Madudu mengine ya William Mhando wa TANESCO!

Status
Not open for further replies.
JokaKuu,

Acha kungangania ya kale hapa Jamvini kumewekwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani ina details za kutosha kuhusu swali la mafuta.

Acha uvivu hivi unajua sheria za manunuzi? Huyo unayemtetea aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco William Mhando ni kihiyo mwenye elimu ya kuungaunga aliyoipata Huko Cuba katika Hali ya kutatanisha. Alifuta Zabuni nyingi kwa visingizio vya hovyo na kuwapatia mafisadi wake wakiongozwa na Rostam Aziz, Yusuf Manji na hayo makampuni ya kichina kununua Vifaa vyenye Kiwango cha chini na kujipatia mabilioni ya fedha na management yake Makao Makuu na Mikoani. Hata nguzo za miradi ya REA zinakaguliwa na Wapambe wa Mhando ni fake na umri wake hazitakaa zaidi ya miaka mitano. JokaKuu soma ,

Mokerema,

..nimeisoma hotuba ya Mnyika and basically haina jipya kuhusu hii sakata ya Tanesco vs Wizara.

..mimi nimependekeza TARATIBU na SHERIA zizingatiwe katika kushughulikia matatizo ya Tanesco.

..sidhani kama huo ni utetezi kwa Mhando, ukizingatia kwamba una ushahidi usio na shaka kwamba anahusika na ufisadi.

NB:

..achana na personal attacks.
 
NasDaz,

..I have seen a picture like this before.

..I dont trust both of them, Mhando, and Maswi.

..kwenye hiyo scenario uliyotuletea umesahau kitu kimoja kwamba Puma walijaribu kuwalangua Tanesco lakini wakashindwa ujanja na walanguzi wenzao.

..ningekuwa Maswi ningefanya uchunguzi, na kutafuta kampuni nyingine tofauti na Puma, itakayoweza ku-supply kwa bei sawa, au ndogo zaidi ya inayopendekezwa na Puma. Vilevile, ningehakikisha zoezi hilo linafuata TARATIBU za manunuzi na mikataba.

..mwisho, Maswi anajitetea kwamba ameamua kupindisha taratibu ili kuokoa fedha, na wewe unamuunga mkono. Je, Mhando naye akisema amempa mke wake tender, kutokana na uzalendo, na nia njema ya kuokoa fedha za shirika, what r u going to say??

..naendelea kusisitiza kwamba TARATIBU na SHERIA zifuatwe wakati wote.

JokaKuu, Una maoni gani kuhusu taarifa hii hapa chini?

AKAUNTI YA KIGOGO TANESCO YAZUIWA

  • Yakutwa na zaidi ya Sh. bilioni moja, uchunguzi waendelea
  • Mpango wa kupandikiza mgawo ‘feki' wa umeme wafichuliwa


SIKU chache baada ya kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme (TANESCO), William Mhando na wenzake: Robert Shemhilu, Lusekelo Kassanga na Haruna Mattambo, akaunti ya mmoja wa vigogo wa shirika hilo ngazi ya menejimenti iliyoko katika moja ya benki nchini imezuiwa na vyombo vya dola nchini, Raia Mwema, limeelezwa.

Akaunti ya kigogo huyo (jina la benki na la mwenye akaunti yanahifadhiwa ili kutoharibu uchunguzi unaoendelea) imekutwa na fedha zaidi ya shilingi bilioni moja na sasa inadaiwa kuzuiwa kwa baraka za mamlaka za juu.

Vyanzo kadhaa vya habari vimeeleza ya kuwa kigogo huyo amekutwa na mabilioni hayo ya fedha huku chanzo cha mapato hayo yasiyolingana na kipato chake kama mtumishi wa umma kikiwa ni utata.
Hata hivyo, wakati uchunguzi huo wa awali unaofanywa na vyombo vya dola nchini ukiwa unaendelea, kwa upande mwingine kumebainika kuwapo na kampeni kali za kuuokoa uongozi wa TANESCO unaochunguzwa kwa sasa, juhudi ambazo zimekuwa zikihusisha hata Kamati za Bunge.

Kamati za Bunge ambazo baadhi ya wajumbe wake wanahusishwa katika ‘kuokoa' jahazi la uongozi wa TANESCO uliosimamishwa ni pamoja na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.

Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo sasa wanatajwa kuanza kumwandama Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi pamoja na Waziri Profesa Sospeter Muhongo na Naibu wake, George Simbachawene, wanaotajwa kuwa na msimamo mkali dhidi ya kile kinachodaiwa kuwa ni uzembe na ubadhirifu ndani ya TANESCO.
Mgawo feki wa umeme
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, kwa muda mrefu sasa kumekuwa na njama za kuandaa na kufanikisha mgawo ‘feki' wa umeme nchini kwa njia mbalimbali. Lengo la mgawo huo ni kuwanufaisha baadhi ya vigogo TANESCO kwa njia ya ununuzi wa mafuta ya kuendeshea mitambo.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili na kuthibitishwa na vyanzo mbalimbali vya habari ndani ya Wizara ya Nishati na Madini pamoja na TANESCO, umebaini kuwa baadhi ya mitambo ya kuzalisha umeme jijini Dar es Salaam, na hasa baadhi ya mitambo iliyopo eneo la Ubungo na Tegeta imekuwa ikizimwa ili kuhalalisha migao na mpango wa ununuzi mafuta unaowaingizia fedha vigogo. Orodha ya mitambo inayozalisha umeme kwa mafuta jijini Dar es Salaam ni pamoja na IPTL, Symbion na Aggreko.

Taarifa zilizopo zinazidi kubainisha kuwa, baada ya kuzima mitambo hiyo na kusababisha mgawo wa umeme (usio wa lazima-feki), wito wa kuzalisha umeme wa mafuta hujitokeza.

Ni katika wito huo ambao msingi wake ni kupandikiza mgawo feki wa umeme, wakati mwingine Serikali hutoa fedha za ununuzi wa mafuta lakini wakati mwingine fedha hizo huchotwa kutoka TANESCO, shirika ambalo kila mwezi hukusanya shilingi karibu ya bilioni 100 kutoka kwa wateja wake.

Katika ununuzi huo wa mafuta kwa ajili ya kuendesha mitambo ili kuongeza uzalishaji wa umeme, mambo kadhaa huzingatiwa ili kunufaisha wahusika.

Jambo la kwanza ni kupatikana kwa kile kinachoitwa "ten percent" kinachogawanywa kwa waliofanikisha mpango huo. Pili, ni kuendelea kufanya wizi katika kiwango cha mafuta kilichokwishakununuliwa kwa ajili ya kuwasha mitambo husika.

Mchezo huo mchafu unadaiwa kuripotiwa kwa baadhi ya viongozi wa TANESCO lakini hapakuwa na hatua zilizopata kuchukuliwa hadi pale suala hilo lilipofika katika uongozi wa Wizara ya Nishati na Madini.
"Suala hili limekuwa likifanyika kwa muda mrefu sasa, umeme unakatwa na kuzalishwa kwa kiwango cha chini ili kuibua mahitaji ya kuzalisha umeme kwa njia ya mafuta ili TANESCO wanunue. Katika ununuzi huo kuna suala la 10% na wizi wa hayo hayo mafuta yanayonunuliwa lakini pia ni manufaa kwa kampuni za uzalishaji umeme huo kwa kuwa zinakuwa zikifanya biashara kwa kuuza umeme huo TANESCO.
"Ni suala lililowahi kuripotiwa lakini likapuuzwa na menejimenti, ila miezi takriban mitatu kupita baada ya kuripotiwa kuliwahi kufanyika kikao cha wafanyakazi wote kupitia TUICO, baada ya wafanyakazi kutia shinikizo kuhusu hujuma hizi Mkurugenzi wa TANESCO, Mhando naye ndipo akadai kupata taarifa hizo hapo kwa mara ya kwanza na aliahidi kuchukua hatua," kilieleza chanzo kimoja cha habari.

Hujuma kwa mtambo wa Kinyerezi

Hujuma nyingine inayotajwa kufanyika ndani ya TANESCO ni kuahirishwa mara kwa mara kwa mchakato wa kuanzisha mtambo wa kuzalisha umeme eneo la Kinyerezi, jijini Dar es Salaam.

Mtambo huo ambao utazalisha umeme kwa kutumia gesi, unatajwa kuwa tishio dhidi ya mtandao wa wauzaji mafuta kwa TANESCO kwa ajili ya uzalishaji umeme kwa kutumia mafuta.

