Mahakama ya Kadhi: Masheikh wakutana na JK

Naomba kuuliza, hivi mfano mwanaume wa kikristo ameoa binti wa kiislam na ikaja kutokea wamtofautiana au mirathi, ndoa hapo masuala ya hukumu yatakuwaje kwa mahakama ya Kadhi? Ukizangatia huyu mume ni mkristo, hapo najaribu kujiuliza. Mwenye uelewa wa hili naomba anifahamishe. Maana baadae yasije ya kutokea ya kutokea. Na katika masuala ya uundaji wa mahakama hii, ni vyema mambo haya na yanayofanana na hili yaangaliwe ili yasijeleta mtafaruku huku siku za mbeleni
 
Tumwache Rais awape pole Masheikh na awape ukweli kwamba ni ruksa kuanzisha mahakama ya Kadhi kwa ajili ya waislamu watakaoamua kufuata mkondo wa kadhi katika masuala ya mirathi na talaka na si zaidi ya hapo.. NA KWAMBA MAHAKAMA HIO HAIPO KWENYE MFUMO WA SERIKALI NA ITAGHARAMIWA NA WAISLAM!!!
 
Naomba kuuliza, hivi mfano mwanaume wa kikristo ameoa binti wa kiislam na ikaja kutokea wamtofautiana au mirathi, ndoa hapo masuala ya hukumu yatakuwaje kwa mahakama ya Kadhi? Ukizangatia huyu mume ni mkristo, hapo najaribu kujiuliza. Mwenye uelewa wa hili naomba anifahamishe. Maana baadae yasije ya kutokea ya kutokea. Na katika masuala ya uundaji wa mahakama hii, ni vyema mambo haya na yanayofanana na hili yaangaliwe ili yasijeleta mtafaruku huku siku za mbeleni

Maamuzi yatatolewa na waliokufungisha ndoa, kama ni bomani basi utakwenda mahakani, (yaani mahakam itaamua) kama ni kanisani vilevile utakwenda mahakani kwakuwa hakuna ndoa ya KIKRISTO, isipokuwa kanisa ni wadhamini wa ndoa tu. Kumbuka ndoa zote zinazofungwa KANISANI ni za serkali, ndo maana hairuhusiwi kufungisha ndoa katika KANISA ikifika saa kumi na mbili jioni au kabla ya saa kumi na mbili asubuhi kwani serkali wakati huo inakuwa imeshashusha bendera! huo ndo ufahamu wangu mdogo. pengine naweza kuwa nimekosea kidogo lkn natumaini nimekujibu.
 
Waislam tuchape kazi, malumbano na fikra potofu ndivyo vinaturudisha nyuma. Hata ukiangalia mikoa ya waislam wengi nje ya Dar iko nyuma kimaendeleo. Mfano: Tabora, Lindi, Mtwara na Kigoma.
nimeipenda hii very good! cha kwanza watu watambue hakuna maendeleo yatakayo kuja kwa msaada bila kazi na kujituma. pili malalamiko huwa yanachelewesha safari ya maendeleo na hasa ya kutafuta mazingira ya kubebwa. ni vizuri tujaribu kutumia akili zinazotumika kulalamika kuwekeza. mwisho wa siku tunahitaji uchumi imara wenye mazingira mazuri na maisha bora. waislamu acheni kulalamika kwa sababu tunaweza kuongeza matabaka yasiyo na msingi. binafsi kwa hili siogopi hata kama mahakama inanza kesho lakini kama hamtabadilika hakuna ufanisi wa maana. wekezeni kwenye huduma za jamii na muone kama serikali haitawapa hayo mafweza, kizuri zaidi zaidi ya asilimia 50% ya huduma za jamii zitolewazo na makanisa hutolewa bila ubaguzi.simameni kwa watu tulio kamilika na tuwe tayari kujifunza na kuiga kwa mafanikio ya walio wengi! wakristo wamekuwa kimya sio kwamba hawayaoni mapungufu lakini wanayapuuza na kuendelea na shughuli zao.tujipange tutoke ili watotowetu wakute tumesogea.kumbuka kuwa wengi wa waharifu walio magerezani ni waislamu hivyo tusiwaongezee wenzetu mahakama.
 
Naomba kuuliza, hivi mfano mwanaume wa kikristo ameoa binti wa kiislam na ikaja kutokea wamtofautiana au mirathi, ndoa hapo masuala ya hukumu yatakuwaje kwa mahakama ya Kadhi? Ukizangatia huyu mume ni mkristo, hapo najaribu kujiuliza. Mwenye uelewa wa hili naomba anifahamishe. Maana baadae yasije ya kutokea ya kutokea. Na katika masuala ya uundaji wa mahakama hii, ni vyema mambo haya na yanayofanana na hili yaangaliwe ili yasijeleta mtafaruku huku siku za mbeleni
well said hapa down
Maamuzi yatatolewa na waliokufungisha ndoa, kama ni bomani basi utakwenda mahakani, (yaani mahakam itaamua) kama ni kanisani vilevile utakwenda mahakani kwakuwa hakuna ndoa ya KIKRISTO, isipokuwa kanisa ni wadhamini wa ndoa tu. Kumbuka ndoa zote zinazofungwa KANISANI ni za serkali, ndo maana hairuhusiwi kufungisha ndoa katika KANISA ikifika saa kumi na mbili jioni au kabla ya saa kumi na mbili asubuhi kwani serkali wakati huo inakuwa imeshashusha bendera! huo ndo ufahamu wangu mdogo. pengine naweza kuwa nimekosea kidogo lkn natumaini nimekujibu.
 
Mfumo kristo umeshikwa kooni unapumulia icu tehe tehe
padre/mchungaji akigombea kwenye siasa uchwara hizi anaonekana ana kipaji cha kuongoza na wala habaguliw kwa dini yake,,masheikh wakijihusisha na chama flani cha siasa uchwara utaskia chama cha kidiniiiiiiii.........
I like vita ije fasta,,wajukuu zetu wataheshimiana sisi tukifa vitani inshallah...
 
kwani wakatoliki wangesimama wenyewe bila kuomba fungu serikalini ingewapungukia kitu gani?


St.Ivuga kama nimewaelewa wachangiaji wengine vyema ni kuwa, concern yao kubwa ni kuwa serikali inachangia katika taasisi ya kikristo ambazo zinahudumia jamii zote za wakristo na wasio wakristo. Huduma hizi ni kama mahospitali ambayo mtu yeyote anaweza kwenda kutibiwa na pengine bila kuulizwa dini yake{kama hali ipo hivyo}. Ni kwa sababu gani? Ni kwamba kama serikali ingekuwa inaweza kutoa huduma hizi zote bila kuhitaji ushirikiano wowote na taasisi za kidini basi nadhani hata misamaha ya kodi kwa taasisi hizo isingekuwepo. Maana yake ni kuwa serikali haina uwezo wa kuwafikia wananchi wote kutokana na kutokuwa na hospitali za kukidhi mahitaji kutokana na idadi ya watu na ndo maana kama wajibu wake, serikali inachangia hizo gharama za kufikisha huduma karibu kwa wananchi na ndo maana umesikia kuna misamaha ya kodi , na vitu kama hivyo. Nimetolea mfano wa hospitali, the same holds for stuff kama hiyo huduma. Na wachangiaji hao hawajaongelea kama serikali inachangia kuendesha seminari au makanisa. Sasa hili la mahakama ya kadhi linatofauti gani kama serikali ingekuwa inachangia kuendesha seminari?ni kwa sababu linawagusa waislam tu na siyo jamii yote.
Na ndo maana katika moja ya comment yangu nimeuliza, ikitokea mwanaume wa kikristo ameoa binti wa kiislam na ikatokea masuala ya kutoelewana na ikahitajika usuluhishi, mirath n.k. Itakuwaje kwa huyu mume ambaye si muislam?
 
kama haina dini kwa nini -Katoliki wanapewa fungu na serikali? Kwa nini kama wanatoa huduma za jamii wasitoe tu kama kanisa? Kwa nini wameingia gentlemen mkataba na serikali ambayo haina dini? Serikali na maaskofu hapa wameteleza kuwanyima waislamu mahakama ya kadhi kama walivyotaka na huu udini wakristo ndio wanauanzisha wenyewe

@Saint Ivuga, hii hoja ya mahakama ya kadhi na MOU ilijadiliwa kwa kina sana siku chache zilizopota lakini bado naona inarudi! Nikumbushe wakristo hawashindwi kuendesha shule, wala hospitali. HAWASHINDWI na hata sasa hivi serikali ikitaka ivunje hiyo MOU lakini miradi yote iliyo chini ya kanisa itaendelea. Ila (ILA) mteja au mpata huduma i.e mgonjwa/ mwanafunzi, atalazimika kulipa 'actual price' tofauti na sasa ambapo MOU ni kama ruzuku ili kumsaidia mwananchi. Na hapa naongelea wakristo, waislam, wapagani etc.

Pili, nirudie tena, mwanadamu hawezi kuishi bila maji, au ukiugua na kama hukupata matibabu upo uwezekano wa wewe kufa. Lakini unaweza kuishi na waislam wameishi kwa decades bila mahakama ya kadhi. Hakuna mtu aliyekufa kwa sababu hakuna mahakama ya kadhi, lakini kila kukicha watoto wachanga wanakufa kwa sababu ya malaria, mama wajawazito wanapoteza maisha kwa sababu ya poor maternity health n.k Ukielewa hili basi utajua msingi wa serikali kuunganisha nguvu na kanisa ili kuokoa maisha ya binadamu. Tofautisha huduma za kibinadamu na imani (dini). Kama waislam nao wangekuwa na hospitali na hakika wangepata MOU yao na watu wengi zaidi wangeweza kupata huduma ya afya kuliko ilivyosasa maana watoa huduma wangekuwa wengi - yaani kanisa, misikiti (jumuiya ya kiislam), serikali n.k.

Kinacholeta sokomoko ni pale kundi moja linaomba msaada ili kutoa huduma muhimu za kibinadamu kwa watu wote, lakini lingine linataka hela kwa shughuli za kutimiza ibada. Hii ni sawa na mkulima kula mbegu.Unakula msaada badala ya kujikita kwenye sustainable project. Kumbuka wakatoliki kwa mfano wanayo mahakama yao lakini hawakuwahi hata siku moja kuomba vijicent serikalini na wala hawakuhitaji 'kamati ya waziri mkuu' ili kuharakisha uundwaji wake. They did it all by themselves na sasa wanaiendesha kwa sadaka zao. Hivi Waislam are that weak kiasi kwamba hata kuandaa Mahakama wanahitaji msaada toka serikali kuu? Achilia mbali pesa kwa ajili ya kununulia viti vya mahaka na mishahara ya mahakimu, lakini hata kuandaa rasimu imeshindikana?. Na kama waislam wanahitaji msaada kwenye maandalizi watawezaje kuindesha? au ndio kama zile za serikali za kuwa na 'warsha' na semina elekezi? Ni kitu gani hasa kinachoongelewa usiku Ikulu?

Na kwa nini waislam wasiombe MOU ili wachimbe visima vya maji, au wajenge vituo vya afya, au shule?Wanataka nani awasomeshee watoto wao? au nani ajenge maternity wards? Hivi kwa muislam mwenye uwezo mdogo/maisha duni ni kwa sababu serikali haitoi hela kuanzisha & kuendesha mahakama ya kadhi? Au haya magonjwa ya mlipuko yanayosababishwa kunywa maji machafu yataisha mara serikali itakapotoa hela kuanzisha mahakama ya kadhi? MwanaJF - Mkandara alieleza juzi kuwa BAKWATA wanavuta hela nzuri tu toka serikali kila mwaka, lakini sijui wamewanywesha waislam wote vikombe vya Babu wa Loliondo ili wasiulize. Hakuna mwislam anayeuliza BAKWATA wanapata kiasa gani na wanafanyia kazi gani hela wanazopata badala yake wamejikita kwenye kulalamika kuwa Wakristo wanapata hela? Kwa nini hamuulizi haya ya BAKWATA? why?
 
Aliyenacho ndiye apewaye.Serikali analipa kanisa ruzuku kwasababu ijuwa inakwenda kuhudumia jamii.kwa mfano: Shule, Hosipitali n.k. Pia kanisa halitegemei ruzuku kwa serikali pekee,waumini ndio wachangiaji wakubwa wa pato la kanisa kwa kutoa sadaka kipindi cha ibada.Pia kanisa lina wadhamini wake.Hivyo wewe wacha kuilalamikia serikali ikupe ruzuku wakati huna hata kianzio. waisilamu nendeni mkachangishane misikitini ndio mwende kudai ruzuku serikalini.Lakini muache mtindo wenu wa kutupiana majini kugonia hiyo michango na ruzuku.
 
FMJ thanks...nitakujibu badae kidogo..ila mimi kinachoniuma ni kwa nini rais kawadanganya waislamu?
 
Endapo makanisa yakaamua kujitoa kwenye hiyo MoU nakuachana kushirikiana na serikali kwa namna ya kifedha kutafanya hoja ya kadhi ife?
Mkuu mbona unazungumza kitu ambacho hakiwezekani? kanisa haliwezi kuvunja mkataba wa MoU kwa hali yoyote ile - I can bet on that!
 
ni kweli Wakristo haiwahusu,tatizo hapa ni nani ataigharamia hii mahakama? je,ni serikali ambayo haina dini ikagharamie mahakama ya kidini?
 
Mfumo kristo umeshikwa kooni unapumulia icu tehe tehe
padre/mchungaji akigombea kwenye siasa uchwara hizi anaonekana ana kipaji cha kuongoza na wala habaguliw kwa dini yake,,masheikh wakijihusisha na chama flani cha siasa uchwara utaskia chama cha kidiniiiiiiii.....
....
I like vita ije fasta,,wajukuu zetu wataheshimiana sisi tukifa vitani inshallah...
ndio maana waislamu wanapata shida sana ....sasa wewe hapa umeshabikia nini? hivi upo serious kweli wewe? point yako hapo iko wapi? wewe na wao nani anpumulia kooni? unajua kitu mlichokiomba kwa jk na yeye alichowaahidi? unajua kaja na jibu gani sasa hivi baada ya kumpa madaraka?
amka acha ushabiki...
 
Ahhhrh.. Nimechoka kusikia hiyo kitu...mimi cjui itanisaidiaje mimi mTZ wa kipato cha chini...
 
maskof wanaishi maisha kama pepon kumbe hela ya walipa kodi wanapatia na mitaji ya biashara za cocaine
La maaskofu kuishi kama peponi nakubaliana na wewe 100% na kwamba wengi wana ukwasi usiomithilika pia ni sawa. Na kwamba baadhi yao wanafanya biashana pia ni sawa (ingawa sidhani kama wote wanauza cocaine) lakini ubadhirifu wa fedha ambao baadhi ya maaskofu wanafanya hautokani tu na hizo Bil 600 za serikali tu bali misaada kutoka kwa wafadhilii Marafiki mbali mbali pamoja na sadaka. Kiukweli kwangu mimi wapo Maaskofu ambao ni wachafu kuliko hata Edward Lowassa.
 
Back
Top Bottom