamu mwaka 1972. Mimi nazungumzia waislamu wapya baada ya uhuru!!!! Ukimzungumzia Tewa Saidi Tewa, huyu alikuwapo tangu enzi za upigania uhuru so ubaguzi hapa usingeweza ku-apply.
Kitu ambacho hamuwezi kukikubali ni kwamba Nyerere aliwaahidi waislamu kwamba akipata urais atawapa kipaumbele kitu ambacho hakukitekeleza baada ya kupata uhuru. Ya nyerere ni kama ya jomo kenyatta wa Kenya. Alimwahidi Jaramogi Oginga Odinga kwamba angempatia nafasi nyeti lakini hakufanya hivyo. Ikumbukwe kwamba Jaramogi alikataa vyeo kadhaa kutoka kwa waingereza mpaka Mzee Jomo atakapotoka gerezani. juhudi za Jaramogi zikafanikiwa mzee akatoka jela lakini Mzee Jommo hakutekeleza wala kutambua mchango wa Jaramogi. Ndipo kulikopelekea mgogoro mkubwa sana na kutoelewana kati Ya Mzee Jomo Kenyatta na Jaramogi Oginga Odinga. Mpaka siku moja walitukanana hadharani kiasi kwamba vrugu kubwa ikatokea na watu 23 waliuawa na polisi.
Kwa Tanzania hii ndo msingi wa waislamu kuona kuwa wanaonewa na wanadhulumiwa. Ikiwa wao ndio waliofunga na kukesha wakisoma dua kali za kung'arisha nyota ya Nyerere mpaka mzungu akachemsha (maana dua ilisomwa kiasi kwamba ukimtafuta Nyerere kwa ubaya humuoni japo unapishana naye) iweje leo uwasahau na kuwatupa? Suala hili linaangaliwa kwa upeo mdogo lakini linamadhara makubwa sana. mfano mwaka 2005 Mahakama ya kadhi ya waislamu iliwekwa kwenye ilani ya uchaguzi lakini baadaye ikafutwa maana yake unawaahidi kitu waislamu kisha unawageuka!!! Kwa kuwa jambo haliwahusu wakristo ndo maana wanasema kirahisi tu kwamba haina haja kuwa na mahakama ya kadhi eti kwamba fedha za kuendeshea hizo mahakama za kadhi zisitoke serikalini!!! Wamesahau kwamba hospitali za mission huwa zinapewa ruzuku ya serikali!!!!! Mgogoro huo ndo utaendelea mpaka siku Tanzania itakapoamua kusikiliza kilio cha waislamu ama Mungu atakapoamua.
 
Lissu yuko sawa kabisa jaji anayebisha aonyeshe hukumu zake alizoandika.kuna wabunge kama lusinde,maji marefu,lakairo.shibuda,sendeka form 6 div 4 ane kilango niwengi sana robo tatu ya wabunge wa ccm hajui kingereza.
 
waosema kiswahili kifundishwe kuanzia chekechea hadi chuo kikuu sijui wana agenda gani. Sasa hebu ona na si majaji tu hata katika maeneo mengi watu hawajui kuongea kingereza. Huo ndio ukweli.

Mkuu si ndo maana wanasema tufundishwe kiswahili, na dogo Tundu anaomba tutumie kiswahili hata kazini, maana hii lugha ya kikoloni imetushinda kabisa, hata hivo kuendelea kutumia kiingereza ni sawa Marekani kuweka bango la Osama ikulu liwe linawakumbusha machungu ya WTC
 
Ndugu msomaji NEGLIGIBLE- Ambaye ulijiunga humu JF juzi Feb,2011 inaonekana huku mwelewa mtoa hoja 'SASATELE' na unajibu kwa jazba.

Ukweli uliousema kwamba kila aliye na degree anajua kiingereza si sahihi!
wewe ni mwasirika wa lugha , pengine unasikia kiingereza kinapoogewa na unapongea unatoa sauti lakini pengine hiyo sauti si lugha fasaha ya kiingereza/ wala unapokiandika.

kwa hiyo usipandishe ukweli unapotajwa- niliwahi kuhudhulia internship kesi za Mahakama Kuu hili jambo nililiona kwa sasa ndio nagundua kuwa hilo lilikuwa tatizo na lipo hadi sasa.
 
