Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 42
Ninashangazwa na wanasiasa na wapambe wa CCM wanaowawekea vikwazo na kuwanyoshea kidole Chadema eti waachane na mpango wa maandamano kwa madai kuwa watanzania hawana utamaduni huo. Naipongeza Chadema kwa kuandaa maandamano ya kupinga ongezeko la asilimia 18.5 ambao wengi wamehusisha ongezeko hilo na ufisadi wa Dowans na Richmond. Haya ni maandamano muhimu sana ya kupinga sera dhalimu za CCM zinazowaumiza wananchi. Kazi ya vyama vya siasa ni kuuza sera. Kwa kuandaa maandamno ya kupinga ongezeko hilo, Chadema inawaunga mkono vilivyo wananchi wa Tanzania ambao wanaumizwa sana na sera za kinyonyaji za CCM. Haya ni maandamano muhumu sana kwetu sisi wananchi. Kitu cha kushangaza ni kuwa CCM huundaa maandamano ya kuunga mkono hotuba za wanasiasa wao akiwemo mwenyekiti wa taifa wa CCM. Ni hivi karibuni tu CCM walitangaza maandamano kupitia TBC1 na kuyafuta baada ya dakika tano. Chadema wasirudie kosa la kuacha kuwaongoza na kuwahimiza wananchi kupinga udhalimu wa CCM kama walivyofanya kwa kuahirisha maandamano ya kupinga uchakachuaji wa kura za urais. Kwa kuahirisha maandamano CCM wamepata kichwa cha kuendelea kuwanyima watanzania haki yao ya kuongozwa na viongozi waliowachagua. Kilichotoa Arusha cha CCM kubaka demokrasia katika uchaguzi wa Meya wa Arusha kisingetokea kama Chadema wangeitisha maadamano mapema ya kupinga urais wa kura za kuchakachua. Wenzetu wa Ivory Coast karibu wanafanikiwa kumrudisha rais waliyemchagua kwa vile wameungwa mkono na jumuia ya kimataifa ikiwemo jumuia ya nchi za Afrika Magharibi. Kilichotokea Arusha ni mwendelezo wa wimbi la CCM kuvunja utawala wa sheria. Wakati CCM wakitenda kinyume na utawala wa sheria, waziri mkuu Mizengo Pinda yeye anauona utawala wa sheria kwa kuunga mkono watanzania wawalipe mafisadi wa Dowans. Tuwaunge mkono Chadema katika maandamano ya kuwatetea wananchi kwa sababu ni chama cha siasa sawa na CCM. Chadema wanahaki ya kuandamana kama CCM wanavyoandaa maandamano kuunga hotuba za wanasiasa wao.