Lt Col Alexander Nyirenda (RIP)

Waga

JF-Expert Member
Feb 6, 2008
322
14
MAJOR ALEX GWEBE NYIRENDA, SHUJAA ALIYEPANDISHA MWENGE WA UHURU JUU YA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO SIKU YA MKESHA WA UHURU WA TANZANIA BARA, HATUNAYE TENA.

HABARI ZILIZOINGIA SASA HIVI TOKA KWA FAMILI YAKE ZINASEMA MAJOR NYIRENDA ALIFARIKI JANA SAA MOJA JIONI KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI ALIKOLAZWA. ALIKUWA NA UMRI WA MIAKA 72.

ALIKUWA AKISUMBULIWA NA MARADHI YA KANSA KWA MUDA MREFU NA AMESHAKWENDA MARA KADHAA NCHINI INDIA KWA MATIBABU.

KWA MUJIBU WA HABARI HIZO ZA KIFAMILIA, MAZISHI YATAFANYIKA DAR JUMATANO KATIKAMAKABURI YA KINONDONI. MSIBA UKO NYUMBANI KWA MAREHEMU MBEZI BEACH, NJIA YA KWENDA AFRICANA, DAR.

SOURCE.. michuzi.blogspot
 
Mungu aifariji familia yake na kuiweka Roho ya Shujaa wetu Maj.Nyirenda mahala pema peponi-amina.
Poleni wananyirenda.
R.I.P. Maj. Nyirenda.
 
Mungu awaifariji familia ya wafiwa wakati tuliobaki tujikumbushe na kuyaiga mazuri yote ambayo marehemu aliyafanya.
 
Ni Major au Brigedia?
Mungu ampumzishe kwa amani. Ni mtu ambaye matebndo yake mengi yanafaa kuigwa
 
Ni Major au Brigedia?
Mungu ampumzishe kwa amani. Ni mtu ambaye matebndo yake mengi yanafaa kuigwa

Mn ninachofahamu alikuwa ni major sina hakika kama alifikia kwenye ngazi ya ubrigedia, labda wanaomjua zaidi watatusaidia hapa
 
ni brigadier general...kuna wakati alipewa u bragedier ..sina record clear ni lini ..lakini ni enzi ya mzee mwinyi....


pole sana washkaji ....
 
Mungu amuweke mahali pema peponi Brigadier Nyirenda, great man great leader, strong character na charismastic pia,

-Ingawa nilikuwa mdogo sana, lakini nakumbuka kwamba he was a big player katika siasa zetu za mwanzoni za taifa kwa sababu he was all over the national political scene, hasa karibu sana na Kambona.

- Mara ya mwisho nilikutana naye Lusaka mwaka 1979, ambako alikuwa akiishi na familia yake, kama kawaida yake full of life na alyways athletic, Mungu amuweke pema huko mbele ya haki, a true son of Africa.
 
kwa wenzetu huyo angeingia kwenye orodha ya heroes lakini bongo hatuelewi hivyo,mungu amsamehe na adhabu za ahera,
 
kwa wenzetu huyo angeingia kwenye orodha ya heroes lakini bongo hatuelewi hivyo,mungu amsamehe na adhabu za ahera,
 
Ni Major au Brigedia?
Mungu ampumzishe kwa amani. Ni mtu ambaye matebndo yake mengi yanafaa kuigwa
...Ni kweli kuna radio moja alitangaza ni brigedia lakini sidhani kama alifikia cheo hicho alikuwa Major!!! RIP Nyirenda!!!
 
Back
Top Bottom