Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

Yuda The Praise

New Member
Jun 5, 2023
2
61
Bwana Yesu Asifiwe. Tusifike mbali maisha ya machimbo ya dhahabu yasikie tu kwa jirani kama unampenda mtoto wako huwezi ruhusu akatafute maisha machimbo sisemi kwamba watu wasiende ila naandika hapa siwezi rudi tena machimbo kwangu mimi ni heri saidia fundi lakini sio maisha ya solovea maporini.

Ilikuwa ni mwaka 2007 nilipelekwa na mdingi wangu Kwenda kuchimba machimbo ya dhahabu CHUNYA Mbeya kufupisha stori ile nimefika tu kijiji napokelewa na watu walio choka balaa wamekunywa pombe na wengine sigala yani mtu ukimuangalia nguo alizo vaa zilivyo chakaa duh nilivyo ona tu hivyo pale kijijini mbona nilianza kudata na Nguvu zilianza niishia kidogo.

Sikueleza jina la kijiji hapo nyuma kijiji nilichofikishwa kilikuwa Kinaitwa Igundu Ila kazi tulikuwa tunafanyia mapori fulani mbali kidogo yani kuna kijiji kingine unakipita Kinaitwa mwankonyonto ndio unafika sasa kwenye Eneo tuliko kuwa tunachimba haya tuendelee.

Basi Baada ya kukutani na zile sura ngumu of course Nguvu ziliniisha Nikaanza muona dingi kama vile kaja kunileta matesoni maana story nilizo kuwa nasikia vijiweni ni kwamba watu wa machimbo wanapesa lakini nilivyo Kutana ni tofauti na mategemeo yangu nilitegemea nitawakuta wapo kawaida na sio kwa kuchakaa waponcha kiukweli walikuwa wamechoka balaa nasikia tu harufu Za sigala basi bwana

Kutokana Na mda nilio kuwa nimefika ulikuwa ni jioni jioni kama saa 11 Au kumi na mbili jioni hivi nikaomba wanipeleke nikampumzike maghetoni mwao basi jamaa mmoja hivi jina nimpe Kibakuli akanipeleka mpaka wanapolala maana ilikuwa ni hapo hapo kijijini Igundu ila pembeni kidogo porini ndio walikuwa wanalala hapo lakini mimi hapo akilini mwangu wakati Kibakuli akanipeleka gheto nikapumzike nikajua ni gheto chumba KIZURI cha kawaida tu kama nilivyo zoea tu Vya mjini.

Basi bwana nikiwa njiani na Kibakuli kuelekea ghetoni sasa Nikakuta huyu mshikaji mbona kama tunatembea mpaka tunaanza kukiacha kijiji cha Igundu na tunaanza ingia porini nikajiuliza gheto gani hili lipo porini hivi basi bwana baada ya kukiacha kijiji cha Igundu kama km moja ndio Nikakuta washikaji kumbe wametengengeza kambi la turubai porini duh hapo ndipo nilipo choka Zaidi maana baada ya kufika hapo kambini yani pale palikuwa hakuna godolo wala branketi nilikuta Chini wametandika mabox na yenyewe yamechakaa balaa na vipisi Vya sigala Vya Kutosha.

Nilivyoyaona Hayo kiukweli nikachoka sana nikasema Hapa ni pa moto aise na hapo ndio mwanzo tu malazi Yapo hivi je hiyo kazi ya kuchimba itakuwaje kiukweli nilichoka na kukata tamaa basi baada ya Kibakuli kuniambia ndio Hapa mwanangu gheto akaniacha Akaniambia dagaa hizo mwanangu na ugali Huo kiberiti hicho kuni utaingia porini humu humu zipo nyingi tu aise kimoyo moyo nikasema Hapa nimefika ni pamoto nikamjibu tu fresh mwanangu mimi kamanda nitaungurumisha.

Lakini kiukweli Nguvu Za kupika nilikuwa sina maana nilikuwa nawaza sijui nirudi nyumbani Au nikiamka kesho Niseme naumwa ili nirudi home maana haya maisha kwa mwanzo tu huu yamenishinda anyway nikawaza waza giza likaingia nikaona nilale tu na wakati Huo mimi Nipo peke yangu hapo porini washikaji wapo kijijini wanakunywa pombe hofu ikaanza niingia Kutokana ndio mara yangu ya kwanza kukaa peke yangu vile Afu porini nasikia kelele Za vyura tu.

