Mafisadi Wizara ya Ardhi

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
Naam GT nimerudi tena baada ya kutoka THA ambako tayari Mheshimiwa JK anapashughulikia nadhani it would be fair tukahamia kule wizara ya ARDHI ambako haijulikani kwa nini TITLE DEEDS zinachukua karne kutoka,MAFAILI YANACHOMWA MOTO/ AU YANAPOTEA kwa kusudi ili kuwe na delays na matokeo yake wananchi ambao kipato chai ni cha chini wanalazimishwa kutoa RUSHWA

sasa nadhani its about time tukawaname and shame wahusika pale na kama wenye JF mkiamua kuihamisha au kuamua kuibadilisha header kama ile thread ya THA na rushwa then hatuna budi kusema kuwa mtakuwa ma mafisadi kama hao ambao tunajaribu kuwa expose.
 
Yaani kama kuna watu wanakula mishahara ya bure ni wafanyakazi wa Ardhi.
Kusema ukweli kama PCCB na UWT wangekuwa n wafanya kazi hata kidogo tu, pale watu wangekuwa wanafungws kila siku. Yaani Pale Document Zinapotea hapana MCHEZO.

Ila kinachosikitisha ni kwamba wafanyakazi wadogo wanakula njama na Mabosi wao. Usitegee utaenda kwa bosi wa anayekutesa ukafikiri utapata msaada. Wote lao ni moja, nafikiri wanakatiana kitu kidogo.

Mimi nimepima kiwanja, mwaka tayari approval ya ramani ya kiwanja bado mpaka navyoandika hapa.!!!!!!!!! Yaani ni matapeli na wanarushwa sijapata kuona.

Hivi document ya mtu inapotea, harafu hakuna hata anayewajibishwa ni sahihi kweli. Wanakujibu ki rahisi tu huku wakati mwingine wakikenua mijino yao
"File lako halionekani" ,Yaani utashangaaa
 
Kwa maendeleo ya hivi karibuni wameteue assistant commissioners of lands kwa kila kanda, mbeya, dsm , mwanza na arusha kwa maana hiyo hati inaandaliwa na manispaa husika , inasainiwa na kamishna aliyeko kwenye kanda husika, inasajiliwa na msajili aliyeko huko, hakuna haja tena hati zote kusainiwa dsm

kama mpango huu ulioanza march 2009 utafanikishwa hati inaweza kuandaliwa kwa wiki moja, kamishna wetu hapa mbeya somebody luvanda amefika tayari na msajili tunae bwana kessy, nasikia hati za mwanzo zinatoka chapuchapu
 
sasa nadhani its about time tukawaname and shame wahusika pale na kama wenye JF mkiamua kuihamisha au kuamua kuibadilisha header kama ile thread ya THA na rushwa then hatuna budi kusema kuwa mtakuwa ma mafisadi kama hao ambao tunajaribu kuwa expose.

Thanks for this point; sielewi kwa nini topic ibadilishwe jina au iunganishwe na thread nyingine hata kama itakuwa inazungumzia shirika moja; e.g THA;kama maudhui ni tofauti alafu wenye jamiiforums wanaiunganisha na thread ambayo ilishajadiliwa muda mrefu uliopita ni sawa na kujaza maji kwenye pakacha; maana hamna mtu atakayeiona.

Sababu inaonekana si active topic. Of course topic yaweza hamishwa kama kama si mahali pale hilo ni rahisi kuelewa.
 
Katika Wizara ninazoona zinabadilika na kutia moyo ni Wizara ya Arthi. Yes, usumbufu upo kwa wafanyakazi wachache wasiojua majukumu yao ya kazi lakini kwa kiasi kikubwa kuna mabadiliko.
 
Yebo Yebo

unless wewe faili lako halijawahi kuchomwa moto....hivi mara ya mwisho title deed yako uliiipata baada ya muda gani?
 
Katika Wizara ninazoona zinabadilika na kutia moyo ni Wizara ya Arthi. Yes, usumbufu upo kwa wafanyakazi wachache wasiojua majukumu yao ya kazi lakini kwa kiasi kikubwa kuna mabadiliko.

Yebo Yebo Are you Serious? You must have a stake in this, or else you are among the dubious officers of Ardhi.
 
Katika Wizara ninazoona zinabadilika na kutia moyo ni Wizara ya Arthi. Yes, usumbufu upo kwa wafanyakazi wachache wasiojua majukumu yao ya kazi lakini kwa kiasi kikubwa kuna mabadiliko.

Ndugu Yeboyebo, ni vizuri ukatoa ushuhuda ulioshiba wa jinsi wizara ya ardhi inavyobalika kiitendaji kwa kuboreshwa zaidi sio tu kusema maneno! Kwa sababu wengi wetu tumeshapata usumbufu sana kwenye wizara hiyo na bado tunandelea kusumbuliwa, ungefafanua zaidi yayo maboresho yametokea idara gani na kivipi ningeelewa!
 
Ni ukiritimba tu ,kwa jinsi Nchi ilivyokuwa kubwa kila mwananchi anaweza akapewa saizi ya uwanja wa mpira na kujijengea ranchi ,ni maendeleo tu lakini lakini wafuasi wa Sultani CCM wameteka kila kitu wanagawa ardhi kama mali yao na si kugawa wanakuuzia.
 
hapana wizara hii ina improve at least from worse to bad! wamejitahidi na wakiendelea hivi wata-improve from bad to good
 
Hivi ni kwanini hao jamaa wanaopima viwanja kila ukiwahitaji- wewe mwananchi ndo inabidi uingie gharama za usafiri?tena hawapandi daladala , wanataka ukodi taxi kama huna gari! Kwani si ndi kazi yao na huko field ndo kama sehemu yao ya kazi? Sasa kwanini tunaotaka kupimiwa viwanja tulipe kuwapeleka 'ofisini' kwao? Hii si sawa na kumkodia taksi polisi kwenda kukukamatia muhalifu?

Halafu kuna kidubwana kimoja wanakiita GPS, ni muhimu kwenye upimaji viwanja lakini cha kushangaza kabla hujawatoa jamaa ofisini kwenda huko field watakuambia wanahitaji hela ya kukodia hicho kifaa! Hivi kuna mtu anajua gharama za kupima kiwanja? Sidhani, manake kila ukitaka ufanyiwe hii shughuli inabidi u bargain, gharama zilizowekwa na serekali kama zipo basi ni siri kubwa sana.

Basi kiwanja nikakipata, tena chenye hati, lakini naenda kufanya 'searching' naambiwa 'rudi baada ya siku nne za kazi uchukue majibu', lakini naona watu wanapewa majibu yao hapohapo, kuulizia wadau pembeni nikaambiwa 'ongea nao vizuri' Na kweli, kutoa buku 10 -baada ya nusu saa majibu tayari! Hiki kingeweza kuwa chanzo cha mapato, waintroduce fee kubwa kwa watu wenye haraka zao kama mimi badala ya kuendelea kuwanufaisha wale wadada pale madirishani.
 
hivi kuna mtu anaweza kupost ramani ya mipaka ya kule KIGAMBONI tukajua wapi serikali haitaki ichukuliwe?

Invisible mbona hupatikani mjomba? sisi leo tutakuwa tunatazama ball kule Irish pub
 
Wanasema kuwa katibu mkuu ardhi sasa hivi hana mfano kwa wizi wanasubiri muda wake wa kustaafu ufike tuu lakini hana mfano
 
Ukweli hawa wanahitaji kushughulikiwa...wizara ya ardhi wanasumbua wananchi utafikiri hawalipwi mshahara.

Yaani ukienda pale ni karaha isiyo na mfano...utazungushwa kama pia..na itachukua muda mrefu kabla hujapata haki yako.

Shida ni nini Jamani mpaka kusumbuana hivyo...no customer care..mwananchi ukifika unashughulikiwa kama mhalifu..au kama omba omba wakati unatoa malipo.