"Kutokana na tishio la mradi huu utakapokamilika kuwanyima ulaji, walikuwa wakiukwamisha. Ni mradi wa megawati 240. Huu (mradi wa Kinyerezi) utaua kabisa mpango wao wa ulaji kwa kuandaa mgawo feki na kuzalisha umeme kwa mafuta. Waziri Muhongo alipoingia alihakikisha mradi unasainiwa ili kuanza....lazima wampige vita na aliwaeleza katika moja ya vikao (waziri) kuchukizwa na tabia hiyo,"


For more information, plz visit: Raia Mwema - Akaunti ya kigogo TANESCO yazuiwa

Je, should we conclude kwamba Raia Mwema linatumiwa na Maswi?! Anyway, I know kwamba everybody has his/her price; hata Raia Mwema nalo linaweza kununuliwa kama ambavyo linavyoonekana Mwanahalisi kutetea upande wa Mhando na wenzake!! Kama ndivyo; nazani na wakati wetu sisi wananchi ku-digest kila habari inayoandikwa na magazeti haya....let's sticky to the real situation!

  • Tarehe 10.07.2012 TANESCO walituletea mgao ambao ulisababisha kikao cha bunge kuahirishwa! Maelezo ya Mhando yalikuwa kwamba, kina cha maji Mtera kilikuwa kimepunguwa kwa kasi mno na hivyo kuhatarisha usalama wa mitambo ya kufulia umeme! Aidha, katika utetezi wake alioutoa kwa Katibu Mkuu tarehe 11.07.2012 alidai kwamba hakukua na mafuta kabisa na hivyo mgao ulikuwa hauepukiki! Hata hivyo, baada ya kubanwa; mgao ule ukatoweka within a day!!
Swali la kujiuliza hapa ni je, ni wapi yalipatakina mafuta ndani ya muda mfupi kiasi hicho?
Au ndo kwamba kina cha maji kiliongezeka within a day tena pasipo na mvua?! Unapata
picha gani kati ya tuko hilo na kauli iliyotolewa leo Bungeni na Waziri wa Nishati, Profesa
Muhongo kwamba nchi kwa sasa hakuna sababu ya kuwa na mgao wa umeme kwakuwa kiasi
kinachozalishwa ni kikubwa! Is it politics?! Vyovyote iwavyo, angalau kwa hapa mtaani
kwetu na ninakofanyia kazi hakuna mgao kwa sasa! So, kwanini nisione kwamba ni kweli
kilichokuwa kinafanywa na Mhando ni hujuma iliyolenga kujinufaisha yeye na vigogo
wenzake wa TANESCO? Why shouldn't I trust Raia Mwema on this?!



  • Miongoni mwa tuhuma ambazo Katibu Mkuu Maswi alizitoa kwa Mhando ni HUJUMA dhidi ya serikali! Tuhuma za Maswi hazikuwa taarifa kwa vyombo vya habari bali ni barua ambayo alimwandikia Mhando! Kimsingi, barua ya Maswi kama Katibu Mkuu wala haikuwa na maana ya hujuma ili Mhando apate fursa ya kufanya biashara ya mafuta; bali ni Hujuma dhidi ya serikali!! Na katika uwanja wa siasa chafu, sina shaka yoyote kwamba alichokuwa analenga Maswi ni kwamba Mhando anatumiwa na vyama vya upinzani kuleta mgao usio na maana ili wananchi wapate kuichukia serikali yao! Trust me, from political point of view, hiki ndicho haswa ambacho kililengwa na Maswi hata kama hilo la kufanya ufisadi halipuuziki! Kimsingi, hakuna tuhuma mbaya kama hizo....nazani tuhuma za hujuma dhidi ya serikali ni mbaya zaidi kuliko tuhuma dhidi ya rushwa!
SWALI: Inakuwaje Mhando akae kimya pamoja na kupewa tuhuma mzito kiasi hicho?! Yanini
basi nisiamini kwamba Mhando ameamua kukaa mkimya kwakuwa anafahamu tuhuma dhidi
yake ni za kweli na zile zinazotolewa dhidi ya Katibu Mkuu hazina mashiko na hivyo hana
ubavu wa kuzithibitisha?! Ikiwa Maswi ametamka wazi kwamba, alichukuwa uamuzi wa
kuipa kazi kampuni ya Puma Energy kwa kuwa ilikuwa inauza mafuta kwa bei ya chini na
kwamba supplier wa TANESCO walikuwa wananunua mafuta kwa bei ya chini Puma Energy
na kuwauzia TANESCO kwa bei ya juu; jambo linalotoa hisia kwamba watendaji wa
TANESCO walikuwa wananufaika na mchezo huo! Sasa, ni kwanini Mhando asisimame kidete
na kutamka wazi kwamba madai hayo ya MAswi si ya kweli na hatua yake ya kuipa kazi
Puma Energy inalenga kumnufaisha Maswi mwenyewe?! Ya nini basi nisiamini kwamba
Mhando ameamua kuwa mpole ili asije akasababisha watu wakayafumua mengi zaidi dhidi
yake?! Hivi kweli mtu msomi na mzito kama Managing Director wa TANESCO anakosa ujasiri
wa kukanusha tuhuma mzito dhidi yake?! Anakosa ujasiri au hana grounds za kujitetea?!
Badala ya kujibu tuhuma hizo mzito Mhando anaishia kutoa majibu mepesi na yasiyo na
mashiko kuhusu tuhuma za kampuni yao aliyoipa tenda ambayo bila hata ya aibu, anadai si
ya familia yake bali ni ya mkewe!
 
NasDaz,

..I have seen a picture like this before.

..I dont trust both of them, Mhando, and Maswi.

..kwenye hiyo scenario uliyotuletea umesahau kitu kimoja kwamba Puma walijaribu kuwalangua Tanesco lakini wakashindwa ujanja na walanguzi wenzao.

..ningekuwa Maswi ningefanya uchunguzi, na kutafuta kampuni nyingine tofauti na Puma, itakayoweza ku-supply kwa bei sawa, au ndogo zaidi ya inayopendekezwa na Puma. Vilevile, ningehakikisha zoezi hilo linafuata TARATIBU za manunuzi na mikataba.

..mwisho, Maswi anajitetea kwamba ameamua kupindisha taratibu ili kuokoa fedha, na wewe unamuunga mkono. Je, Mhando naye akisema amempa mke wake tender, kutokana na uzalendo, na nia njema ya kuokoa fedha za shirika, what r u going to say??

..naendelea kusisitiza kwamba TARATIBU na SHERIA zifuatwe wakati wote.


Jambo la kukumbuka pia ni kuwa PUMA ni kampuni yenye wanahisa wawili, PUMA (50%) na Serikali (50%). Kwa hiyo kampuni hii kama ikioperate kwa faida mgao ni nusu kwa nusu. Na hasara vilevile. Kwa kuwa kampuni hii ilikuwa na bei ndogo, na ni sehemu ya serikali inaleta sense kuwapa tenda hiyo ili kupata saving lakini pia faids yeyote itakayopatikana hapo baadaye.
 
Jamani lini mtanichagua niwe Mkurugenzu wa Tanesco ili mke wangu aweze kupata tender hata kama ni conflict of interest?
 
Jambo la kukumbuka pia ni kuwa PUMA ni kampuni yenye wanahisa wawili, PUMA (50%) na Serikali (50%). Kwa hiyo kampuni hii kama ikioperate kwa faida mgao ni nusu kwa nusu. Na hasara vilevile. Kwa kuwa kampuni hii ilikuwa na bei ndogo, na ni sehemu ya serikali inaleta sense kuwapa tenda hiyo ili kupata saving lakini pia faids yeyote itakayopatikana hapo baadaye.

Fofader,

..sasa kama PUMA ni 50/50 btn serikali na mwekezaji kwanini ktk tenda ya mwanzo walijaribu kuilangua Tanesco? yaani waliweka bei kubwa mpaka wakashindwa ktk tender na wateja wao wenyewe!! labda tuchunguze serikali inashirikiana na kina nani ktk kuendesha kampuni ya PUMA.
 
NasDaz said:
Je, should we conclude kwamba Raia Mwema linatumiwa na Maswi?! Anyway, I know kwamba everybody has his/her price; hata Raia Mwema nalo linaweza kununuliwa kama ambavyo linavyoonekana Mwanahalisi kutetea upande wa Mhando na wenzake!! Kama ndivyo; nazani na wakati wetu sisi wananchi ku-digest kila habari inayoandikwa na magazeti haya....let's sticky to the real situation!


Tarehe 10.07.2012 TANESCO walituletea mgao ambao ulisababisha kikao cha bunge kuahirishwa! Maelezo ya Mhando yalikuwa kwamba, kina cha maji Mtera kilikuwa kimepunguwa kwa kasi mno na hivyo kuhatarisha usalama wa mitambo ya kufulia umeme! Aidha, katika utetezi wake alioutoa kwa Katibu Mkuu tarehe 11.07.2012 alidai kwamba hakukua na mafuta kabisa na hivyo mgao ulikuwa hauepukiki! Hata hivyo, baada ya kubanwa; mgao ule ukatoweka within a day!!


Swali la kujiuliza hapa ni je, ni wapi yalipatakina mafuta ndani ya muda mfupi kiasi hicho?
Au ndo kwamba kina cha maji kiliongezeka within a day tena pasipo na mvua?! Unapata
picha gani kati ya tuko hilo na kauli iliyotolewa leo Bungeni na Waziri wa Nishati, Profesa
Muhongo kwamba nchi kwa sasa hakuna sababu ya kuwa na mgao wa umeme kwakuwa kiasi
kinachozalishwa ni kikubwa! Is it politics?! Vyovyote iwavyo, angalau kwa hapa mtaani
kwetu na ninakofanyia kazi hakuna mgao kwa sasa! So, kwanini nisione kwamba ni kweli
kilichokuwa kinafanywa na Mhando ni hujuma iliyolenga kujinufaisha yeye na vigogo
wenzake wa TANESCO? Why shouldn't I trust Raia Mwema on this?!






Miongoni mwa tuhuma ambazo Katibu Mkuu Maswi alizitoa kwa Mhando ni HUJUMA dhidi ya serikali! Tuhuma za Maswi hazikuwa taarifa kwa vyombo vya habari bali ni barua ambayo alimwandikia Mhando! Kimsingi, barua ya Maswi kama Katibu Mkuu wala haikuwa na maana ya hujuma ili Mhando apate fursa ya kufanya biashara ya mafuta; bali ni Hujuma dhidi ya serikali!! Na katika uwanja wa siasa chafu, sina shaka yoyote kwamba alichokuwa analenga Maswi ni kwamba Mhando anatumiwa na vyama vya upinzani kuleta mgao usio na maana ili wananchi wapate kuichukia serikali yao! Trust me, from political point of view, hiki ndicho haswa ambacho kililengwa na Maswi hata kama hilo la kufanya ufisadi halipuuziki! Kimsingi, hakuna tuhuma mbaya kama hizo....nazani tuhuma za hujuma dhidi ya serikali ni mbaya zaidi kuliko tuhuma dhidi ya rushwa!


SWALI: Inakuwaje Mhando akae kimya pamoja na kupewa tuhuma mzito kiasi hicho?! Yanini
basi nisiamini kwamba Mhando ameamua kukaa mkimya kwakuwa anafahamu tuhuma dhidi
yake ni za kweli na zile zinazotolewa dhidi ya Katibu Mkuu hazina mashiko na hivyo hana
ubavu wa kuzithibitisha?! Ikiwa Maswi ametamka wazi kwamba, alichukuwa uamuzi wa
kuipa kazi kampuni ya Puma Energy kwa kuwa ilikuwa inauza mafuta kwa bei ya chini na
kwamba supplier wa TANESCO walikuwa wananunua mafuta kwa bei ya chini Puma Energy
na kuwauzia TANESCO kwa bei ya juu; jambo linalotoa hisia kwamba watendaji wa
TANESCO walikuwa wananufaika na mchezo huo! Sasa, ni kwanini Mhando asisimame kidete
na kutamka wazi kwamba madai hayo ya MAswi si ya kweli na hatua yake ya kuipa kazi
Puma Energy inalenga kumnufaisha Maswi mwenyewe?! Ya nini basi nisiamini kwamba
Mhando ameamua kuwa mpole ili asije akasababisha watu wakayafumua mengi zaidi dhidi
yake?! Hivi kweli mtu msomi na mzito kama Managing Director wa TANESCO anakosa ujasiri
wa kukanusha tuhuma mzito dhidi yake?! Anakosa ujasiri au hana grounds za kujitetea?!
Badala ya kujibu tuhuma hizo mzito Mhando anaishia kutoa majibu mepesi na yasiyo na
mashiko kuhusu tuhuma za kampuni yao aliyoipa tenda ambayo bila hata ya aibu, anadai si
ya familia yake bali ni ya mkewe!

NasDaz,

..umeandika kwa kirefu sana.

..personally I am not ready kuwa upande wowote ule.

..kwa hapa tulipofikia nadhani inatakiwa iundwe TUME HURU ichunguze utendaji wa tanesco, na wizara.

..tuhuma dhidi ya Mhando ni nzito sana. kwa kweli hata mimi nashangaa mtu anayetuhumiwa kwa njama za KUIHUJUMU SERIKALI, which to me is UHAINI, pamoja na UFISADI, halafu ana-react kwa namna ambayo Mhando amefanya.

..zaidi, je Katibu Mkuu wizara ya nishati ndiye mwenye jukumu la kumshughulikia mpanga njama za kuihujumu serikali?? mimi nilifikiri ikifikia mkurugenzi wa tanesco anapanga njama za kuihujumu serikali basi suala lake linapaswa kushughulikiwa na wizara ya mambo ya ndani au idara ya usalama wa taifa. kwanini mpaka sasa hivi tunaambiwa ni bodi ya tanesco tu ndiyo inashughulikia suala hili?

.. pia kwanini Mhando ajaribu kushiriki njama za kuihujumu serikali? je, Mhando anashirikiana na watu gani, au chama gani cha upinzani, ktk kuihujumu serikali iliyoko madarakani? je, Mhando atafaidika namna gani ikiwa njama zake zitafanikiwa??

..kuhusu suala la mgao feki na ununuzi wa mafuta mazito; kutokana na maelezo yako ni kwamba dili la ununuzi wa mafuta ya mitambo ya uzalishaji umeme wa dharura lilikwisha baada ya ujio wa kampuni ya puma. kwa msingi huo nilidhani Mhando hatakuwa na kishawishi cha kuendesha mitambo ya dharura kwasababu kampuni zake zimeondolewa ktk tender ya ku-supply mafuta mazito. wewe unalionaje suala hili??

..kwa mtizamo wangu nadhani iundwe TUME HURU ichunguze tatizo la umeme nchini. tume hiyo ichunguze chanzo cha mgao wa umeme tangu miaka ya 90 mpaka sasa, pamoja na response ya Tanesco na serikali ktk kushughulikia tatizo hilo. zaidi, tuhuma zote dhidi ya Mhando zichunguzwe, kuhakikiwa, na ikiwezekana apelekwe mahakamani.

NB:

..I am very curious kujua chama cha siasa[inasemekana cha upinzani lakini mimi siamini] kinachoshirikiana na Mhando kusababisha mgao wa umeme. those r very serious allegations kutolewa. nimeona watu wamehama hawazungumzii hili suala tena.
 
aisee, hivi kumbe inakubalika kuweka pembeni sheria na kutumia 'busara' kulingana na mahitaji ya circumstances? but seriously speaking, hatuoni kama we are setting a very complicated precedent ambayo inaweza kuja kusumbua sana siku zijazo?
 
Yaani hi serikali yetu kama baba wa kambo vile anayejitahidi kwa kila hali na mali ili apendwe na watoto wa mke wake. Sasa kila uozo wa mashirika yake mwishowe atafungua mfuko wake ili awakwamue na matatizo yao ya kujitakia.
 
Sasa napata Picha kwanini Ngeleja alimkumbatia Yule katibu Mkuu aliyetimuliwa baada ya Kurudi oisini, na kwanini wale watumishi walisukuma gari! Mwenye picha ile ya Jairo naomba ailete jamani!!!!
 
Jamani hebu mwenye update atunyetishe kuhusu huyu fisadi aliyesimamishwa uchunguzi wake umeishia wapi au ndo style ileile ya kibongo...kwa kua Budget imeshapita basi wameamua kupotezea??
 
Ni nchi yetu tu ndiyo tunachezeana. Huyu anapaswa kuwa mahakamani na baadaye kufungwa na kufilisiwa kabisa! Wananchi tuna hasira sana juu ya uzembe wa kutowachukulia hatua hawa na wale wabunge aliokuwa anawahonga fedha zetu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom