robinson crusoe
JF-Expert Member
- Oct 22, 2020
- 740
- 1,214
Waziri Mkuu Majaliwa, Asante kwa kufika mjini Bukoba haraka baada ya ajali ya ndege. Hata hivyo kuna ajali nyingi zilizopoteza maisha ya wengi kuliko hata hii ya Precision, lakini hazikupata nafasi ya kiserikali kama hii. Hazikupewa hadhi ya maafa ya kitaifa kwa uharaka. na hasa kutembelewa na kiongozi wa kitaifa kwa umuhimu siku hiyo hiyo na kuahirisha shughuli zingine. Je, hadhi ya marehemu inatokana na aina ya usafiri:
1. Mama wa ajali zote nchini ni May 1996, MV Bukoba ilizama na kupoteza idadi isiyojulikana (zaidi ya 800) ya abiria.
-Hii Waziri mkuu Sumaye aliendelea na safari yake kama kawaida bila hisia.
2. April 2007 Abiria 22 walifariki kwa ajali ya basi la Buffalo likielekea Arusha.
-Hakuna kiongozi wa kitaifa aliyefika eneo la tukio
3. May 2017 wanafunzi 32, dereva 1 na waalimu 2 (jumla 35) wa Lucky Vincent Arusha walifariki kwa ajali
-Hakuna kiongozi wa kitaifa aliyefika eneo la tukio
4. Miezi mitatu iliyopita basi la shule limeua watu 13 mikindani mtwara.
-Hakuna kiongozi wa kitaifa aliyefika eneo la tukio
Ni kweli kwamba thamani ya marehemu ni aina ya usafiri? Kizuri ni kwamba Abiria wa Ndege wameokolewa na mitumbwi ya kasia. Na wasio na ajira za serikali au shirika. Asanteni kwa mawazo yenu.
1. Mama wa ajali zote nchini ni May 1996, MV Bukoba ilizama na kupoteza idadi isiyojulikana (zaidi ya 800) ya abiria.
-Hii Waziri mkuu Sumaye aliendelea na safari yake kama kawaida bila hisia.
2. April 2007 Abiria 22 walifariki kwa ajali ya basi la Buffalo likielekea Arusha.
-Hakuna kiongozi wa kitaifa aliyefika eneo la tukio
3. May 2017 wanafunzi 32, dereva 1 na waalimu 2 (jumla 35) wa Lucky Vincent Arusha walifariki kwa ajali
-Hakuna kiongozi wa kitaifa aliyefika eneo la tukio
4. Miezi mitatu iliyopita basi la shule limeua watu 13 mikindani mtwara.
-Hakuna kiongozi wa kitaifa aliyefika eneo la tukio
Ni kweli kwamba thamani ya marehemu ni aina ya usafiri? Kizuri ni kwamba Abiria wa Ndege wameokolewa na mitumbwi ya kasia. Na wasio na ajira za serikali au shirika. Asanteni kwa mawazo yenu.