SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,151
- 7,918
Kwanza naomba mods msihamishe uzi huu kwa kuupeleka kwenye jukwaa la dini maana nataka tumjadili huyu Shetani katika misingi ya maisha yetu ya kila siku na si katika misingi ya dini.
Naileta mada hii kwa tahadhari kubwa sana. Sina nia ya kumpromote huyu jamaa ila nadhani imefika wakati tumuangalie katika uhalisia. Siwezi kuimagine dunia bila kuwa na miongozo ya maisha yenye kusisitiza upendo, amani, mshikamano na umoja kati ya wanadamu. Miongozo yote hii tumeambiwa ndiyo njia ambayo Mwenyezi Mungu anataka tupite. Shetani kwa upande mwingine tumefundishwa, mambo yake na njia zake ni potofu, ovu na zitakazopelekea uangamie katika moto wa milele. Maandiko yameenda mbali zaidi na kutuambia tajiri atapata wakati mgumu sana kuuona ufalme wa Mungu. Hili jambo ukilifirkia vizuri, linafikirisha sana.
Kutokuwa na maarifa kumeelezewa katika maandiko kuwa ni kitu hatari na kibaya, lakini pia kuwa na maarifa na kwenyewe kumehusishwa na shetani kwa sababu kunaweza kumfanya mtu kuwa na majivuno na kwamba majivuno yanakuja kabla ya maangamizi. Kwa hiyo kiufupi maandiko yame discourage sana kuwa na maarifa kutokana na sababu nyingi ambazo ukiziangalia kweli zina mashiko.
Mimi nimeanza kufikiri kuna jinsi ambayo maandiko yamepotoshwa sehemu. Upotofu unaweza kuwa kwa njia ya kuficha taarifa muhimu kuhusu mtu au kitu fulani, taarifa ambazo kama ukiwa nazo zinaweza kubadili ufahamu wako kuhusu jambo hilo. Nayasema maneno haya kwa tahadhari kubwa naomba nieleweke vizuri. Nahisi kuna watu wamehodhi maarifa haya na wanayatumia kwa ajili ya ku control watu na dunia.
Tunaishi maisha ambayo hatujijui sisi ni nani, asili yetu, nguvu zetu na hata madhaifu yetu. Wakati huo huo ufahamu wa shetani ni mdogo saaana. Ukikaa ukafikiria jinsi gani hatumjui shetani utashangaa sana. Sun Tzu aliwahi kusema ili kumshinda adui yako inabidi kwanza ujijue wewe vizuri na umjue adui yako vizuri, hapo unajiweka katika nafasi ya kushinda vita. Kama Shetani ni adui yetu namba moja kama tunavyofundishwa, nadhani tuanze kwanza kufundishana ili mimi na wewe kila mmoja wetu ajijue YEYE NI NANI na pia kuwe na mafundisho ya kutosha na deep sana kuhusu Shetani.
Uzi huu ni wa maarifa hatari. Naomba tujadili mada hii kwa staha ili wote tutoke na kitu cha kutujenga katika maisha yetu hapa duniani.
Naileta mada hii kwa tahadhari kubwa sana. Sina nia ya kumpromote huyu jamaa ila nadhani imefika wakati tumuangalie katika uhalisia. Siwezi kuimagine dunia bila kuwa na miongozo ya maisha yenye kusisitiza upendo, amani, mshikamano na umoja kati ya wanadamu. Miongozo yote hii tumeambiwa ndiyo njia ambayo Mwenyezi Mungu anataka tupite. Shetani kwa upande mwingine tumefundishwa, mambo yake na njia zake ni potofu, ovu na zitakazopelekea uangamie katika moto wa milele. Maandiko yameenda mbali zaidi na kutuambia tajiri atapata wakati mgumu sana kuuona ufalme wa Mungu. Hili jambo ukilifirkia vizuri, linafikirisha sana.
Kutokuwa na maarifa kumeelezewa katika maandiko kuwa ni kitu hatari na kibaya, lakini pia kuwa na maarifa na kwenyewe kumehusishwa na shetani kwa sababu kunaweza kumfanya mtu kuwa na majivuno na kwamba majivuno yanakuja kabla ya maangamizi. Kwa hiyo kiufupi maandiko yame discourage sana kuwa na maarifa kutokana na sababu nyingi ambazo ukiziangalia kweli zina mashiko.
Mimi nimeanza kufikiri kuna jinsi ambayo maandiko yamepotoshwa sehemu. Upotofu unaweza kuwa kwa njia ya kuficha taarifa muhimu kuhusu mtu au kitu fulani, taarifa ambazo kama ukiwa nazo zinaweza kubadili ufahamu wako kuhusu jambo hilo. Nayasema maneno haya kwa tahadhari kubwa naomba nieleweke vizuri. Nahisi kuna watu wamehodhi maarifa haya na wanayatumia kwa ajili ya ku control watu na dunia.
Tunaishi maisha ambayo hatujijui sisi ni nani, asili yetu, nguvu zetu na hata madhaifu yetu. Wakati huo huo ufahamu wa shetani ni mdogo saaana. Ukikaa ukafikiria jinsi gani hatumjui shetani utashangaa sana. Sun Tzu aliwahi kusema ili kumshinda adui yako inabidi kwanza ujijue wewe vizuri na umjue adui yako vizuri, hapo unajiweka katika nafasi ya kushinda vita. Kama Shetani ni adui yetu namba moja kama tunavyofundishwa, nadhani tuanze kwanza kufundishana ili mimi na wewe kila mmoja wetu ajijue YEYE NI NANI na pia kuwe na mafundisho ya kutosha na deep sana kuhusu Shetani.
Uzi huu ni wa maarifa hatari. Naomba tujadili mada hii kwa staha ili wote tutoke na kitu cha kutujenga katika maisha yetu hapa duniani.