Mabishano yatokea kati ya mbunge na daktari MNH.

Nyalotsi

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
6,978
5,025
Kuna mbunge wa CCM leo kaja OPD ya surgery na ndugu yake mgonjwa ili apewe referal kwenda india kwa sababu ya kuvunjika mbavu moja tatizo ambalo hutibika humu nchini. Vipimo vilivyofanyika vimeonesha ana single rib fracture with no lung involvement lakini mbunge huyo akawa analazimisha daktari amsainie barua ya kwenda india kwa matibabu kwa gharama za serikali. Kawaida mtu aliyevunjika mbavu mpaka tatu bila kuumiza mapafu huwa anapewa bed rest,analgesics na antibiotics kama unahisi kutatokea infection. Baada ya kuelimishwa hivyo mbunge huyo akaendele kulazimimisha na kuanza kumtisha daktari kwamba UNAJUA MI NI MBUNGE! Daktari huyo wa kitengo cha surgery akamwambia yule mzee siwezi kuabisha hadhi yangu kumpa mtu rufaa ambaye najua watakachomwambia ndicho nilichokuambia,kama huamini unaweza kwenda kwa hela yako lakini siyo kwa idhini ya serikali ambayo mimi ndo nitakaeitoa. Baadaye huyo mzee akatoka na huyo ndugu yake ambaye ni mtumishi wa tra. Hii ndo ambayo madaktari walikuwa wanaipigia kelele lakini takwimu za watu wanaokwenda nje zikatolewa za uongo. Kwenye zile list ukiangalia kunakuwa na ndugu wengi wa viongozi ambao hushinikiza wapewe referal kwa gharama za serikali. Mtu anaambiwa kabisa prognosis ya mgonjwa lakini kwa sababu tu ya kutaka kutumia fedha za umma analazimisha. Kuna haja ya kuipitia upya sheria waliyojiwekea ya kwenda nje ili wanaotaka waende kwa gharama zao wenyewe mpaka pale inaposhindikana,hii itasaidia wazithamini na kuzijali huduma za afya humu nchini. Sijaweka jina la huyo daktari kwa usalama na huyo mbunge simfahamu kwa jina wala jimbo lake kwani ni mara ya kwanza kumuona.
 
kazi kweli kweli tunapenda mno bure bure hata kama tunaweza kumudu wenyewe! na hili ndilo tatizo linalotufanya tusiendelee tunadeka mno! na kibaya zaidi wenzako wanatafuta mkate wewe unalazimishwa upewe keki na unaamini ni halali na haki yako kufanya hivyo
lakini mwisho wa siku cc ndo tunawachagua hawa wabunge wapumbafu wasio weza kufikiria mbali kwa wao kutupikia pilau kidogo na tunauza utu wetu! hivyo tujadili nini kifanyike ili tuepukane na kupewa kidogo na kufanya maamuzi ya kuangamiza raslimali zetu!
 
Mimi sijaelewa kwani ndugu wa wabunge wakiumwa wanagharamikiwa na serikali.Kama ni hivyo basi nishajua kwa sababu gani sisi ni masikini
 
Haha, kazi ipo.. 2015 watakuja kutueleza haya yote.

Ndo hapa unapoona umuhimu wa kuwa na kituo cha habari cha demokrasia.

Naomba gazeti la Mwananchi wachapishe hii habari kwenye front page kesho.
Ili wananchi walipa kodi, waipate hii maneno.

Chadema, harakisheni TV yenu. Mnatukosesha mengi. Mambo kama haya Hayapaswi kupita kimya kimya humu kwenye JF. Ambayo wanasoma watu wachache sana. Yanapaswa kuwekwa hadharani.
 
kama humjui, je umejuaje kuwa ni Mb wa CCM?

Wanajulikana tabia zao... si umemsikia alivyolazimisha aidhinishiwe ndugu yake kwenda kutibiwa nje kwa kodi za walala hoi!!! Wamekaa kiwiziwizi...
 
Mimi sijaelewa kwani ndugu wa wabunge wakiumwa wanagharamikiwa na serikali.Kama ni hivyo basi nishajua kwa sababu gani sisi ni masikini

yawezekana wanagharamiwa wao na watoto wao kama sijakose. Nakumbuka hii kitu aliwahi kuitamka kafulila bungeni.
 
kama humjui, je umejuaje kuwa ni Mb wa CCM?

alikuwa amevaa shati la ccm lenye maandi tumethubutu,tumeweza na tunasonga mbele. What a shame jamani msifanye madaktari wakawa biased kutoa huduma kwa kuja na utambulisho wa kichama. Hospitali siyo eneo la kueneza sera,njoo na nguo za kawaida utahudumiwa kama inawezekana na unaondoka. Yawezekana na nguo alizovaa na kauli zake zilimfanya daktari awe firm zaidi kwani inafahamika moja ya maadui wa sekta ya afya nchini ni wabunge na viongozi.
 
Ingejulikana jina la mbunge huyo ingekuwa much beeeeeeeter. Otherwise ataenda kwa daktari mwingine atamwandikia referral. Najua wapo watakaosema confidentiality.
 
hatukatazi watu kupewa referal pale inaposhindikana au kama vifaa hatuna lakini siyo kwa magonjwa yanayopona yenyewe! Imagine mtu anataka kwenda nje akatibiwe mafua, kwa gharama ambazo zingesaidia kununulia dawa na vifaa vya kutibu watu wengi zaidi. HUU NI UBINAFSI. Inatakiwa tuupige vita ili kuokoa sekta ya afya. Kama wanataka kwenda nje si waende moja kwa moja kwa gharama zao? Kwa ni utake kulipiwa nauli,chakula,matibabu,malazi kwa kodi za wananchi? Yule daktari alimwambia mimi ni specialist trained kwa zaidi ya miaka kumi siwezi kufanya hayo maamuzi ya ajabu!
 
Ingejulikana jina la mbunge huyo ingekuwa much beeeeeeeter. Otherwise ataenda kwa daktari mwingine atamwandikia referral. Najua wapo watakaosema confidentiality.

hiyo huhitaji panel discusion, na kwa utaratibu wa mnh mgonjwa wa clinic moja hawezi kutolewa maamuzi na watu tofauti,hata kama ni ndugu yako we utatoa ushauri tu! Ndo maana kuna siku ukienda wanakwambia wewe sio mgonjwa wetu,kama umezidiwa utapewa emergence care na kuhamishiwa kwa wahusika. Mi mwenyewe nilitamani kufahamu jina lake lakini cjafanikiwa kwani kuna wabunge wengi siwafahamu sura zao mf aeshi, wale wa mufindi, machemuli,bukoba ndo karibu wote.
 
mhh!!! hii kali, kumbe ndio mchezo wao.
siku zao zinahesabika.
 
Back
Top Bottom