M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,734
- 405
Tumsaidieni dada huyu wanaJF na tutajifunza mengi kwa hiki kisa chake.
Mimi nimeolewa miaka 2 iliyopita tunaishi vizuri na mume wangu japo mi sina raha na hivi ninavyoandika hii msg nimenuna toka jana. Tatizo langu ni huyu mume ananijali ananitimizia ila uhusiano wetu ni kama baba na mtoto kasoro ni kwamba tunakula chakula cha ndoa. Yaani heshima nayoitaka mi nimechoka jamani. ndoa haina utani, hakuna kucheza, yaani ni mama mama mama basi. hicho chakula cha ndoa ni lazima kitandani na style ni ile ile kila siku. nimejaribu kumueleza ananimbia mimi ni mkewe sio mwanamke wa mtaani so lazima aniheshimu. nimejaribu kumuwekea movies za kumchangamsha anajidai kama haelewi. kuna siku nikamfuma yuko na rafiki zake stories alizokuwa anapiga huwezi amini nipotokea alibadilika ghafla. jana nikatumia msg ya kichekesho chenye matusi kidogo tu nikamforwadia nae acheke jamani hakujibu jioni amenisema kuwa natarajia nini kutuma msg kama ile lazima nijiheshimu nk nk hadi nimenuna. naombeni msaada nimfanyaje maana nishaanza kuboreka. sikumjua wakati wa uchumba maana uchumba wetu ulikuwa wa mbali. yaaani natamani nipige kelele