Tatizo liko wapi la kutoshoghulikiwa ipasavyo? Maendeleo yatapatikana hivi kweli?
Kama mtu anataka kiwanja ajenge nyumba yake nzuri..hamuoni kuwa ni maendeleo..sasa mtu anazungushwa mpaka anakuja ahata kukata tamaa ya kuwa na nyumba. Waziri husika..hiyo wizara baddoooo.

Sasa pia tatizo lingine ukishapata kiwanja..ile taasisi ya kutoa permit ya ujenzi..huko ndio matatizo kwa kwenda mbele..yaani inaweza kuchukua hata miaka miwili permit haijatoka...wakati inatakiwa iwe simple logistics..Mtu ana hati ya kiwanja..anaenda apate permit ya kujenga..aaambiwe taratibu zinazotakiwa kufuata..mwananchi atimilishe na apewe permit. Lakini huko pia mtu utazungushwa..kisa mpaka rushwa itoke kwa kila taratibu unayotakiwa kufanya.

Nitaquote statement anayopenda kutumia Judge wa American Idol.."This is Indulgent Rubbish" na inasikitisha jinsi Watanzania tunavyoumizana wenyewe kwa wenyewe..kwa manufaa ya nani?
 
Wanasema kuwa katibu mkuu ardhi sasa hivi hana mfano kwa wizi wanasubiri muda wake wa kustaafu ufike tuu lakini hana mfano

Wakati fulani Ardhi kulikuwa na katibu mkuu mchapa kazi na mlokole hivi,kaenda wapi huyo na sasa hivi ni nani?
 
Jamani niambieni yule mama Salome Sijaona si ndie alikuwa Kaatibu Mkuu aliyeleta ufanisi sana ardhi wakati wa kupima vile viwanja 20,000?

Hivi siku hizi amehamishwa!!!?? Nilipeleka search yangu ya kiwanja na property nataka kununua na imeshachukua almost 2 weeks (10 working days) na niliambiwa mara file litatafutwa Jumamosi na niende tena Jumanne hii. Kwa kweli kama una haraka lazima pesa ikutoke.

Kuna siku nilikuwa nashughulika transfer, amini it took a day plus its new search done! Unajua nilipitia njia gani????! God knows! Natumaini naweza kumtafuta mwananchi wa kawaida nimuunganishe na PCCB ili jamaa wakamatwe maana nikifanya mimi itakuwa beyond their imagination!
 
Hivi kwa nini mkuu wa Kaya (pengine kwa ushauri wa EL) alimtoa Magufuli pale Ardhi? maana nasikia kulikuwa na kambi mbili - Salome Sijaona (corrupt) akiwa na wafanyakazi wengi (corrupt) upande mmoja na Magufuli na wafanyakazi wachache (clean) upande mwingine! Chiligati ni kama vile hayupo kabisa yuko busy na propaganda za ccm.

Mkulu angalau mrudishe Magufuli.
 
Jamani niambieni yule mama Salome Sijaona si ndie alikuwa Kaatibu Mkuu aliyeleta ufanisi sana ardhi wakati wa kupima vile viwanja 20,000?? Hiv siku hizi amehamishwa!!!?? Nilipeleka search yangu ya kiwanja na property nataka kununua na imeshachukua almost 2 weeks (10 working days) na niliambiwa mara file litatafutwa Jumamosi na niende tena Jumanne hii. Kwa kweli kama una haraka lazima pesa ikutoke. Kuna siku nilikuwa nashughulika transfer, amini it took a day plus its new search done!!!!! Unajua nilipitia njia gani????!!!!! God knows!!!!! Natumaini naweza kumtafuta mwananchi wa kawaida nimuunganishe na PCCB ili jamaa wakamatwe maana nikifanya mimi itakuwa beyond their imagination!!!!

Ufanisi? fuatilia plots zilizopo kwenye prime area uone!
 
Back
Top Bottom