Mabadiliko yanayotakiwa

KAKA A TAIFA

JF-Expert Member
Apr 27, 2011
566
80
Utashi na mtu atkavyokuwa baadaye huanzia tumboni mwa *****.yapo mambo mengi yanayotokea wakati mtoto anakuwa tumboni na baada ya kuzaliwa.yote haya yana sababishwa na mambo mengi sana ya kibailojia na kimazingira.mtu fulani anaweza kuiga tabia ya mzazi/wazazi,rafiki au watu wengine anaokuwa nao,mazingira fulani ,kusafiri nk.:sasa kama mtu atakuwa kiongozi ambaye hana maadili na malezi ambayo yamechangiwa na kuona, kuiga, kurithi ,kuzaliwa nayo, yaliyokuwa ni maendeleo.ufanisi katika utendaji basi hata huo uongozi na utendaji utakuwa kazi bure tu.Ndiyo maana unaona kiongozi anabakia kusema mimi siwajui hawa/hao,au nawajua lakini wajitoe wenyewe.kwa kiongozi huu ni upungufu mkubwa sana.Kiongozi anatakiwa apimwe na anaowaongoza,na kama wengi wao wakinuna au kugunaguna basi ajue huyo kiongozi ana tatizo.tuwe makini wakati wa kuchagua viongozi ambao watachukua majukumu mazito ya kuongoza nchi
 
Atapimwaje na wananchi wakati NEC miungu ya chama imeshampitisha. Kosa si wananchi kumchagua msanii, wapo waliohusika kwa hali ya juu kabisa, hawa ni miungu ya NEC. Wao walimfahamu kabla. Walifahamu utendaji wake. Hebu jiulize ni wananchi wangapi waliojua utendaji wake akiwa waziri wa mambo ya nje? Ni NEC pekee. Hawa watalaumiwa siku zote za maisha yao. Wao na vizazi vyao watalaaniwa kwa kukubali kutuchagulia kiongozi asiyejua kwa kila jambo. Dhami hii haitaondoka kwao, wao, watoto wao, wajukuu na vijuukuu. Mpaka kipite kizazi cha nne.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom