Ndyali
JF-Expert Member
- Nov 24, 2011
- 1,661
- 948
Mchungaji Lusekelo awaponda
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) lililopo Kibangu jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako amewafananisha na wauaji wa albino madaktari waliogoma wakiishinikiza serikali iwatimizie madai yao.
Lusekelo aliyekuwa akizungumza na waandishi wa habari alisema wanachokifanya madaktari hakina tofauti na watu wanaofanya mauaji ya albino ili wapate fedha zaidi ambazo hazina baraka za Mungu.
Aliongeza kuwa, madai hayo ya madaktari ni sawa na ufisadi zaidi ya ule uliofanyika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje Benki Kuu (EPA).
Madaktari wanafanya uuaji . wanawaadhibu wananchi wasio na hatia, wao wanaidai serikali, sasa kwanini wanawaacha wagonjwa wafe ili kushinikiza kupata fedha zao? alisema.
Aliongeza kuwa madaktari wanatakiwa kufahamu kuwa hicho wanachokidai kitawalazimu wananchi watozwe kodi kubwa jambo ambalo litawazidishia ugumu wa maisha.
Alisema madaktari wanapaswa kumuogopa Mungu na kurejea kazini kwani binadamu wanaishi kwa kutegemeana, hivyo wataalamu hao wasijione ni muhimu kuliko watu wengine.
Mchungaji Lusekelo alisema madaktari wamefanya dharau kubwa kukataa kuonana na waziri mkuu kuzungumzia madai yao.
SOURCE: TANZANIA DAIMA
My take: Tapeli mkuu huyu anayetumia jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo,kuwatapeli watanzania ana usafi wowote wakuwakoromea Ma-Dr. wetu kwa kuwalinganisha na wauji wa Maalbino? Au ndo janja ya agent wa Shetani huyu kutafuta kulindwa na serikali ya magamba?
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) lililopo Kibangu jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako amewafananisha na wauaji wa albino madaktari waliogoma wakiishinikiza serikali iwatimizie madai yao.
Lusekelo aliyekuwa akizungumza na waandishi wa habari alisema wanachokifanya madaktari hakina tofauti na watu wanaofanya mauaji ya albino ili wapate fedha zaidi ambazo hazina baraka za Mungu.
Aliongeza kuwa, madai hayo ya madaktari ni sawa na ufisadi zaidi ya ule uliofanyika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje Benki Kuu (EPA).
Madaktari wanafanya uuaji . wanawaadhibu wananchi wasio na hatia, wao wanaidai serikali, sasa kwanini wanawaacha wagonjwa wafe ili kushinikiza kupata fedha zao? alisema.
Aliongeza kuwa madaktari wanatakiwa kufahamu kuwa hicho wanachokidai kitawalazimu wananchi watozwe kodi kubwa jambo ambalo litawazidishia ugumu wa maisha.
Alisema madaktari wanapaswa kumuogopa Mungu na kurejea kazini kwani binadamu wanaishi kwa kutegemeana, hivyo wataalamu hao wasijione ni muhimu kuliko watu wengine.
Mchungaji Lusekelo alisema madaktari wamefanya dharau kubwa kukataa kuonana na waziri mkuu kuzungumzia madai yao.
SOURCE: TANZANIA DAIMA
My take: Tapeli mkuu huyu anayetumia jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo,kuwatapeli watanzania ana usafi wowote wakuwakoromea Ma-Dr. wetu kwa kuwalinganisha na wauji wa Maalbino? Au ndo janja ya agent wa Shetani huyu kutafuta kulindwa na serikali ya magamba?