ipogolo
JF-Expert Member
- Aug 15, 2011
- 6,275
- 5,961
Habari zilizopatiikana kutoka katika jiji la mbeya zinasema kuwa jumla ya madiwani 18 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) wametoka nje ya ukumbi wa mkutano kupinga ajenda zilizowasilishwa mbele yao kwa madai kuwa zilipitwa na wakati. Miongoni mwa ajenda ni suala la mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi katika jiji la Mbeya. Madiwani hao wakiongozwa na Mbunge wa CDM jimbo la uchaguzi Mbeya mjini Mh Mbilinyi aka SUGU walitaka miongoni mwa ajenda ijumuishwe inayohusu tatizo la kuungua kwa masoko mjini Mbeya. HOJA YAO NI YA MSINGI NA INA MASHIKO.