Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,447
- 7,829
Mamlaka za Marekani zimeipiga faini ya dola milioni 222 kampuni ya programu kwa kutoa rushwa katika nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Tanzania, nchi nyingine ni Kenya, Afrika Kusini, Ghana, Malawi. Pia zipo Azerbaijan na Indonesia.
Maafisa wa mamlaka ya bandari Tanzania(TPA) wanatuhumiwa kupokea bilioni 2.1($ 800,000) kama rushwa ili kuipa tenda yenye thamani ya $ 6,635,000 kampuni inayojihusisha na programu(software) Tenda ilihusisha kutoa leseni na huduma, tenda hiyo ilipewa kampuni ya Twenty Third Century Systems ambayo imesajiliwa Zimbabwe.
Maafisa hao wanadaiwa kupokea pesa hizo kwenye sanduku. Pamoja na kampuni hiyo kulipwa $ 4,000,000 kampuni hiyo ilishindwa kutimiza chochote. Mwaka 2022 Tanzania ilibatilisha mkataba baina yao ulioingiwa mwaka 2014/15 na kuwafungulia kesi maafisa waliohusika.
Inaaminika pia kampuni hiyo iliweka gharama mara mbili ya gharama za kukodi program hiyo, TPA ililipa $ 404,029 badala ya gharama halisi ya $ 190,643.
Pia Mwezi Septemba 2019 TPA ililipa kampuni hiyo hiyo kutoka Ujerumani $400,000 kupitia kazi zake zilizofanywa na kampuni yake iliyosajiliwa Zimbabwe. Pia TPA iliipa mkataba mwingine wenye thamani ya $ 997,647 kutoa huduma ambayo haikutajwa.
Maafisa wa mamlaka ya bandari Tanzania(TPA) wanatuhumiwa kupokea bilioni 2.1($ 800,000) kama rushwa ili kuipa tenda yenye thamani ya $ 6,635,000 kampuni inayojihusisha na programu(software) Tenda ilihusisha kutoa leseni na huduma, tenda hiyo ilipewa kampuni ya Twenty Third Century Systems ambayo imesajiliwa Zimbabwe.
Maafisa hao wanadaiwa kupokea pesa hizo kwenye sanduku. Pamoja na kampuni hiyo kulipwa $ 4,000,000 kampuni hiyo ilishindwa kutimiza chochote. Mwaka 2022 Tanzania ilibatilisha mkataba baina yao ulioingiwa mwaka 2014/15 na kuwafungulia kesi maafisa waliohusika.
Inaaminika pia kampuni hiyo iliweka gharama mara mbili ya gharama za kukodi program hiyo, TPA ililipa $ 404,029 badala ya gharama halisi ya $ 190,643.
Pia Mwezi Septemba 2019 TPA ililipa kampuni hiyo hiyo kutoka Ujerumani $400,000 kupitia kazi zake zilizofanywa na kampuni yake iliyosajiliwa Zimbabwe. Pia TPA iliipa mkataba mwingine wenye thamani ya $ 997,647 kutoa huduma ambayo haikutajwa.