Mimi naomba nipingane ma Mh. Tundu lissu. Akisema majaji wa Tanzania hawajui kingereza anakuwa amekosea lakini angesema MAJAJI WA KIKWETE HAWAJUI KINGEREZA ningemuunga mkono kwa asilimia 100,000,000%
 
language ni tatizo la msingi hasa kwa wataalamu wengi tu hapa tanzania, hiyo c hoja ya kufanyia dhihaka, bora kwenye field nyingine lakini sio m2 mwenye inclination ya kuwa judge...! ni janga kama majanga mengine... ukiweka pembeni changamoto nyingine katika tasnia ya utoaj hak nchini, bado lugha ni jambo la kutizamwa kwa jicho la kipekee! bila kusahau pia wapo wengi sana tu wanaojua lugha vizur. tatizo kubwa na la msingi Lissu anataka kuonesha hapa ni kwamba, mamlaka za uteuz zinafanya maamuz ama ya kukurupuka,upendeleo, au zinazembea.
 
Kama amesema majaji wote hapo kakosea na anapaswa kuomba radhi; kama wapo, awataje kwa majina yao, aache huu unafiki! Majaji wetu kama Samatta, Mwalusanya, Ramadhani, Sekule, Chande, Rugakingira, Kyando, NYALALI, Mzavans, Massati, Kalegeya, Utamwa...na wengine wengi wako vizuri sana! Kama yupo anayemjua hajui kiingereza na amseme sasa la sivyo anyamaze milele, sipendi unafiki huu wa kudhalilisha mahakama kiasi hiki.

Na kama yeye anaona anauwezo sana basi kwanini amekacha kuja JUDICIARY kutumikia taifa?! Kama anaona hawana uwezo hata wa kujua hicho kiingereza kwanini asiombe kazi judiciary?! Watu wengine bwana, hivi unafikiri kama wewe uko huko pembeni unalalamika eti watumishi wa serikali hawana uwezo mzuri, kutokana pamoja na mambo mengine, kutofanya vizuri kwenye masomo yao ya taaluma zao, na wakati unamaliza chuo ukakimbia utumishi wa ummana ufaulu wako wa juu kwa kutaka maslahi, unategemea nini?!

Leo hii tuongee hapa, unalalamika kuhusu may be Hosea wa PCCB, hivi unafikiri kuna mtu watamtoa kutoka huko mtaani aje kuwa D.G wa PCCB?! Lazima atatoka kwenye system.

Narudia tena, kama unawajua hao majaji wasio jua hicho kiingereza wasema hapa, na sio kusema majaji wa Tanzania hawajui kiingereza.

Thats very cheap popularity gentlemen.
 
alicho ongea Tundu Lissu ni ukweli mtupu maana majaji, mahakimu kuligana na lugha iliyotumiwa (lugha ya kisheria) kiukweli ni lugha ambayo iko ndani sana inahitaji kuwa makini na kujua nini unafanya na kwa wakati gani
 
Acheni ukabila na udini ninyi..... Kuna rais katika nchi aliyekuwa akiteua mawaziri zero brain kama julius nyerere? au kwa kuwa KIKWETE ni kabila lisilotoka "kaskazini?" Nitajie orodha ya mawaziri alioteua Nyerere enzi zile kisha weka na CV zao, utanieleza kati ya mawaziri wa Nyere na Kikwete wapi kuna afadhali kitaaluma? Mnamsakama Kikwete kwa kuwa majaji aliowateua ni waislamu? Katika historia ya nchi hii jaji mkuu yupi alikuwa mwislamu? Kumteua CHANDE imekuwa nongwa..... Tumechoka na ubaguzi wenu na udini na ukabila wa CHADEMA.....!!!!!!!
Punguza povu ilo ukwel unalia nn sasa...
 
Lissu yuko sawa kabisa jaji anayebisha aonyeshe hukumu zake alizoandika.kuna wabunge kama lusinde,maji marefu,lakairo.shibuda,sendeka form 6 div 4 ane kilango niwengi sana robo tatu ya wabunge wa ccm hajui kingereza.

Hata yeye TL aliwaambia "ndani ya bunge hili kuna wabunge hawajui kabisa kiingereza" alianza kwa kumrekebisha Hamad Rashid ambaye alikosea kutafsiri maneno ya kiingereza kwa kiswahili.
 
Mimi naomba nipingane ma Mh. Tundu lissu. Akisema majaji wa Tanzania hawajui kingereza anakuwa amekosea lakini angesema MAJAJI WA KIKWETE HAWAJUI KINGEREZA ningemuunga mkono kwa asilimia 100,000,000%

Ndio hao hao hapa alibadilisha tu maneno ili wasijisikie vibaya kwa sababu wanajijua.
 
Tundu Lissu bhana, mi huwa namkubali kwa sababu kwake NYEUSI NI NYEUSI, NYEUPE NI NYEUPE, NJANO NI NJANO, NYEKUNDU NI NYEKUNDU. Kwa kweli hili Taifa linahitaji watu wanaosema ukweli, sio hawa wanafiki wa ccm kina werema, lukuvi, pinda, chikawe, kabaka, stella manyanya n.k. yaani wao wanaamini katika uongo kwa faida ya matumbo yao na familia zao.
 
Tundu Lissu bhana, mi huwa namkubali kwa sababu kwake NYEUSI NI NYEUSI, NYEUPE NI NYEUPE, NJANO NI NJANO, NYEKUNDU NI NYEKUNDU. Kwa kweli hili Taifa linahitaji watu wanaosema ukweli, sio hawa wanafiki wa ccm kina werema, lukuvi, pinda, chikawe, kabaka, stella manyanya n.k. yaani wao wanaamini katika uongo kwa faida ya matumbo yao na familia zao.

umenikumbusha silly season.
 
Mkuu, EMT rushwa inayoongelewa kwenye link yako ni ya kawaida hasa katika nchi zetu za Afrika

Sisi mjadala wetu hapa ni je majaji wanajua kiingereza au kuna umuhimu wa kuvitafsiri vitabu vyetu vya sheria ili kuepuka mkanganyo wa lugha?

Kwa kusema ukweli nahisi huyu mama analindwa na nchi yake Uingereza na nisingeshangaa kama kesi ya namna hiyo ingekuwa imetokea mfano Zambia au kokote kule Afrika bado angetumia vigezo hivyo hivyo kwamba zitolewe pesa TASLIMU za fidia iwapo atashinda kesi kwasababu kama itakuwa ni fidia ya ahadi ya maneno na siyo pesa taslimu, na kwa jinsi Mengi alivyokuwa ni mtu mzito kwenye jamii ya Kitanzania kuna uwezekano wa kucheleweshewa malipo. Ndo akatoa mifano ya hizo kesi.

Kumbuka huyo mama anashitakiwa na Mengi huko huko kwao Uingereza. Kwanini Waingereza wasimjengee Mengi mazingira ya kumkatisha tamaa. Na ukitazama vizuri hicho kipengele cha mahakama Tanzania zimejaa rushwa kimewekwa kiufundi hapo ili Mengi alazimike kulipa dhamana(fidia) keshi ukijumlisha na gharama zingine tutategemea Mengi kukata tamaa na huyo mama kuweza kupeta. Ni hivyo tu
 
  • Thanks
Reactions: EMT
95% ya law maker wetu hawajui kiingereza,unategemea nini?:cheer2:

Watunga sheria wetu ni wazee wa ndiyoooooo bila hata kuhoji,kwa sababu hawajui ngeli,hivyo nashauri sheria ziandikwe kiswahili tu kuepusha marumbano.
 
Watunga sheria wetu ni wazee wa ndiyoooooo bila hata kuhoji,kwa sababu hawajui ngeli,hivyo nashauri sheria ziandikwe kiswahili tu kuepusha marumbano.

Hiyo ni kweli kabisa ndiyo maana sheria zinazohusika na masilahi ya wananchi zinapita pasipo umakini wowote, k.m.
- Sheria ya NSSF (ilipitishwa na sasa inaleta kigugumizi)
- Employment and Labour Relations Act, 2004 (Kwa kuzingatia masilahi Kiwira Colliery ya Mkapa)
 
Salaam wanabodi

Mbunge wa Singida na mwanasiasa machachari Katika siasa za Tanzania ndugu Tundu Lissu ameendelea kuwasakama majaji wa Tanzania kwa kusema hawajui kiingereza.

Akichangia leo bungeni amesema ukisoma hukumu nyingi za majaji wa Tanzania utasikitika 'watu wanahukumiwa vifungo vya maisha na kunyongwa kwa sababu majaji hawajui kiingereza ambayo ndiyo lugha inayotumiwa kwenye sheria za Tanzania,hivyo ameshauri sheria zote ziandikwe kiswahili.
mfano mzuri Sofia Simba kwenye Cv yake ana masters ya law sasa mwambie aongee kiingereza atakuangalia vibaya huyo.
 
Back
Top Bottom