LOWASSA hajatangaza kuwa atagombea Urais,tayari Msuguano umeanza! siku akitangaza!??

sokoinei

JF-Expert Member
Feb 27, 2012
1,832
566
Waziri mkuu wa zamani aliejiuzulu kwa kashfa ya Richmond na mbunge wa Monduli mh Edward Ngoyai Lowassa,ndie mwanasiasa ambae amekuwa akitajwa sana na kuandikwa na vyombo vya habari kwa takriban wiki mbili sasa!

Hii ni baada ya tar 1/1/2014 akiwa Jimboni kwake Monduli ktk sherehe za mwaka mpya,akizungumza na wageni waalikwa alisema kuwa safari yake imeanza baada ya mateso ya muda mrefu!

Tumesikia baadhi ya viongozi wa Ccm wakilumbana kuhusu Kauli za mh Lowassa,,hata wengine wamediriki kusema wazi wazi kuwa Lowassa anavuruga Chama na hata wakaenda mbali zaidi na kudai kuwa hana sifa ya kuwa kiongozi,,wala kuwa Amiri jeshi mkuu na Mwenyekiti wa Ccm!

Sijui na wala Siamini km kuna siku mh Lowassa ameitisha Waandishi wa habari na kutangaza nia yake ya kugombea Urais!

Ninajua mh Lowassa anajiandaa na anayo nia ya kuwa mgombea kwa Ccm na siku moja awe Amirijeshi mkuu wa majeshi ya Ulinzi na Usalama!
Lakini kiukweli itakua vigumu sana kwa mh Lowassa kuwa Rais wa Tanzania,hii inatokana na kwamba hakubaliki na Watanzania walio wengi nje na ndani ya Ccm!
Lakini pamoja na haya bado baadhi ya Wana Ccm wanachanganyikiwa na jitihada hizi za Lowassa hata kuwafanya wawe wanatoa matamko juu yake.

Nachojiuliza ikiwa Lowassa hajatangaza kuwa atagombea Urais ni kwanini basi viongozi wengi wa Ccm wanahaha?
Hajatangaza hali iko hivi je siku akitangaza itakuaje?

Mwenye jibu anisaidie!
 
alisema ameanza safari ya kwenda wapi? kufanya nini?

mateso ya muda mrefu ni yepi?

nani anamtesa? kwa nini?
 
mie natafakari kiinua mgongo cha kutoka milioni 60 hadi milioni 160........................?
huko kwa lowasa p kabisa.
 
Mkuu atangaze mara ngapi??

Ni kweli kwa mwonekano wa kawauda ni sawa kesha tangaza ijapo sio rasmi,lakini tunajua kwamba kuna baadhi ya viongozi wengine wa Ccm km.Samwel Sitta,,Bernad Membe,,Fredrick Sumay nk ambao nao pia wameshaonyesha nia pia ya kugombea kupitia chama cha mapinduzi!
Lakini hatusikii hawa wengine wakisemwa au kuandamwa km Mh Lowassa huku nao wakiwa wameonyesha Wazi wazi kwamba wanatamani kuchukua nafasi hiyo kubwa ktk nchi hii.

Ndipo napo pata mashaka juu ya uwezo wa Viongozi wakuu wa Ccm ambao wameshindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu Makada wao hawa wanaokivuruga chama na badala yake wamebakia kutoa matamko.

Wakati Chadema inawaadabisha viongozi wake kwa makosa yanayofanana na haya ya kina Lowassa,,Wana CCM walio wengi waligeuka na kuwa watetezi wa Wasaliti hao wa Chadema.

Najiuliza tena ikiwa Lowassa hajatangaza rasmi kuwa atagombea lakini baadhi ya viongzi wa Chama chake wameanza Sarakasi na kuchanganyikiwa,je siku akitangaza rasmi itakuaje????
 
Ni kweli kwa mwonekano wa kawauda ni sawa kesha tangaza ijapo sio rasmi,lakini tunajua kwamba kuna baadhi ya viongozi wengine wa Ccm km.Samwel Sitta,,Bernad Membe,,Fredrick Sumay nk ambao nao pia wameshaonyesha nia pia ya kugombea kupitia chama cha mapinduzi!
Lakini hatusikii hawa wengine wakisemwa au kuandamwa km Mh Lowassa huku nao wakiwa wameonyesha Wazi wazi kwamba wanatamani kuchukua nafasi hiyo kubwa ktk nchi hii.