Lakini nikajipa moyo kwamba washkaji watakuja hata saa tatu usiku lakini ikafika saa tatu usiku hola kimya saa NNE hola pia saa tano hola mpaka saa 6 NA nusu ndio nikawa nasikia kama watu wanaoongea Afu wanakuja upande wangu kwanza wenge likanishika nikawa na mashaka lakini kwa kadili walivyo kuwa wanasogea na Maongezi yao nikawasoma tu kwamba Ni Kama watu waliolewa pombe na kweli baada ya sekunde kadhaa watu hawa Hapa "dogo vepe umelala mimi sikuwajibu Kitu ila mwisho Kutokana Na kelele zao nikawajibu kama mtu alie kwenye usingizi ndio nimelala"

Basi Baada ya kuwajibu wakaanza story zao yani kesho tunapiga hela na mgeni amekuja pale lazima tuwashe mkanda "maana ya Kuwasha mkanda ni dhahabu Kutoka nyingi" Basi wakapiga story sana mimi zile story zao zikanipa Nguvu nikasema moyoni yesi kesho siondoki kumbe tunaenda Kuwasha mkanda Lakini mimi siku hiyo sikulala maana usingizi haukuja Kutokana Na sehemu ile panavyo minya aise.

Basi kulivyo kucha asubuhi mapema masela walikuwa wameamka walikuwa watatu jumla na huyo Nilie mpa jina Kibakuli basi tukasalimiana maana hapo wote walikuwa na akili zao na sio Za pombe basi wakasema tufanye fasta ili tukachukue kipimo kijijini Igundu na sululu na makoleo sehemu wanapoachaga vyombo basi tukabeba unga wa ugali kwenye vile vibegi vyeusi wanaita vibobu na dagaa kidogo mimi sasa nikaawambia mbona mnabeba unga mwingi sana hivyo na mimi sili sana chakula basi wakacheka wa kaniambia we wa Town tu.

Basi tulivyo Fika kijijini Igundu tukachukua kipimo na sululu na makoleo na kipimo fulani kidogo Kinaitwa Fisher gold Bug 2 kina kasahani kadogo sana Basi bwana baada ya kuchukua hivyo vifaa tukanunua na mafuta ya kupikia ya mia tano safari ya kuelekea kazini ikaanza aise tulitembea sana kama km 3 hivi maana ni Mbele ya kijiji fulani Kinaitwa mwankonyonto ukivuka hicho kijiji kwa Mbele ndio Unakuwa umefika na hapo ni umebaba sululu na koleo kila mmoja

Basi Baada ya kutembea sana tukafika Eneo la kuchimba tukawakuta na baadhi ya watu wanachimba basi Yule mjomba mwingine tumpe jina sekesa Akaniambia Wewe dogo utachimba Hapa nikasema poa tena kwa Nguvu yote basi bwana nikaanga kuchimba aise ile kazi ni Ngumu Kuliko kazi zote maana nilichimba mpaka Nikaanza kuona kizungu zungu na hewa nakosa basi nikauliza kwa sauti Kubwa jamani maji Yapo Hapa mmoja wa wale Jamaa tulio wakuta Akaniambia yale pale kwenye mti aise nikaenda fasta nikanywa yale ndio kujisikia Nafuu.

Basi sasa ikawa nikichimba kidogo naenda kupozea na maji kidogo maana nilikuwa nikipiga ile sululu ndefu iliyofulishwa (chongwa) kifua kilikuwa kina pata moto mpaka wale Jamaa wengine tulio wakuta wakasema huyu atamaliza kweli hii kazi basi nikaenda na mwendo Huo lakini kazi haisogei Jua linapiga balaa aise kazi ya kuchimba ni ngumu sana nikaenda nayo wee mpaka saa tisa kazi imesogea kidogo udongo nilio chimba ili kipimo kije kinipimie ulikuwa mdogo sana na nimechoka balaa basi akaja Jamaa wa kipimo akazungushia ule udongo wangu wanaita kibongo Bongo hola hakuna cha dhahabu wala nini Akaniambia nianze kusambaza ili wapime kwa kusambaza aise nilisambaza udongo ule lakini hola hakuna cha dhahabu wala nini Mpaka namaliza kusambaza hakuna cha dhahabu wala nini nikapolola (kukosa) dhahabu.

Kufupisha stori nikakomaa machimbo na hali ya kupolola ilikuwa Kubwa Japo siku Zingine tunapata point tatu Au tano na kipindi hicho point moja ni ilikuwa Elfu 8 kwa Kifupi hali ya machimbo ni ngumu maana unga mda mwingine ulikuwa unakata na mpo polini chawa zikaanza kunitesa maana mda wa kuoga ukaanza kuwa hadithi kwangu Kutokana Na mda ninao rudi mbovu na hela sina mfukoni nimepolola chakula mda mwingine hamna labda ukaombe kambi lingine maisha ya kushindia matunda ya porini matoo na michongoma ndio yakawa kawaida yetu Nikaanza Kushinda vilabuni na wale masela kwa Kifupi kipindi KILE nawaona wale masela wamechoka hawachani nywele wamevaa nguo zimechanika chanika yani mimi Na wao tukawa sawa tu.

Maisha yakawa ni Kushinda VILABUNI Lakini asubuhi mapema unajikaza uende kazini ukipata point moja mbili sawa Japo kukosa ilikuwa ni mara nyingi sana ukifika kijiji ni kushindia pombe Au na viazi Vya kugongea ili baki kidogo tu nianze kuvuta sigara na bangi kwa Kifupi nilichakaa kuzidi wale Jamaa nilio wakuta KUMBU KUMBU YA MWISHO WALITUMWA NDUGU TU KUJA KUNICHUKUA MAANA.

Katika Wale Jamaa Watatu Wawili Nilikuja Kusikia Walipata Ukimwi Na Yule Mmoja kibakuli sijui aliishia Wapi.

MIMI KWA SASA NASHUKULU NI MZIMA NA POMBE NILIACHA NAENDELEA NA MISHE ZANGU TU HAPA MBEYA TOWN ILA NIMALIZE TU KWA KUSEMA MACHIMBO YA DHAHABU NI ZAIDI YA JESHI LA TALIBANI SIJI KURUDI.

MGODINI%2001.jpg
 
Bwana Yesu Asifiwe. Tusifike mbali maisha ya machimbo ya dhahabu yasikie tu kwa jirani kama unampenda mtoto wako huwezi ruhusu akatafute maisha machimbo sisemi kwamba watu wasiende ila naandika hapa siwezi rudi tena machimbo kwangu mimi ni heri saidia fundi lakini sio maisha ya solovea maporini.

Ilikuwa ni mwaka 2007 nilipelekwa na mdingi wangu Kwenda kuchimba machimbo ya dhahabu CHUNYA Mbeya kufupisha stori ile nimefika tu kijiji napokelewa na watu walio choka balaa wamekunywa pombe na wengine sigala yani mtu ukimuangalia nguo alizo vaa zilivyo chakaa duh nilivyo ona tu hivyo pale kijijini mbona nilianza kudata na Nguvu zilianza niishia kidogo.

Sikueleza jina la kijiji hapo nyuma kijiji nilichofikishwa kilikuwa Kinaitwa Igundu Ila kazi tulikuwa tunafanyia mapori fulani mbali kidogo yani kuna kijiji kingine unakipita Kinaitwa mwankonyonto ndio unafika sasa kwenye Eneo tuliko kuwa tunachimba haya tuendelee.

Basi Baada ya kukutani na zile sura ngumu of course Nguvu ziliniisha Nikaanza muona dingi kama vile kaja kunileta matesoni maana story nilizo kuwa nasikia vijiweni ni kwamba watu wa machimbo wanapesa lakini nilivyo Kutana ni tofauti na mategemeo yangu nilitegemea nitawakuta wapo kawaida na sio kwa kuchakaa waponcha kiukweli walikuwa wamechoka balaa nasikia tu harufu Za sigala basi bwana

Kutokana Na mda nilio kuwa nimefika ulikuwa ni jioni jioni kama saa 11 Au kumi na mbili jioni hivi nikaomba wanipeleke nikampumzike maghetoni mwao basi jamaa mmoja hivi jina nimpe Kibakuli akanipeleka mpaka wanapolala maana ilikuwa ni hapo hapo kijijini Igundu ila pembeni kidogo porini ndio walikuwa wanalala hapo lakini mimi hapo akilini mwangu wakati Kibakuli akanipeleka gheto nikapumzike nikajua ni gheto chumba KIZURI cha kawaida tu kama nilivyo zoea tu Vya mjini.

Basi bwana nikiwa njiani na Kibakuli kuelekea ghetoni sasa Nikakuta huyu mshikaji mbona kama tunatembea mpaka tunaanza kukiacha kijiji cha Igundu na tunaanza ingia porini nikajiuliza gheto gani hili lipo porini hivi basi bwana baada ya kukiacha kijiji cha Igundu kama km moja ndio Nikakuta washikaji kumbe wametengengeza kambi la turubai porini duh hapo ndipo nilipo choka Zaidi maana baada ya kufika hapo kambini yani pale palikuwa hakuna godolo wala branketi nilikuta Chini wametandika mabox na yenyewe yamechakaa balaa na vipisi Vya sigala Vya Kutosha.

Nilivyoyaona Hayo kiukweli nikachoka sana nikasema Hapa ni pa moto aise na hapo ndio mwanzo tu malazi Yapo hivi je hiyo kazi ya kuchimba itakuwaje kiukweli nilichoka na kukata tamaa basi baada ya Kibakuli kuniambia ndio Hapa mwanangu gheto akaniacha Akaniambia dagaa hizo mwanangu na ugali Huo kiberiti hicho kuni utaingia porini humu humu zipo nyingi tu aise kimoyo moyo nikasema Hapa nimefika ni pamoto nikamjibu tu fresh mwanangu mimi kamanda nitaungurumisha.

Lakini kiukweli Nguvu Za kupika nilikuwa sina maana nilikuwa nawaza sijui nirudi nyumbani Au nikiamka kesho Niseme naumwa ili nirudi home maana haya maisha kwa mwanzo tu huu yamenishinda anyway nikawaza waza giza likaingia nikaona nilale tu na wakati Huo mimi Nipo peke yangu hapo porini washikaji wapo kijijini wanakunywa pombe hofu ikaanza niingia Kutokana ndio mara yangu ya kwanza kukaa peke yangu vile Afu porini nasikia kelele Za vyura tu.

Lakini nikajipa moyo kwamba washkaji watakuja hata saa tatu usiku lakini ikafika saa tatu usiku hola kimya saa NNE hola pia saa tano hola mpaka saa 6 NA nusu ndio nikawa nasikia kama watu wanaoongea Afu wanakuja upande wangu kwanza wenge likanishika nikawa na mashaka lakini kwa kadili walivyo kuwa wanasogea na Maongezi yao nikawasoma tu kwamba Ni Kama watu waliolewa pombe na kweli baada ya sekunde kadhaa watu hawa Hapa "dogo vepe umelala mimi sikuwajibu Kitu ila mwisho Kutokana Na kelele zao nikawajibu kama mtu alie kwenye usingizi ndio nimelala"

Basi Baada ya kuwajibu wakaanza story zao yani kesho tunapiga hela na mgeni amekuja pale lazima tuwashe mkanda "maana ya Kuwasha mkanda ni dhahabu Kutoka nyingi" Basi wakapiga story sana mimi zile story zao zikanipa Nguvu nikasema moyoni yesi kesho siondoki kumbe tunaenda Kuwasha mkanda Lakini mimi siku hiyo sikulala maana usingizi haukuja Kutokana Na sehemu ile panavyo minya aise.

Basi kulivyo kucha asubuhi mapema masela walikuwa wameamka walikuwa watatu jumla na huyo Nilie mpa jina Kibakuli basi tukasalimiana maana hapo wote walikuwa na akili zao na sio Za pombe basi wakasema tufanye fasta ili tukachukue kipimo kijijini Igundu na sululu na makoleo sehemu wanapoachaga vyombo basi tukabeba unga wa ugali kwenye vile vibegi vyeusi wanaita vibobu na dagaa kidogo mimi sasa nikaawambia mbona mnabeba unga mwingi sana hivyo na mimi sili sana chakula basi wakacheka wa kaniambia we wa Town tu.

