Madaktari, Hivi hamjui kuandika vizuri au mnafanya makusudi?

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
doctor.png
...atakuwa pia MziziMkavu

doctor.png

Pia soma >Kwanini Madaktari huandika mwandiko usiosomeka? Husababishia vifo watu 7000 kwa mwaka Marekani

Habarini za leo wajameni!

Jana nilikwenda Pharmacy nikakuta mtu analalamika kwamba amekwenda kwenye Pharmacy karibia tatu wameshindwa kutambua baadhi ya majina ya dawa alizoandikiwa na Doctor kwa sababu ya mwandiko (hand write).

Alipofika kwenye Pharmacy ambayo na mimi nilikuwepo akampa Mfamasia ile karatasi, na yeye akamwambia mimi sina hiyo dawa, jamaa akamwambia yule dada naomba uniandikie vizuri jina la hiyo dawa hapo chini ili nikienda kwengine huenda nikaipata.

Kwa kuwa wanashindwa kuisoma vizuri, yule dada hakuweza kuandika akazuga zuga akamwambia we nenda tu kawaonyeshe watakupa.

Badilikeni Madaktari mnasumbua watu na miandiko yenu.
 
Last edited by a moderator:
hawa watu bwana cjui ni wabinafsi au vp maana hiyo mwandiko yao bwaga madhara makubwaana inaweza kusababisha mtu apewe dozi nyingine tofauti na ile aliyo andikiwa kwa mfano umenda zako kupima umeandikiwa dawa umeenda zako maduka ya madawa yule kashindwa kusoma si atakupa dawa tofauti na ulizo andikiwa sababu yeye pale huwa anatafuta pesa bwana kwa ushauri wajaribu kubadilisha miandiko yao maana watakuja let
 
Ni mazoea tu,si kwamba kila doctor anaandika vibaya.Ila wengi wamekuwa wakifanya hivi ili wale wasio na medics profession wasiweze kuelewa vitu ambavyo doctors wanaandika,kama prescriptions,lab results,kwasababu patient informations are confidential.kwa mfano ukafanya HIV test,ukiona yale matokeo ukajua pengine unao,inaweza ikaleta madhara,ndo maana unafanyiwa counselling ili uweze kukabiliana na matokeo.Medical ethics zinawataka doctors wawe wanaandika vitu vinavyoweza kusomeka ili pharmacists watoe dawa sahihi kwa mlengwa.
 
hawa watu bwana cjui ni wabinafsi au vp maana hiyo mwandiko yao bwaga madhara makubwaana inaweza kusababisha mtu apewe dozi nyingine tofauti na ile aliyo andikiwa kwa mfano umenda zako kupima umeandikiwa dawa umeenda zako maduka ya madawa yule kashindwa kusoma si atakupa dawa tofauti na ulizo andikiwa sababu yeye pale huwa anatafuta pesa bwana kwa ushauri wajaribu kubadilisha miandiko yao maana watakuja let

Ktk mazingira ya kawaida, madaktari hawa wana miandiko mizuri tu. Akiwa kwa job, loooh, balaa tupu. BTW, nadhani ni ubize wa kazi na idadi kubwa ya wagonjwa wanaokuwa attended.
 
Ktk mazingira ya kawaida, madaktari hawa wana miandiko mizuri tu. Akiwa kwa job, loooh, balaa tupu. BTW, nadhani ni ubize wa kazi na idadi kubwa ya wagonjwa wanaokuwa attended.
sio hata ubize sema wanakua wanafanya makusudi maana loo inatisha kwa kweli unakuta hata akiwa hana mgonjwa lkn mwandiko ni uleule
 
Ni mazoea tu,si kwamba kila doctor anaandika vibaya.Ila wengi wamekuwa wakifanya hivi ili wale wasio na medics profession wasiweze kuelewa vitu ambavyo doctors wanaandika,kama prescriptions,lab results,kwasababu patient informations are confidential.kwa mfano ukafanya HIV test,ukiona yale matokeo ukajua pengine unao,inaweza ikaleta madhara,ndo maana unafanyiwa counselling ili uweze kukabiliana na matokeo.Medical ethics zinawataka doctors wawe wanaandika vitu vinavyoweza kusomeka ili pharmacists watoe dawa sahihi kwa mlengwa.
Sikubaliani na hapo kwenye highlight... inakuwaje information hiyo inakuwa confidential hata kwa mgonjwa mwenyewe!
 
Baba V mie ni doctor kabisa, huku kwenye kompyuta naibia ibia, mie niko certified kabisa, sema najua siwezi kumtoa MziziMkavu kwenye jukwaa lake nikaamua nijichukulie umaarufu jukwaa lingine kabisa, si unajua mafahari wawili hawakai zizi moja,
 
Last edited by a moderator:
Baba V mie ni doctor kabisa, huku kwenye kompyuta naibia ibia, mie niko certified kabisa, sema najua siwezi kumtoa MziziMkavu kwenye jukwaa lake nikaamua nijichukulie umaarufu jukwaa lingine kabisa, si unajua mafahari wawili hawakai zizi moja,

Kumbe ee!!! e bana ee watu ni multi-purpose humu, very nice
 
Last edited by a moderator:
Isaac Chikoma we bwana acha kupotosha watu, mwandiko mbaya hauzii watu kujua vilivyoandikwa, ila sisi uwa tuna tumia coded language, mfano: prescription itaandikwa: pcm tab 100mg t.i.d x3 anaesoma atajua ni paracetamol vidonge viwili kila baada ya masaa manane kwa siku tatu,pia dawa zinatajwa kwa vifupi au lugha ya mficho mfano, NVP=nevirapine, EFV=efavirenz nakadhalikakama huamini muulize MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
Sikubaliani na hapo kwenye highlight... inakuwaje information hiyo inakuwa confidential hata kwa mgonjwa mwenyewe!

In some cases yes,nafkiri huo mfano unaweza ukauelewa vizuri,imagine mgonjwa mwenye presha,accidentaly anone karatasi ya matokeo yake imeandikwa ''HIV positive''what will that do to him?.ndo maana doctors wanasoma patients psychology,n they will explain it to you in a way that wont affect u that much.kuandika vibaya its not some protocol that doctors follow,but i think for some reasons, inawalazimu kuandika wanavyoandika.
 
Ni mazoea tu,si kwamba kila doctor anaandika vibaya.Ila wengi wamekuwa wakifanya hivi ili wale wasio na medics profession wasiweze kuelewa vitu ambavyo doctors wanaandika,kama prescriptions,lab results,kwasababu patient informations are confidential.kwa mfano ukafanya HIV test,ukiona yale matokeo ukajua pengine unao,inaweza ikaleta madhara,ndo maana unafanyiwa counselling ili uweze kukabiliana na matokeo.Medical ethics zinawataka doctors wawe wanaandika vitu vinavyoweza kusomeka ili pharmacists watoe dawa sahihi kwa mlengwa.


Au ukiandikiwa sindano usije ukakimbia!!!
 
Isaac Chikoma we bwana acha kupotosha watu, mwandiko mbaya hauzii watu kujua vilivyoandikwa, ila sisi uwa tuna tumia coded language, mfano: prescription itaandikwa: pcm tab 100mg t.i.d x3 anaesoma atajua ni paracetamol vidonge viwili kila baada ya masaa manane kwa siku tatu,pia dawa zinatajwa kwa vifupi au lugha ya mficho mfano, NVP=nevirapine, EFV=efavirenz nakadhalikakama huamini muulize MziziMkavu

Naelewa hivyo vifupisho,Kwangu mimi nimefikiri hiyo ni sababu inayowapelekea kuandika vibaya.ngoja tuuangalie huu uzi kwa upande mwingine,wewe unafikiri ni kwanini asilimia kubwa ya doctors lets put it 70 percent wanaandika manyongonyongo japokuwa yanasomeka.kwanini wanaandika vibaya.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom