Mabalozi wa CCM na Vitambulisho vya Uraia: Hii imekaaje?

Amiliki

JF-Expert Member
May 6, 2011
2,085
1,004
Wakati najaza fomu ya kuniwezesha kuja kupata Kitambulisho cha Uraia, niliona Watu wawili wakija pale bila ya kuwa na Viambatanisho vilivyoorodheshwa kwenye fomu, lakini wakiwa na barua za Mabalozi wao wa Nyumba kumikumi ambao ni waajiriwa wa CCM (Na si kutoka kwa Watendaji wa kata ambao wanatambulika Kiserikali).

Je hawa Mabalozi wa nyumba kumi kumi wa CCM bado wanatambulika Kisheria na kwenye shughuli nyingine za kiserikali kama Mahakamani pia? Maana nimeambiwa kuwa huwa wanatoa pia barua za kudhamini mtuhumiwa mahakamani na zinakubalika.

Hivi kama wanafanya pia kazi za kiserikali, ni nani anawalipa? Je CUF na CDM viongozi wao wa huko mitaani wana nguvu hizo hizo pia, yaani wanaweza kutoa barua za Udhamini na zikakubalika?
 
Nadhani itakuwa nzuri sana kama hii ikafanyika practically, nikimaanisha kuwa mtu mmoja achukue muda wake aende akatafute barua kutoka kwa balozi wa nyumba kumi kumi kutoka CUF au CDM then atie mguu kutaka kitambulisho. Matokeo nadhani 60% wanaweza kukataa. Vipi hiyo barua ilikuwa inatoka kwa balozi kweli au M/kiti wa mtaa/kitongoji?
NB: Kama mtaa fulani una balozi wa nyumba kumi kutoka CCM ni lazima pia wawepo wa CDM na CUF au vyama vingine au navyo vinashindaniwa? Kama kila chama kinalazimika kuweka balozi wake basi ni makanjanja bado mfumo wa chama kimoja unatutafuna.
 
Mkuu Barua zinazokunaliwa ni za kiongozi wa serikali za mitaa, hao wajumbe wanamwandikia barua mwenyekiti wa serikali za mitaa kuwa hawa watu ni wakazi wa shina langu then mWenyekiti anaiandikia NIDA, nimefuata hii process kwenye mtaa wangu..
 
Mkuu Barua zinazokunaliwa ni za kiongozi wa serikali za mitaa, hao wajumbe wanamwandikia barua mwenyekiti wa serikali za mitaa kuwa hawa watu ni wakazi wa shina langu then mWenyekiti anaiandikia NIDA, nimefuata hii process kwenye mtaa wangu..
Mkuu, Hapo kwenye bolded black unamaanisha mabalozi si ndiyo; kama nii Ndiyo je hao wajumbe ni kutoka chama chochote au ni lazima awe kutoka CCM tu? Na kwenye bolded red nako unamaanisha M/kiti wa kitongoji/Mtaa.
 
Mkuu Barua zinazokunaliwa ni za kiongozi wa serikali za mitaa, hao wajumbe wanamwandikia barua mwenyekiti wa serikali za mitaa kuwa hawa watu ni wakazi wa shina langu then mWenyekiti anaiandikia NIDA, nimefuata hii process kwenye mtaa wangu..
Mimi mwenyewe nimeshuhudia mtu akija na barua ya Balozi wa CCM wa Mtaa watu ambaye ninamfahamu na si ya Mwenyekiti wa Mtaa. Kwa hiyo ninazungumza kitu ninachokijua.
 
Mimi mwenyewe nimeshuhudia mtu akija na barua ya Balozi wa CCM wa Mtaa watu ambaye ninamfahamu na si ya Mwenyekiti wa Mtaa. Kwa hiyo ninazungumza kitu ninachokijua.


hiyo barua ilikublika ya kutoka kwa mjumbe wa nyumba 10? hapa nadhani ni makosa kuwatumia hawa wajumbe wa myumba 10 kisheria wanatambuliwa na sheria ipi ya nchi? tatizo letu watanzania tunaishi kimazoea tunaishi kama tuko enzi za chama kimoja ambapo kila mwaananchi alikuwa mwanachama wa ccm, tubadilike viongozi wanaotambulika ni wenyeviti wa mitaa/vitongoji.
 
hiyo barua ilikublika ya kutoka kwa mjumbe wa nyumba 10? hapa nadhani ni makosa kuwatumia hawa wajumbe wa myumba 10 kisheria wanatambuliwa na sheria ipi ya nchi? tatizo letu watanzania tunaishi kimazoea tunaishi kama tuko enzi za chama kimoja ambapo kila mwaananchi alikuwa mwanachama wa ccm, tubadilike viongozi wanaotambulika ni wenyeviti wa mitaa/vitongoji.
NIDA kwa ujumla hawakujipanga...Bora wangekuja na Affidavit..Kiapo cha mahakama kama hauna kitambulisho chochote
 
Nadhani itakuwa nzuri sana kama hii ikafanyika practically, nikimaanisha kuwa mtu mmoja achukue muda wake aende akatafute barua kutoka kwa balozi wa nyumba kumi kumi kutoka CUF au CDM then atie mguu kutaka kitambulisho. Matokeo nadhani 60% wanaweza kukataa. Vipi hiyo barua ilikuwa inatoka kwa balozi kweli au M/kiti wa mtaa/kitongoji?
NB: Kama mtaa fulani una balozi wa nyumba kumi kutoka CCM ni lazima pia wawepo wa CDM na CUF au vyama vingine au navyo vinashindaniwa? Kama kila chama kinalazimika kuweka balozi wake basi ni makanjanja bado mfumo wa chama kimoja unatutafuna.

Kuna thread nyingine humu inazungumzia suala hili hili. Mimi nilikataliwa kuandikishwa nikidaiwa lazima niwe na barua ya balozi wa CCM. Nilijaribu kumwambia yule dada kwamba kwanini atake barua ya balozi na sio barua kutoka kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa, lakini alisisitiza kwamba anataka barua ya balozi. Kwa kuwa mabalozi hawalipwi mishahara, wanalazimisha kwa kila barua wanayoandika walipwe Tshs. 2,000

Huu ni uhuni uliopitiliza!!!!

Tiba
 
Hawa mabalozi wanatumika kwa sababu ndiyo wanawajua wkazi wao hapo mtaani tofauti na m/kiti wa Serikali ya mtaa ambao una maelfu ya watu ambao ni ngumu kuwatambua.Japo hawa watu hawapo kisheria ingekuwa wakati mwafaka kuwaweka kisheria ili watambulike kwa vyama vyao kwa kupigiwa kura na watu wote.
 
Wakati najaza fomu ya kuniwezesha kuja kupata Kitambulisho cha Uraia, niliona Watu wawili wakija pale bila ya kuwa na Viambatanisho vilivyoorodheshwa kwenye fomu, lakini wakiwa na barua za Mabalozi wao wa Nyumba kumikumi ambao ni waajiriwa wa CCM( Na si kutoka kwa Watendaji wa kata ambao wanatambulika Kiserikali)....

Kimsingi hao hawatambuliki na si viongozi halali. Mimi nimeshagombana nao sana na hadi tukapelekana mahakamani na nikawashinda.Katiba haiwatambui hao.

Tatizo linakuja kuwa viongozi wengi wa serikali wanawaogopa sana hawa jamaa kana kwamba ni viongozi.

Wanaiogopa CCM. Mimi siwaogopi na hata wanapojifanya kupita majumbani kuleta mambo yao huwa nawaambia sitofanya kwani nyie ni watu wa ccm na mimi si mwanachama wenu.Elimu ya uraia wengi hawana.

Bado wapo enzi za "viongozi wa chama na serikali". Wagomee hao wakija kwako na wakitaka kwenda mahakamani waambie wakimbie badala ya kutembea ili wafike haraka mahakamani. Watanzania tuna woga sana na ccm.
 
Hawa mabalozi wanatumika kwa sababu ndiyo wanawajua wkazi wao hapo mtaani tofauti na m/kiti wa Serikali ya mtaa ambao una maelfu ya watu ambao ni ngumu kuwatambua.Japo hawa watu hawapo kisheria ingekuwa wakati mwafaka kuwaweka kisheria ili watambulike kwa vyama vyao kwa kupigiwa kura na watu wote.

Unachokisema si sahihi.Hao ni mawakala wa ccm. Kwanza leo hii hakuna tena nyumba kumi kumi.Mwenyekiti serikali za mitaa anawajua kwani zipo kamati ndogo ndogo ambazo wengi wao wanaishi hapo hapo mtaani.Hawafai hao jamaa.Tambueni kwa sasa kuwa hatutawaliwi tena na mabalozi kama ilivyokuwa enzi za chama kimoja. Ukitaka mabalozi wapitishwe basi vyama vyote viwe vimeingizwa katika utaratibu huo.
 
Back
Top Bottom