Basi tulivyo Fika kijijini Igundu tukachukua kipimo na sululu na makoleo na kipimo fulani kidogo Kinaitwa Fisher gold Bug 2 kina kasahani kadogo sana Basi bwana baada ya kuchukua hivyo vifaa tukanunua na mafuta ya kupikia ya mia tano safari ya kuelekea kazini ikaanza aise tulitembea sana kama km 3 hivi maana ni Mbele ya kijiji fulani Kinaitwa mwankonyonto ukivuka hicho kijiji kwa Mbele ndio Unakuwa umefika na hapo ni umebaba sululu na koleo kila mmoja

Basi Baada ya kutembea sana tukafika Eneo la kuchimba tukawakuta na baadhi ya watu wanachimba basi Yule mjomba mwingine tumpe jina sekesa Akaniambia Wewe dogo utachimba Hapa nikasema poa tena kwa Nguvu yote basi bwana nikaanga kuchimba aise ile kazi ni Ngumu Kuliko kazi zote maana nilichimba mpaka Nikaanza kuona kizungu zungu na hewa nakosa basi nikauliza kwa sauti Kubwa jamani maji Yapo Hapa mmoja wa wale Jamaa tulio wakuta Akaniambia yale pale kwenye mti aise nikaenda fasta nikanywa yale ndio kujisikia Nafuu.

Basi sasa ikawa nikichimba kidogo naenda kupozea na maji kidogo maana nilikuwa nikipiga ile sululu ndefu iliyofulishwa (chongwa) kifua kilikuwa kina pata moto mpaka wale Jamaa wengine tulio wakuta wakasema huyu atamaliza kweli hii kazi basi nikaenda na mwendo Huo lakini kazi haisogei Jua linapiga balaa aise kazi ya kuchimba ni ngumu sana nikaenda nayo wee mpaka saa tisa kazi imesogea kidogo udongo nilio chimba ili kipimo kije kinipimie ulikuwa mdogo sana na nimechoka balaa basi akaja Jamaa wa kipimo akazungushia ule udongo wangu wanaita kibongo Bongo hola hakuna cha dhahabu wala nini Akaniambia nianze kusambaza ili wapime kwa kusambaza aise nilisambaza udongo ule lakini hola hakuna cha dhahabu wala nini Mpaka namaliza kusambaza hakuna cha dhahabu wala nini nikapolola (kukosa) dhahabu.

Kufupisha stori nikakomaa machimbo na hali ya kupolola ilikuwa Kubwa Japo siku Zingine tunapata point tatu Au tano na kipindi hicho point moja ni ilikuwa Elfu 8 kwa Kifupi hali ya machimbo ni ngumu maana unga mda mwingine ulikuwa unakata na mpo polini chawa zikaanza kunitesa maana mda wa kuoga ukaanza kuwa hadithi kwangu Kutokana Na mda ninao rudi mbovu na hela sina mfukoni nimepolola chakula mda mwingine hamna labda ukaombe kambi lingine maisha ya kushindia matunda ya porini matoo na michongoma ndio yakawa kawaida yetu Nikaanza Kushinda vilabuni na wale masela kwa Kifupi kipindi KILE nawaona wale masela wamechoka hawachani nywele wamevaa nguo zimechanika chanika yani mimi Na wao tukawa sawa tu.

Maisha yakawa ni Kushinda VILABUNI Lakini asubuhi mapema unajikaza uende kazini ukipata point moja mbili sawa Japo kukosa ilikuwa ni mara nyingi sana ukifika kijiji ni kushindia pombe Au na viazi Vya kugongea ili baki kidogo tu nianze kuvuta sigara na bangi kwa Kifupi nilichakaa kuzidi wale Jamaa nilio wakuta KUMBU KUMBU YA MWISHO WALITUMWA NDUGU TU KUJA KUNICHUKUA MAANA.

Katika Wale Jamaa Watatu Wawili Nilikuja Kusikia Walipata Ukimwi Na Yule Mmoja kibakuli sijui aliishia Wapi.

MIMI KWA SASA NASHUKULU NI MZIMA NA POMBE NILIACHA NAENDELEA NA MISHE ZANGU TU HAPA MBEYA TOWN ILA NIMALIZE TU KWA KUSEMA MACHIMBO YA DHAHABU NI ZAIDI YA JESHI LA TALIBANI SIJI KURUDI.

Machimboni wanawake hawaruhusiwi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom