Kwa mara nyingine tena mafisadi wameibuka na kuendelea kuisogeza mbele ajenda yao ya urais 2015 kwa kuja na ujumbe mfupi wa maandishi ambao kwa sasa unaenea kwa kasi jijini Dar es Salaam. Ujumbe huu unawahusisha baadhi ya vigogo wa CCM ambao wanawaona kuwa ni mahasimu wao wa kisiasa, na harakati na maandamano yanaoyoendelea kwa sasa nchini. Ujumbe huo unasomeka hivi: "NJAMA ZAFICHUKA!!! mpango wa CHADEMA ni hatari tayari wamejipanga kupita kila mkoa kuhamasisha vurugu na maandamano za kuikataa serikali, pindi hatuwa za kuwadhibiti zitakapofanyika kuna mawaziri na wakuu wa mikoa wamekubaliana watajiuzulu kuunga mkono waandamanaji kwa kisingizio cha kutetea haki za binadamu. Mawaziri hao wametajwa kuwa ni samwel sitta, mwakyembe na membe na mkuu wa mkoa wa kigoma bwana Simbakalia!!?"
Kwa kuangalia mantiki ya ujumbe huu, hupati shida kugundua kwamba hii ni sehemu ya siasa za maji taka zilizoasisiwa na kuratibu vizuri na vinara wa ufisadi ambao akili yao ni kufanya kila liwezekananlo kuingia ikulu 2015, licha ya dhambi zao za unyonyaji ambazo zimetufikisha hapa watanzania. Hawa wamekuwa na mtindo wa kujifanya kumtetea Rais lakini wakati huo wakifanya vikao vya usiku vy kumhujumu na wakati huo huo kutumia vyombo vyao vya habari na vile walivyovinunua kuunga mkono maandamano ya nchi za kiarabu na wakati huo huo wakionyesha kwamba sababu za maandamano aktika nchi hizo, zipo pia hapa nchini kwetu. Ndiyo hawa hawa waliotoa kwenye RAI wiki mbili zilizopita kwamba kuna njama za kumuangusha Rais na kuwahusisha viongozi na wafanyabiashara kwenye mpango huu. Nashangaa hakuna hatua zilizochukuliwa dhidi ya gazeti hili, mmiliki na mhariri wake! Jambo lililo dhahiri ni kwamba watanzania HAWADANGANIKI NA HILA NA GHILBA HIZI!
Kwa kuangalia mantiki ya ujumbe huu, hupati shida kugundua kwamba hii ni sehemu ya siasa za maji taka zilizoasisiwa na kuratibu vizuri na vinara wa ufisadi ambao akili yao ni kufanya kila liwezekananlo kuingia ikulu 2015, licha ya dhambi zao za unyonyaji ambazo zimetufikisha hapa watanzania. Hawa wamekuwa na mtindo wa kujifanya kumtetea Rais lakini wakati huo wakifanya vikao vya usiku vy kumhujumu na wakati huo huo kutumia vyombo vyao vya habari na vile walivyovinunua kuunga mkono maandamano ya nchi za kiarabu na wakati huo huo wakionyesha kwamba sababu za maandamano aktika nchi hizo, zipo pia hapa nchini kwetu. Ndiyo hawa hawa waliotoa kwenye RAI wiki mbili zilizopita kwamba kuna njama za kumuangusha Rais na kuwahusisha viongozi na wafanyabiashara kwenye mpango huu. Nashangaa hakuna hatua zilizochukuliwa dhidi ya gazeti hili, mmiliki na mhariri wake! Jambo lililo dhahiri ni kwamba watanzania HAWADANGANIKI NA HILA NA GHILBA HIZI!