Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,978
- 5,025
Kuna mbunge wa CCM leo kaja OPD ya surgery na ndugu yake mgonjwa ili apewe referal kwenda india kwa sababu ya kuvunjika mbavu moja tatizo ambalo hutibika humu nchini. Vipimo vilivyofanyika vimeonesha ana single rib fracture with no lung involvement lakini mbunge huyo akawa analazimisha daktari amsainie barua ya kwenda india kwa matibabu kwa gharama za serikali. Kawaida mtu aliyevunjika mbavu mpaka tatu bila kuumiza mapafu huwa anapewa bed rest,analgesics na antibiotics kama unahisi kutatokea infection. Baada ya kuelimishwa hivyo mbunge huyo akaendele kulazimimisha na kuanza kumtisha daktari kwamba UNAJUA MI NI MBUNGE! Daktari huyo wa kitengo cha surgery akamwambia yule mzee siwezi kuabisha hadhi yangu kumpa mtu rufaa ambaye najua watakachomwambia ndicho nilichokuambia,kama huamini unaweza kwenda kwa hela yako lakini siyo kwa idhini ya serikali ambayo mimi ndo nitakaeitoa. Baadaye huyo mzee akatoka na huyo ndugu yake ambaye ni mtumishi wa tra. Hii ndo ambayo madaktari walikuwa wanaipigia kelele lakini takwimu za watu wanaokwenda nje zikatolewa za uongo. Kwenye zile list ukiangalia kunakuwa na ndugu wengi wa viongozi ambao hushinikiza wapewe referal kwa gharama za serikali. Mtu anaambiwa kabisa prognosis ya mgonjwa lakini kwa sababu tu ya kutaka kutumia fedha za umma analazimisha. Kuna haja ya kuipitia upya sheria waliyojiwekea ya kwenda nje ili wanaotaka waende kwa gharama zao wenyewe mpaka pale inaposhindikana,hii itasaidia wazithamini na kuzijali huduma za afya humu nchini. Sijaweka jina la huyo daktari kwa usalama na huyo mbunge simfahamu kwa jina wala jimbo lake kwani ni mara ya kwanza kumuona.