Ndugu wanajamvi, kama mnavyojua ni takribani miezi miwili imebaki kukamilisha miaka miwili ya awamu ya pili (ya miaka mitano) ya raisi wa JMT, Mh J. M Kikwete.
Kwa maoni yangu ni jambo la busara tukikumbushana mambo makubwa ambayo yametokea katika uongozi wa raisi huyu katika miaka miwili iliyopita. Hii itasaidia kutathmini tunakoenda kwa kuangalia tulikotoka.
Kisiasa, kiuchumi, kijamii na kadhalika, ni mambo gani ungependa kuyaorodhesha ambayo kwako yalikuwa makubwa katika kipindi hiki cha miaka miwili ya awamu ya pili ya Kikwete?
Mi kwa kuanzia tu, nakumbuka mambo yafuatayo
1. Kikwete aliridhia na kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya
2. Kikwete alikubali kw kiasi kikubwa kuwasikiliza na kujumuisha mapendekezo ya CHADEMA katika sheria ya kuandika katiba
3. Serikali ya Kikwete ilichafuliwa kwa kusababisha mauaji ya wananchi wasio na hatia kule Arusha, Songea, na Morogoro kupitia jeshi la polisi kwa kisingizio cha vurugu za kisiasa, na hivi karibuni kumuua mwandishi wa habari Daudi Mwangosi
4. Kwa mara ya kwanza katika uongozi wake, Kikwete alikumbana na changamoto ya kukataliwa kwa bajeti ya nishati na madini na bunge, hadi ilipofanyiwa marekebisho
5. Kwa shinikizo la wananchi, Kikwete alilazimika kuvunja na kuunda upya baraza la mawaziri.
6. Serikali ya Kikwete ilikumbana na changamoto ya maandamano ya kundi la UAMSHO kule Zanzibar, na kutokea kwa vurugu zilizochochewa na askari.
7. Serikali ya Kikwete ilifanikiwa kuendesha zoezi la sensa, ambalo nalo lilikumbwa na changamoto ya kugomewa na baadhi ya taasisi za kiislamu na makundi mengine ya watu
Naomba tuongeze matukio, katika kuyapa uzito maadhimisho haya.
Pia naomba uchambuzi, je kwa tunavyoona utendaji wa serikali hii, nini kitarajiwe kwa miaka mitatu ijayo?
Kwa maoni yangu ni jambo la busara tukikumbushana mambo makubwa ambayo yametokea katika uongozi wa raisi huyu katika miaka miwili iliyopita. Hii itasaidia kutathmini tunakoenda kwa kuangalia tulikotoka.
Kisiasa, kiuchumi, kijamii na kadhalika, ni mambo gani ungependa kuyaorodhesha ambayo kwako yalikuwa makubwa katika kipindi hiki cha miaka miwili ya awamu ya pili ya Kikwete?
Mi kwa kuanzia tu, nakumbuka mambo yafuatayo
1. Kikwete aliridhia na kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya
2. Kikwete alikubali kw kiasi kikubwa kuwasikiliza na kujumuisha mapendekezo ya CHADEMA katika sheria ya kuandika katiba
3. Serikali ya Kikwete ilichafuliwa kwa kusababisha mauaji ya wananchi wasio na hatia kule Arusha, Songea, na Morogoro kupitia jeshi la polisi kwa kisingizio cha vurugu za kisiasa, na hivi karibuni kumuua mwandishi wa habari Daudi Mwangosi
4. Kwa mara ya kwanza katika uongozi wake, Kikwete alikumbana na changamoto ya kukataliwa kwa bajeti ya nishati na madini na bunge, hadi ilipofanyiwa marekebisho
5. Kwa shinikizo la wananchi, Kikwete alilazimika kuvunja na kuunda upya baraza la mawaziri.
6. Serikali ya Kikwete ilikumbana na changamoto ya maandamano ya kundi la UAMSHO kule Zanzibar, na kutokea kwa vurugu zilizochochewa na askari.
7. Serikali ya Kikwete ilifanikiwa kuendesha zoezi la sensa, ambalo nalo lilikumbwa na changamoto ya kugomewa na baadhi ya taasisi za kiislamu na makundi mengine ya watu
Naomba tuongeze matukio, katika kuyapa uzito maadhimisho haya.
Pia naomba uchambuzi, je kwa tunavyoona utendaji wa serikali hii, nini kitarajiwe kwa miaka mitatu ijayo?