February
Member
- Nov 15, 2011
- 90
- 21
Nimesoma kwenye mtandao wa tanuru la fikra. David Kafulila anasema mh Machali anafanya kazi ya kuhamisha mjadala kutoka hoja ya wajumbe kukosa imani na Mbatia kama mpinzani.
Katika maelezo yake Kafulila anasema mfano mdogo wa kupima kama mbatia sio mpinzani ni kesi ya kawe. Kwamba alimshauri afute kesi kwa maslahi ya chama lakini akagoma kwa hoja kuwa Mdee alimchafua sana. Kafulila anaendelea kusema kuwa walimwambia Mbatia kama hoja nikuchafuliwa afungue kesi ya kudhalilishwa badala ya kesi ya kupinga matokeo. Lakini Mbatia amegoma.
Hapa kwakweli ndipo naona Machali anapomtetea mwana ccm Mbatia bila kujijua. Kafulila kwenye ujumbe huo anasema Mbatia akishinda kesi hiyo na ikatokea CCM wanapora jimbo wao NCCR wataweka wapi sura zao? Watajiteteje kuwa sio sisiemuB?
Naomba mh Machali ufunguke macho. Hata hapa huoni mbatia anafanya kazi ya CCM? Kwa mazingira haya ni mgonjwa wa akili pekee atashindwa kuamini kuwa kesi hii ya Mbatia katumwa na CCM.
Katika maelezo yake Kafulila anasema mfano mdogo wa kupima kama mbatia sio mpinzani ni kesi ya kawe. Kwamba alimshauri afute kesi kwa maslahi ya chama lakini akagoma kwa hoja kuwa Mdee alimchafua sana. Kafulila anaendelea kusema kuwa walimwambia Mbatia kama hoja nikuchafuliwa afungue kesi ya kudhalilishwa badala ya kesi ya kupinga matokeo. Lakini Mbatia amegoma.
Hapa kwakweli ndipo naona Machali anapomtetea mwana ccm Mbatia bila kujijua. Kafulila kwenye ujumbe huo anasema Mbatia akishinda kesi hiyo na ikatokea CCM wanapora jimbo wao NCCR wataweka wapi sura zao? Watajiteteje kuwa sio sisiemuB?
Naomba mh Machali ufunguke macho. Hata hapa huoni mbatia anafanya kazi ya CCM? Kwa mazingira haya ni mgonjwa wa akili pekee atashindwa kuamini kuwa kesi hii ya Mbatia katumwa na CCM.