Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Kwa mtazamo wangu, Tanzania tumefika mahali tunahitaji kuupindua mfumo mzima wa kifisadi, kuondosha u-mungu mtu na kusimika rasmi misingi ya utawala wa sheria - iwe wazi kuwa hata rais anapaswa kuheshimu sheria na asiwe na uhuru wa kutumia vyombo vya dola kwa maslahi binafsi. Huo ndio mfumo wa ovyo uliojengwa na CCM.

HIVYO, PA KUANZIA ni kuiondoa CCM madarakani ili kwanza kuvunja dhana ya chama dola - kwamba chama kilichopo madarakani kinatumia nyenzo za dola (NEC, TISS, Polisi, BOT, n.k.) kujihakikishia ushindi katika chaguzi. Kumhakikishia mwanasiasa au chama cha siasa ushindi wa kudumu hata iweje ni hatari sana kwa mustakabali wa taifa.
 
CCM halisi itajulikana ikiwa nje ya dola. Hapo ndipo mafisadi wote waliojazana kutumia nyenzo za dola kujichotea na kukandamiza haki za watanzania watakapokikimbia chama na kuwaachia wenyewe rasmi. Na ndipo chama kitakapoweza kurejea kwenye misingi yake halisi.

Naamini UKAWA wanaweza kipindi hiki kutoa rais bora hata kama hatakuwa "perfect". Ilmuradi ajue kuwa wananchi hawatampa "guarantee" ya kuendeleza ujinga unaoendekezwa na CCM leo hii. Suala si kuwa na kiongozi perfect. Bali wananchi kuwa na uwezo wa kuwadhibiti viongozi waperform.
 
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it

wewe ni team shein,nani asiyekujua
 
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it


kwahiyo tumchague nani?
 
utakuwa umetumwa wewe, wewe umemuona lowassa tu, uchambuzi wako ungekuwa wa msingi kama ungefanya comparison na wengine
 
kwa historia ya nchi yetu imedhihirika pasipo na shaka kuwa kiongozi aliyetoka jamii ya kimasai ni watu shupavu na wameonyesha kwa vitendo utendaji kazi wengine ni maneno matamu utafikiri wanatongoza binti wa kike. wa kwanza alikuwa ni Edward Sokoine na wa pili alikuwa ni Edward Lowassa.

siri kubwa ya kupingwa kwa lowassa ni Ukaskazini wake na Uthibitisho ni kauli iliyowahi kutolewa na Mmoja wa makada wa CCM kutoka Bagamoyo kuwa raisi hatatoka kaskazini.

Hili suala la kuchafua watu wa Kaskazini limekuwa pia likishikiwa bango na baadhi ya makada wa CCM dhidi ya CDM.


hivi nyie wanasiasa mnaohubiri ukanda mnayo akili kweli? nani kawamilikisha Tanzania?
 
Lowasa angebaki na utajiri wake wa asili, ng'ombe hakuna mtu angepiga kelele. Kosa amelifanya pale alipoanza kujiingiza kwenye kashfa za ufisadi
 
lnakera sana eti. ""RAIS HATATOKA KASKAZINI HUU NDIO UKABILA NDANI YA NCHI YETU DHANA HII NDIO YA KUIOGOPA KAMA UKOMA WATANZANIA WATACHAGUA RAIS YULE WANAEMUONA ANAWAFAA NO MATTER NI UPANDE GANI ANATOKEA YAPO MAMBO NA MISEMO INAYOSTAHILI KUPUUZWA NA KUCHOMWA MOTO"""
 
Weweeee judge weeee!!!???? umeshaleta balaaa huku!! najua team lowasa wameshajua kuwa hawana chao maskini,, na kumchafua huyu jaji inabidi utumie taa ya meli kumulikia chumbani!!!! japo kwa ccm hata aje nani ni wale wale tu, Hizo sababu ulizoongea ni za kipuuzi tu, lowasa si mtu safi kamwe, na ndio maana anatumia pesa kuonyesha kuwa anapendwa sana!! ili kutisha chama chake!! kwani anachofanya sasa si kutafuta udhamini bali ni kampeni tu. MABADILIKO YA KWELI YATATOKA UKAWA. "msitu ni ule ule ila nyani mpya"
 
Weweeee judge weeee!!!???? umeshaleta balaaa huku!! najua team lowasa wameshajua kuwa hawana chao maskini,, na kumchafua huyu jaji inabidi utumie taa ya meli kumulikia chumbani!!!! japo kwa ccm hata aje nani ni wale wale tu, Hizo sababu ulizoongea ni za kipuuzi tu, lowasa si mtu safi kamwe, na ndio maana anatumia pesa kuonyesha kuwa anapendwa sana!! ili kutisha chama chake!! kwani anachofanya sasa si kutafuta udhamini bali ni kampeni tu. MABADILIKO YA KWELI YATATOKA UKAWA. "msitu ni ule ule ila nyani mpya"

ukawa wakisimama pamoja mambo yataenda ikiwa ndivyo sivyo CDM watasema Ukaskazini na CUF watasema Uisilamu. haya ndio msingi wa hoja yangu
 
kwani huyo jamaa ni mmasai?
pia acheni siasa zenu za kikabila.
Mshaurini apumzike.

aliyeanzisha siasa za kikabila ni hao makada wa CCM walionukuliwa na vyombo vya habari wakihubiri ukanda. naona una mazoea ya kubishana maana unapingana na ukweli ulionukuliwa
 
Ah, tumechoka kila siku lazima atajwe humu na usanii wake anaofanya kila mkoa ili aonekane anapedwa. Huyo ni UNFIT
 
Lowasa angebaki na utajiri wake wa asili, ng'ombe hakuna mtu angepiga kelele. Kosa amelifanya pale alipoanza kujiingiza kwenye kashfa za ufisadi

lizaboni hivi kwa nini huyu ndugu yenu hamumpeleki mahakamani? kuna haja gani ya kuwa na chama kinachojua mafisadi alafu hakiwachukulii hatua
 
lizaboni hivi kwa nini huyu ndugu yenu hamumpeleki mahakamani? kuna haja gani ya kuwa na chama kinachojua mafisadi alafu hakiwachukulii hatua
Mahakama ya Lowasa kwa ufisadi wake ipo mikononi mwa Mangula. Soon atajua nini maana ya mtu kuwa safi
 
Ah, tumechoka kila siku lazima atajwe humu na usanii wake anaofanya kila mkoa ili aonekane anapedwa. Huyo ni UNFIT

mbona tunaona wanaohudhuria ni wanaCCM tena wanashangilia kweli kweli. msitulaumu sisi wachambuzi laumuni wanaCCM wenzenu. na ni aibu mwanaCCM kusema mbele ya uma kuwa wanaCCM wenzake wananunulika. hii ni uthibitisho kuwa hata viongozi wetu wanaotuongoza labda wananunulika pia na mafisadi kutoka nje kwa mlango wa wawekezaji
 
Mahakama ya Lowasa kwa ufisadi wake ipo mikononi mwa Mangula. Soon atajua nini maana ya mtu kuwa safi

Ndugu Lizabon Mangula siku hizi amekuwa mahakama? Ufisadi ni kosa la Jinai Mangula atamsikiliza kwenye Mahakama ipi ya JMT.
 
Back
Top Bottom