babalao 2
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 5,400
- 3,245
Habari zilizotufikia hivi punde
zinadai kuwa Mahakama kuu
ya Tanzania imemwachia kwa
dhamana msanii wa filamu
nchini Tanzania, Elizabeth
Michael aka Lulu aliyekuwa
mahabusu katika gereza la
Segerea jijini Dar es Salaam.
Wiki iliyopita mawakili wa
muigizaji huyo waliwasilisha
maombi ya dhamana kwa
mahakama hiyo kuu ya
Tanzania.
Wanasheria hao Peter Kibatala,
Kennedy Fungamtama na
Fulgence Massawe waliomba
dhamana hiyo itolewe haraka
kwakuwa muombaji amekaa
mahabusu kwa zaidi ya miezi
saba na kwamba kosa lake
linaweza kupewa dhamana.
Lulu anakabiliwa na kesi ya
kumuua bila kukusudia Steven
Kanumba April 7, 2012, huko
Sinza Vatican, jijini Dar es
Salaam.Kanumba alidaiwa
kuwa kwenye ugomvi na Lulu
aliyekuwa mpenzi wake
nyumbani kwake Sinza.