Moo Click
JF-Expert Member
- Feb 18, 2015
- 3,496
- 3,233
Wana Jf ni matumaini yangu nyote humu mu wazima. Ninaomba kufahamishwa kwa wanao ifahamu njia ya ya sinza kijiweni kupita Tandale mpaka kawawa road kuna magari mengi sana ambayo ni kama yametelekezwa na yanazidi kuongezwa, mengi ni mabovu yamepata ajali na naona kila kukicha yanazidi kulundikwa. Mengine ni 90% bado mazima kama last week nimeona kuna Prado TX nyeupe na Land Cruiser G100 zimeongezwa kwenye list.
sasa kwa Muda mrefu sana kuna maswali nimekua nikijiuliza sasa ningependa kufamishwa.
1. Je, ni nani ana husika nayo moja kwa moja maana kuna mengine naona bado yanafaa kwa spare parts
2. Je, kuna utaratibu wowote ule endapo mtu atataka kujing'olea spares maana ni kama yametelekezwa.
3. Ni kwa nini yanatelekezwa eneo kama lile lisilo rasmi maana ni pembezoni mwa barabara kabisa.
Naomba kuwasilsha.
sasa kwa Muda mrefu sana kuna maswali nimekua nikijiuliza sasa ningependa kufamishwa.
1. Je, ni nani ana husika nayo moja kwa moja maana kuna mengine naona bado yanafaa kwa spare parts
2. Je, kuna utaratibu wowote ule endapo mtu atataka kujing'olea spares maana ni kama yametelekezwa.
3. Ni kwa nini yanatelekezwa eneo kama lile lisilo rasmi maana ni pembezoni mwa barabara kabisa.
Naomba kuwasilsha.