Ndipo napo pata mashaka juu ya uwezo wa Viongozi wakuu wa Ccm ambao wameshindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu Makada wao hawa wanaokivuruga chama na badala yake wamebakia kutoa matamko.

Wakati Chadema inawaadabisha viongozi wake kwa makosa yanayofanana na haya ya kina Lowassa,,Wana CCM walio wengi waligeuka na kuwa watetezi wa Wasaliti hao wa Chadema.

Najiuliza tena ikiwa Lowassa hajatangaza rasmi kuwa atagombea lakini baadhi ya viongzi wa Chama chake wameanza Sarakasi na kuchanganyikiwa,je siku akitangaza rasmi itakuaje????

Lowassa ni mwiba kwa wapnzan wake ndan ya chama
 
Lowassa ni mwiba kwa wapnzan wake ndan ya chama
Sita,Mangula,Mwakyembe nk niviongozi wabaya sana na wafitini.Hao ndio walitia zengwe hadi Lowasa akajihudhuru.Ili wakae kwa amani ni lazima wamuue kisiasa.Chuki zao zinatuletea madhara sisi wadogo.
 
Mtoa hoja anaishi nchi gani? EL kisha tangaza na watu kama Mwenyekiti wa CCM Singida akatoa tamko la kumuunga mkono. Malumbano yanayoendelea ndani ya CCM yanatokana na tukio la la Januari Mosi. Mwenye masikio na asikie.
 
Mtoa hoja anaishi nchi gani? EL kisha tangaza na watu kama Mwenyekiti wa CCM Singida akatoa tamko la kumuunga mkono. Malumbano yanayoendelea ndani ya CCM yanatokana na tukio la la Januari Mosi. Mwenye masikio na asikie.

acha majungu ww,huna jipya
 
Mi mtazamo wangu ni kwamba hii ni mbinu yenye lengo flani mahsusi, si kweli kwamba wanaompinga wote waibuke kwa wingi sasa wakati jamaa kaanza muda sana maandalizi. Kutokana na huko kuanza muda sana, kumzuia si rahisi hata kidogo hivyo hapa wanatucheza shere tuuu, hao wanaompinga na wanaomtetea wote timu moja.

Tusubiri tuone
 
Sita,Mangula,Mwakyembe nk niviongozi wabaya sana na wafitini.Hao ndio walitia zengwe hadi Lowasa akajihudhuru.Ili wakae kwa amani ni lazima wamuue kisiasa.Chuki zao zinatuletea madhara sisi wadogo.

kwa hyo mwanao akiwa malaya utaacha kumwadhibu kisa kesho aweza kuwa na uwezo akakutenga mzazi? wanaccm mnasiasa za kinafki sana. kama uchunguz ulifanywa na kamati ya bunge taarifa ikahakikiwa iweje leo mgeuke? acheni ujinga...nyoka na aitwe nyoka..ndicho tutakacho watanzania...
 
Ni kweli kwa mwonekano wa kawauda ni sawa kesha tangaza ijapo sio rasmi,lakini tunajua kwamba kuna baadhi ya viongozi wengine wa Ccm km.Samwel Sitta,,Bernad Membe,,Fredrick Sumay nk ambao nao pia wameshaonyesha nia pia ya kugombea kupitia chama cha mapinduzi!
Lakini hatusikii hawa wengine wakisemwa au kuandamwa km Mh Lowassa huku nao wakiwa wameonyesha Wazi wazi kwamba wanatamani kuchukua nafasi hiyo kubwa ktk nchi hii.

Ndipo napo pata mashaka juu ya uwezo wa Viongozi wakuu wa Ccm ambao wameshindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu Makada wao hawa wanaokivuruga chama na badala yake wamebakia kutoa matamko.

Wakati Chadema inawaadabisha viongozi wake kwa makosa yanayofanana na haya ya kina Lowassa,,Wana CCM walio wengi waligeuka na kuwa watetezi wa Wasaliti hao wa Chadema.

Najiuliza tena ikiwa Lowassa hajatangaza rasmi kuwa atagombea lakini baadhi ya viongzi wa Chama chake wameanza Sarakasi na kuchanganyikiwa,je siku akitangaza rasmi itakuaje????

watauana wana ccm, na tena CCM wanachama wake walio wengi ni wanafiki, wanajifanya kumpaka matope ilihali wakijua na mtu anayekubalika!!.. Sasa wanajichanganya tu hao wameshajua jamaa akishika usukani patakuwa hapatoshi..
 
Back
Top Bottom