Madaktari wa Muhimbili: This is unprofessional....!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,811
15,404
Mama mkwe wangu alilazwa Muhimbili kwa wiki moja, lakini jana nililazimika kumtoa kutokana na kile nilichokishuhudia pale. Pamoja na vituko vingi tu tulivyoviona kutoka kwa manesi wa ward ya Mwaisela, lakini nisingependa kuzungumzia hayo kwa kuwa si mageni masikioni mwa wengi. Tulimpeleka mgonjwa wetu kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na kuwa na complication nyingi nadhani ni kutokana na uzee (mkwe wangu ana miaka 70 hivi sasa)

Tulipofika pale alichukuliwa vipimo vyote ikiwapo x-ray, tatizo lilikuwa ni pale madaktari wanapopita round kuona wagonjwa. kwanza walikuwa wamemgeuza mama mkwe wangu kama vile ni darasa la kufundishia wanafunzi, kila daktari alikuwa anafika na wanafunzi wake na kufungua darasa. Cha kushangaza walikuwa wameyakalia majibu ya mgonjwa wetu huku wakiendelea kumuweka pale kama mtu wa kufundishia wanafunzi.

Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.
 
Mtambuzi pole sana, wanaacha kumkomoa Kikwete na CCM yake, wanatukomoa sisi ambao hatuna uwezo hata wa kulipia hospitali kama ya Aga Khan.
Waganga wa kienyeji nao feki ile mbaya,
waombeaji nao wamekuwa magumashi ile mbaya.
Sijui tukimbilie wapi ili tupone.
Na wakati huohuo kila tunachokula na tunywacho tunaambiwa eti ni sumu.
Duhh
 
Last edited by a moderator:
Pole sana mkuu.

Ni kweli kabisa kitendo kilichofanywa na hao madaktari siyo cha kiungwana lakini na wewe haukupaswa kususa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mama mkwe wangu alilazwa Muhimbili kwa wiki moja, lakini jana nililazimika kumtoa kutokana na kile nilichokishuhudia pale. Pamoja na vituko vingi tu tulivyoviona kutoka kwa manesi wa ward ya Mwaisela, lakini nisingependa kuzungumzia hayo kwa kuwa si mageni masikioni mwa wengi. Tulimpeleka mgonjwa wetu kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na kuwa na complication nyingi nadhani ni kutokana na uzee (mkwe wangu ana miaka 70 hivi sasa)

Tulipofika pale alichukuliwa vipimo vyote ikiwapo x-ray, tatizo lilikuwa ni pale madaktari wanapopita round kuona wagonjwa. kwanza walikuwa wamemgeuza mama mkwe wangu kama vile ni darasa la kufundishia wanafunzi, kila daktari alikuwa anafika na wanafunzi wake na kufungua darasa. Cha kushangaza walikuwa wameyakalia majibu ya mgonjwa wetu huku wakiendelea kumuweka pale kama mtu wa kufundishia wanafunzi.

Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.


Mie ningewashtaki.....haiwezekani wamfanyie hivyo mama wa watu.
Poleni sana mkuu.
 
That's very unprofessional. Sijui kama na huyo aliyekuwa anawaelekeza hao wanafunzi siyo mwanafunzi mnayampara? They have to learn their professional ethics kwakweli.
 
Pole sana. Nadhani na Hao madaktari wanapaswa kujifunza kutokana na hilo. wao wanaongea kiingereza wanafikiri watu hawaelewi. siku hizi wasomi ni wengi hata huyo mzee anaweza kuwaelewa pia. Ni vizuri swala la ugonjwa wamshirikishe vizuri mhusika ili ajue tatizo lake.
 
ETHICS! ETHICS! ETHICS! Hata sie twaambiwa tu report with highest professionalism and Integrity ila ndo kwanzaaa mpango wa Tax evasion, mambo ya dressing of FS na Ukwapuaji wa kumzidi akili Auditor! We are who we are and we do what we do!
 
Mie ningewashtaki.....haiwezekani wamfanyie hivyo mama wa watu.
Poleni sana mkuu.
Tatizo sio kuwashtaki mkuu. Tatizo ni unawashtakia kwa nani???? Kuna sekta nyingi sana Tanzania zinatakiwa kuvunjwa na kuundwa upya ikiwepo hii ya Afya. Hao Madaktari kutokuwa weledi ni tatizo kubwa sana. Nilishawahi kumpeleka Wife kwa Daktari mmoja wa wanawake(Gyno) kwa check up ya kawaida kwa akina mama. Baada ya kuingia kwa Dr. Akaanza kueleza matatizo ya mgonjwa aliyetoka kumuona,yaani aliyekuwa mbele kwenye foleni kabla ya Wife. Alikuwa anaeleza vitu personal sana mpaka Wife aliponielezea nilichanganyikiwa. Halafu cha kushangaza Huyo Dr. Alikuwa ni mwanamke. Kwa hiyo Ina maana hata Issue za Mke wangu alimuelezea huyo anayefuata. Ethics Zero kabisa.

Pole sana Mtambuzi na familia kwa kuuguliwa na Mama.
 
So sad, hawa ndio watabibu wetu ethic zero kabisa, washazoea kuchinja hawajali kabisa.
Kwa kweliTZ inatisha sana, pole sana Mtambuzi
 
Last edited by a moderator:
Kimaadili, katika hospitali ambayo kuna chuo cha kufundisha madaktari inatakiwa mgonjwa wakati analazwa apewe form ya kujaza kama anakubali au kukataa kutumika katika kufundishia madaktari. Je, fomu hii mlipewa?

Kuhusu daktari kutamka lugha hiyo mbele ya mgonjwa inasikitisha, lakini turudi nyuma kidogo. Je, mgonjwa alipewa taarifa kuwa yuko kwenye terminal stage kabla ya tukio hilo? if yes, je aliipokeaje taarifa hiyo? Iwapo mawasiliano kati ya mgonjwa na daktari yamefanikiwa, mgonjwa akajua hali yake na kuikubali, kunakuwa hakuna kosa kuwaambia wanafunzi mbele yake. Tatizo linakuja pale mgonjwa anapojua kwa maa ya kwanza kuwa yuko kwenye terminal stage kupitia maneno ya daktari akiongea na wanafunzi wake!!!
 
Kimaadili, katika hospitali ambayo kuna chuo cha kufundisha madaktari inatakiwa mgonjwa wakati analazwa apewe form ya kujaza kama anakubali au kukataa kutumika katika kufundishia madaktari. Je, fomu hii mlipewa?

Kuhusu daktari kutamka lugha hiyo mbele ya mgonjwa inasikitisha, lakini turudi nyuma kidogo. Je, mgonjwa alipewa taarifa kuwa yuko kwenye terminal stage kabla ya tukio hilo? if yes, je aliipokeaje taarifa hiyo? Iwapo mawasiliano kati ya mgonjwa na daktari yamefanikiwa, mgonjwa akajua hali yake na kuikubali, kunakuwa hakuna kosa kuwaambia wanafunzi mbele yake. Tatizo linakuja pale mgonjwa anapojua kwa maa ya kwanza kuwa yuko kwenye terminal stage kupitia maneno ya daktari akiongea na wanafunzi wake!!!

Mkuu hakuna form yoyote tuliyojaza mgonjwa wetu kutumika kwa ajili ya kufundishia, lakini pia hakuwahi kumbiwa kwamba yuko kwenye terminal stage, kwa hiyo yeye na wanaye wamesikia taarifa hizo wakati daktari akiwafundisha wanafunzi wake... nilipofika niliwakuta nje wakilia na baada ya kuwadadisi wakaniambia kwamba daktari alikuwa anawaambia wanafunzi wake kwamba mama yuko kwenye terminal stage wakati anawafundisha na haikuwa ni taarifa kwao bali ilikuwa ni sehemu ya darasa huku akiwaonyesha dalili zinazothibitisha kwamba mgonjwa wetu yuko kwenye hali hiyo, kitu ambacho kiliwashtua sana.

Hata hivyo tumemrudisha mama nyumbani na hali yake inaonyesha kuimarika tangu jana jioni na leo asubihi amefanyiwa mazoezi ya kunyanyuka na kutembea na amemudu........
 
Mama mkwe wangu alilazwa Muhimbili kwa wiki moja, lakini jana nililazimika kumtoa kutokana na kile nilichokishuhudia pale. Pamoja na vituko vingi tu tulivyoviona kutoka kwa manesi wa ward ya Mwaisela, lakini nisingependa kuzungumzia hayo kwa kuwa si mageni masikioni mwa wengi. Tulimpeleka mgonjwa wetu kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na kuwa na complication nyingi nadhani ni kutokana na uzee (mkwe wangu ana miaka 70 hivi sasa)

Tulipofika pale alichukuliwa vipimo vyote ikiwapo x-ray, tatizo lilikuwa ni pale madaktari wanapopita round kuona wagonjwa. kwanza walikuwa wamemgeuza mama mkwe wangu kama vile ni darasa la kufundishia wanafunzi, kila daktari alikuwa anafika na wanafunzi wake na kufungua darasa. Cha kushangaza walikuwa wameyakalia majibu ya mgonjwa wetu huku wakiendelea kumuweka pale kama mtu wa kufundishia wanafunzi.

Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.
Pole sana mtambuzi,lakini tatizo letu wabongo tunapenda kudanganywa mgonjwa akiambiwa ukweli hatupendi.Pili muhimbili ni hospitali ya kufundishia,kwahiyo huwezi kwepa mgonjwa wako kutumika kama kitabu.
 
pole sana, mi nilienda kwa dentist, jino langu ndio likawa lakufundishia, nilipata maumivu makali mno mpaka nikachomoko na lile likiti likiwa limeunganishwa na mawaya ya umeme, pipe za maji safi na maji taka, we acha tu!
 
Mkuu hakuna form yoyote tuliyojaza mgonjwa wetu kutumika kwa ajili ya kufundishia, lakini pia hakuwahi kumbiwa kwamba yuko kwenye terminal stage, kwa hiyo yeye na wanaye wamesikia taarifa hizo wakati daktari akiwafundisha wanafunzi wake... nilipofika niliwakuta nje wakilia na baada ya kuwadadisi wakaniambia kwamba daktari alikuwa anawaambia wanafunzi wake kwamba mama yuko kwenye terminal stage wakati anawafundisha na haikuwa ni taarifa kwao bali ilikuwa ni sehemu ya darasa huku akiwaonyesha dalili zinazothibitisha kwamba mgonjwa wetu yuko kwenye hali hiyo, kitu ambacho kiliwashtua sana.

Hata hivyo tumemrudisha mama nyumbani na hali yake inaonyesha kuimarika tangu jana jioni na leo asubihi amefanyiwa mazoezi ya kunyanyuka na kutembea na amemudu........

Kama ndio hivyo basi yamefanyika makosa makubwa haya:

1. Kutokumpa mgonjwa opportunity ya kuopt out kutumika katika kufundisha wanafunzi. Hii ni haki ya mgonjwa kuamua kama yuko tayari kutumiwa kimasomo au la.

2. Mgonjwa kutojulishwa taarifa ya hali yake mapema. Majibu ya mgonjwa yakipatikana tu ni wajibu wa daktari kumjulihsa mgonjwa juu ya majibu hayo mapema iwezekanavyo.

3. Kupita round na wanafunzi mbele ya ndugu za mgonjwa. Kunaweza kuwa na mambo ambayo mgonjwa hataki ndugu zake wajue. Kuzungumza kuhusu afya ya mgonjwa mbele ya watu ambao si wahudumu wa afya wanaomhudumia ni kosa la kimaadili unless mgonjwa mwenyewe atoe ruhusu.

4.Kutoa taarifa mpya kwa watu wengine (wanafunzi) mbele ya mgonjwa bila kumshirikisha mgonjwa.

Watanzania huwa tunapenda sana kukesha tukiwalaumu wanasiasa, lakini inatakiwa ifike mahali tujiangalie kila mmoja katika kazi yake, je anaifanya kwa ufanisi???
 
Mkuu hakuna form yoyote tuliyojaza mgonjwa wetu kutumika kwa ajili ya kufundishia, lakini pia hakuwahi kumbiwa kwamba yuko kwenye terminal stage, kwa hiyo yeye na wanaye wamesikia taarifa hizo wakati daktari akiwafundisha wanafunzi wake... nilipofika niliwakuta nje wakilia na baada ya kuwadadisi wakaniambia kwamba daktari alikuwa anawaambia wanafunzi wake kwamba mama yuko kwenye terminal stage wakati anawafundisha na haikuwa ni taarifa kwao bali ilikuwa ni sehemu ya darasa huku akiwaonyesha dalili zinazothibitisha kwamba mgonjwa wetu yuko kwenye hali hiyo, kitu ambacho kiliwashtua sana.

Hata hivyo tumemrudisha mama nyumbani na hali yake inaonyesha kuimarika tangu jana jioni na leo asubihi amefanyiwa mazoezi ya kunyanyuka na kutembea na amemudu........
hapo kweli walikosea, kimaadili walihitaji consent yake before kumgeuza lecture. unaweza kuwashtaki lakini si unajua uwajibikaji hapa TZ ni 0, piga moyo konde na Mungu atasaidia. pole kwa kuuguliwa
 
Mama mkwe wangu alilazwa Muhimbili kwa wiki moja, lakini jana nililazimika kumtoa kutokana na kile nilichokishuhudia pale. Pamoja na vituko vingi tu tulivyoviona kutoka kwa manesi wa ward ya Mwaisela, lakini nisingependa kuzungumzia hayo kwa kuwa si mageni masikioni mwa wengi. Tulimpeleka mgonjwa wetu kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na kuwa na complication nyingi nadhani ni kutokana na uzee (mkwe wangu ana miaka 70 hivi sasa)

Tulipofika pale alichukuliwa vipimo vyote ikiwapo x-ray, tatizo lilikuwa ni pale madaktari wanapopita round kuona wagonjwa. kwanza walikuwa wamemgeuza mama mkwe wangu kama vile ni darasa la kufundishia wanafunzi, kila daktari alikuwa anafika na wanafunzi wake na kufungua darasa. Cha kushangaza walikuwa wameyakalia majibu ya mgonjwa wetu huku wakiendelea kumuweka pale kama mtu wa kufundishia wanafunzi.

Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.

So sad,pole sana Mtambuzi with ur family for that incidence,inakatisha tamaa sana
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom