Maisha Plus: Picha halisi ya upeo wa kijana

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,882
2,762
Sijajua kama kuna topic kama hii, ila ukweli ndo huo kuwa kuna tabaka kubwa sana la vijana HAWAJITAMBUI!

Wana upeo mdogo hadi inatia aibu. Wengi wamefika 4m4 na ndo hivyo. Wanachojua ni ngono, burudani na starehe. Tatizo ni wao au walimu au wazazi?

Naomba hili lijadiliwe
 
Sijajua kama kuna topic kama hii, ila ukweli ndo huo kuwa kuna tabaka kubwa sana la vijana HAWAJITAMBUI! Wana upeo mdogo hadi inatia aibu. Wengi wamefika 4m4 na ndo hivyo. Wanachojua ni ngono, burudani na starehe. Tatizo ni wao au walimu au wazazi? Naomba hili lijadiliwe
 
Sijajua kama kuna topic kama hii, ila ukweli ndo huo kuwa kuna tabaka kubwa sana la vijana HAWAJITAMBUI! Wana upeo mdogo hadi inatia aibu. Wengi wamefika 4m4 na ndo hivyo. Wanachojua ni ngono, burudani na starehe. Tatizo ni wao au walimu au wazazi? Naomba hili lijadiliwe

Mziwanda,
Usemayo ni kweli, lakini mimi binafsi niseme kwamba ni ukweli unaosikitisha sana..Ila jibu la hoja yako linapatikana ndani ya hiyo hoja.

Ukiangalia hiyo kijani, utagundua kwamba elimu hiyo ya 4m4 kwa sasa ni ndogo mno, ni kama L.Y.! nikimaanisha `la saba`!

Watu wenyewe kama wale wa jana(20/9/09) ni wa mkoani huko, ambako bila ya kuficha, hali ya uchumi iko duni kulinganisha na mahali ulipo wewe, mostly uko Dar! Kwahiyo, uwezekano wa kupata gazeti au kuingia cafe kujifunza haupo. Lakini hiyo ndo Tanzania ya Nyerere, ndo nchi yetu hii!
Serikali inapaswa kujifunza kinachoendelea nchini kupitia vipindi kama hivi, ili ijue aina ya watu inaotegemea wajenge Taifa imara na lenye Maendeleo.Huenda mitaala ikafanyiwa kazi baadae na kuongeza kiwango cha uelewa.
Mungu Bariki INJI hii!
 
Mziwanda,
Usemayo ni kweli, lakini mimi binafsi niseme kwamba ni ukweli unaosikitisha sana..Ila jibu la hoja yako linapatikana ndani ya hiyo hoja.

Ukiangalia hiyo kijani, utagundua kwamba elimu hiyo ya 4m4 kwa sasa ni ndogo mno, ni kama L.Y.! nikimaanisha `la saba`!

Watu wenyewe kama wale wa jana(20/9/09) ni wa mkoani huko, ambako bila ya kuficha, hali ya uchumi iko duni kulinganisha na mahali ulipo wewe, mostly uko Dar! Kwahiyo, uwezekano wa kupata gazeti au kuingia cafe kujifunza haupo. Lakini hiyo ndo Tanzania ya Nyerere, ndo nchi yetu hii!
Serikali inapaswa kujifunza kinachoendelea nchini kupitia vipindi kama hivi, ili ijue aina ya watu inaotegemea wajenge Taifa imara na lenye Maendeleo.Huenda mitaala ikafanyiwa kazi baadae na kuongeza kiwango cha uelewa.
Mungu Bariki INJI hii!

Mkuu hata kwa mitaala ya Oxford, Cambridge nk, wengi tuna matatizo ya kufikiri, sisi ni wajinga. Tukianza hapo tutajifunza na tutasonga mbele. Tuache uvivu tujisomee na tufanye kazi kwa bidii. Tuna ushamba wa jumla 'collective village heroism'
 
"The only problem with Africans is implementation and maintenance"- Mziwanda.
 
Kwani kina Masoud wanawalenga kina nani? Walio na upeo wako schools. Waliolobaki na wale wachache wenye bahati mbaya ndio haswa targeted group. Kwa hiyo usishanagae ukiona ni mambumbu karibu wote.
 
kinacho takiwa ni watanzania tuongeze bidii ktk nyanja zote za maendeleo, tuache kujicheka wenyewe, nchi nyingine hawafanyi hivyo.

Matatizo ya vijana hao mnaowacheka ndo matatizo ya tanzania. Kinacho sikitisha ni sisi wenyewe hasa hapa JF, tunajifanya tunawacheka watanzania wenzetu ambao wana hali ya chini eti kwa sababu labda tuko nje, tujiulize hapo awali tulikuwa wapi??

Mbona nchi kibao tu watu ni maskini wa kutupwa? lakini hawachekani ila wanahimizana kujishughulisha na kwa kufanya hivyo nchi zao zina endelea. Ni kweli hatuna uongozi lakini sisi kama jamii lazima tutafute njia za kujikwamua na siyo kuchekana.
 
Kwani kina Masoud wanawalenga kina nani? Walio na upeo wako schools. Waliolobaki na wale wachache wenye bahati mbaya ndio haswa targeted group. Kwa hiyo usishanagae ukiona ni mambumbu karibu wote.

lakini hata kujua maarifa ya kawaida? Najua kina masudi wakiamua kuingia vyuoni usishangae hali kuwa the same. Tathmini ni vijana wangapi wamefanyiwa usaili wa maisha plus. Ni haohao wanaoambiwa, "nenda hata ualimu basi". Ndio hao wanaokuwa manesi. Serikali makini inapaswa kung'amua matatizo kupitia mazingira kama haya ili mwisho wa siku mh. Rais asiseme eti hajui why TZ ni masikini
 
Kwani kina Masoud wanawalenga kina nani? Walio na upeo wako schools. Waliolobaki na wale wachache wenye bahati mbaya ndio haswa targeted group. Kwa hiyo usishanagae ukiona ni mambumbu karibu wote.

Mkuu Mfamaji
kwa mfano mdogo sayansikimu inafundishwa shule ya msingi (kama hawajaifuta hawa wanga wa Wizara ya Elimu). Mtu aliyesoma na aliyeelewa sayansikimu ni tofauti. Malaria, kipindupindu, minyoo, funza ni magonjwa yanayozuilika bila mzungu. Mitanzania iwe shule au isiwe shule ina ujinga wa aina fulani na utaona jinsi inaugua malaria, funza, kipindupindu, minyoo ikisubiri serikali. Hivyo usishangae hao mnaowaona mambumbumbu huko Maisha Plus shule walikwenda ila ndio hivyo
 
General knowledge ya hao wanaofanya huo usaili pia ina utata, jana kuna kuna dada alisema mke wa raisi anaitwa "ladies first", i laughed and slept like a baby after that, uuwii
 
Kuingia darasani na kuelimiaka ni vitu viwili tofauti, watanzania tunapenda kuhesabu madarasa na vyeti badala ya elimu yenyewe. Elimu ya ukweli inapatikana kwa kuitafuta kila siku ya maisha yako na kila mahali bila kuchoka.Naunapopatakitu ili kiwe elimu lazima ukichakate kwa kutumia uwezo wako wa kufikiri,jambo ambalo watanzania wengi hatupependi, tunabaki kuwa wazee wa madesa, Chambilecho Ben Mkapa,kuwa watanzania wengi ni wavivu wa kufikiri
 
Kwani kina Masoud wanawalenga kina nani? Walio na upeo wako schools. Waliolobaki na wale wachache wenye bahati mbaya ndio haswa targeted group. Kwa hiyo usishanagae ukiona ni mambumbu karibu wote.

,.,.
Anawalenga vijana zaidi.
Uwezo wa uelewa wa vijana wengi upo chini na unaendelea kushuka.angalia takwimu za afya za watanzania.
Tatizo ni lishe duni na mfumo wa maisha wa kisasa.
HAIWEZEKANI ALIYEMALIZA KIDATO CHA NNE/SITA HAJUI CHOCHOTE KUHUSU WALAO CHANZO KIMOJA CHA MIMBA MASHULENI.HAIWEZEKANI!KUNA TATIZO
 
kinacho takiwa ni watanzania tuongeze bidii ktk nyanja zote za maendeleo, tuache kujicheka wenyewe, nchi nyingine hawafanyi hivyo.

Matatizo ya vijana hao mnaowacheka ndo matatizo ya tanzania. Kinacho sikitisha ni sisi wenyewe hasa hapa JF, tunajifanya tunawacheka watanzania wenzetu ambao wana hali ya chini eti kwa sababu labda tuko nje, tujiulize hapo awali tulikuwa wapi??

