HOMOSAPIEN
JF-Expert Member
- Mar 31, 2011
- 745
- 271
Nilikuwa naangalia Taarifa ya habari ya ITV tarehe 3/7/2012 mara nikamuona kijana mmoja akitoa ushuhuda wa kuwa alikuwa anachimba dhahabu huko Mara karibu na mgodi wa North Mara mara wakatokea watu na kuwashawishi kuwa wana mgodi wao huko Kenya na wangependa kuwachukua huko kuwapa ajira ya kuchimba madini na vijana 3 wakakubali na wakaenda huko lakini walipofika kaskazini mwa Kenya wakapitishwa katika njia wasizojua tena usiku na kuishia katika mapori ya Ethiopia huko waliwakuta waTZ wengi wakifundishwa kutumia silaha idadi yao zaidi ya elfu 50.Nao wakaanza kupewa hayo mafunzo katika hali ya taabu sana,mtoa ushuhuda anadai yeye alitoroka na kufanikiwa kurudi TZ na amewaacha wenzake huko kwa mtazamo wake wako vijana wa TZ kam laki 5 hivi wakiendelea kupewa mafunzo hayo,naomba mnisaidie huu siyo mpango mbaya kwa nchi yetu?vyombo vya usalama vinazichukuliaje taarifa hizi?mbona sijasikia hata kiongozi mmoja akikanusha au kuguswa na jambo hili?au kulifuatilia kwa kuwa limetolewa hadharani,wasiwasi wangu ni kupuuzwa kwa taarifa kama hizi ambazo kama ni kweli zinaweza kutuletea hatari kubwa hata kama malengo ya mafunzo hayo siyo kwetu ni Somalia Djibuti Uganda Kenya n.k