Mbona nchi kibao tu watu ni maskini wa kutupwa? lakini hawachekani ila wanahimizana kujishughulisha na kwa kufanya hivyo nchi zao zina endelea. Ni kweli hatuna uongozi lakini sisi kama jamii lazima tutafute njia za kujikwamua na siyo kuchekana.

siamini kama kuna mtu kajaribu kucheka bali tunaona aibu ktk hili. Mama Sitta eti ni naibu spika?! Tunaungana na ww ktk msiba huu
 
Mkuu Mfamaji
kwa mfano mdogo sayansikimu inafundishwa shule ya msingi (kama hawajaifuta hawa wanga wa Wizara ya Elimu). Mtu aliyesoma na aliyeelewa sayansikimu ni tofauti. Malaria, kipindupindu, minyoo, funza ni magonjwa yanayozuilika bila mzungu. Mitanzania iwe shule au isiwe shule ina ujinga wa aina fulani na utaona jinsi inaugua malaria, funza, kipindupindu, minyoo ikisubiri serikali. Hivyo usishangae hao mnaowaona mambumbumbu huko Maisha Plus shule walikwenda ila ndio hivyo

.........walilifuta aisee........yaani siku hizi ni maudhi tupu......damn
 
Some people readily embrace wallowing in a pond of mediocrity, you can't tell them nothing about it.They will eloquently invoke humility, cite patriotism, call on history, use the excuse of culture or even launch a torrent of vehement abusive diction, you name it.

Just to swim in that tepid molasses-like mud of everlasting effortless mediocrity.
 
Some people readily embrace wallowing in a pond of mediocrity, you can't tell them nothing about it.They will eloquently invoke humility, cite patriotism, call on history, use the excuse of culture or even launch a torrent of vehement abusive diction, you name it.

Just to swim in that tepid molasses-like mud of everlasting effortless mediocrity.

mkuu kwa faida ya umma hebu tutafsirie kwa lugha ya taifa
 
Mimi ningeomba waheshimiwa wetu wangetumia hii kama research ya bure, vijana wengi ufahamu upo chini sana. wakiitumia in a positive way itaweza kusaidia kwa baadaye kututoa hapa tulipo....kuna mdau amesema hapo juu kuwa wenye upeo wapo shule/vyuo amesahau ndo hao ambao wametutia aibu kwenye Zain Africa Challenge hakuna hata chuo kimoja cha tz kilichosongasonga....yale maswali ya ZAC ni ya general knowledge kwa sehemu kubwa....Tukubali vijana wengi au watz kwa ujumla ni wavivu wa kufikiri na kujifunza. Mdau m1 hapo juu anasema vijana wetu wanajua ngono na starehe...! mimi nina wasiwasi hata hizo ngono hawazijui,sema kwa kuwa wanakuwa sirini huko tunahisi wanajua,kwa upeo ule watavaa hata hizo condom?na starehe ndo kabisaaaaa vijana wa kibongo kuwastarehesha ni kazi kubwa sana...wanaweza kuimba wasanii hata 6 mtu asifurahi hata kidogo,unakuta amenuna kama yuko kwenye maziko, kama huamini nenda kwenye concert ya nchi za jirani linganisha na za hapa home........
cha msingi ni kuanza kubadilika,kila mtu aanze na yeye mwenyewe kwa kuwa waathirika wa hii maneno ni wote kama sio wewe moja kwa moja basi ni ndugu yako wa karibu au hata mwanao, anza na hao wabadilishe ukawafanye wapende kujisomea na kujifunza...Mimi nshaanza na wanangu.
 
.........walilifuta aisee........yaani siku hizi ni maudhi tupu......damn

Makubwa! Halafu tunakimbilia kuomba hela kwa Bush kupambana na malaria? Sisi ni wajinga sana. Unajua Mkuu Ogah, nilihisi hili somo halipo maana watoto na hasa vijana hawajui usafi wa mwili ni nini. Ingia kwenye daladala utashangaa. Hayo yanayoonekana kuwa upeo mdogo wa vijana kufikiri kwenye Maisha Plus, ni mkusanyiko wa mambo mengi. Kweli tuko bado karne ya 19. Yaani alipoachia mkoloni, tumerudi tena nyuma karne moja
 
Hofu yangu, haya yataachwa yaishie hewani. Wazazi msitegemee haya yakarekebishwa na wenye mamlaka. Wazazi ndo wana majukumu ya kuhakikisha mtoto wake ana UFAHAMU. Tatizo jingine, hao vijana wa maisha plus ndo watakaokuwa wazazi siku za mbele
 
Back
Top Bottom